Mliambiwa lakini hamkusikia, sasa ni muda wa mavuno ya awali ya kile tulichopanda

Mliambiwa lakini hamkusikia, sasa ni muda wa mavuno ya awali ya kile tulichopanda

Kwema wakuu!

Hizi habari za kuchapiwa, kuchapiana Wake na Wachumba hizi ni Mvua tuu za rasharasha. Tunasema haya ni mavuno ya awali, bado mambo hayajachanganya. Mambo yakichanganya hapa Dunia itakuwa na tafrani.

1. Mliambiwa Mwanamke anatakiwa Aolewe akiwa Bikra, mkasema bikra haimfanyi Mwanamke kuwa mwaminifu. Mkajiona mnaakili kuwashinda Mababu zenu.
Sawasawa, huu ndio muda wa kuvuna mlichopanda.

2. Mliambiwa na Mababu zenu kuwa Mwanamke hapaswi kumiliki uchumi, kupewa nafasi za utawala.
Ninyi mkajiona mnaakili kuwashinda wazee wenu. Hizi ni Mvua za rasharasha tuu. Nafikiri kizazi kinachofuata ndio mavuno yatachanganya.

3. Mliambiwa na Wazee wenu kuwa Hakuna urafiki baina ya mwanaume na Mwanamke. Mkawaona wazee wenu ni hamnazo.
Ati MTU anaruhusu Mkewe ataniwe taniwe hovyo, simu ya Mkeo imejaa chatting akichat na wanaume, Kwa kisingizio ni marafiki zake, sijui wafanyakazi wenzake, sijui classmates gani Huko.
Mtavuna mlichokipanda.
Eleweni kuwa NI ngumu Sana Mwanamke kuchapwa ndani ya siku moja bila mazoea.

4. Mliambiwa mkapuuza, msioe Wanawake wenye watoto, hasa Kwa kijana ambaye ni mdogo. Mkajifanya mnayajua mapenzi kuliko waliowazaa.
Sasa yakiwakuteni mnaanza kupiga mayowe.
Vijana lazima mjue kuwa kuna tofauti ya mapenzi na Ndoa. Mapenzi ni hisia lakini ndoa au familia ni taasisi inayoongozwa Kwa sheria na kanuni. Wakati mapenzi hayana Kanuni wala sheria.
Sio kosa kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na single mother, Ila ni kosa la kimkakati kuingia ndoani na Single mother.

Na hapa nazungumzia Kwa vijana wadogo wenye umri Chini ya miaka 40. Wazee mnaweza kuoa Mwanamke yeyote.

5. Mliambiwa msioe makabila tofauti. Mkajifanya mnaakili kuliko Babu zenu. ATI Kwa kudanganywa na maneno ya kisiasa. Ni kweli Sisi ni taifa moja lakini Sisi ni makabila tofauti yanayounda taifa moja.
Utofauti wa kimakuzi, desturi na Mila huchangia pakubwa kuvurugana ndani ya Familia.
Lakini hamtaki, kisa mnajifanya mmesoma, sijui mnashahada za uzamivu🤣🤣🤣 sasa mtavuna maumivu.

6. Mliambiwa Msiwe na huruma Sana na Wanawake na msiwaamini. Lakini Kwa ulofa wenu mmejichanganya.
Ni kweli wanasura za huruma, ni kweli wanatoaga machozi, ni kweli wanauwezo wa kuigiza ili waonewe huruma lakini kamwe usijichanganye.

Tumieni Akili, tumieni busara na hekima lakini msiongozwe na Huruma za kitoto na mihemko.
Oooh! Nimechepuka mara moja, nisamehe, ni Shetani, hakika Mimi ni Mwanadamu, huku anapiga magoti na kujiuliza. Upuuzi tuu! Sisi kama waafrika hakunaga kitu kinaitwa Msamaha Kwa kesi kama hizo.
Oooh! Huyu mtoto sio wako, Hana kosa lolote. Penda boga na Ua lake. Come on! Mmelogwa

Ooh! Taikon unachuki na Wanawake, hapana sina chuki. Hayo ni matunzo kila mwanaume lazima ayajue.
Vinginevyo vilio havikomi.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Chifu hapo namba 5,nakupinga mpaka naingia kabulini
 
Mkuu ulishamkosea mapema sana huyo mwanamke .Hawez thubutu nambia hivyo.Yan huyo nikirudi safarin tu (kama ningekua ndio wewe) huyo nafukuza nyumbani.

Huyo mwanamke ana nguvu kubwa sana ya kukufanya hata ukajiue na hiyo yote umempa wewe power over you.

Umenisikitisha na kunikera kwa wakati mmoja
Mkuu Ni stori ndefu sana
 
5. Mliambiwa msioe makabila tofauti. Mkajifanya mnaakili kuliko Babu zenu. ATI Kwa kudanganywa na maneno ya kisiasa. Ni kweli Sisi ni taifa moja lakini Sisi ni makabila tofauti yanayounda taifa moja.
Utofauti wa kimakuzi, desturi na Mila huchangia pakubwa kuvurugana ndani ya Familia.
Hii huwa nawaambia hujiulizi why ubunge unarudi kuomba kuchaguliwa ulipozaliwa
 
Pole sana aisee..Simuamini mwanamke mimi maisha yangu yote hii 13 tuko pamoja..japo sijawah kumkuta na mazonge ila hawa hawachelewi unaweza kuta analianzisha uzeeni unabaki unasha gaa..hawa viumbe hawa!!!!!
Mimi pia ni mwanachama wa kutokuwaamini wanawake hata 1% yalishanikuta makubwa.
 
Mzee hio stage nishaivuka kitambo saaana nipo stage nyingine kabisa ya uelewa, wewe endelea kugongewa
Zikabili changamoto zako binafsi mzee ,usiweke majumuisho ukataka kuona kana kwamba uliyokutana nayo wewe yanafanana na kwa wengine, kila mtu ana path yake ishi mzee acha uoga maisha ni ya kufurahia sio kuujaza moyo sumu na kuwajaza wengine sumu ya kuwa ndoa ni eneo la uwanja wa vita eneo hatarishi eneo lilojaa damu za vita eneo lisilo na amani mentality yako isiwe General,kila mmoja wetu ana case tofauti so usiwe na ubutu zaidi kuliko makali , sisi tunamakili ndiyo maana changamoto zako haziwezi fanana na zetu kamwe juu ya ndoa ukapandikiza mabaya tu,

mbona hata siku moja hamuongelei mazuri ya ndoa kizazi cha ajabu sana hichi kizazi lege lege
 
Back
Top Bottom