Mpambano wa Freeman Mbowe na Tundu Lissu: Wajue wagombea hawa wawili

Hoja mojawapo ni kuwa Mbowe kafikia mwisho wa kukalia kiti hicho, na hili ni takwa la wakati. Mgombea wangu kashasema akipata hiyo nafasi atafanya nini. Ifahamike kuambiwa ukweli si kuchafuliwa.
 
Wajumbe wafanye wafanyavyo wanachadema wanamtaka tundu lissu, wakikosea watakuwa wamekizika chama rasmi.
 
..sawa mkuu, endeleeni kushupaza shingo, chadema isikilize maoni ya umma, chama kinaweza endelea kubaki kwa msajili kikafa huku mtaani
 
Wapi Molemo Media imetukana mgombea? Unaweza kuripoti kwa Moderators wakaondoa hayo matusi?
 
Wajumbe wafanye wafanyavyo wanachadema wanamtaka tundu lissu, wakikosea watakuwa wamekizika chama rasmi.
Wajumbe hawatachagua mgombea kwa kushurutishwa wala kwa matusi bali kwa hekima na busara wakitizama chama chao kwa miaka 5 ijayo.

Ni vyema sasa wagombea wakajikita kutangaza sera zao bila kukashifu upande wowote
 
..sawa mkuu, endeleeni kushupaza shingo, chadema isikilize maoni ya umma, chama kinaweza endelea kubaki kwa msajili kikafa huku mtaani
Wala Chadema haiwezi kufa kwa sababu chama ni cha wanachama na siyo viongozi.Yeyote atakayechaguliwa ataungwa mkono na wananchi kwani ndivyo demokrasia inavyotutaka kuwa
 
Hoja mojawapo ni kuwa Mbowe kafikia mwisho wa kukalia kiti hicho, na hili ni takwa la wakati. Mgombea wangu kashasema akipata hiyo nafasi atafanya nini. Ifahamike kuambiwa ukweli si kuchafuliwa.
Ni vizuri sasa kwa vile umesema una mgombea wako ukamshauri ajikite kushawishi wajumbe wa mkutano mkuu wampe ridhaa.Kushinda uchaguzi ni ushawishi wa hoja na sera.Bila kufafanua vizuri sera zako unaweza usieleweke vyema.
 
Tunasubiria kwa hamu,hakika CDM imekuwa gumzo kila mahali.
Ni kweli kabisa imekuwa gumzo, nchi nzima imejikita kuzungumzia uchaguzi wa Chaddma hasa kwa ushawishi wa wagombea wake

Molemo media itajitahidi kufanya mahojiano na wagombea wote
 
Unaweza kuonyesha hata mstari mmoja tumeandika kwenye taarifa hii halina ukweli?
Sana. Mtu yeyote mwenye uhuru wa akili ataona kasoro kubwa kwenye andiko hilo. Ila kwa kuwa wewe tayari umejifunga pingu upande huo, kamwe huwezi ona tofauti na hayo unayo yafikiri wewe.
 
Unaweza kuweka haba utafiti wako usiotia shaka kwamba yatatokea uliyoyaandika.Kwa sasa Chadema kimekuwa kikubwa kuliko personalities.Aondoke Freeman au Tundu chama hiki hakiwezi kufa kiko mioyoni mwa watu
LOooh!
Mkuu 'Molemo, ni bora ulijipumzisha kuingia humu JF; kwa sababu inaelekea huko uliko sasa kunakuonyesha utofauti na dunia ya sasa ilivyo huku.
CHADEMA ina hali mbaya sana wakati huu. Ipo ukingoni kabisa. Ikikosea tu kidogo kumbakisha Mbowe; kazi itakuwa imekwisha.
 
Sana. Mtu yeyote mwenye uhuru wa akili ataona kasoro kubwa kwenye andiko hilo. Ila kwa kuwa wewe tayari umejifunga pingu upande huo, kamwe huwezi ona tofauti na hayo unayo yafikiri wewe.
Msomaji wetu tumesema onyesha jambo lolote ambalo si la kweli tuliloliandika

Molemo media tutaendelea kutoa habari kwa uhuru bila kuhofia yeyote kwa sababu tunaamini huo ndiyo ukweli
 
Tukukumbushe tu mwaka 2016 kuna kiongozi alitabiri Chadema itakufa kabla ya 2020

Naona na wewe unatabiri kama huyo kiongozi, tukuhakikishie tu wewe siyo Mungu kutaka kusema hivyo.

Chama hiki kimejengwa mioyoni mwa watu.Kudhani kitakufa unajidanganya sana.Binafsi nimetoka ziara Katavi ya wiki 3 kuna maelfu ya wanachadema wala hawana habari na vituko mnavyoandika mitandaoni.

Wanachama wa ukweli vijijini wala hawana habari ya upuuzi unaoitwa makundi
 
Mdahalo wa Chief Odemba ujibu haya:
Who, did, what , when and how? Hiyo iwe ni cross examination kwa wote- Mbowe na Lissu katika nyanja zote za contentious issues, vinginevyo itakuwa ni kupuyanga tu.
 
Mdahalo wa Chief Odemba ujibu haya:
Who, did, what , when and how? Hiyo iwe ni cross examination kwa wote- Mbowe na Lissu katika nyanja zote za contentious issues, vinginevyo itakuwa ni kupuyanga tu.
Kuna watu wenye busara na heshima katika jamii Molemo media ilizungumza nao na wakashauri mdahalo huo usifanyike

Sababu wanayotoa ni kwamba mdahalo huo uaweza kutumika kupakana matope na kusingiziana uongo usiomithilika.

Pia kuna hofu mdahalo huo unaweza kutumika kuanika siri za chama na kukitia doa chama hicho
 
.......

Freeman Mbowe mwanasiasa mfanyabiashara mwenye ukwasi mkubwa mpaka sasa anaungwa mkono na wenyeviti 9 wa Kanda kati ya 10 waliopo huku pia akiungwa mkono na wenyeviti wa mikoa 24 kati ya 30 iliyopo.....
Kwa hiyo wapiga kura ni hao wenyeviti 10 wa kanda na wenyeviti 30 wa mikoa!!!???
 
Molemo Media inakushauri kutumia njia mbalimbali kushawishi wajumbe wa mkutano mkuu kumpigia kura mgombea unayempenda.
Njia mbalimbali kushawishi wajumbe wa mkutano mkuu kumpigia kura mgombea ni pamoja na kutoa rushwa na vitisho!!?

Mimi nasubiria clips za watu wanavyoshawishi wajumbe kwa rushwa zianze kutolewa ndio watu mtaumbuka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…