Mnawachukuliaje watu wa GNLD na Forever Living Products?

Mnawachukuliaje watu wa GNLD na Forever Living Products?

Biashara gani unatafuta zaidi watu wa kuuza kama wewe badala ya kutafuta wateja wa kuwauzia bidhaa
 
Nilishawah kwenda moja ya mikutano ya GNLD nilimkuta mpangaji mmoja wa bi mkubwa akitoa ushuhuda kwamba GNLD imemsaidia kuishi kwenye nyumba yake mwenyewe na kumiliki gari zuri wakat ile ki ukweli jamaa sijawah kumuona akimiliki ata pikipiki ni mwendo wa kubanana asubuh kwa daladala tu kama mm,hawa jamaa ni wahongo sana na wanalipwa kwa kutoa ushuhuda wa uhongo
 
kuna mwanamke mmoja anajihusisha na forever living product,sasa anapotaka kumkamata mtu ili kumuingiza kwenye biashara hii ya forever hasemi moja kwa moja anasema oh kuna biashara flani ya ujasiria mali nzuri tu kwahyo unatakiwa uje sehemu flani tukutane tukupe details zaidi ukimuuliza biashara gani hyo hajibu,anakwambia ww njoo tu,,sasa kwann hawasemi ukweli kuhusiana na biashara hii au wengi hawaipendi biashara hii na ndo maana hutumia mbinu hyo kukamata watu??
 
Wanajua wakisema hautoenda,ila ukienda bila kujua utakutana na watu wana upako wa kushawishi utaletewa watu waliofanikiwa na hiyo bizness mpaka mwenyewe utaona yes hii ndio bizness ila kati ya 100 wanaoingia anaofanikiwa ni m1 tu au hakuna kabisa.
 
Hakuna kazi isiyokuwa na "title", ukisikia wanakwambia njoo tu ujue kazi za kutembeza dawa au vyombo, kazi kwako!
 
Wanajua wakisema hautoenda,ila ukienda bila kujua utakutana na watu wana upako wa kushawishi utaletewa watu waliofanikiwa na hiyo bizness mpaka mwenyewe utaona yes hii ndio bizness ila kati ya 100 wanaoingia anaofanikiwa ni m1 tu au hakuna kabisa.
Hao jamaa wamebobea kwenye lugha ya ushawishi sijapata kuona......yaani unaweza kuacha kazi yako nzuri kwa maneno yao matamu....ndio maana wanawakamata sana wadada.....
 
mambo ya kufanya biashara ya kudanganya watu mi siyawezi.

mtu unakuta ye mwenyewe ni m'bomboo ila anakwambia dawa anazouza zinapunguza unene!! shit!!
 
kuna mwanamke mmoja anajihusisha na forever living product,sasa anapotaka kumkamata mtu ili kumuingiza kwenye biashara hii ya forever hasemi moja kwa moja anasema oh kuna biashara flani ya ujasiria mali nzuri tu kwahyo unatakiwa uje sehemu flani tukutane tukupe details zaidi ukimuuliza biashara gani hyo hajibu,anakwambia ww njoo tu,,sasa kwann hawasemi ukweli kuhusiana na biashara hii au wengi hawaipendi biashara hii na ndo maana hutumia mbinu hyo kukamata watu??

Ni utapeli mtupu.na siyo hiyo tu, kulikuwa na gnld,swissgard, Tianshi, edmark nk zote zimetapeli watu na zimetoweka.Fanya biashara yenye leseni!
 
Wanajua wakisema hautoenda,ila ukienda bila kujua utakutana na watu wana upako wa kushawishi utaletewa watu waliofanikiwa na hiyo bizness mpaka mwenyewe utaona yes hii ndio bizness ila kati ya 100 wanaoingia anaofanikiwa ni m1 tu au hakuna kabisa.

Mmoja lazima awe muuzaji, wengi wawe wanunuzi.
 
aisee wengi mmeponda GNLD sasa mtupe altenative pia mana kwa wengne sie hao ni wakombozi wetu
 
Biashara gani unatafuta zaidi watu wa kuuza kama wewe badala ya kutafuta wateja wa kuwauzia bidhaa

Sina uelewa sana na hii, lakini wenyewe wanaita network marketing, kwa maana hao watu unaowatafuta ndio itakuwa network yako ambapo itakapozidi kuongezeka na ndio pato lako litakapoongeezeka, hao watu wakati huo huo wanakuwa wateja wa bidhaa zao, kwa hiyo wewe unaona unatafuta watu kumbe ndio wateja hao,

Pamoja na watu wengi wanaibeza hii biashara lakini iko poa sana, tatizo kubwa linalofanya watu waibeze na kuona ngumu ni kama ifuatavyo

1. Watu wengi wanaoenda kujaribu hii biashara hawana asili ya biashara, kwa iyo hawana sifa km za ushawishi na nyinginezo hivyo inakuwa ngumu sana kwake.

2. Bidhaa zao zina asili moja yaani madawa tu, hii ngumu sana kwa mtu ambaye hausiani na masuala ya afya kupata soko, ndio maana utaona kuna mwingine anasema alinunua akabaki nazo akaamua kutumia mwenyewe, na mwingine akasema yy alinunua akapona gout na network yake inategemea anayemjua amepona gout ambayo ni ndogo.

3 Jinsi ya kutafuta watu/wateja(network) imekaa kimachinga (samahani kwa kutumia neno hili) au wale wa promotion zaidi, ndio hapo ugumu unaanza mtu anajiona graduate halaf leo afanye promotion! !!! haiwezekani.

Hivo ndio vikwazo ambapo watu wanaona ni kma ndoto kufanikisha.

Nimewaona jamaa wengine wapo pale sinza na wao wanafanya network narketing lakini wao bidhaa zao ni nguo, viatu, mabegi na vitu vinavyofanana na hivyo wao unaweka (deposit) elfu hamsini halaf kila unaponunua vitu vyao unapata points na unalipwa posho. kulingana na points zako.

kwa hiyo ukiamua kununua kwa ajili ya kuvaa au kuuza shauri yako.

Na hawa nao tatizo lao km wengine bidhaa zao ni ghali kama wengine.
Na kuna watu nimewaona wamekurupuka huku hawana asili ya biashara nao hao watakuja kuibeza
 
aisee wengi mmeponda GNLD sasa mtupe altenative pia mana kwa wengne sie hao ni wakombozi wetu

Kama umepata laki 7 ya kujiunga nao basi ungeweza kuwekeza hiyo hela kwa jambo lako la msingi na kuzalisha pesa nzuri sana
 
Kuna dada namfahamu tena tulipanga sehemu moja akaenda huko akahubirhwa alivyorudi akaingia benki akalamba mkopo wa 2m zote akapeleka kununua products za forever akawa member,akaanza kuzipeleka mtaani,alianza dar ikaonekana hailipi akaamua kwenda kwao moshi huko nako yakawa majanga na kwanzia hapo akaanza kurandaranda kutafuta wateja,alihangaika mpaka huruma si kwa keshi si kwa mkopo ngoma ikagoma,alipata hasara ya kutupwa mpaka na sie tuliokuwa anatushawishi tukaamua kuusoma mchezo tukampiga marufuku asirudie kuwarubuni watu huku wakijua wazi ni kuwaibia pesa zao ..eti mafuta tu ya nywele 80elfu,sabuni ya kuoga 40elfu duh!
 
Sina uelewa sana na hii, lakini wenyewe wanaita network marketing, kwa maana hao watu unaowatafuta ndio itakuwa network yako ambapo itakapozidi kuongezeka na ndio pato lako litakapoongeezeka, hao watu wakati huo huo wanakuwa wateja wa bidhaa zao, kwa hiyo wewe unaona unatafuta watu kumbe ndio wateja hao,

Pamoja na watu wengi wanaibeza hii biashara lakini iko poa sana, tatizo kubwa linalofanya watu waibeze na kuona ngumu ni kama ifuatavyo

1. Watu wengi wanaoenda kujaribu hii biashara hawana asili ya biashara, kwa iyo hawana sifa km za ushawishi na nyinginezo hivyo inakuwa ngumu sana kwake.

2. Bidhaa zao zina asili moja yaani madawa tu, hii ngumu sana kwa mtu ambaye hausiani na masuala ya afya kupata soko, ndio maana utaona kuna mwingine anasema alinunua akabaki nazo akaamua kutumia mwenyewe, na mwingine akasema yy alinunua akapona gout na network yake inategemea anayemjua amepona gout ambayo ni ndogo.

3 Jinsi ya kutafuta watu/wateja(network) imekaa kimachinga (samahani kwa kutumia neno hili) au wale wa promotion zaidi, ndio hapo ugumu unaanza mtu anajiona graduate halaf leo afanye promotion! !!! haiwezekani.

Hivo ndio vikwazo ambapo watu wanaona ni kma ndoto kufanikisha.

Nimewaona jamaa wengine wapo pale sinza na wao wanafanya network narketing lakini wao bidhaa zao ni nguo, viatu, mabegi na vitu vinavyofanana na hivyo wao unaweka (deposit) elfu hamsini halaf kila unaponunua vitu vyao unapata points na unalipwa posho. kulingana na points zako.

kwa hiyo ukiamua kununua kwa ajili ya kuvaa au kuuza shauri yako.

Na hawa nao tatizo lao km wengine bidhaa zao ni ghali kama wengine.
Na kuna watu nimewaona wamekurupuka huku hawana asili ya biashara nao hao watakuja kuibeza

Mkuu kwenye red ndio msingi na maana ya Ponzi scheme aka pyramid scheme
Kama unaelewa maana ya pyramid scheme utaweza kuelewa namaanisha nini.
Hizo products ni geresha tu kinachotakiwa pale ni laki saba yako tu
Pyramid scheme unapeleka pesa kuwekeza then unaambiwa shawishi watu waingie kwenye network yako na kila atakaye ingia kwa net yako unapata gawio, sasa hawa jamaa wakaona badala ya kukwambia lete pesa kavu kavu wakaja na gia ya kukuzia product,
 
Back
Top Bottom