Mkuu wa Wilaya Arusha na mbwembwe za misafara

Mkuu wa Wilaya Arusha na mbwembwe za misafara

Anapoenda kukagua miradi wakuu wa idara wanaenda na nini kama sio usafiri wa magari, acheni majungu.
 
Queen Sendinga RC wa Iringa nae jana nimeona 'convoy' yake ikiongozwa na FOTON ya Polisi na pia GX nyingine sijui ya nani. Kwa hiyo 'convoy' yake ni gari 3, ya kwanza PT yenye king'ora na mataa, inafuata yake RC na ya tatu GX yenye namba STL. Hapo trafiki anasimamisha magari yampishe RC anaenda home kwake.

Nchi hii ina matukio sana
 
Queen Sendinga RC wa Iringa nae jana nimeona 'convoy' yake ikiongozwa na FOTON ya Polisi na pia GX nyingine sijui ya nani. Kwa hiyo 'convoy' yake ni gari 3, ya kwanza PT yenye king'ora na mataa, inafuata yake RC na ya tatu GX yenye namba STL. Hapo trafiki anasimamisha magari yampishe RC anaenda home kwake.

Nchi hii ina matukio sana

Tulio pata bahati ya kuona awamu ya kwanza huu ujinga haukuwepo kabisa.
 
Nimemwandikia mam warak kwenye mkeka wake niwemo, hususan anipangie Kaskazini

Nikifika TUTAELEWANA tu.
Ila anipe na mtu anayejua hata kusoma maana mi darasa la Saba B
 
Heshima sana wanajamvi,

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini ni kijana mdogo lakini mwenye mbwembwe nyingi na vituko vya ujana uliopitiliza.Katika siku za karibu amekuwa na tabia ya kusindikizwa na gari la polisi ikiambatana na ving'ora vingi pengine ungefikiri kuna mgonjwa wa Covid 19 anakimbizwa Hospital kuwahi huduma za kitabibu.

Mwezi uliopita kama kumbukumbu zangu zipo sana alizindua mradi mdogo {mradi uchwara} wa kufyatua matofali wa halmashauri ya Jiji la Arusha.Huo msafari ungefikiri anakwenda kuzindia kinu cha Nyuklia gari zilikuwa zinakimbizwa,ving'ora na taa za magari yote zikiwashwa full light.Tutakae tukubali Vijana wakipewa madaraka kidogo wanaharibu sana,wanaumiza wananchi sana,wanatumia madaraka vibaya sana bahati mbaya Mkuu wa Wilaya ya Arusha yumo katika kundi hilo.

Mwaka jana alishiriki zoezi la kuwachapa viboko wafanyabiashara kwa madai ya kununua thamani za shule.DC kawa mpelelezi,akajivika ujaji na mwisho wa siku akamalizia kudhalilisha wananchi pasipo uchunguzi wa haki.
Juzi wakati nipo Samunge gari iliyokuwa inaongoza msafara wake kidogo inigonge yaani
 
Juzi wakati nipo Samunge gari iliyokuwa inaongoza msafara wake kidogo inigonge yaani

Anaongozwa na ulimbukeni wa madaraka.Barabara zenyewe za Arusha zimeshavamiwa na machinga halafu anatokea mshamba anakimbiza magari bila sababu za msingi ukiuliza anachokimbilia nini hana majibu.
 
Kwakweli huyu mkuu wa wilaya ya Arusha simjui vizuri ila ni mtu poa sana.

Nakumbuka mwishoni mwa mwaka jana alitusaidia kupata mafao yetu NSSF baada ya kusumbuliwa karibia mwaka mzima.
Nnachokumbuka tulimfata siku moja tuna akatuambia turudi baada ya siku 3, na tulivyorudi aliondoka na sisi hadi kwenye ofisi za nssf pale Arusha na akaingia na sisi hadi ndani, akakagua computer za pale kwa sababu tulimweleza namna tunavyopigwa danadana muda mrefu bila majibu ya kueleweka....
Meneja alijitahidi kujitetea kwa uongo mwingi lakini kupitia mkuu huyu wa wilaya tulipata mafao yetu bila kuchelewa.

Kumbuka tulikua wengi hivyo alitusaidia sana
Namkubali sana maana amesaidia watu wengi kuanzia waliodhulumiwa maeneo yao, migogoro ya kifamilia na mengine mengi... Kwakweli nilimkubali hadi nikawa nahudhuria kwenye ziara zake za kusikiliza kero za wananchi.

Yule aliyekuwepo kabla yake tulimfata akatufukuza na maneno mbovumbovu bahati nzuri hakumaliza mwezi akaondolewa ndio akaletwa aliyepo sasa.
Naam, wewe utakua ni mkazi wa Arusha. Huyu kijana amesaidia wananchi wengi Sana,, bila kujali itikadi zao. Binafsi niliwahi kufika Mara kadhaa ofisini kwake, akifika anawasalimia wananchi kwa nidham huezi amini ni Mkuu wa wilaya. Kuna wanasheria zaidi ya kumi pale ofisini kwake wa kujitolea kwa ajili ya kuwasaidia wananchi yeye ndo naskia anawafadhili. Amekua anafanya semina za ujasiriamali kuwafundisha Wanawake na vijana ujasiriamali.
Nachokiona mh. Mbunge hataki Wala hapendi kuona yule KIJANA anakubalika na kufanya KAZI. Majuzi bila aibu Eti akaitisha kikao Cha bajaji akapanga watu wakumchafua huyu DC. Gambo usipojirekebisha na kufanya hizi siasa zako chafu hatutakuchagua Tena hakika nakuambia.
 
Majungu si MTAJI useme utafanikiwa.......

Baadhi ya watu wa ARUSHA NA KILIMANJARO hawawapendi MADC NA MARC wenye misimamo dhidi ya "MADILI YAO"...

Yaani kusikia tu mh.Rais anaandaa "MKEKA WA MADC" basi watu wanajiandaa kuwachafua WENGINE(TARNISHING OF IMAGE)....



#KaziIendelee
Hii ni KAZI ya Gambo, sio MTU mwingine
 
Wakati mwingine uwe unauliza sisi wa zamani tunajua ni kamati ya ulinzi na usalama yenye DC ,ocd dso mkuu wa kikosi jwtz uhamiaji magereza takukuru fire na das wanakagua miradi itakayozinduliwa na mwenge wa uhuru.muache kuandika mambo msiyoyajua.
Halafu wanatuona sisi wananchi ni hamnazo. Huyu DC wengi wanaomba abaki, isipokua Gambo. Sasa sijui atafanya KAZI na nani
 
Mkuu umekata mzizi wa fitina kabisa hiyo mikoa miwili kila siku ma DC na RC wanaoneka wabaya tu gambo wakati wake alikuwa strong sana na alifanya kazi nzuri sana,hao wafanya biashara na wanasiasa hasa hao wawili ni shida sana wanataka waangaliwe tu kwa chochote wanachotaka hata kama si halali kwa manufaa yao binafsi, suala la Sabaya kuna uwezekano mkubwa kuna watu nyuma yake wameunda hayo mambo busara na umakini unahitajika sana maana kila kukicha watu wanaibuka tu sijui kabla walikuwa wapi.
Gambo alikua mwonevu, na sasa hapendi viongozi wenzake. Amejisahau kwamba yeye saivi sio mkuu wa mkoa Bali ni mbunge. KILA Rc, DC Ras na Def yeye hua lazma awakatae. Majungu anavyofanywa saizi ni sababu huyo DC anapita hiki KWENYE kata kutatua kero za wananchi. Sasa Gambo yeye hataki, anataka yeye ndo aonekane KILA kitu anafanya.
Sasa Gambo huyu Rc wa sasa ni mpya kwanini umeanza figisu za chini chini, Rc huyu amekufanyaje,, KUMBUKA huyu alikuja Arusha KABLA yako
 
Chondechonde Mhe Rais
Huyu kijana mwenzetu hastahili kabisa kuwepo kwenye mkeka wako wowote ule.
Hivi kweli kabisa kijana mdogo kama huyu kuwachapa watu wazima viboko hadharani ni utawala bora kweli.
Hata huko magereza waliohukumiwa viboko wanachapwa faragha.
Mhe. Rais huyu kijana hana sifa za uongozi kabisa.
Kwanza anamajivuno
Pili anapenda kujichukulia sheria mikononi.
Tatu anadharau kwa viongozi hata watendaji wa chini
Anaonyesha uwezo wake wa kufikiri ni Mdogo Sana ukifuatilia mambo anayofanya.
Duuu mwogope Mungu. Wananchi yupo na tunaona. Halafu mama hafanyi KAZI kupitia mitandao ama kwa kuskiza cheap gossips. Uraisi ni TAASIS, taarifa za jinsi huyo DC anafanyaje majukumu yake zipo kwa usahihi
 
Mwezi uliopita kama kumbukumbu zangu zipo sana alizindua mradi mdogo {mradi uchwara} wa kufyatua matofali wa halmashauri ya Jiji la Arusha.Huo msafari ungefikiri anakwenda kuzindia kinu cha Nyuklia gari zilikuwa zinakimbizwa,ving'ora na taa za magari yote zikiwashwa full light.Tutakae tukubali Vijana wakipewa madaraka kidogo wanaharibu sana,wanaumiza wananchi sana,wanatumia madaraka vibaya sana bahati mbaya Mkuu wa Wilaya ya Arusha yumo katika kundi hilo.
Sabaya alipokuwa anakuja kufanya fujo hapo yeye alikuwa wapi?
 
Tatizo sio Ma DC vijana kiongozi,, tatizo ni Ma DC wanaotokea UVCCM.
Nimetazama hii video kidogo tu nikashindwa kuendelea...jamani tuelezane ukweli, hii tabia ya kishenzi ya kuwadhalilisha wananchi imetoka wapi?

Najua hawa vijana wanaoteuliwa wanatokea huko huko UVCCM, je ni huko ndiko wanalelewa na kuwa kama wanyama wa porini kwa jinsi walivyokosa malezi bora, duh!

Halafu kwa ujeuri hajali anachukuliwa kwenye video! Ni kama vile anajua hiyo video itamuongezea CV akaweza kupanda zaidi labda na kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa!



Asante Mungu kwa kutuepusha japo kwa muda na hili wimbi la ukatili na mateso lililotuandama kwa miaka mitano!

Unamkuta polisi na nyota zake eti anatii maagizo ya vijana wakora kama hawa na kuwaumiza wananchi hadi ndugu zake wa kuzaliwa!

Unamkuta hakimu kwa maagizo kutoka juu na bila kujali miiko yake ya kazi anatoa hukumu kwa kesi si za hovyo tu bali na za kubambikiza!

Na hivyo hivyo katika taasisi zote za serikali ambako ungetegemea kupata ulinzi, haki na usalama kama mwananchi...hakika tulifikia pabaya!
 
Back
Top Bottom