Uchaguzi 2020 Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani

Uchaguzi 2020 Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani

Recent Publication;
-Assessment on the Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
weka citation... Masters umesoma wapi? Kampala Uni? weka resume, siyo unaleta matatizo hapa JF.
Una kesi ya pragialism hapa JF
 
wacha tugawane mbao zetu chama kimekwisha....sasa kila mtu achukue chake mapema, kamwe hatuwezi kuburuzwa tu kila siku.
 
😂😂 uteuzi utausikia kwa first ladies wa R chuga, Kisarawe tu!! Labda badili jinsia.
 
Kuna tetesi kuwa wabunge 19 wa viti maalumu wa CHADEMA wanapanga kugomea wito uliotolewa na Katibu Mkuu J. Mnyika kufika mbele ya Kamati Kuu kesho tarehe 27.

Kitendo cha wabunge hao kutofika mbele ya KK kitaonyesha mwendelezo wa dharau nyingine kwa mamlaka hiyo, vilevile watakuwa wamepoteza haki yao ya msingi ya kujitetea ikiwa ni pamoja na kujibu kwanini wasifutiwe uanachama.

Ifahamike kwamba Kamati Kuu ndiyo yenye mamlaka ya kuteua majina ya viti maalumu, KK imepewa mamlaka ya kusimamisha au kufuta uanachama wa mwanachama yeyote.

Kama bado ni wanachama wa Chadema nawashauri waendelee kuheshimu mamlaka za chama ikiwemo KK na viongozi wakuu wa chama.
 
Katika CHADEMA kuna watu Mbowe hawezi kuwafanya lolote ni inner circle yake, mmojawapo ni Mdee na Lema. Endeleeni kujidanganya. Ni rahisi Lissu kufukuzwa uanachama au Mnyika kuambiwa ajiuzulu lakini sio kumfukuza Halima Mdee.
 
Ndugu yangu tumia akili angalau kidogo...jifunze kupambanua mambo...usikariri tu mambo...kwa mawazo yako serikali imefoji...hivi Mdee na wenzake wanaweza kukubali serikali ifoji halafu wao waapishwe?!? Kama ni kufoji kwanini usifikirie kuwa pengine baadhi ndani ya Chadema wamefoji saini za kiongozi wao na kuwasilisha majina bungeni?!...
Kwa uwezo wa akili yako hayo ndio uliyoyaona. Hali halisi nchi haikufanya chaguzi zozote.

Pili nchi sasa hivi hakuna sheria zinazofanya kazi kwa manufaa ya umma.

Bado kilomita kadhaa tutafika kwenye ukuta hakuna pa kukimbilia hapo ndipo tutajua kweli amani ni asili yetu.

Chadema inao utaratibu wake wa kuteuwa hao wabunge Je ulifuatwa? Kuna nini serikali nzima kuingilia huo mchakato? Naomba nisiendelee nisije chafua hali ya hewa.

Kama u sehemu ya napenda amani acha kufunga mkono serikali na Bunge kwa hili wamechemsha sana na kilitua aibu taifa. Kuendelea kuwaunga mkono ni kuzidisha chuki kwa waonewaji na wanaweza kufanya mambo magumu na taifa likaathirika
 
1. Kuna uwezekano Mh Mbowe anahusika katika sakata hili,hivyo Ni muda muafaka wakujiuzuru uwenyekiti Mara moja
2. Kamati kuu iwafute Mara moja hata bila kupoteza muda
3. Inasemekana Salum Mwalimu anahusika pia nae Ajiuzuru Mara moja
3. Chama kiongozwe kwa muda na baraza la wazee kwa muda huu,John Mnyika akae pembeni kwa muda kwani amekosa nguvu ya kuepusha usaliti
 
Back
Top Bottom