Modi kamchana live Puttin uso kwa uso bila kupepesa macho

Mnafiki wa kwanza ni PM Modi na India yake, wana endelea kufadhili OP ya Russia kupitia ununuzi wao mkubwa wa gas na oil hao ndio wanafiki wakubwa wala sio Russia.
 
Siasa tu hizo kuzuga mapopoma, angekua anamaanisha angeacha ushirikiano wa aina yeyote na mrusi
 
Wewe umefika ukraine?...ukweli mchungu russia kapigika sasa hiv anaomba mazungumzo ajiondoe ukraine dogo hataki
 
Jamaa anasema urusi itafilisika wakati mpaka wamarekani wanaendelea kununua baadhi ya bidhaa kutoka urusi hapo.bado nchi za ulaya wananunua mafuta na SASA hivi nchi za Asia zinashindana kununua mafuta ya urusi.
Jifariji tu[emoji12]
 
Inshu sio hiyo, ili kuingia vitani lazima kuna malengo yaliyokufanya uingie katika vita hiyo, na mwisho wa siku tutaangalia je hayo malengo umeyafikia?kama URUSI kila siku vita hiyo ina mgharimu karibia dola bilioni moja, leo ni miezi 7!!ni kiasi gani ametumia?na hakuna alichofanikiwa kukupata hadi sasa, labda kama lengo lake lilikuwa ni kuharibu miundo mbinu na kuua watu lakini hakusema!!na pesa zake zilizoko nje ndizo zitatumika kuijenga upya ukraine!!na kinachoendelea hata ile KRIMEA, aliyoichukua mwaka 2014, sasa inaenda kurudi ukraine haya sasa hapo nani mwenye hasara?
 
Nipe darasa hapa mtumishi.
Russia, Iran, the Orientals na possibly Turkey have an appointment with a destiny.

Ezekiel 38-39 is the answer
Sample: Ezekiel 38
1Neno la BWANA likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, kaza uso wako, umwelekee Gogu, wa nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki, na Tubali, ukatabiri juu yake, 3useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe Gogu, mkuu wa Roshi, na Mesheki, na Tubali; 4 nami nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako, nami nitakutoa, pamoja na jeshi lako lote, farasi na hao wapandao farasi, wote wamevaa silaha za namna zote, jeshi kubwa sana, wenye ngao na kigao, wote wakishika upanga; 5Uajemi, na Kushi, na Putu, pamoja nao; wote wana ngao na chapeo; 6 Gomeri, na vikosi vyake vyote; nyumba ya Togarma, pande za mwisho za kaskazini, na vikosi vyake vyote; naam, watu wengi pamoja nawe.

7 Ujiweke tayari, naam, jiweke tayari, wewe na majeshi yako yote waliokuzunguka, nawe uwe jemadari wao. 8 Na baada ya siku nyingi utakusanywa; katika miaka ya mwisho, utaingia nchi iliyorudishiwa hali yake ya kwanza, baada ya kupigwa kwa upanga, iliyokusanywa toka kabila nyingi za watu, juu ya milima ya Israeli, iliyokuwa ukiwa wa daima; lakini imetolewa katika makabila ya watu, nao watakaa salama salimini wote pia. 9 Nawe utapaa juu, utakuja kama tufani, utakuwa kama wingu kuifunika nchi, wewe, na vikosi vyako vyote, na kabila nyingi za watu pamoja nawe.

10Bwana MUNGU asema hivi; Itakuwa katika siku hiyo, mawazo yataingia moyoni mwako, nawe utakusudia kusudi baya; 11 nawe utasema, Nitapanda juu niiendee nchi yenye vijiji visivyo na maboma; nitawaendea watu wanaostarehe, wanaokaa salama, wote wakikaa pasipo kuta, ambao hawana makomeo wala malango; 12ili kuteka mateka, na kuwinda mawindo; uugeuze mkono wako juu ya mahali palipoharibika, ambapo sasa panakaliwa na watu, na juu ya watu waliokusanyika toka mataifa, waliopata ng'ombe na mali, wakaao katikati ya dunia. 13 Sheba, na Dedani, na wafanya biashara wa Tarshishi, pamoja na wanasimba wake wote, watakuambia, Je! Umekuja kuteka mateka? Umekusanya jeshi lako, ili kuwinda mawindo? Kuchukua fedha na dhahabu, kuchukua ng'ombe na mali, kuteka kiasi kikubwa cha nyara?

14 Basi, mwanadamu, tabiri, umwambie Gogu, Bwana MUNGU asema hivi; Katika siku ile watu wangu, Israeli, watakapokaa salama, hutapata habari? 15 Nawe utakuja kutoka mahali pako, kutoka pande za mwisho za kaskazini, wewe, na watu wa kabila nyingi pamoja nawe, wote wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, na jeshi kuu; 16 nawe utapanda juu uwajie watu wangu, Israeli, kama wingu likiifunika nchi; itakuwa katika siku za mwisho, nitakuleta upigane na nchi yangu, ili mataifa wanijue, nitakapotakaswa kupitia kwako, Ewe Gogu, mbele ya macho yao.

Hiyo hapo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…