Mobhare Matinyi ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari–MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali

Mobhare Matinyi ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari–MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali

Kuna nchi jeshi linaamua kuchukua madaraka... na hawana hitaji la kujenga chama chochote kiuchumi!
Ila umefanya vizuri kuliweka bayana... kumbe ccm inajijenga kwa Kodi za waTanzania.
Kwaiyo unafananisha jeshi na chama cha siasa tena cha upinzani ambacho hata hakijawai kushuka dola ?AMKA KIONGOZI UMELALA
 
Kuna nchi jeshi linaamua kuchukua madaraka... na hawana hitaji la kujenga chama chochote kiuchumi!
Ila umefanya vizuri kuliweka bayana... kumbe ccm inajijenga kwa Kodi za waTanzania.
Ccm ilishajijenga muda mrefu ni tofauti na chama kinachoenda kuanza moja
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Mobhare Matinyi kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari–MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Matinyi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.

Uteuzi huu unaanza mara moja.

Julai 2, 2023, Rais Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Mwanahabari Mobhare Matinyi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam. Miezi mitatu baadaye amemteua Matinyi kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Matinyi mbali na kuwahi kuwa Mkufunzi katika Kituo cha Diplomasia cha Msumbiji-Tanzania amekuwa Mwanahabari na Mchambuzi wa Maswala mbalimbali mengi yakilenga kuitetea Tanzania. Pia amewahi kuwa na ukurasa – column katika Gazeti la Kingereza la ‘The Citizen’ – The Eagle’s Eye na ameandika Makala mbalimbali kupitia Gazeti la Jamhuri.

Wengi wanamkumbuka Matinyi kwa uchambuzi wake tunduizi wa mabendekezo ya CHADEMA kuhusu Katiba Mpya wakati huo akiwa kama Mshauri Mwelekezi nchini Marekani.

Hata hivyo, kabla ya kuwa Mkuu wa Wilaya, Mwanahabari huyu kitaaluma, alikuwa akitumika kwenye jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika maarufu kama SADC. Kwa sasa Matinyi anaenda kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Gerson Msigwa, aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

MAJUKUMU YA KAZI
Lecturer
Mozambique-Tanzania Centre for Foreign Relations
Oct 2013 - Present · 10 yrs 1 mo

Analyst, Columnist
VoA, BBC, RFI, The Citizen, Majira
May 2003 - Sep 2013 · 10 yrs 5 mos
International affairs, Tanzanian and American issues, etc.

Instructor
United States Foreign Service
Feb 2008 - May 2013 · 5 yrs 4 mos
Washington DC

Consultant
Foreign service and educational institutions
Oct 2003 - May 2013 · 9 yrs 8 mos

Marketing executive, bank manager
Corporate America (various)
Oct 2003 - Jan 2008 · 4 yrs 4 mos
Washington D.C. Metro Area

Chief Editor
Business Times Limited
Jun 1998 - May 2003 · 5 yrs
Dar es Salaam, Tanzania
Editor June 1998 - Jan 2000


Instructor
Tanzania School of Journalism
Jan 2002 - May 2002 · 5 mos
Dar es Salaam

Journalist
Business Times Limited
Nov 1993 - Oct 1995 · 2 yrs
Dar es Salaam, Tanzania

ELIMU
American
Master of Arts (M.A.)
2010 - 20122010 - 2012

American
Master of Arts (MA)
2008 – 2010

Johns Hopkins
Master of Arts (M.A.)
2006 - 2008

Osmania
Bachelor of Arts (B.A.)
1995 – 1998

Azania O-Level
Tambaza A-Level

Chanzo: Ukurasa wa Linkedin wa Mobhare Matinyi
Hongera kwake sana tu ila
 
Nawaza tu endapo nchi hii itachukuliwa na chadema au upinzani ,je itachukua miaka mingapi kukijenga chama hicho kiuchumi kwa pesa ya walipa kodi wa Tanzania ndio maendeleo ya nchi yaje badae?nikiyakumbuka haya naamua kusimama na mama 2025
Ningesema una fikra potofu kama wengi wasiokuwa na uelewa, lakini kwa mtu kama wewe, siyo fikra potofu, bali ni kupigania maslahi yanayopatikana toka huko CCM.

CHADEMA kuiondoa CCM haina maana na wao wabakie madarakani kwa ung'ang'anizi kama wanavyofanya CCM.
Kipaumbele sasa hivi ni jinsi ya kuiondoa CCM madarakani, ili tuanze safari mpya bila ya CCM.
Hata chama cha mzee Rungwe kingejitutumua na kuiondoa CCM, ni bora zaidi.

Sasa najua kwa mtu kama wewe huwezi/hutaki kuyaelewa haya.

Sasa mnataka hadi iweje, tuwalilie ili ya Gabon yaje hapa?
 
Ningesema una fikra potofu kama wengi wasiokuwa na uelewa, lakini kwa mtu kama wewe, siyo fikra potofu, bali ni kupigania maslahi yanayopatikana toka huko CCM.

CHADEMA kuiondoa CCM haina maana na wao wabakie madarakani kwa ung'ang'anizi kama wanavyofanya CCM.
Kipaumbele sasa hivi ni jinsi ya kuiondoa CCM madarakani, ili tuanze safari mpya bila ya CCM.
Hata chama cha mzee Rungwe kingejitutumua na kuiondoa CCM, ni bora zaidi.

Sasa najua kwa mtu kama wewe huwezi/hutaki kuyaelewa haya.

Sasa mnataka hadi iweje, tuwalilie ili ya Gabon yaje hapa?
Hujanielewa sehemu mkuu wasiwasi wangu ni kwamba je hicho chama pinzani kikija unahisi kitaweka maendeleo ya nchi mbele kuliko maendeleo ya chama?wote ndo walewale kujilimbikizia mali ndio kipaumbele
 
Hujanielewa sehemu mkuu wasiwasi wangu ni kwamba je hicho chama pinzani kikija unahisi kitaweka maendeleo ya nchi mbele kuliko maendeleo ya chama?wote ndo walewale kujilimbikizia mali ndio kipaumbele
Nilikuelewa vizuri tu, ila naona ni wewe hutaki kuelewa ninayoeleza mimi.
Ni hivi: Tuweke "maendeleo ya nchi" pembeni kwanza; kwani tayari tunajua, chini ya CCM hata ikiendelea kuwepo madarakani miaka mia moja, kama ilivyo hivi sasa maendeleo ya nchi itabaki kuwa hadithi tu.

Nasema kuwa CHADEMA, au chama kingine chochote cha siasa, au hata nje ya siasa, kipaumbele kwa sasa ni kuiondoa CCM, ambayo imekataa kuondoka kwa hiari, kwa kutumia njia mbalimbali zisizo halali kubaki madarakani.

Kwa sasa hivi, ni CHADEMA pekee wanaoonyesha dalili kidogo ya kuwa na uwezo huo, wa kuiondoa CCM. Hiyo ndiyo kazi tunayotaka waifanye.
Hayo ya kuleta maendeleo, tutashughulika nayo baada ya hili la kutokuwepo madarakani CCM.
 
Hakudhaniwa kuwa msemaji mkuu wa serikali. Kikeke alambishwe tu ukuu wa wilaya and then aje apate appontment nyingine kubwa kulingana carier yake. TBC ipo anaweza kuwa bosi huko na Rioba akapanda ngazi ya juu
 
View attachment 2769068

Na Kevin Lameck

Kama ipo sehemu ambayo Rais Samia Suluhu Hassan amepatia katika teuzi zake za karibuni, bhasi miongoni mwake ni uteuzi wa sasa wa kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Gerson Msigwa.

Bwana Mobhare Matinyi, Mkuu wa wilaya ya Temeke ameteuliwa kuwa Msemaji mkuu wa serikali na Mkurugenzi wa Idara ya habari - Maelezo.

Kabla ya kuwa Mkuu wa Wilaya mwezi wa saba mwaka huu, Mwanahabari huyu kitaaluma, alikuwa akitumika kwenye jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika maarufu kama SADC.

Muda mfupi kabla ya uteuzi huu, wiki iliyopita, nikiri kuwa nilibahatika kuzungumza naye kupitia kipindi chetu cha runinga kiitwacho #TheBantu sambamba na mazungumzo mafupi baada ya kipindi.

Bahati iliyoje kuwa tuligusia pia kuhusu sehemu muhimu ya mawasiliano na mahusiano ya umma kwa serikali ya Rais Samia na namna ilivyo muhimu katika kujenga picha na sifa nzuri ya serikali.

Nitasema machache kumuhusu ili kuchagiza maoni yangu ya awali kuhusu ubora na uzuri wa uteuzi huu wa Bwana Matinyi.

Mosi, Mh. Matinyi ana exposure ya juu sana ambayo ni nadra kuikuta kwa viongozi wengi wa sasa. Nafasi alizopita awali kuanzia kwenye uandishi wa habari, Uhariri mkuu wa magazeti kadhaa na kwenye jumuiya za kimataifa kumemfanya kuwa na utashi,m na mwenye kujaa maarifa na taarifa nyingi zilizomjengea upekee wa aina yake.

Pili; Mh. Matinyi ana uelewa mpana kuhusu siasa za ndani ya nchi, za jumuiya za kimataifa pamoja na hadhira yake kwa ujumla. Suala hili litampa wakati mzuri kuwa msaada kwa Rais na Chama chake katika kushauri na kuupasha umma taarifa zenye kujitosheleza katika urari wa habari na mawasiliano ya umma.

Tatu; Mh Matinyi ni mzungumzaji mzuri sana. Anajua kupangilia na kuumba maneno vyema akiongozwa na hekima ya kufahamu cha kusema na kisemwe wakati gani.

Nne;Mh Matinyi ni msikilizaji mzuri sana wa maoni ya watu. Kwa takribani muda wote niliokuwa naye alielekeza masikio yake zaidi kwangu kusikiliza na kujaribu kupata mtazamo na maoni mbalimbali na kutamani kusikia ninavyoyaangalia mambo.

Mwisho,Niliuona uwezo wake pia mkubwa katika nidhamu na kufuatilia masuala mbalimbali yahusuyo kazi yake. Sio kiongozi wa kukaa ofisini. Wingi wa taarifa alizonazo kuhusu wilaya yake kwa miezi mitatu tu aliyotumika kama Mkuu wa Wilaya ulitosha kuonesha namna ambavyo si kiongozi wa kupokea taarifa tu ofisini.

Kwa muda wa miezi mitatu ya uDC ameiacha Temeke ikiwa kinara wa usafi miongoni mwa wilaya tano za Dar es salaam, Amefanikiwa kuhuisha data za kodi kwa wafanyabiashara wote wa Temeke, amewezesha pia ongezeko la makusanyo ya kodi na usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo.

Aidha Mobhare aliwezesha mpangilio mzuri wa wafanya biashara wadogo maarufu kama Machinga , bila ya kutumia nguvu na hatukumsikia popote akilumbana na wahusika ama waathirika wa mageuzi mbalimbali huko wilayani Temeke.


Msingi wake mkubwa umekuwa ni kutoa elimu ya ufahamu kwa wananchi na kuacha wahusika wajiongoze na kujiiamulie mambo yao katika namna nzuri kulingana na matakwa ya serikali.


Kila la Kheri Comrade Matinyi Mobhare.


[emoji1241][emoji1241][emoji1241]

Ndugu yangu. Hizo sifa zote ulizompatia kama hana ushawishi “orator” wa kusikilizwa ni kazi bure. Ndo maana unaona ZnZ walimchukua Charles Hilary. Salim Kikeke alikua mtu sahihi kwa sababu ana ushawishi wa kusikilizwa na kifuatiliwa
 
Huyu jamaa hata hajawahi kusikika popote duuuh hii noma sasa si atakua ana-mute tu mda wote maana sio mpigadomo km Ally Kamwe Mo Ally na wengine ambao ni 'Wasemaji' huwezi kua msemaji alafu haujui kupigadomo
Mobare matinyi ni mwandishi nguli labda wewe ndio hujamsikia ,usemaji wa serikali hauhitaji domo kama wafanyavyo kina kamwe na manara ile ni nafasi ya kuisemea serikali mambo ya msingi
 
Back
Top Bottom