Mlinzi wa Rais kuvaa sare za chama ni sahihi?

Mlinzi wa Rais kuvaa sare za chama ni sahihi?

Katiba inakataza watumishi wa umma kujihusisha na shughuli za vyama vya siasa, hasa majeshi kwa namna yoyote ile. Kuvaa sare ya chama cha siasa ni dhahiri kuwa una mahaba na chama husika.

Liko wazi kuwa katiba yetu ina mapungufu juu ya Urais mara bunge linapovunjwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu, kwani Rais anaendelea mpaka mwingine atakapoapishwa.

Kama kifungu ndio kinafuatwa, kwa nini hao walinzi wa Rais wavae ki-CCM wakati wana sare zao rasmi? Hivi na walinzi wa wagombea wengine nao wanavaa sare za vyama vile? Nimeuliza hivi kwani hawa wa Rais sura zao na maumbile yao ya muonekano wa mwili kwa nje yanafahamika.

Safari hii mishale itakuwa ya kutosha, mpaka kila kitu kwenu kinakuwa uvunjifu wa katiba.
 
Magufuli ana walinzi wa Serikali, kama Rais aliyeko madarakani, pia ana walinzi wa chama kiongozi mkuu. Nawe umeonyesha Lissu ana walinzi.

Mleta mada tafuta hoja nyingine ya kumwondoa Magufuli kwenye kampeni baada ya pingamizi la Lissu kutupiliwa mbali.
Atajiondoa kwa hoja zake tu Dr Alexander
 
Katiba inakataza watumishi wa umma kujihusisha na shughuli za vyama vya siasa, hasa majeshi kwa namna yoyote ile. Kuvaa sare ya chama cha siasa ni dhahiri kuwa una mahaba na chama husika.

Liko wazi kuwa katiba yetu ina mapungufu juu ya Urais mara bunge linapovunjwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu, kwani Rais anaendelea mpaka mwingine atakapoapishwa.

Kama kifungu ndio kinafuatwa, kwa nini hao walinzi wa Rais wavae ki-CCM wakati wana sare zao rasmi? Hivi na walinzi wa wagombea wengine nao wanavaa sare za vyama vile? Nimeuliza hivi kwani hawa wa Rais sura zao na maumbile yao ya muonekano wa mwili kwa nje yanafahamika.

Hata wewe ni usalama wa taifa..... Muhimu ni uzalendo mavazi kitu gani bwashee!
 
Unachokiona wewe ni tofauti na yeye anachokikusudia
Yeye anakusudia nini?!

Hapo itakuwa sawa endapo tu hao jamaa sio TISS bali ni walinzi wa kawaida walio kwenye payroll ya CCM!

Lakini kwavile JPM bado ni rais, hata anapofanya shughuli za chama bado urais wake upo pale pale na kwahiyo bado Walinzi wa Rais ambao ni mali ya serikali wataendelea kutekeleza wajibu wao.

Hata hivyo, hawatakuwa wanatekeleza wajibu wako kwa Mwenyekiti wa chama bali kwa rais, na wao watakuwa hapo kwa niaba ya serikali na sio kwa niaba ya chama hadi wafikie kuvaa sare za chama!!
 
Kama kifungu ndio kinafuatwa, kwa nini hao walinzi wa Rais wavae ki-CCM wakati wana sare zao rasmi?
Kabla sijakujibu kwa nini wanavaa hivyo hebu nijibu maswali haya
  1. Sare rasmi ya usalama wa taifa (TISS) ni ipi?
  2. Nani kakuambia kuwa kila mlinzi wa rais ni usalama wa taifa (TISS)
  3. Ni sheria ipi inayowazuia usalama wa taifa (TISS) kuvaa nguo za vyama?
 
Katiba na Sheria za Tanzania hairuhusu Mtumishi wa umma kuwa mwanachama wa chama cha siasa
Watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama ndio hawaruhusiwi.Watumishi wengine wanaruhusiwa isipokuwa hawatakiwi kufanya siasa katika maeneo ya kazi.
 
Wenzako wako ki professional, wewe unatema pumba. Hivi Rais angekuwa wa Chadema, na hao walinzi wakavaa jezi ya Chadema ungelalamika?
Zama za chama kushika hatamu zimepita., mlinzi wake ni mtumishi wa umma just keep it on your mind
 
Back
Top Bottom