Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa hiyo wewe ndio unaujua uonevu zaidi kuliko Mdee, Matiko,Bulaya na wengine?! wote hao ni wanachama halali wa chadema tena viongozi, Halima Jems Mdee ni Mwenyekiti wa umoja wa wanawake chadema Taifa sio mtu mdogo ndani ya chadema,Uzalendo gani huo? Kutwa kubambikiwa kesi kupigwa risasi uonevu kibao kisha useme kuna Uzalendo huko?
Mbona sijaona taarabu hapo? Mjibuni tuwaite CCM A?Mkuu kuna jukwaa la taarabu fuatilia upewe mwongozo hii sio mahala pake...
Mdee ni lawyer wa Mahakama ipi? Alishawahi hata kusimamia kesi ya kuku?Majina ya wanawake wa viti maalum huchakatwa mapema hata kabla ya uchaguzi mkuu. Hili ni swala la kisheria zaidi na mdee ni lawyer.
Amen na iwe hivyo ukasikie sauti ya Bwana ambayo ayaambia makanisa....
Haya mwanasheria kafungue kesi yakupinga basiUnaelewa kuwa kisheria chama hakiwezi kuteua wala kupeleka jina NEC la viti maalum la mtu ambae yupo jela? Unaelewa kuwa leo kesi ya kina Nusrat imeitwa Jaji akabaki anashangaa maana hakuona watuhumiwa wala mawakili wa pande zote mbili?...
sio mimi nasema bali alishawahi kusema Mbowe mwenyewe akimuambia katibu mkuu aliehama chama Dr VIcent MashinjiK
Kwa hiyo unasema kuwa chadema ni mali ya mbowe?
Yaani kesi ya Tumbili nipeleke kwa Ngedere?Hapo kuna kutolewa haki kweli?Unaelewa kuwa kwa sasa hivi mahakama imewekwa mfukoni na mtu mmoja,tena mfuko wa shati?Haya mwanasheria kafungue kesi yakupinga basi
sasa kinachokuliza humu kuwa ni haki yako ni haki yako ni nini? tulia wewe ulichelewa kutambua kuwa chadema ni kampuni tena ya mtu binafsi utaumia sana huku wenyewe wanakula maisha wewe endelea kudai haki wakati unatambua kabisa haki zote zimehifaziwa.Yaani kesi ya Tumbili nipeleke kwa Ngedere?Hapo kuna kutolewa haki kweli?Unaelewa kuwa kwa sasa hivi mahakama imewekwa mfukoni na mtu mmoja,tena mfuko wa shati?View attachment 1634566
Chama kimewafaidi vya kutosha. walikuwa mirija ya kupeleka pesa kwa mbowe. Wafukuzeni sasa tuone, jinsi mtakavyozidi kuwa imara kwa uchache wenu.Wanafukuzwa bila kujali jinsia yao kwakuwa wamejiteua wenyewe wanafukuzwa vizuri kabisa bora kuwa na chama cha watu wachache kuliko hao wanaopigania matumbo yao. Demokrasia ina Faida zaidi kuliko matumbo ya hao wachache. Wamejulikana kwa sababu ya chama hivo wao siyo wakubwa kuliko chama kuwa wataachwa wakiuke sheria na katiba ya chama
Ila DJ mbaya aisee, hahaha.
Mimi nipo hapa nacheki hii move yenye visa vya kusisimua ikiongozwa na shujaa Mbowe.Tunasubiri mahakama ikanushe mtu kuteuliwa na NEC akiwa gerezani.
Kwa Chama kinachojinasibu kua na Intel nzuri kama Chadema,na baadhi ya wabunge kuwa wake wa viongozi wa juu wa Chana bado unaamini Boss wao hakuwa na taarifa?!Inamaana unataka kusema kuwa wanawake wote 19 walienda kula kiapo bila hata mmoja wao kumwaga bosi wao? Dahh
Unaujua mchakato wake? Kaa kimya kama hujui, dada zetu wanadhalilishwachadema ilipitisha wanawake 68 kugombea majimboni hebu tuambie hao wanawake nani aliwadhalilisha kingono na wapi mpaka kuwapa hizo nafasi?
Mdee ni lawyer wa Mahakama ipi? Alishawahi hata kusimamia kesi ya kuku?
Hivi hujui hata Paskal Mayalla ni mwanasheria lakini siyo lawyer.?