Morogoro ndio mkoa uliotoa vipaji vingi Tanzania kuliko mikoa mingine.

Morogoro ndio mkoa uliotoa vipaji vingi Tanzania kuliko mikoa mingine.

Ni mkoa mzuri sana na wenye vipaji lukuki lakini naungana na MINOCYCLINE hapo juu kwa hoja alizotoa maana ni ukweli mtupu,japokuwa vipaji ni kweli vipo aisee maana tukiangalia nyanja hizi tunapata jibu...

1.Kisoka...
Ukiachana na timu za Dar Morogoro inafuatia kuwa na timu nyingu zilizowahi kutwaa taji la ligi kuu nazo ni Mtibwa Sugar na Mseto ukiachana na Tukuyu stars ya Mbeya hakuna mkoa uliowah kufanya hivyo hapa Tz..na kuna timu ilikuwa inaitwa reli "kiboko ya vigogo" Simba na Yanga zilikuwa hazitoki zikicheza na timu hii

Morogoro ni nyumba ya vipaji vya soka tangu zamani Kina Mohamed Msomali,Malota Soma,Zamoyoni Mogella,Charles Boniface Mkwasa(alilelewa na dada yake mtaa wa karume Morogoro tangu akiwa kijana mdogo) na wengineo magwiji wa zamani,kwa sasa wapo kina Mkude kibabage,Dickson Job,Aishi Manula,Kelvin wa Genk,Shomari Kapombe,Kibwana Shomari n.k
2.Ngumi
Hakuna asiyejua kwamba ukitoa Dar Moro ina ufalme wake katika ngumi Francis Cheka,Cosmas Cheka,Twaha Kiduku,Mandonga na wengine kibao wanatoka Moro
3.Muziki
Zamani watu dansi walikuwa wanalifuata Moro kutoka dar kuja kuwaona Cuban Marimba ya Salum abdallah na baadae Juma Kilaza na Moro Jazz ya Mbaraka Mimi Mwishehe,,Wasanii wa Moro kwa sasa ni Rich Mavoco,Jay Melody,Belle 9,Dayna,Conboi,Tundaman na wengineo hata Salam, Babu Tale wanatokea Moro

Mwandishi wa comment hii aliishi Moro kuanzia 1982-1993
Ahahaha,mkuu uliishi Moro mitaa gani,
 
Tunaongelea talent kuanzia 1961 mpaka leo hebu wataje?
1.Sumalee
2 Cpwaa{halifa ilunga}
3 Matonya{Sefu Shabani}
4 Kassim Mganga
5 Wagosi wa Kaya
6 Ring 2be aka Pete{Rashidi Ngayama}
7 Mwana FA{Hamisi Mwinjuma}
8 Bwana Misosi
9 Q Chilla{Abubakari Katwila}
10 MB Doggy{Mbwana}
11 R.O.M.A{Ibrahim Mussa}
12 Top C
13 Dr Karim
14 John Walker
15 Gelly wa rhym
16 Hemed Phd{Hemed Suleiman}
17 Sharomillionear{Mohamed Mtikey}
18 Danny Msimamo
19.kusah
20.ruby
21.platfom Tz
22.producer bonga
23.y Dash
24.TNG SQUARD jimbo bongo.com iikuwa National anthem
25.mwandei
List ni ndefu haya leta hapa hiyo ni bongo fleva sijafika kweny band ,dance wala taarabu
 
Mkoa wa morogoro ndio tunu ya sanaa, burudani na michezo. Huo mkoa umetoa vipaji adhimu na adimu sana na ndio tegemeo kubwa kwa taifa kwenye kuzalisha burudani na michezo.

Hapo Morogoro wametoka akina Albert Mangwea, mbaraka mwinshehe, twaha kiduku, francis Cheka, shomari kapombe n.k.

Huwezi kwa sasa Tanzania kuulinganisha mkoa wa morogoro kwenye burudani na michezo na mkoa wowote ule hata kigoma bado ipo mbali na itasubiri kwa morogoro

Kigoma unaiacha wapi?
 
Morogoro ni namba moja, hilo nadhani halina mjadala.
Miaka ya tisini tulikuwa tunaenda uwanja wa jamuhuri kuangalia mpira,Sasa tunakuwa hatuna pesa ya kiingilio, tukawa tunapenya kwenye mifereji ya kutolea maji nje ya uwanja, tulikuwa na hatari, Kuna mshkaji mmoja alivunjikaga mguu, alipanda ukuta wa uwanja kwa nje hili aingie ndani ya uwanja, eeh bwana hile anamaliza ukuta kwa ndani akachezea virungu vya Askari akajikuta amedondokea Tena nje na kuvunjika miguu,

Nilikuwaga na mshkaji wangu mmoja alikuwaga Refa wa ligi kuu,sijui alifiaga wapi yule mwamba, alikuwa anaitwa Mwarabu mumba
 
Linapokuja suala la burudani hususani muziki, Kigoma iko sayari ya 7 kutoka sayari ya Tanzania.

Tangu huko nyuma kuna wasanii wengi nguli kama akina Bichuka n.k, hivyo vyovyote utakavyo linganisha, Kigoma hailinganishwi na mkoa wowote.

Ni sawa uilinganishe Mbeya na mkoa wowote kwenye masuala ya Ukristo(uimbaji wa Gospel, idadi ya nyumba za ibada n.k), hapo unakuwa unajilisha upepo maana ina watu ngulii haswaa kibao ambao mikoa mingine hawapo.
Morogoro jazz band
Ilianzishwa mwaka 1930 ndio band yakwanza Tanzania nzima na ndio chimbuko la band zote Tanzania. Mziki ulizaliwa morogoro na mpira ulizaliwa morogoro wengine wote wanafata.
Hata Fifa pia ilizaliwa Morogoro.
 
Mwenye listi kamili ya Morogoro kuanzia kwa akina Hayati Mbaraka Mwinshehe tunaomba aiweke hapa.
 
Mkoa wa morogoro ndio tunu ya sanaa, burudani na michezo. Huo mkoa umetoa vipaji adhimu na adimu sana na ndio tegemeo kubwa kwa taifa kwenye kuzalisha burudani na michezo.

Hapo Morogoro wametoka akina Albert Mangwea, mbaraka mwinshehe, twaha kiduku, francis Cheka, shomari kapombe n.k.

Huwezi kwa sasa Tanzania kuulinganisha mkoa wa morogoro kwenye burudani na michezo na mkoa wowote ule hata kigoma bado ipo mbali na itasubiri kwa morogoro

Vipaji gani? Vya kama wakina Thomas Edson?
 
Mwenye listi kamili ya Morogoro kuanzia kwa akina Hayati Mbaraka Mwinshehe tunaomba aiweke hapa.
😂😂😂 Msanii mkubwa ni afande Sela nakutajia vijana wa ngumi wawili Tena wadigo wakipigana nje mwakinyo na Salim mtango

Tanga ni talents walimake hit ukikuta top ten ya ngoma mb Tanga wasanii hata wanne enzi izo tuongee ukweli ,nilikuwa enzi nakaa Tanga nawaona sana wakina j plus sijui na seba Kuna jamaa alikuwa anaitwa kaini wakifanya mazoezi ya movie pal mkwakwani kipind icho chuchu hansy ni mdogo sana na mzee majuto akiigiza standup comedy pale majestic
 
Tukuyu nayo ilitupa ule Mwamba Godwin Aswille kwa ujumla Bongo Kauntri inavipaji.
 
Tanga vipaji vipo ila sio level za morogoro kwa maana morogoro haijawahi kupokoa hata siku moja kwenye kuzalisha vipaji?
 
Ukiangalia kwenye mabingwa wa nchi upande wa soka ukizitoa timu za dar ni morogoro inafata kwenye kutwa ubingwa.
 
Haya jazz nyingi wakati huo ziliundwa morogoro hata dar ikiwa bado haijachangamka.
 
Back
Top Bottom