Mliowahi kutumia bati za kampuni ya BATI BOMBA LTD au kampuni zozote ndogo za mabati

Mliowahi kutumia bati za kampuni ya BATI BOMBA LTD au kampuni zozote ndogo za mabati

Nataman sana ila mambo yameumana balaa. Budget kikomo. Nishasqueez to the last point

Na siwezi fika mwezi Feb bila kuwa sijapaua aisee

Hapo ada ya dogo inadai na huku nategemea chalii tena
Usiwe na papara kwenye upauji. Endelea kudunduliza uweke kitu cha ALAF. Baadae Unaweza kujikuta unajuta na kujilaumu kwa papara uliyoifanya
 
Hivi tunapozungumzia ubora wa bati tunaangalia muda mpaka bati ianze kupata kutu au muda ambao rangi itaanza kupauka?

Maana hizo unazosema za bei ndogo zimepitishwa na TBS,na wanatoa warranty ya miaka 10,sasa kigezo cha kuzipitisha ni nini? ina maana zinakidhi viwango.

Mi naona mambo mengine hapa ni mfuko wa mtu,weka bati kulingana na uwezo wako,kwani wengi wetu nchi nzima tunaweka haya viwanda vidogo na hayo maswala ya kutu au rangi tutadanganyana tu humu...
TBS wanatoa uthibitisho kwa kutumia vipimo vya maabara. Huko duniani ndio kuna ukweli wa namna gani bati ita-perfom. Watu wanaogopa hizi kampuni ndogo ndogo kwa sababu hazina muda mrefu kwenye soko. Utajuaje performance yake kwa hiyo miaka 10? Kuna mdau hapa amesema ametumia miaka 3 na hajaona shida, hii ni feedback nzuri, ila kuamini tu TBS unaweza ukalia baada ya muda.

Kuna maeneo chumvi ni nyingi, mengine tofauti ya joto usiku na mchana ni kubwa, sehemu nyingine kuna mvua za mawe; hayo mambo yote ni ngumu TBS kufanya vipimo.
 
Mkuu,Mimi nimekuwa sales officer wa kampuni mbili za mabati Kwa wakati tofauti. Watu wengi wanashindwa kuelewa kuwa kampuni zote za mabati,bati zao huwa zinapauka ila hutofautiana kutegemeana na mazingira uliyopo, pamoja na ubora wa rangi iliyokuwa prepainted kwenye materials pamoja na thickness ya coating.
Kuhusu suala la ubora wa mabati ni kweli ALAF ni leading company kwenye industry ya mabati lakini hata naye huwa anapata changamoto ya bati kupauka kabla ya muda tegemewa.
USHAURI.
Mkitaka kununua bati ni kheri muwe mnaenda kununua kiwandani Moja kwa moja na siyo kwenda kwenye maduka.
Pia suala la msingi kabisa ni kuwa HAKUNA BATI YA GAUGE 30 ILIYOTIMIA AMBAYO INAUZWA CHINI YA SH25000/= ZA UPANA MDOGO NA SH 33,000/= UPANA MKUBWA(KWA DAR) NA 27,000/= UPANA MDOGO NA 35,000/36000 ZA UPANA MKUBWA (MIKOANI).HIZO ZOTE MNAZOAMBIWA NI GJ 30 NA INAUZWA KWA 23,000/= SI KWELI BALI HIYO NI GJ 30 INAYOELEKEA KWENYE GJ 32 AU NI GJ 32 KABISA.
KWA MASWALI NA MAELEZO ZAIDI MNAWEZA KUNIULIZA MASWALI NAMI NITAJIBU KWA KILE NINACHOKIJUA.
KARIBUNI SANA KINGLION MABATI.
LAZIMA TUAMBIANE UKWELI ILI TUSAIDIANE.
Utatambuaje bati original ya ALAF..?
 
Nunua bati za dragon kama utahitaji njoo inbox nikupe mtu akusaidie na utapata punguzo la mwisho wa mwaka.

Nataka niwashauri wengi waliopo hapa. Bati zote huchakaa rangi isipokuwa namna ya uchaakaji unatofautiana kati ya rangi na rangi zingine na kati ya kampuni moja na ingine.

Rangi zenye kung'aa sana mfano Red, Maroon, Blue, Navy Blue huchakaa haraka zaidi kulinganisha na rangi zingine.

Hivyo kuna rangi ukiweka hata baada ya miaka 20 utaziona zikiwa kama ulivyonunua.

Pili upigaji wa misumari nao unaweza kufanya bati kuoza haraka kwani misumari ya bati huwekwa raba kuzuia maji na hewa kwenye tundu la msumari lakini mafundi wengi hupiga bati pasipo kuhakikisha msumari unaraba yake bati linaanza kuoza sehemu msumari na kuelekea sehemu zingine.

Mwisho hali ya hewa hasa maeneo ya pwani ni changamoto kwa bati aina zote. Hivyo kichukua bati zenge unene mzuri unaipa paa lako miaka minvi zaidi. Hivyo gauge 28 kushuka chini inalipa uhai paa lako kuliko gauge 30 au 32

Ni hayo kwa leo
Mkuu, ni rangi gani ambayo sio rahisi kupauka tofauti na hizo rangi ulizo zitaja?
 
Utatambuaje bati original ya ALAF..?
Mkuu Mimi nimekuwa sales officer wa dragon na Sasa niko na Kinglion,Si sales wa ALAF ila Kwa uzoefu wangu wa mabati naweza kutambua bati original ya ALAF kwa kuzingatia vitu viwili;
1. Muhuri wa moto ule wa vinundu(sijakua kama nitakuwa sahihi) ila ni ule muhuri unaobonyeza bati kabisa.
2. Kwenye migongo mipana katikati ya migongo huwa na vibaraza vya kumwagia maji,Sasa kwenye vile vibaraza utaona Kuna vimistari vitatu.
Naruhusu kurekebishwa pale nilipokosea.
 
Nimeona wana test nzuri ya bati hizo dots nimezipenda
 

Attachments

  • FB_IMG_1671269889584.jpg
    FB_IMG_1671269889584.jpg
    100.6 KB · Views: 95
Kiwanda kama alaf au sunshire kinakufaje kizembe mkuu?
Achana na huzo story.

Kaa na hela yako. Badae unaweza badili mawazo au unaweza pata shida kubwa ya kifamilia ukaitumia hiyo hela.
 
Hizi ni materials ambazo baadhi ya makampuni tunaita matte wengine wanaita royal ila Kwa kiswahili tunaita mchanga mchanga/chengachenga.
Ni matirio mazuri Sana na bati yake Ina Bei kubwa kulinganisha na Bei ya bati la rangi mterezo
zinapendezesha sana paa
 
Hizi ni materials ambazo baadhi ya makampuni tunaita matte wengine wanaita royal ila Kwa kiswahili tunaita mchanga mchanga/chengachenga.
Ni matirio mazuri Sana na bati yake Ina Bei kubwa kulinganisha na Bei ya bati la rangi mterezo
Shida inawahi kupata ukungu kama vigae nyumba inaonekana chafu kama vigae vya nyumba za Mbezi beach.
Old fashion, kitu msauzi Alaf utojutia kampuni zingine jiandae na kopo la rangi juu baada ya miaka 2.
 
Kitu low price kitakuaje quality sasa, ukiezeka umeezeka
 
Shida inawahi kupata ukungu kama vigae nyumba inaonekana chafu kama vigae vya nyumba za Mbezi beach.
Old fashion, kitu msauzi Alaf utojutia kampuni zingine jiandae na kopo la rangi juu baada ya miaka 2.
[emoji23][emoji23][emoji23]shida mfuko ndugu. Alaf ni mkasi kweli kweli
 
Hizi ni materials ambazo baadhi ya makampuni tunaita matte wengine wanaita royal ila Kwa kiswahili tunaita mchanga mchanga/chengachenga.
Ni matirio mazuri Sana na bati yake Ina Bei kubwa kulinganisha na Bei ya bati la rangi mterezo
Kuna sister napiga nae nyumba yake alipiga hii chenachenga ya C.gray toka dragon. Nyumba inawaka balaa. Since 2020 bado kanadunda fresssh
 
Back
Top Bottom