Mlikutana wapi wewe na mke/mume au mpenzi wako?

Mlikutana wapi wewe na mke/mume au mpenzi wako?

Chuo alinielewa mwenyewe akatafuta namba yangu kwa washkaji flani ambao alikua anaona tupo Karibu wanasoma kozi moja!
Nikakuta ghafla napigiwa simu mi flani tumesoma wote o'level na alikua ameshatafuta information zangu zote nkakwambia simkumbuki kumbe ilikua gia ya kuchek ntampokeaje!
Baada ya kumwambia simkumbuki nkawa namuomba anikumbushe akaniambia kama nimemsahau basi akakata simu......

Badae akanitumia text km mi ni fulani akanielekeza alivyo na mara nyingi huwa ananiona wapi na tumeshawahi gongana macho sehemu gani!
Story ni ndefu........

Sijui hata nilimkosea nini mpaka leo sijui yuko wapi ila nadhan anafamilia yake
Mkuu story tamu fanya kuimalizia
 
Wewe na mpenzi wako katika kuanzisha mahusiano yenu ya kimapenzi.

Je, at the first day mlimeet mahala gani?
sie tumekulia mtaa mmoja so tumecheza kombolela pa1, tumepka ugali mchangan pamoja, michezo ya baba na mama shule ya primary na secondary i-iv pamoja

ni miaka 10 sasa hakka sijawah kuijutia ndoa yetu
 
She is my neighbor "a little far from home"
Nilimfundisha hesabu alipo kua form 2 hapo mimi nimemaliza form 4.
Kamaliza form 6 tukaanza ku date rasmi till now.

Mama Zetu ni marafiki sana toka kitambo
Nakumbuka siku moja Mama aliwahi nitamkia "ingekua ni zile Zama zetu za kuchaguliwa mke ningependa uje uoe kwa flani 'kwao uyo binti', ila mwanangu najua wakati bado ila Muangalie binti wa kwa flani napendezwa nae hata ukianza nae urafiki sio mbaya miaka minne mi tano sio mbali " .
Kimoyoni nikajisemea mother ungejua.
Ila sasa nahis Mama anafaham japo hana uwakika.

Kati ya wanaume wenye binti mrembo basi nami ni mmoja wapo, she is beautiful very beautiful she is smart too.
Mungu mlinde mrembo wangu.
umemsifia xn aisee,

ntumie no ake nmpe hongera ake
 
Nilienda kwao kupeleka mzigo flani ile nagonga yeye ndo akaja kufungua tuliooangaliana wote tukawa kama tumepigwa ganzi Mimi mdomo ukawa mzito nikaishia kuuliza mama yupo? Nikaungia ndani kukabidhi ule mzigo nilipokua natoka tukaaonana tena akanipa bonge la smile kilichofuata hapo ni historia
 
Nikikutana nae ntakuja kuleta story hapa...
 
Tulikutana kwenye ndege tulikua tunaenda kwa malkia, mimi ndio ilikua mara yangu ya kwanza kupanda ndege na kusafiri nje ya nchi.. so ule ushamba na hofu ya ndege + vishuzi vya kimya kimya alinigundua maana tulikaa siti moja, basi akaanza kunisemesha kunitoa hofu na akanipa ushirikiano mkubwa sana ili nipoteze mawazo na hofu kufikiria mambo ya kipuuzi ndani ya ndege. basi tulikutana hapo tukapeana namba tukaanza kuwasiliana baada ya muda mimi niliwahi kurudi bongo, then nae akarudi bila kupoteza muda tukaanzisha mahusiano.
 
Noma sana, tulikutana viwanja vya Soweto A city mtoto wa mashavuni naona alielewa slang za mselaa wa kidevuni. Nikapiga masauti mtoto akajaa mwaka wa 4 huu tupo kwa fasi ni toto kali laana
 
Mpenzi wangu tulikutana 1931 nijijini wakati naenda kupeleka ngombe malisho ndiyo ikawa first time, amekuwa mchumba tumeenda hadi leo n mke wangu, ambae leo n bibi yenu
 
Nilipewa namba na dogo baada ya kumuoa dem ni makali na akili ipo. Then nikampigia tukaonana na mahusiano yetu yalianzia hapo mpaka leo ndo wife.
 
Back
Top Bottom