Mkuu wa wilaya Kigamboni asema wanajeshi wanapiga na kuua wananchi

Mkuu wa wilaya Kigamboni asema wanajeshi wanapiga na kuua wananchi

Jeshi la tanzania ndo jeshi linaloongoza kwa ushamba kuliko majeshi yote duniani.
Vita ya leo na kesho ni shule kubwa drone,sophisticated weapons ambazo zinahitaji shule si kuvunja matofali.

Tumekuwa tukiongeza idadi kubwa ya wapiganaji badala ya kuwekeza kwenye science & technology.

Makambi yanaongezwa pasipo kuangalia mahitaji halisi ya sasa na wakati ujao.

Tumeongeza idadi kubwa ya Generals ambao wengi wapo kisiasa zaidi.Hatuhitaji wapiganaji wengi na wapiganishaji wengi.
 
Mkuu wa wilaya yupo sahihi,kama amejiridhisha kwa hizo tuhuma kwanini asiseme! Juzijuzi kule Vunjo kuna raia aliuawa na askari wa Tanapa na maiti yake kukutwa huko msituni lakini kuna kiongozi mmoja alitoa taarifa kwamba marehemu alijinyonga lakini uchunguzi wa daktari ulibaini mwili ulikuwa na majeraha ya risasi.
Je mlitaka huyo DC wa Kigamboni naye aseme wananchi wamejipiga na kujiua wenyewe?
 
Mkuu wa Wilaya ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama katika eneo lake la Utawala,hivyo majeshi yote yaliyopo ndani ya mipaka yake ya Utawala yapo chini yake.Hakupaswa kulalamika mbele ya Rc bali alitakiwa kuwachukulia hatua kama ni kweli au angepeleka taarifa hizo kwa Rc ofisini na si public.
Hujui ulichoandika. Hakuna kongozi yeyote wa utawala wa kiraia mwenye mamlaka ndani ya jeshi na ndio maana umeona mkuu wa mkoa amesema ataonana na mkuu wa majeshi.
 
Ni muda sasa askari wa jeshi wapewe elimu kuwa mtu wa kwanza kumheshimu kabla ya yeyote ni Raia na ndio maana jeshi likaitwa Jeshi la Wanainchi wa TanZanai (JWTZ).

Sasa kikatiba ni uhaini kwa askari wa jeshi kushambulia raia kwasababu yoyote ile ya kawaida hata kama ni makosa sababu yeye yupo trained kulinda mipaka ya inchi na raia wake kwa mujibu wa sheria za kijeshi sio kwa mujibu wa hisia na akili zake.

Ndio maana mazingira ambayo kikundi cha jeshi kinapokutana na raia inatakiwa iwe kwa shughuli za kiulinzi, kusaidia maafa au ujenzi wa dharula wa kusaidia jamii kwenye shughuli za kijamii kama ujenzi wa barabara na miundombinu na sio kunyanyasa raia, kuwatisha, kuhatarisha usalama wao au kuharibu mali zao.
 
Ni muda sasa askari wa jeshi wapewe elimu kuwa mtu wa kwanza kumheshimu kabla ya yeyote ni Raia na ndio maana jeshi likaitwa Jeshi la Wanainchi wa TanZanai (JWTZ).

Sasa kikatiba ni uhaini kwa askari wa jeshi kushambulia raia kwasababu yoyote ile ya kawaida hata kama ni makosa sababu yeye yupo trained kulinda mipaka ya inchi na raia wake kwa mujibu wa sheria za kijeshi sio kwa mujibu wa hisia na akili zake.

Ndio maana mazingira ambayo kikundi cha jeshi kinapokutana na raia inatakiwa iwe kwa shughuli za kiulinzi, kusaidia maafa au ujenzi wa dharula wa kusaidia jamii kwenye shughuli za kijamii kama ujenzi wa barabara na miundombinu na sio kunyanyasa raia, kuwatisha, kuhatarisha usalama wao au kuharibu mali zao.
Wakivaa zile gwanda wanaona wamemaliza dunia
 
Kwa kweli baadhi ya wanajeshi wana ubabe wa kishamba sana. Juzi wametaka kutuua pale mbezi beach, tangi bovu.
Lori la jeshi lilikuwa likipita service road kwa spidi kubwa sambamba na daladala niliyopanda.
Lilipofika ukingoni mwa service road dereva wa jeshi aliingiza lori wangu-wangu main road, bila kujali hata usalama wa askari jeshi aliowapakia nyuma.
Ilibidi dreva wa daladala ashike break ya nguvu sana mpaka gari likazimika, abiria wameangukiana hovyo.
Jamaa wakatuangalia kwa jicho la "mngetugusa muone" na hawakusimama wala kuonesha kujali, bila kufikiri kwamba ajali ingetokea isingebagua.
Kila abiria aliyetaka kutukana akabaki anamung'unya maneno kooni baada ya kuona jamaa wa mabakabaka ndiyo waliotaka kutusabishia ajali. Nilisikitika sana.
Ninaye mwanangu wa damu kabisa yaani tangu ametoka huko ubabe na ukali ukali,,namuonya sana awe humble kuna wananchi wamevurugwa asije akakipata.
 
Mkuu wa Wilaya ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama katika eneo lake la Utawala,hivyo majeshi yote yaliyopo ndani ya mipaka yake ya Utawala yapo chini yake.Hakupaswa kulalamika mbele ya Rc bali alitakiwa kuwachukulia hatua kama ni kweli au angepeleka taarifa hizo kwa Rc ofisini na si public.
Angalia jina la.mwishoooo mkuu utagundua shida sioyake
 
Ninaye mwanangu wa damu kabisa yaani tangu ametoka huko ubabe na ukali ukali,,namuonya sana awe humble kuna wananchi wamevurugwa asije akakipata.
Hawa wa vyeo vya chini ndio wenye shida. Wengi wao wanaingia wakitoka depo akili zinawatuma kuja kulipa visasi vya unyonge na ufakara wao. Matokeo yake ni kunyanyasa wananchi hata katika issue ndogo zinazohitaji kumwelewesha mtu.
 
Kitendo Cha yeye kuwa kada Kisha mbunge halafu kaja kwenye ukuu wa wilaya kashindwa kutafsiri nguvu ya mamlaka aliyo nayo
kaongea kama mbunge zaidi
anyway wafanyie kazi Hilo swala
 
Mkuu wa wilaya yupo sahihi,kama amejiridhisha kwa hizo tuhuma kwanini asiseme! Juzijuzi kule Vunjo kuna raia aliuawa na askari wa Tanapa na maiti yake kukutwa huko msituni lakini kuna kiongozi mmoja alitoa taarifa kwamba marehemu alijinyonga lakini uchunguzi wa daktari ulibaini mwili ulikuwa na majeraha ya risasi.
Je mlitaka huyo DC wa Kigamboni naye aseme wananchi wamejipiga na kujiua wenyewe?
Shida sio kutoa taarifa, shida ni kutofata utaratibu wa kutoa taarifa. Hizo ni tuhuma ambazo zinaweza mrudi na kumuweka pabaya. Taarifa yake yenyewe sio kwamba kashuhudia, ni ameambiwa na wananchi kama malalamiko.

Mahakama pekee ndio ina haki ya kuthibitisha na kutoa hukumu. Otherwise ni tuhuma ambazo zunaweza kuwa kweli au uongo.
 
Back
Top Bottom