Mkuu wa nchi lazima awe mkali na aogopwe. Asipoogopwa kila kitu kitakwenda mrama. Hata hayati Julius Nyerere aliogopwa na alikuwa mkali

Hata Mimi nilishangaa,Rais wetu aliposema hatafokea MTU yeyote.

Toka enzi za utawala wa kifalme na usultan,Mtawala Ni Lazima aogopwe,vinginevyo,Kazi zitafanyika kwa kulipua,na wizi wa Mali ya Uma utakuwa mkubwa Sana.

Ukichukulia pia Rais wetu Ni wa Jinsia ya Kike,Asicheke na wezi wa Mali ya umma.

Ikithibitika umeiba Mali ya Uma,Wezi hao wafilisiwe na kufidia mpaka centi ya mwisho iliyoibiwa,pesa irudishwe kwenye mfuko wa Serikali kuu.

HAKUNA KUCHEKA NA WEZI WA MALI YA UMA,NA WANAOCHEZEA NIDHAMU YA KAZI KATIKA UTUMISHI WA UMA.
 
Huyu Mama bwana anatulostisha sana, akiachana na Kikwete pamoja na wale mawaziri useless waliotemwa na Jiwe angetupeleka mbali sana.
 

Kwanini kwenye kila kitu aigwe Nyerere?

Watu milioni 60 tunatawaliwa na kuongozwa kwa fikra za mtu mmoja tuu, kwani sisi North Korea?

Nyerere kweli aliwaloga Watanzania na ndiyo maana tunakwama kwenye mambo mengi sana.
 
Hawatakaa waguse tena. Imeisha hiyo
Achana na hawa watu wamezoea kuchunga ng'ombe, wanafikiri na binadamu anachapwa tu mijeledi kama ngombe,

Ndo maana nyumba nyeupe hawatakaa wapate bahati tena ya kuingia!
 
hayo yoote yalikuwepo wakati wa huyo unayemtaja
 
Macho yenyewe yameshalegea sijui kama yanaona ofisi zote ni hovyoooo tunadaiwa rushwa wazi wazi wala hawajali huduma mbovu mwacheni Magu aitwe Magu alikuwa kiboko na hatutapata tena rais kama Magu mkimtaka mtu wa aina ya Magu nichagueni mimi na ntashika adabu
 
Kutokana na yaliyotokea 2019 na 2020 hakuna asiye na guilty conscience. Watu wanaoficha ukweli hawawezi kuwa huru mioyoni mwao na mbele za Mungu. Mengine yote ni matokeo!
 
Huu ndio ujinga wetu watanzania, nyinyi ni wauwaji Kama wauwaji wengine tu,Yani unashindwa kuwatibia ndugu zako kisa raisi hakutishii kukufukuza kazi?huu ni ujinga uliopitiliza
 
Kwanini kwenye kila kitu aigwe Nyerere?

Watu milioni 60 tunatawaliwa na kuongozwa kwa fikra za mtu mmoja tuu, kwani sisi North Korea?

Nyerere kweli aliwaloga Watanzania na ndiyo maana tunakwama kwenye mambo mengi sana.
Nimetolea mfano tu, sijasema aigwe. Lakini kwa taifa lolote mkuu wa nchi lazima awe mkali na kuogopwa ili asimamie taifa lake vizuri
 
Marekani na Ulaya, ambapo tunawaiga kwa demokrasia, hawabembelezani.

Trump alikuwa anafukuza watu karibu kila siku.

Hakuna kitu kinachoitwa nidhamu ya moyoni!
Yaani unadiriki kutoa mfano wa Trump...pua,puaa,puaaaaaa
 
Tatizo unadandia mada ambazo huna hata uwezo wa kuzielewa.

Ni kama familia ambayo baba hana sauti na watoto hawamuogopi . Unategemea nini? Kwa nini usikae kimya ili tusikuome mpumbavu.
 
Na this time itakuwa worse kuliko hata awamu ya nne.
 
Kiongozi Ukiwa mwadilifu,mpen da haki,muwazi, unauependa matokeo mazuri.na makubwa, ...honest,Integrity,principled(Kingereza kwa msisitizo) ...watu watakuogopa by Default...!
JPM hakuwa na hayo ,kama alikuwa nayo kidogo sana ....yeye aliogopwa Kwa kuwa alikuwa mkali ,anatisha,haaminiki,hatabiriki,roho Mbaya,fyatu.....Ili uelewe ZAIDI ilikuwa mi sawa na Mtu Mwenye Sura Mbaya ambaye watoto hutishiwa wasifanye Kitu Fulani!
Nyerere alikuwa anaogopwa kutokana na uadilifu wake,matendo yake mazuri Kwa umma yalimfanya atishe....tena waliokuwa wanamwogopa ZAIDI,ni wazembe,wasio waadilifu ...wasiojiamini...vilaza!
Unafikiri Mtei,Sokoine au Kambona Walikuwa wanamwogopa...Tafuta picha za Nyerere na Sokoime uone body language ya Mwalimu AKIWA na Sokoine 😁
Bahati Mbaya hivi vitu havilazimishwi vinakuja tu na Karama kutoka Kwa Mungu!
Ukilazimisha itafikia kuanzaa kutesa,kukandamiza watu ,pengine hata kuua!
Kwa Chief Hangaya...wote mnamjua ...no comment?🀭🀭😁😁
Mwisho,hata sisi wananchi tupo tulio na Karama hizo...basi tu hatujapewa jukwaa ,Ndio maana Tunadai Katiba Mpya Ili I- Gorvene ' Uendeshaji wa Nchi ..kuwathibiti Makarmastili kama Nyerere na wale wanaotaka kuwa Makarasmatiki kimichongo!
Na wasio eleweka pia !
Mungu Ibariki TANZANIA!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…