Mkuu wa wilaya Kigamboni asema wanajeshi wanapiga na kuua wananchi

Mkuu wa wilaya Kigamboni asema wanajeshi wanapiga na kuua wananchi

Kwa kweli baadhi ya wanajeshi wana ubabe wa kishamba sana. Juzi wametaka kutuua pale mbezi beach, tangi bovu.
Lori la jeshi lilikuwa likipita service road kwa spidi kubwa sambamba na daladala niliyopanda.
Lilipofika ukingoni mwa service road dereva wa jeshi aliingiza lori wangu-wangu main road, bila kujali hata usalama wa askari jeshi aliowapakia nyuma.
Ilibidi dreva wa daladala ashike break ya nguvu sana mpaka gari likazimika, abiria wameangukiana hovyo.
Jamaa wakatuangalia kwa jicho la "mngetugusa muone" na hawakusimama wala kuonesha kujali, bila kufikiri kwamba ajali ingetokea isingebagua.
Kila abiria aliyetaka kutukana akabaki anamung'unya maneno kooni baada ya kuona jamaa wa mabakabaka ndiyo waliotaka kutusabishia ajali. Nilisikitika sana.
Brake✔
Break❌
 
Wanajeshi wanatakiwa wajue kuwa kazi tuliyowatuma ni kutulinda dhidi ya Maadui wa kutoka nje sio kutugeukia sisi wenyewe ambao ndio walipaji mishahara yao.
 
Tatizo tuna Jeshi kubwa wakati hakuna hata dalili za vita.
You're completely Wrong in this idea.

Tatizo lipo ktk Jeshi lenyewe, hususani kwenye suala la Mitaala yao ya Mafunzo, Nidhamu, na mifumo yao yote ya Utawala sambamba na ubovu wa Sheria za nchi zilizopo ukianzia na Katiba ya nchi hii.
 
Tatizo tuna Jeshi kubwa wakati hakuna hata dalili za vita.
Hivi huwa hawawapeleki kwenye mission? Ujue wasoja wa Bongo wapo wapo tu yaani, wengine wanauza na kupangisha fremu na maduka
 
Ameyasema hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa Mh Chalamila alipofanya ziara wilayani hapo. Mheshimiwa Chalamila ameahidi kukutana na Mkuu wa Majeshi.

Hii imekaaje wadau maana naona kiongozi wa Serikali anaituhumu Serikali yake mbele ya wananchi . Nadhani angefanya vile Mbunge au Diwani ndio ingekuwa sahii, lakini kwa mkuu wa wilaya asingetakiwa kusubiria ziara ya mkuu wa Mkoa .

Anyway huyo Mhe ni Mtoto wa Mzee Bulembo.

Tuhuma za kuua wananchi ni kubwa sana na ni vema kama ni kweli basi hatua zichukuliwe
Ndio shida ya, hv vyeo vya kuteuliwa, MTU hana elimu hata ya kuwa mama, ntilie, kisa, baba ni kada wa CCM, anateuliwa kuwa DC!
Na, yeye analalamika! Mwenyekiti wa, kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya! Ambayo Ina officer wa, jeshi kama liaison officer na jeshi!
Hili swala angeweza kulitatua, vzr tu kwa kufata taratibu ndogo,
M jeshi kapiga raia,mtafute raia andikisha maelezo polisi, mfate huyo mjeda,atiwe mitama kidogo baaasi!
 
Ki Katiba na Utendaji Jeshi letu liko karibu sana na WANANCHI ndio maana likaitwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania

Watuhumiwa wasakwe wavuliwe Magwanda tukutane MAHAKAMANI!!!!
 
Ameyasema hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa Mh Chalamila alipofanya ziara wilayani hapo. Mheshimiwa Chalamila ameahidi kukutana na Mkuu wa Majeshi.

Hii imekaaje wadau maana naona kiongozi wa Serikali anaituhumu Serikali yake mbele ya wananchi . Nadhani angefanya vile Mbunge au Diwani ndio ingekuwa sahii, lakini kwa mkuu wa wilaya asingetakiwa kusubiria ziara ya mkuu
Wanajeshi kuua Wananchi siyo jukumu lao wao waende wakatulindie mipaka huko.
 
Ameyasema hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa Mh Chalamila alipofanya ziara wilayani hapo. Mheshimiwa Chalamila ameahidi kukutana na Mkuu wa Majeshi.

Hii imekaaje wadau maana naona kiongozi wa Serikali anaituhumu Serikali yake mbele ya wananchi . Nadhani angefanya vile Mbunge au Diwani ndio ingekuwa sahii, lakini kwa mkuu wa wilaya asingetakiwa kusubiria ziara ya mkuu wa Mkoa .

Anyway huyo Mhe ni Mtoto wa Mzee Bulembo.

Tuhuma za kuua wananchi ni kubwa sana na ni vema kama ni kweli basi hatua zichukuliwe
Huyu ni DC kwa sababu ni mtoto wa mzee Bulembo na ni muumini mwenzetu!! Nje ya vigezo hivyo huyo binti na mama yake mdogo ambaye ni DC wa Bagamoyo hawakustahili hata Utendaji wa Kata
 
You're completely Wrong in this idea.

Tatizo lipo ktk Jeshi lenyewe, hususani kwenye suala la Mitaala yao ya Mafunzo, Nidhamu, na mifumo yao yote ya Utawala sambamba na ubovu wa Sheria za nchi zilizopo ukianzia na Katiba ya nchi hii.
Mie naona KATIBA NDIO INAMAPUNGUFU MENGI SANA
 
Tatizo tuna Jeshi kubwa wakati hakuna hata dalili za vita.
Hili tatizo ni la siku zote. Halijaanza leo. Na serikali haitaki kulimaliza kwani wanataka wananchi waogope wanajeshi ili hata wakiibiwa kura waogope kupigania haki yao. BTW mna uhakika huyo mkuu wa wilaya hanyemelei hilo jimbo kiubunge? Unachaguzi unapokaribia kila mwanasiasa anajifanya yuko upande wa wananchi.
 
Back
Top Bottom