Mliofanikiwa kutoa Zaka asilimia 10% ya vipato vyenu mmewezaje? Binafsi naishia kusaidia 2% hadi 4%

Mliofanikiwa kutoa Zaka asilimia 10% ya vipato vyenu mmewezaje? Binafsi naishia kusaidia 2% hadi 4%

Ni utayari tu na kuamini kuwa ukitoa utapokea vingi.

Tena unatakiwa kutoa kwa moyo wa ukarimu [emoji4]

Hapo utaona mambo yako mengi yakifunguka na kuwa wazi.

Tena toa kwa Siri ujitangazie kwa mtu awaye yote.

Utakuja ushuhudie ukuu wa Mungu kwenye maisha yako.
 
Mkuu

Uko sahihi,coz hiyo ndio sheria pekee ninayohubiriwa katika ulimwengu wa agano jipya tulilonalo!

Yaani watumishi wameacha SHERIA zote za israel na kukomalia hilo Moja wakiisapoti na Malaki 3;3!

Wakati kuna sheria NYINGI tu ambazo wameziacha wakisema hayupo chini ya SHERIA!

Yesu

Alileta mbadala wa kila sheria

-Amri kumi za Mungu zilinebwa na upendo!yaani mpendane kama Amri mpya!

-Matoleo yalibebwa na kutoa KWA kadiri ulivobarikiwa bila kiwango chochote kama kristo alijitoa mwili wake wote iweje wewe ujitoe KWA asilimia!!?

Ndio maana mtu akiguswa na Roho hawezi toa KWA asilimia kama zakayo alivotoa!!

Pia asili na chimbuko la zaka HALIKUWA AGIZO LA MUNGU KWA WATU WAKE BALI ILIKUWA AHADI ;-

KWANZA KWA IBRAHIMU ALIYETOA NYARA KWA MELKIZEDEK KUHANI MKUU

BAADAE

YAKOBO WAKATI AKIENDA KWA LABAN ALIAHIDI KUTOA SEHEMU YA KUMI YA MALI ZAKE NA IKAFANYIKA SHERIA ILIYOWAKIZA WATOTO WAKE NDIO MANA MUNGU ANAIDAI AHADI ILE KATIKA MALAKI 3;3!

HAYA SHALOM WAKRISTO
 
Sijui wewe ni wa imani ipi ila kama imani yako iko kwenye maandiko ya Biblia basi hicho unachota sio fungu la kumi.
Twende taratibu nitakuonesha fungu la kumi ni nini kisha utajua kwanini ninasema hicho unachotoa sio fungu la kumi.

Kwa mara ya kwanza fungu la kumi limeandikwa katika Biblia kwenye kitabu cha Mwanzo 14:20, ambapo Abraham akampatia Mfalme wa Salemu, ambaye alikuwa ni Kuhani wa Mungu aliye juu sana aliyeitwa Melkizedeki fungu la kumi la nyara zote alizozipata kutokana na ushindi katika vita alivyopigana.

Sasa turudi nyuma kidogo kabla ya Abraham kutoa fungu la kumi nini kilitokea mpaka Abrahamu akatoa fungu la kumi?

Abrahamu alikuwa na mpwa wake aliyeitwa Lutu aliyekaa Sodoma. Kulikuwa na vita baina ya falme (Sodoma, Gomora, Adma, Seboimu na Bela) famle tano zilishindana na falme nne (Elamu, Goimu, Shinari, Elasari) na hizi tano zikapigwa na ufalme wa Sodoma na Gomora mahali ambapo Lutu alikuwa anakaa wakachukuliwa mateka na kila kitu walicho nacho kikanyang’anywa soma Mwanzo 14:1-14

Abrahamu aliposikia kwamba Lutu nduguye ametekwa na mali zake zote zimechukuliwa akatoka ili kumkomboa ndugu yake akiwa na vijakazi wake akawafuata na kuwapiga na kumkomboa ndugu yake Lutu na alifanikiwa kurudisha vyote. Alipokuwa njiani kurudi nyumbani kwake akiwa na mateka wake na mali zao mfalme wa Salemu Melkizedeki akaleta mkate na divai kisha akasema Abraham na abarikiwe na Mungu aliye juu sana Muumba wa Mbingu na nchi, Ahidimiwe Mungu aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako (Mwanzo 14:19-20)

Kumbuka Abrahamu alienda kupigana na majeshi ya nchi nne yaliyo zishinda nchi tano na Abrahamu hakuwa na jeshi bali vijana mia tatu na kumi na nane waliozaliwa kwenye nyumba yake, kitendo cha Abrahamu kuwapiga majeshi ya nchi nne tena akiwa hana jeshi kilimfanya Mungu amtume Melkizedeki kumkumbusha Abrahamu kwamba si yeye Abrahamu amewapiga wale Wafalme bali Mungu aliemtangulia ndio amewapiga wale Wafalme. Kwasababu hiyo Abrahamu aliamua kumtolea Mungu fungu la kumi la mali yote aliyoipata kama ishara ya kutambua ukuu wa Mungu aliovyomshindia katika vita yake na kwasababu Mungu haonekani Abrahamu alimpa Melkizedeki hilo fungu la kumi sababu Melkizdedki alikuwa kuhani wa Mungu aliye juu sana.

Utaona kuwa Melkizedeki alimbariki Abrahamu kisha Abrahamu akampa fungu la kumi. Hivyo sehemu ya kwanza fungu la kumi linatolewa kwa mtumishi wa Mungu na mtumishi wa Mungu anatakiwa kutamka maneno ya baraka kwa mtoaji. Ongeza na andiko la msisitizo Hesabu 18:21-24 Mungu ameweka mkazo fungu la kumi ni urithi wa Walawi ambao ni watumishi wa Mungu.

Sehemu ya Pili ya kutoa fungu la kumi tunaipata Malaki 3: 8-12 Mungu ametutaka tutoe zaka kamili nyumbani mwake ambapo kimsingi ndipo watumishi wa Mungu wanapatikana.

Hivyo ni makossa kutoa fungu la kumi nje na hapo na pia ni makossa kutoa fungu la kumi pungufu. Hatari ya kutoa fungu la kumi pungufu tunaisoma katika Matendo ya Mitume 5:1-10 Anania na mkewe walikufa sababu walidanganya katika kutoa fungu la kumi.

Fungu la kumi sio Sadaka hivyo usitoe kama upendavyo ni amri na utekelezaji wake ni wa kisheria. Wala usichepushe kwa kuwapa wale unaoona wanafaa. Fungu la kumi linalipwa kwa;

1. Mtumishi wa Mungu na yeye anapaswa kumshukuru Mungu kwa ajili yako na kisha kukubariki.
mfano;
  • Baba yako wa Kiroho​
  • Mchungaji​
  • Askofu​
  • Nabii​
  • Mwalimu wa neo la Mungu​
  • Mwinjilisti​
  • Mtume​
  • Kuhani​
2. Kanisani ili itumike katika ujenzi wa ufalme wa Mungu

Sadaka hazina ahadi ya Mungu ila fungu la kumi lina ahadi ya Mungu juu ya kufanikiwa kwetu. Lipa zaka kamili na ukumbuke na dhabihu ili ufanikiwe katika Maisha yako. Mungu wa Bwana wangu Yesu Kristo akubariki sana.



Mkuu safi sana kwa maelezo mazuri.
Najaribu kutafakari kwanini kwenye agano jipya hakuna mistari inayoeleza suala la zaka? Kama ipo naomba kueleweshwa.
 
Kila nikifikiria kiasi nachotenga kwenye starehe na matanuzi mengine najikuta tu nshachkua bahasha kuweka zaka asee..

Yani matanuzi unaweza kutoa yanazidi hata hiyo 10% ya kipato chako ila unaskia Uzito kutoa kwa Mungu...
Shetani yupo kazini siku zote
 
Kwangu mimi kwa lgha nyepesi Zaka ni kutoa 10% ya ulichopata kwa jasho lako kihalali kiende kubeba wenye shida, binafsi naiona ni kama kodi fair kabisa ya kuweza kuishi na kupata rizki kwenye dunia hii ambayo ina mwenye nae alieiumba.

Nadhani huwa inahesabiwa zaidi unapomsaidia mtu mwenye shida na hawana ukaribu na wewe ama mnajuana kwa mbali, wale mnaojuana karibu huwa ni msaada na si zaka.

Ni adaka pekee huwa natoa kanisani lakini kuhusu Zaka huwa najaribu kuitoa kwa watu wenye shida naokutana nao ila hadi sasa sijawai toa 10%>

Binafsi nineshindwa kuweza kufikia hio asilimia 10, huwa bili zinanizonga najikuta bili zangu inabidi ziwe na kipaumbele kuliko hii zaka ambayo naichukulia kama kodi ya Sir God alienipa uhai moaka sasa.

Tangu naanza kupata elf 30 kwa mwezi hadi sasa nikiwa naweza kupata milioni 2 hadi 3 kila mwezi nikiri wazi nilikuwa nahitahidi kutoa fungu la kumi ila sijaweza mpaka sasa.

Mfano kwa mwezi uliopita nilipata kama milioni 2 na laki 3 hibi hivi ila nikajikuta naishia kutoa zaka kama elf 80 hivi, Mtindo wangu wa kutoa zaka Huwa nagawa gawa hizi buku buku na elf 2 kwa watoto wa mtaani, nikikuta mtu anauza miwa na karanga kwenye ungo nampa elf 2 nasema ntapitia baadae ila sirudi, n.k.

Yani kiufupi nakuta matumizi yananibana sana na naanza kujidanganya yana umuhimu sana kuzidi zaka, mlioweza kufikisha hio 10% ya kipato kile halali naombeni ujuzi.
Zaka inatolewa hekaluni tu na hekalu la mungu lilikuwa moja tu kabla ya kujengwa na baada ya kujengwa hekalu...kasome vizuri zaka ya fungu la 10 ilianzaje na ilitolewa wapi.
 
Usisahau pia kuisha maisha ya utakatifu kwamaana haitasaidia kitu kutoa zaka then hutendi yaliyo mema
Anapotoa pia maombi huwa yanatolewa na mpokea zaka, hivyo lazima yatamkumbusha kuishi impavyo MUNGU wake.
 
Embu angalia watu wakistaafu wanavyobadilikaga akili pension yao, ukiwa unajitambua wengi humtolea MUNGU kisha wanakaa chini kufikiria atumie vipi! Mungu hawezi kukuacha uaibike kama upo naye karibu.
 
Daah aisee... Zaka Ni amri sio hiari ujue? Hata kiwe kidgo vipi Ni lazima utoe!! Lengo la zaka Ni kumwonesha Mwenyezi Mungu utii wetu je tutamheshimu kwa kila Pato letu? Kimbula imeandikwa mheshimu Bwana MUNGU wako kwa Mali yako yote... Hivyo Zaka ni agano la MUNGU na mwanadamu lililoasisiwa na Yakobo.... Zaka imekua shida ivi je Malimbuko itakuaje sasa😄
Malimbuko nayo ni amri kama zaka?
 
Back
Top Bottom