Mnawachukuliaje watu wa GNLD na Forever Living Products?


Hawa jamaa wanatofauti gani na telexfree..??! Hawa si tu ni mbwa.., bali ni mijibwa mijizi kabisaaa!!! Hivi wewe leo hii mkubaliane eti kwamba kila mtu aweke elfu kumi kwenye kapu moja alafu eti mgawane hilo kapu kila mtu sawa sawa alafu eti mtegemee kupata pesa zaidi ya ile elfu kumi uliyoweka..???! hivi kweli kama si wizi wa ki-mbwa huu ni wizi wa kinini.., mi nilichomoa japo walijaribu kuni-brain wash na shuhuda za ki-mbwa kabisa. wanaofaidika ni wale walio anza mwanzoni.., wengine ni mazezeta a.k.a mazombie yakuwa nenepesha wale upliners.., em' tumia asilimia 0.0001 tu ya ubongo wako huo na utanielewa kwa asilimia 20,000..!!!!
 

ndugu hujui kabisa hawa forever living wanavyofanya kazi na unawahukumu wakati hata hujui wanachofanya. hayo unayoyasema hapo juu hamna hata moja la ukweli. hawa wanauza products, sio kama deci au telexfree hawana chochote wanachouza.
 
ndugu hujui kabisa hawa forever living wanavyofanya kazi na unawahukumu wakati hata hujui wanachofanya. hayo unayoyasema hapo juu hamna hata moja la ukweli. hawa wanauza products, sio kama deci au telexfree hawana chochote wanachouza.

Yaan kweli umeshindwa kutumia hata 0.0001% ya ubongo wako kweli..??! Em' wauze iphone5 au nyanya au hata vitunguu tu uone kama mi nitaongea kitu.., tatizo mnauza rubbish ambayo gharama yake si zaidi ya 20k kwa shs. laki saba...!! hio kusema mnuza dawa sijui nini ni ujanja wa kuficha sura halisi ya hii pyramid scheme ili serikali wasiweze kuwafungia..! mbwa kabisa..!!
 
ndugu hujui kabisa hawa forever living wanavyofanya kazi na unawahukumu wakati hata hujui wanachofanya. hayo unayoyasema hapo juu hamna hata moja la ukweli. hawa wanauza products, sio kama deci au telexfree hawana chochote wanachouza.

forever LIVING,sijui GNLD wote ni wezi watupu,ni DECI ile. Ila kwa kua watanzania wengi mnapenda shortcut,utajiri wa fasta nendeni,ila I am telling you,FOREVER LIVING,GNLD,KUPANDA MBEGU ni WIZI mtupu.

Siku zote watu hutajirika kupitia ujinga wa watu wengine na tamaa.

MAKE NO MISTAKE ABOUT IT.
 
ni kweli wanao wapata ni maboya tu....jamaa hao wezi tu
 

kuna moja umeisahau nao wasani ina itwa .. tianshi alikuwepo mke wa kigogo mmja mrs mwap..... nao hivyo hivyo ila naona hawapo sahv... FRANCIS DA DON
 
Last edited by a moderator:
Huo upuuzi juzi kati amenipgia simu mpenzi wangu eti nimuungishe hizo products anataka kujiunga sijui nini na nini....! nikampa makavu kuwa sijihusishi na utumbo huo na you should immediately stop and evacuate from such silly business unless nakupga chini.
 
Biashara inahitaji kupambana nawajua wadau wa 4ever living wanapiga hela sana kuna m1 ana nyumba ya ghorofa na anapush ndinga ya 0 km biashara nzuri hii ukijituma! iendelee.
 
asanteni wakuu kwa kunifumbua macho mana juzi kati kuna mchizi kanisomesha ila nlikuwa bado natafakari
 
Kwa kweli hata mimi nilichomoa tena nilimchomolea rafiki yangu wa karibu kiaina kwani sababu ya kumheshimu nilimpa lugha ya kumdanganya ili asinielewe vby. Lakini kiukweli ile ni DECI nyingine hapa nchini

mkuu ata mim kuna rafiki yng wa karibu sana anani convince nijiunge na GNLD ila mim mpk dakika hii hatujaafikiana bado,ni zaidi ya mwezi sasa tangu aanze kuniletea hizo swagga ila mim namkwepa mpk leo hii.hawa members wanatusumbua sana sisi tusiokuwa wadau.
 
Duuuh aixee mi kuna jirani angu kila cku anazunguka na bdhaa zake cna uhakika kama kauza hata moja, alafu kuna rafk angu katumia product yao foreva ya kupunguza uzito! Haaaah hadi dawa zmeisha hajapungua hata nusu kilo, na aliinunua laki 3, kabaki amenuna tu...
 

Naona unaendeleza hii biashara kuisifia katika ulimwengu wa kuwakandamiza wanyonge... At the bottom are the one suffer most. Nimeshuhudia watu wanachukua mikopo na kushindwa kuirejesha ili wanunue hizo product na kuziuza. Pia kuna jamaa yangu wamemdanganya kuwa kuna hizo juisi zenu zinatibu kisukari.... hadi sasa ninavyo andika hii kitu ni mwaka watatu na hajapona zaidi kinazidi kupanda. Ni vema tukawa na utu.... Hawa watu na GNLD nathubutu kusema ni matepeli wa mchana kweupe. Nunua product lakini sio kuingia katika hiyo biashara ni bora ukafanya biashara nyingine..... Hadi sasa sijaona waliofanikiwa hapa Bongo kiasi wanacho advertise wao. Akili za kuambiwa changanya na zako.
 

huyo lazima atafunga nazo ndoa hizo bidhaaa....imekula kwake
 

Ukiwaambia kuwa hao ni matapeli mnakosana kabisa. Elimu hii iende na kwa wengine. Niwe mkweli hawa watu hii biashara si ya kuwashirikisha watu wanaotaka kufanya ujasiriamali wenye maendeleo ya kweli sio hii biashara.
 
Hizi ni mbinu za wizi na wanatumia mwanya wa watu kutafuta badi wamebuni mbinu hii kuwaibia watu na kujitajirisha.
Sio kampuni hii tu inayofanya wizi ..sasa zipo nyingi.
Ushauri kama mtu unayo laki saba bora kutengeneza vitumbua na chapati ukauza utapata faida

Pia hii ni mbinu ya kukwepa kulipa ushuru kwa bidhaa zao.TRA labda waingilie kama hawajawekwa sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…