Mliofanikiwa kutoa Zaka asilimia 10% ya vipato vyenu mmewezaje? Binafsi naishia kusaidia 2% hadi 4%

Mliofanikiwa kutoa Zaka asilimia 10% ya vipato vyenu mmewezaje? Binafsi naishia kusaidia 2% hadi 4%

Sadaka zenyewe ndiyo hizi wanatumia kuwahonga Dada zetu 😢

Kuna Kanisa niliacha kusali hapo DSM baada ya kuambiwa niwapelekee Salary Slip yangu ili wa impose Fungu la Kumi.

Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, Sadaka iliyobora ni ya kusaidia Yatima, Wajane na watu wasiojiweza. Saivi Sadaka yangu imeegemea upande huo
 
Nani mwaminifu wa kupokea zaka, kwa matumizi gani au inakuwa kama unaitupa tu bora nia yako ni kutoa zaka?
Kama sio mwaminifu kwann uabudu kwnye Hilo kanisa? Mkuu hili swala hutaezalielewa Kama huongozwi na Roho mtakatifu kulijua neno la MUNGU... Ayub 22:21 insema mjue Sana MUNGU ili uwe na amani,,, hivyo mkuu nakushauri mjue kwanza MUNGU kupitia neno lake takatifu.
 
Ss hivi makanisa yamekomaa na zaka,usipotoa zako wanakutenga [emoji23][emoji23] potelea mbali acha wafanye wanachoona kwao ni sahihi,ila haya makanisa yamekua ni biashara sio rc wala lutheran
 
Sadaka zenyewe ndiyo hizi wanatumia kuwahonga Dada zetu 😢

Kuna Kanisa niliacha kusali hapo DSM baada ya kuambiwa niwapelekee Salary Slip yangu ili wa impose Fungu la Kumi.

Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, Sadaka iliyobora ni ya kusaidia Yatima, Wajane na watu wasiojiweza.
Usipindishe maandiko ndugu,,, kasome Malaki 3:8-11..... Pia sadaka humfaidishi Padri au Mchungaji Bali unajenga mahusiano yako na MUNGU ilo kanisa uliloona Ni kwamba wanalitaja tu jina la MUNGU Ila hawamwabudu kisawasawa!!!
 
Sadaka zenyewe ndiyo hizi wanatumia kuwahonga Dada zetu 😢

Kuna Kanisa niliacha kusali hapo DSM baada ya kuambiwa niwapelekee Salary Slip yangu ili wa impose Fungu la Kumi.

Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, Sadaka iliyobora ni ya kusaidia Yatima, Wajane na watu wasiojiweza. Saivi Sadaka yangu imeegemea upande huo
Duuuh
 
Kwangu mimi kwa lgha nyepesi Zaka ni kutoa 10% ya ulichopata kwa jasho lako kihalali kiende kubeba wenye shida, binafsi naiona ni kama kodi fair kabisa ya kuweza kuishi na kupata rizki kwenye dunia hii ambayo ina mwenye nae alieiumba.

Nadhani huwa inahesabiwa zaidi unapomsaidia mtu mwenye shida na hawana ukaribu na wewe ama mnajuana kwa mbali, wale mnaojuana karibu huwa ni msaada na si zaka.

Ni adaka pekee huwa natoa kanisani lakini kuhusu Zaka huwa najaribu kuitoa kwa watu wenye shida naokutana nao ila hadi sasa sijawai toa 10%>

Binafsi nineshindwa kuweza kufikia hio asilimia 10, huwa bili zinanizonga najikuta bili zangu inabidi ziwe na kipaumbele kuliko hii zaka ambayo naichukulia kama kodi ya Sir God alienipa uhai moaka sasa.

Tangu naanza kupata elf 30 kwa mwezi hadi sasa nikiwa naweza kupata milioni 2 hadi 3 kila mwezi nikiri wazi nilikuwa nahitahidi kutoa fungu la kumi ila sijaweza mpaka sasa.

Mfano kwa mwezi uliopita nilipata kama milioni 2 na laki 3 hibi hivi ila nikajikuta naishia kutoa zaka kama elf 80 hivi, Mtindo wangu wa kutoa zaka Huwa nagawa gawa hizi buku buku na elf 2 kwa watoto wa mtaani, nikikuta mtu anauza miwa na karanga kwenye ungo nampa elf 2 nasema ntapitia baadae ila sirudi, n.k.

Yani kiufupi nakuta matumizi yananibana sana na naanza kujidanganya yana umuhimu sana kuzidi zaka, mlioweza kufikisha hio 10% ya kipato kile halali naombeni ujuzi.
Umejitahidi hata hizo.
 
Kwangu mimi kwa lgha nyepesi Zaka ni kutoa 10% ya ulichopata kwa jasho lako kihalali kiende kubeba wenye shida, binafsi naiona ni kama kodi fair kabisa ya kuweza kuishi na kupata rizki kwenye dunia hii ambayo ina mwenye nae alieiumba.

Nadhani huwa inahesabiwa zaidi unapomsaidia mtu mwenye shida na hawana ukaribu na wewe ama mnajuana kwa mbali, wale mnaojuana karibu huwa ni msaada na si zaka.

Ni adaka pekee huwa natoa kanisani lakini kuhusu Zaka huwa najaribu kuitoa kwa watu wenye shida naokutana nao ila hadi sasa sijawai toa 10%>

Binafsi nineshindwa kuweza kufikia hio asilimia 10, huwa bili zinanizonga najikuta bili zangu inabidi ziwe na kipaumbele kuliko hii zaka ambayo naichukulia kama kodi ya Sir God alienipa uhai moaka sasa.

Tangu naanza kupata elf 30 kwa mwezi hadi sasa nikiwa naweza kupata milioni 2 hadi 3 kila mwezi nikiri wazi nilikuwa nahitahidi kutoa fungu la kumi ila sijaweza mpaka sasa.

Mfano kwa mwezi uliopita nilipata kama milioni 2 na laki 3 hibi hivi ila nikajikuta naishia kutoa zaka kama elf 80 hivi, Mtindo wangu wa kutoa zaka Huwa nagawa gawa hizi buku buku na elf 2 kwa watoto wa mtaani, nikikuta mtu anauza miwa na karanga kwenye ungo nampa elf 2 nasema ntapitia baadae ila sirudi, n.k.

Yani kiufupi nakuta matumizi yananibana sana na naanza kujidanganya yana umuhimu sana kuzidi zaka, mlioweza kufikisha hio 10% ya kipato kile halali naombeni ujuzi.
Sijui wewe ni wa imani ipi ila kama imani yako iko kwenye maandiko ya Biblia basi hicho unachota sio fungu la kumi.
Twende taratibu nitakuonesha fungu la kumi ni nini kisha utajua kwanini ninasema hicho unachotoa sio fungu la kumi.

Kwa mara ya kwanza fungu la kumi limeandikwa katika Biblia kwenye kitabu cha Mwanzo 14:20, ambapo Abraham akampatia Mfalme wa Salemu, ambaye alikuwa ni Kuhani wa Mungu aliye juu sana aliyeitwa Melkizedeki fungu la kumi la nyara zote alizozipata kutokana na ushindi katika vita alivyopigana.

Sasa turudi nyuma kidogo kabla ya Abraham kutoa fungu la kumi nini kilitokea mpaka Abrahamu akatoa fungu la kumi?

Abrahamu alikuwa na mpwa wake aliyeitwa Lutu aliyekaa Sodoma. Kulikuwa na vita baina ya falme (Sodoma, Gomora, Adma, Seboimu na Bela) famle tano zilishindana na falme nne (Elamu, Goimu, Shinari, Elasari) na hizi tano zikapigwa na ufalme wa Sodoma na Gomora mahali ambapo Lutu alikuwa anakaa wakachukuliwa mateka na kila kitu walicho nacho kikanyang’anywa soma Mwanzo 14:1-14

Abrahamu aliposikia kwamba Lutu nduguye ametekwa na mali zake zote zimechukuliwa akatoka ili kumkomboa ndugu yake akiwa na vijakazi wake akawafuata na kuwapiga na kumkomboa ndugu yake Lutu na alifanikiwa kurudisha vyote. Alipokuwa njiani kurudi nyumbani kwake akiwa na mateka wake na mali zao mfalme wa Salemu Melkizedeki akaleta mkate na divai kisha akasema Abraham na abarikiwe na Mungu aliye juu sana Muumba wa Mbingu na nchi, Ahidimiwe Mungu aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako (Mwanzo 14:19-20)

Kumbuka Abrahamu alienda kupigana na majeshi ya nchi nne yaliyo zishinda nchi tano na Abrahamu hakuwa na jeshi bali vijana mia tatu na kumi na nane waliozaliwa kwenye nyumba yake, kitendo cha Abrahamu kuwapiga majeshi ya nchi nne tena akiwa hana jeshi kilimfanya Mungu amtume Melkizedeki kumkumbusha Abrahamu kwamba si yeye Abrahamu amewapiga wale Wafalme bali Mungu aliemtangulia ndio amewapiga wale Wafalme. Kwasababu hiyo Abrahamu aliamua kumtolea Mungu fungu la kumi la mali yote aliyoipata kama ishara ya kutambua ukuu wa Mungu aliovyomshindia katika vita yake na kwasababu Mungu haonekani Abrahamu alimpa Melkizedeki hilo fungu la kumi sababu Melkizdedki alikuwa kuhani wa Mungu aliye juu sana.

Utaona kuwa Melkizedeki alimbariki Abrahamu kisha Abrahamu akampa fungu la kumi. Hivyo sehemu ya kwanza fungu la kumi linatolewa kwa mtumishi wa Mungu na mtumishi wa Mungu anatakiwa kutamka maneno ya baraka kwa mtoaji. Ongeza na andiko la msisitizo Hesabu 18:21-24 Mungu ameweka mkazo fungu la kumi ni urithi wa Walawi ambao ni watumishi wa Mungu.

Sehemu ya Pili ya kutoa fungu la kumi tunaipata Malaki 3: 8-12 Mungu ametutaka tutoe zaka kamili nyumbani mwake ambapo kimsingi ndipo watumishi wa Mungu wanapatikana.

Hivyo ni makossa kutoa fungu la kumi nje na hapo na pia ni makossa kutoa fungu la kumi pungufu. Hatari ya kutoa fungu la kumi pungufu tunaisoma katika Matendo ya Mitume 5:1-10 Anania na mkewe walikufa sababu walidanganya katika kutoa fungu la kumi.

Fungu la kumi sio Sadaka hivyo usitoe kama upendavyo ni amri na utekelezaji wake ni wa kisheria. Wala usichepushe kwa kuwapa wale unaoona wanafaa. Fungu la kumi linalipwa kwa;

1. Mtumishi wa Mungu na yeye anapaswa kumshukuru Mungu kwa ajili yako na kisha kukubariki.
mfano;
  • Baba yako wa Kiroho​
  • Mchungaji​
  • Askofu​
  • Nabii​
  • Mwalimu wa neo la Mungu​
  • Mwinjilisti​
  • Mtume​
  • Kuhani​
2. Kanisani ili itumike katika ujenzi wa ufalme wa Mungu

Sadaka hazina ahadi ya Mungu ila fungu la kumi lina ahadi ya Mungu juu ya kufanikiwa kwetu. Lipa zaka kamili na ukumbuke na dhabihu ili ufanikiwe katika Maisha yako. Mungu wa Bwana wangu Yesu Kristo akubariki sana.



 
Mkuu jitahidi sana kutohukumu .huyu mpendwa amejieleza ukweli na anayoyatamania .kumcha mungu ni jambo la kujiboresha kwa bidiii kila siku .kupeana moyo kuombeana mnafika hatua za juu.nilipwe mil 1 mwanangu ahitaji mil 1 ya operation ya moyo unataka nizoe laki 1 kwa yatima wale soda mwanangu afe??
Uko sahihi mkuu,kuna usemi usemao "Charity begins at home,but should not end there".Kwamba "Ukarimu huanzia nyumbani lakini usiishie hapo".
 
Sijui wewe ni wa imani ipi ila kama imani yako iko kwenye maandiko ya Biblia basi hicho unachota sio fungu la kumi.
Twende taratibu nitakuonesha fungu la kumi ni nini kisha utajua kwanini ninasema hicho unachotoa sio fungu la kumi.

Kwa mara ya kwanza fungu la kumi limeandikwa katika Biblia kwenye kitabu cha Mwanzo 14:20, ambapo Abraham akampatia Mfalme wa Salemu, ambaye alikuwa ni Kuhani wa Mungu aliye juu sana aliyeitwa Melkizedeki fungu la kumi la nyara zote alizozipata kutokana na ushindi katika vita alivyopigana.

Sasa turudi nyuma kidogo kabla ya Abraham kutoa fungu la kumi nini kilitokea mpaka Abrahamu akatoa fungu la kumi?

Abrahamu alikuwa na mpwa wake aliyeitwa Lutu aliyekaa Sodoma. Kulikuwa na vita baina ya falme (Sodoma, Gomora, Adma, Seboimu na Bela) famle tano zilishindana na falme nne (Elamu, Goimu, Shinari, Elasari) na hizi tano zikapigwa na ufalme wa Sodoma na Gomora mahali ambapo Lutu alikuwa anakaa wakachukuliwa mateka na kila kitu walicho nacho kikanyang’anywa soma Mwanzo 14:1-14

Abrahamu aliposikia kwamba Lutu nduguye ametekwa na mali zake zote zimechukuliwa akatoka ili kumkomboa ndugu yake akiwa na vijakazi wake akawafuata na kuwapiga na kumkomboa ndugu yake Lutu na alifanikiwa kurudisha vyote. Alipokuwa njiani kurudi nyumbani kwake akiwa na mateka wake na mali zao mfalme wa Salemu Melkizedeki akaleta mkate na divai kisha akasema Abraham na abarikiwe na Mungu aliye juu sana Muumba wa Mbingu na nchi, Ahidimiwe Mungu aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako (Mwanzo 14:19-20)

Kumbuka Abrahamu alienda kupigana na majeshi ya nchi nne yaliyo zishinda nchi tano na Abrahamu hakuwa na jeshi bali vijana mia tatu na kumi na nane waliozaliwa kwenye nyumba yake, kitendo cha Abrahamu kuwapiga majeshi ya nchi nne tena akiwa hana jeshi kilimfanya Mungu amtume Melkizedeki kumkumbusha Abrahamu kwamba si yeye Abrahamu amewapiga wale Wafalme bali Mungu aliemtangulia ndio amewapiga wale Wafalme. Kwasababu hiyo Abrahamu aliamua kumtolea Mungu fungu la kumi la mali yote aliyoipata kama ishara ya kutambua ukuu wa Mungu aliovyomshindia katika vita yake na kwasababu Mungu haonekani Abrahamu alimpa Melkizedeki hilo fungu la kumi sababu Melkizdedki alikuwa kuhani wa Mungu aliye juu sana.

Utaona kuwa Melkizedeki alimbariki Abrahamu kisha Abrahamu akampa fungu la kumi. Hivyo sehemu ya kwanza fungu la kumi linatolewa kwa mtumishi wa Mungu na mtumishi wa Mungu anatakiwa kutamka maneno ya baraka kwa mtoaji. Ongeza na andiko la msisitizo Hesabu 18:21-24 Mungu ameweka mkazo fungu la kumi ni urithi wa Walawi ambao ni watumishi wa Mungu.

Sehemu ya Pili ya kutoa fungu la kumi tunaipata Malaki 3: 8-12 Mungu ametutaka tutoe zaka kamili nyumbani mwake ambapo kimsingi ndipo watumishi wa Mungu wanapatikana.

Hivyo ni makossa kutoa fungu la kumi nje na hapo na pia ni makossa kutoa fungu la kumi pungufu. Hatari ya kutoa fungu la kumi pungufu tunaisoma katika Matendo ya Mitume 5:1-10 Anania na mkewe walikufa sababu walidanganya katika kutoa fungu la kumi.

Fungu la kumi sio Sadaka hivyo usitoe kama upendavyo ni amri na utekelezaji wake ni wa kisheria. Wala usichepushe kwa kuwapa wale unaoona wanafaa. Fungu la kumi linalipwa kwa;

1. Mtumishi wa Mungu na yeye anapaswa kumshukuru Mungu kwa ajili yako na kisha kukubariki.
mfano;
  • Baba yako wa Kiroho​
  • Mchungaji​
  • Askofu​
  • Nabii​
  • Mwalimu wa neo la Mungu​
  • Mwinjilisti​
  • Mtume​
  • Kuhani​
2. Kanisani ili itumike katika ujenzi wa ufalme wa Mungu

Sadaka hazina ahadi ya Mungu ila fungu la kumi lina ahadi ya Mungu juu ya kufanikiwa kwetu. Lipa zaka kamili na ukumbuke na dhabihu ili ufanikiwe katika Maisha yako. Mungu wa Bwana wangu Yesu Kristo akubariki sana.



Mkuu umedadavua vizuri sana..ila tuje sasa ktk agano jipya, ni wapi Yesu alifundisha kuhusu kutoa zaka??
 
Zaka ni ishara ya utii kwa Mungu, na Sadaka ni ishara ya upendo kwake.

“Mpende Bwana Mungu wako...”

Kutoa zaka na sadaka ni kutekeleza amri za Mungu.

Kama unaye Mungu.
 
Mkuu umedadavua vizuri sana..ila tuje sasa ktk agano jipya, ni wapi Yesu alifundisha kuhusu kutoa zaka??
Yesu aliishika kikamilifu tolati maisha yake yote na alisema alikuja kuikamilisha sio kuibatilisha ambapo hakugusa hata yy alipaishi
 
Kwangu mimi kwa lgha nyepesi Zaka ni kutoa 10% ya ulichopata kwa jasho lako kihalali kiende kubeba wenye shida, binafsi naiona ni kama kodi fair kabisa ya kuweza kuishi na kupata rizki kwenye dunia hii ambayo ina mwenye nae alieiumba.

Nadhani huwa inahesabiwa zaidi unapomsaidia mtu mwenye shida na hawana ukaribu na wewe ama mnajuana kwa mbali, wale mnaojuana karibu huwa ni msaada na si zaka.

Ni adaka pekee huwa natoa kanisani lakini kuhusu Zaka huwa najaribu kuitoa kwa watu wenye shida naokutana nao ila hadi sasa sijawai toa 10%>

Binafsi nineshindwa kuweza kufikia hio asilimia 10, huwa bili zinanizonga najikuta bili zangu inabidi ziwe na kipaumbele kuliko hii zaka ambayo naichukulia kama kodi ya Sir God alienipa uhai moaka sasa.

Tangu naanza kupata elf 30 kwa mwezi hadi sasa nikiwa naweza kupata milioni 2 hadi 3 kila mwezi nikiri wazi nilikuwa nahitahidi kutoa fungu la kumi ila sijaweza mpaka sasa.

Mfano kwa mwezi uliopita nilipata kama milioni 2 na laki 3 hibi hivi ila nikajikuta naishia kutoa zaka kama elf 80 hivi, Mtindo wangu wa kutoa zaka Huwa nagawa gawa hizi buku buku na elf 2 kwa watoto wa mtaani, nikikuta mtu anauza miwa na karanga kwenye ungo nampa elf 2 nasema ntapitia baadae ila sirudi, n.k.

Yani kiufupi nakuta matumizi yananibana sana na naanza kujidanganya yana umuhimu sana kuzidi zaka, mlioweza kufikisha hio 10% ya kipato kile halali naombeni ujuzi.
Toa hyo 10 % kwa watumishi ,
Toa shukrani za week kanisani
Toa ahadi na collecti
Toa zaka
Toa malimbuko
Toa sadaka za siri
Toa jengo na inakuwa na bahasha yake rasm
Toa sadak ya chakula cha bwana kama ipo



Kwa wale wa KKKT hzo sadaka siyo ngeni kwako

Kwa mwamposa

Ipo sadaka
Ipo ya shukktan
Ipo ya kijimaliza
Ipo kuinua huduma

Kwa kifupi hzo ndio sadka nakutana nazo na kama mfuko upo vzr nazitoa zoteee namtoleaa bwana MUNGU bila manunguniko
 
Back
Top Bottom