Mohamed Said alifungwa wakati wa Nyerere, asamehewa wakati wa Rais Samia

Aache porojo na kutafuta huruma kwa baadhi ya makundi! Kimsingi huyu alikuwa ni mhalifu tu kama wahalifu wengine. Ashukuru alipata hata huo msamaha.

Yaani kirahisi tu uende na silaha bar, huku umeiweka kwenye begi! Unakunywa pombe! Unalewa! Baadaye unaondoka kwenda kujisaidia, huku begi umeliacha mezani! Unarudi na kuendelea tu kunywa! Mwishoni unakuta begi na silaha havipo!!

Uzembe wa aina gani huu kwa mtu anayeitwa Mwanajeshi?
 
Yaani utoke Lindo uingie mtaani kulewa na silaha?,halafu aseme alionewa kwa kuibiwa silaha halafu ikatumike kufanyia uharifu?

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
Mohamed Said aseme tu ukweli kuwa alikodisha silaha na vitambulisho vyake Kwa ma-jambazi wakatekeleza tukio!
Huwezi kukodisha silaha na vitambulisho, no way. Theory ni kwamba alikimbizwa au aliondoka eneo la tukio kwa haraka kiasi begi lenye vitambulisho likabaki, na pia silaha ikabaki. Lakini najiuliza, hao wahudumu wa Bar hawakwenda kutoa ushahidi kwamba walimuona akija na hilo begi na ghafla hawakuliona? Pengine ingemsaidia
 
Kwamba aliporudi hata hakugundua kwamba begi halipo, hadi baadaeeee, hapo ndio nimechoka; maana yake huyu hata angeweza kurudi nyumbani bila hilo begi, akalala hadi asubuhi ndio akashtuka kaacha begi bar..
 
Adhabu aliyopewa alistahili
 

Inafikilisha kwa kweli.. watu waliiba kibegi chake siku hiyo hiyo na wakaenda kupigia tukio siku hiyo hiyo.. jamaa inabidi amshukuru MAMA
 
Anasema kulikuwa na watu wengine waliohusika na tukio walikuwa nje so pengine ndio waliocheza na mashahidi.
 
Kuna ukweli kaamua kuuficha.Nahisi alikuwa mhalifu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…