Morogoro: Mauaji ya wakulima na wafugaji, IGP Wambura aagiza askari wapishe uchunguzi

Morogoro: Mauaji ya wakulima na wafugaji, IGP Wambura aagiza askari wapishe uchunguzi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
1666600785798.png

1666600818516.png


IGP Camillus Wambura ametoa maagizo hayo kutokana na watu wawili kuuawa kwa silaha za moto na wawili kujeruhiwa wakati Polisi wakizuia vurugu Kijiji cha Ikwambi Kata ya Mofu, Wilaya ya Kilombero, Oktoba 23, 2022.

IGP Wambura amesema “Nimeunda Tume Huru kuchunguza vurugu zinazotokea, lengo kujua nguvu iliyotumika kama kudhibiti ilikuwa inaendana na uhalisia, askari wote waliohusika wakae kando na ikibainika kuna uzembe au mapungufu hatua za kisheria zitachukuliwa.”

Awali, ilidaiwa baadhi ya wananchi walichoma moto ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Mofu ikielezwa hawaridhishwi na maamuzi yanayotolewa na viongozi wakati wa utatuzi wa migogoro ya wakulima na wafugaji.

Pia soma: Morogoro: Wananchi wachoma ofisi ya kijiji Kilombero, wawili wauawa
 
Mwenyenzi Mungu Mtakatifu akubariki sana na kukupa uhai Mrefu IGP umetumia Busara na Hekima kubwa sana
Nakutakia majukumu Mema ni Mimi Mkulima wa Kahawa Moshi Kibosho
 
Jeshi la polisi nchi hii lilishapoteza mwelekeo na kudhani mabavu ya kutumia risasi ndiyo suluhisho ya kila kitu kinachojitokeza mbele yao!
 
“Nimeunda Tume Huru kuchunguza vurugu zinazotokea, lengo kujua nguvu iliyotumika kama kudhibiti ilikuwa inaendana na uhalisia, askari wote waliohusika wakae kando na ikibainika kuna uzembe au mapungufu hatua za kisheria zitachukuliwa.”

composition ya hiyo "tume" haiwezi kuwa urukama inatoka kwako na DPP, never! Weka independent people, eg retired judger, TLS rep, Wakili binafsi, mkulima 2. mfugaji 2, dini etc.
 
Maigizo tu haya , polisi waue then wajichunguze wenyewe, hii imekaaje? any way yetu macho katika hili, mtakumbuka hata ile ripoti aliyoipeleka Diblo dibala kwa Rais, hakuna kilichoendelea maana ungeiona ungeshangaa, yaani watu wanaua wanachinja wanafira wanafanya kila aina ya uhuni kisa wamevaa uniforms za polisi, katika hili ni kuomba Alah aingilie kati tu maana hakuna msaada. Watu wanaonewa sana na wenye mamlaka hawana habari kabisaaaa
 
... wafugaji wasipothibitiwa sio tu watapelekea unnecessary social unrests nchini, bali pia ni janga kubwa la kimazingira. Huko walikotoka (usukumani na umasaini) walishaharibu mazingira kwa kiwango cha kitisha, sasa wanaenda kuharibu kwingineko alimradi nchi yote igeuke jangwa!
 
... wafugaji wasipothibitiwa sio tu watapelekea unnecessary social unrests nchini, bali pia ni janga kubwa la kimazingira. Huko walikotoka (usukumani na umasaini) walishaharibu mazingira kwa kiwango cha kitisha, sasa wanaenda kuharibu kwingineko alimradi nchi yote igeuke jangwa!
Kule ni wamang'ati ,ni jamii za kimasai ,na ni wakorofi sana
 
Kule ni wamang'ati ,ni jamii za kimasai ,na ni wakorofi sana
... wote hao; wameharibu sana mazingira kwao huko then wanakimbilia maeneo mengine kuyaharibu. Bila kuwadhibiti nchi itageuka jangwa hii.
 

IGP Camillus Wambura ametoa maagizo hayo kutokana na watu wawili kuuawa kwa silaha za moto na wawili kujeruhiwa wakati Polisi wakizuia vurugu Kijiji cha Ikwambi Kata ya Mofu, Wilaya ya Kilombero, Oktoba 23, 2022.

IGP Wambura amesema “Nimeunda Tume Huru kuchunguza vurugu zinazotokea, lengo kujua nguvu iliyotumika kama kudhibiti ilikuwa inaendana na uhalisia, askari wote waliohusika wakae kando na ikibainika kuna uzembe au mapungufu hatua za kisheria zitachukuliwa.”

Awali, ilidaiwa baadhi ya wananchi walichoma moto ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Mofu ikielezwa hawaridhishwi na maamuzi yanayotolewa na viongozi wakati wa utatuzi wa migogoro ya wakulima na wafugaji.

Pia soma: Morogoro: Wananchi wachoma ofisi ya kijiji Kilombero, wawili wauawa
Nilishasema hii hama hama ya wasukuma na kuvamia maeneo ya watu italeta shida sana na bado wanafyatua kama nguruwe.
 
... wote hao; wameharibu sana mazingira kwao huko then wanakimbilia maeneo mengine kuyaharibu. Bila kuwadhibiti nchi itageuka jangwa hii.
Yaan nimeona hii katika tarafa moja inaiitwa mwaya huko mahenge.wafugaji wakisukuma wanashindana kufyeka miti tena kuelekea milimani.unashangaa kuna uongozi tokea katibu tarafa hadi kijiji,lakini hatua wala karipio lolote limefanywa

Sent from my Redmi Y1 using JamiiForums mobile app
 
Viongozi wa vijiji na police walioko kwenye migogoro hii ya wafugaji na wakulima ni wala rushwa wakubwa na wafugaji ndiyo wanaowahonga ndiyo maana migogoro ya wakulima na wafugaji haikomi kwa sababu wenye mamlaka wanapewa mlungula.
 
Sawa, mmeunda Timu ya kuchunguza mauaji ya Raia,
vipi kuhusu kiini cha Tatizo , mgogoro wa wakulima na wafugaji ? kwanini hamtumii sheria na sheria zipo.
huu mtindo wenu wa kujifanya mnatatua hili tatizo kwa kutumia busara na kuacha kutumia sheria , hayaa !
 
Jamii ya wakulima vs jamii ya wafugaji vs jamii ya polisi. Jamii ya polisi wamezoea kuua.
 
Back
Top Bottom