Mnaonaje Rais Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035?

Mnaonaje Rais Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035?

Sura ya Pili, Sehemu ya Kwanza, Ibara za 38, 39 na 40.

Ibara ya 40 (1) na (2)

Kifungu (1)
"Bila kuathiri masharti ya mengineyo yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote ambaye ni Rais anaweza kuchaguliwa tena kushika kiti hicho" Siyo kuteuliwa na Katiba.

Kifungu (2)
"Hakuna mtu atakayechaguliwa zaidi ya mara mbili kushika kiti cha Rais"

Mhe. Rais Samia hajachaguliwa, atachaguliwa kwa mara ya kwanza 2025 na hivyo kwa mara ya pili kama atagombea na kushinda 2030 na hivyo kuhitimisha awamu zake 2035.

Bado tunaye sana tu!
Kwa mujibu wa muongozo huo acha kazi iendeleeeeeeeeee
 
Mshaanza kumchulia ,atakata MOTO kama Mtangulizi wake....Kuchezea katiba bila ridhaa ya wananchi wenyewe ni mikosi ,wabunge hawatuwakilishi sisi bungeni bali wanawakilisha chama,matumbo yao na serikali.
Mkuu, serikali ni nani? Siyo mimi na wewe na wao? Kama ni mimi na wewe basi wanatuwakilisha sisi.
 
Tupe reference na wewe pia, madhali kwenye mada kuu nilisema mwishoni kuwa tupe ushahidi.

Bunge ndiyo inaisimamia serikali japokuwa zote ni mihimili huru na serikali ndiyo mhimili anaoongoza rais, lakini Bunge hilo hilo linaloisimamia serikali bado nalo na mamlaka makubwa hayo linakaguliwa na CAG. Mhimili wa Mahakama ambao uko huru kabisa pia na ambao unatoa haki kwa kila mtu na kwa mihimili iliyobaki nao unakaguliwa na CAG. Madaraka ya CAG yako kikatiba na hakuna nchi hii sehemu ambayo katiba inazuiliwa kutenda mamlaka yake. Soma Katiba ya JMT ya 1977 ibara za 143 na 144 kuhusu CAG na mamlaka yake ya utendaji.

Huna ujualo zaidi ya kupiga siasa mfu hapa jukwaani. Naona umejaa nadharia zisizoendana na uhalisia.
 
Nachokoza mada.

Wadau mnaonaje kama Rais Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035? Kwa kuwa Rais Samia alichukuwa nafasi yake kufuatia mauti ya mtangulizi wake mwanzo wa safari na kwamba hakukuwa na utaratibu wa mila na desturi ya uchaguzi bali ilikuwa ni kutimiza matakwa ya katiba.


Kiuhalali na kwa haki kwake, anastahili kuwa wa pili nyuma ya Mwl Nyerere kwa kukaa ofisini kwa miaka 15 kwa maana ya miaka aliyopokea kijiti kwa sharti la katiba na ndipo sasa astahili utaratibu wa mila na desturi yetu ya uchaguzi ambapo anaruhusiwa awamu mbili 2025 – 2035?

Nini maarifa yako, tupe maoni kwa vigezo na ushahidi.
Kwanini usitumie muda wako kurudi shule ukasome upate elimu ili uweze kuwaza kama mtu!!!?
 
Huna ujualo zaidi ya kupiga siasa mfu hapa jukwaani. Naona umejaa nadharia zisizoendana na uhalisia.
Tupe ushahidi wa unachokisimamia na kukiamini na kujaribu kulisha umma sumu kwamba CAG hana uwezo wa kukagua fedha za Ikulu.
 
Kwanini usitumie muda wako kurudi shule ukasome upate elimu ili uweze kuwaza kama mtu!!!?
Tupe hiyo elimu yako bora uliyonayo badala ya kunyooshea kidole elimu yangu ambayo umeona haitoshi nirudi shule. Mwisho wa mada kuu niliandika hivi:-
"Nini maarifa yako, tupe maoni kwa vigezo na ushahidi"
 
Nachokoza mada.

Wadau mnaonaje kama Rais Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035? Kwa kuwa Rais Samia alichukuwa nafasi yake kufuatia mauti ya mtangulizi wake mwanzo wa safari na kwamba hakukuwa na utaratibu wa mila na desturi ya uchaguzi bali ilikuwa ni kutimiza matakwa ya katiba.


Kiuhalali na kwa haki kwake, anastahili kuwa wa pili nyuma ya Mwl Nyerere kwa kukaa ofisini kwa miaka 15 kwa maana ya miaka aliyopokea kijiti kwa sharti la katiba na ndipo sasa astahili utaratibu wa mila na desturi yetu ya uchaguzi ambapo anaruhusiwa awamu mbili 2025 – 2035?

Nini maarifa yako, tupe maoni kwa vigezo na ushahidi.
Naunga mkono hoja!
 
Back
Top Bottom