Hoja mojawapo ni kuwa Mbowe kafikia mwisho wa kukalia kiti hicho, na hili ni takwa la wakati. Mgombea wangu kashasema akipata hiyo nafasi atafanya nini. Ifahamike kuambiwa ukweli si kuchafuliwa.Molemo Media inakushauri kutumia njia mbalimbali kushawishi wajumbe wa mkutano mkuu kumpigia kura mgombea unayempenda.
Pia ni vizuri wagombea wetu wakajikita kutoa sera nzuri ili kushawushi wapiga kura na kuachana na mtindo wa kuchafuana na kutuhumiana bila hoja za msingi
Wajumbe wafanye wafanyavyo wanachadema wanamtaka tundu lissu, wakikosea watakuwa wamekizika chama rasmi.Ilikuwa kama utani na ilianza tetesi kwamba Tundu Lissu ameamua kupambana na Mwenyekiti wake ili kumpata kiongozi mpya atakayekiongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo
Sasa ni rasmi mafahali hawa wawili wameingia ulingoni ili kuamua ugomvi wao kupitia sanduku la kura.
Freeman Mbowe amekiongoza chama hicho kwa mafanikio makubwa mpaka zasa kiasi kwamba hata washindani wake wanakosa hoja ya msingi sana ya kushindana naye badala yake zimebaki tu propaganda za hapa na pale.
Freeman Mbowe mwanasiasa mfanyabiashara mwenye ukwasi mkubwa mpaka sasa anaungwa mkono na wenyeviti 9 wa Kanda kati ya 10 waliopo huku pia akiungwa mkono na wenyeviti wa mikoa 24 kati ya 30 iliyopo
Freeman Mbowe amekuwa mwanasiasa na kiongozi mtulivu zaidi, anayesikiliza, anayeshaurika na ambaye hana maneno mengi sana bali vitendo kwa wingi.
Freeman Mbowe ni kiongozi anayesimamia na kuliamini jambo lililopitishwa na vikao hata kama baadhi ya watu watalipinga na mfano mzuri ni maridhiano kati ya chama chake na serikali ya CCM.
Tundu Lissu msanaharakati na mtetezi wa haki za binadamu kwa muda mrefu ametangaza kugombea uenyekiti Chadema miezi mitatu tu tangu kutangaza kugombea Makamo Mwenyekiti wa chama hicho.Hajaweka wazi kwanini ghafla amebadili uamuzi wake
Tundu Lissu mwanasheria aliyebobea ni kiongozi ambaye ana misimamo mikali na ambaye haamini katika maridhiano.
Baadhi ya wapinzani wa Tundu Lissu wanamuona kama ni mtu anayeungwa mkono zaidi na makundi yaliyo nje ya Chadema hasa wanaharakati na watanzania waishio nje ya nchi.
Kingine ambacho wapinzani wa Tundu Lissu wanamwandama nacho ni tabia yake ya kupenda sana kuzungumza sana na vyombo vya habari hasa mitandao ya kijamii kama vile Club House, Spaces, Digital channels nk ambapo imedaiwa amekuwa akizungumza wakati mwingine mambo ya ndani ya chama.
Yote kwa yote msema kweli ni tarehe 21/1/2025 ambapo Mkutano Mkuu utachagua Mwenyekiti mpya kati ya miamba hii miwili ya siasa za Chadema na Tanzania kwa ujumla.
Sisi wa Molemo Media Tutawabarisha mambo mbalimbali kuhusu wagombea hawa kuelekea Januari 21 inayosubiriwa kwa hamu na Watanzania kwa ujumla.
..sawa mkuu, endeleeni kushupaza shingo, chadema isikilize maoni ya umma, chama kinaweza endelea kubaki kwa msajili kikafa huku mtaaniChadema ni chama cha kidemokrasia sanduku la kura ndiyo linaamua.Wala hakuna haja yamalumbano.Wanaopiga kura ni wajumbe wa mkutano mkuu waache waamue juu ya hatma ya chama chao
Kudhani kwamba mmojawapo akishinda Chadema itakufa ni kujidanganya kwa kiwango kikubwa chama hiki kilishavuka level hiyo
Wapi Molemo Media imetukana mgombea? Unaweza kuripoti kwa Moderators wakaondoa hayo matusi?🚮🚮🚮🚮
Nilikuwa nakuheshimu enzi zile wakati una ripoti habari zako lakini kwa andiko lako la Leo nimekushusha thamani yote.
Umeegemea upande mmoja kwa kusifia na upande mwingine umeusiriba tope. Hivi Unaweza ukasimama mtaani na kuanza kumsifia FAM na kumtukana TAL?
Aisee Meku Nimekushusha sana thamani
Wajumbe hawatachagua mgombea kwa kushurutishwa wala kwa matusi bali kwa hekima na busara wakitizama chama chao kwa miaka 5 ijayo.Wajumbe wafanye wafanyavyo wanachadema wanamtaka tundu lissu, wakikosea watakuwa wamekizika chama rasmi.
Daudi ni Tundu LisuGoliath ni nani na Daudi ni nani?
Wala Chadema haiwezi kufa kwa sababu chama ni cha wanachama na siyo viongozi.Yeyote atakayechaguliwa ataungwa mkono na wananchi kwani ndivyo demokrasia inavyotutaka kuwa..sawa mkuu, endeleeni kushupaza shingo, chadema isikilize maoni ya umma, chama kinaweza endelea kubaki kwa msajili kikafa huku mtaani
Ni vizuri sasa kwa vile umesema una mgombea wako ukamshauri ajikite kushawishi wajumbe wa mkutano mkuu wampe ridhaa.Kushinda uchaguzi ni ushawishi wa hoja na sera.Bila kufafanua vizuri sera zako unaweza usieleweke vyema.Hoja mojawapo ni kuwa Mbowe kafikia mwisho wa kukalia kiti hicho, na hili ni takwa la wakati. Mgombea wangu kashasema akipata hiyo nafasi atafanya nini. Ifahamike kuambiwa ukweli si kuchafuliwa.
Tunasubiria kwa hamu,hakika CDM imekuwa gumzo kila mahali.Ni kweli kabisa, baada ya uchaguzi Chadema wanapaswa kuwa imara kuliko mwanzo
Ni kweli kabisa imekuwa gumzo, nchi nzima imejikita kuzungumzia uchaguzi wa Chaddma hasa kwa ushawishi wa wagombea wakeTunasubiria kwa hamu,hakika CDM imekuwa gumzo kila mahali.
Ni vyema ukitoa hoja uwe na ushahidi kidogo, Je CCM ndiyo wamemsaidia Freema kuifanya Chadema ilivyo sasa?Mbowe na ccm lao moja
Sana. Mtu yeyote mwenye uhuru wa akili ataona kasoro kubwa kwenye andiko hilo. Ila kwa kuwa wewe tayari umejifunga pingu upande huo, kamwe huwezi ona tofauti na hayo unayo yafikiri wewe.Unaweza kuonyesha hata mstari mmoja tumeandika kwenye taarifa hii halina ukweli?
LOooh!Unaweza kuweka haba utafiti wako usiotia shaka kwamba yatatokea uliyoyaandika.Kwa sasa Chadema kimekuwa kikubwa kuliko personalities.Aondoke Freeman au Tundu chama hiki hakiwezi kufa kiko mioyoni mwa watu
Msomaji wetu tumesema onyesha jambo lolote ambalo si la kweli tuliloliandikaSana. Mtu yeyote mwenye uhuru wa akili ataona kasoro kubwa kwenye andiko hilo. Ila kwa kuwa wewe tayari umejifunga pingu upande huo, kamwe huwezi ona tofauti na hayo unayo yafikiri wewe.
Tukukumbushe tu mwaka 2016 kuna kiongozi alitabiri Chadema itakufa kabla ya 2020LOooh!
Mkuu 'Molemo, ni bora ulijipumzisha kuingia humu JF; kwa sababu inaelekea huko uliko sasa kunakuonyesha utofauti na dunia ya sasa ilivyo huku.
CHADEMA ina hali mbaya sana wakati huu. Ipo ukingoni kabisa. Ikikosea tu kidogo kumbakisha Mbowe; kazi itakuwa imekwisha.
Kuna watu wenye busara na heshima katika jamii Molemo media ilizungumza nao na wakashauri mdahalo huo usifanyikeMdahalo wa Chief Odemba ujibu haya:
Who, did, what , when and how? Hiyo iwe ni cross examination kwa wote- Mbowe na Lissu katika nyanja zote za contentious issues, vinginevyo itakuwa ni kupuyanga tu.
Kwa hiyo wapiga kura ni hao wenyeviti 10 wa kanda na wenyeviti 30 wa mikoa!!!???.......
Freeman Mbowe mwanasiasa mfanyabiashara mwenye ukwasi mkubwa mpaka sasa anaungwa mkono na wenyeviti 9 wa Kanda kati ya 10 waliopo huku pia akiungwa mkono na wenyeviti wa mikoa 24 kati ya 30 iliyopo.....
Njia mbalimbali kushawishi wajumbe wa mkutano mkuu kumpigia kura mgombea ni pamoja na kutoa rushwa na vitisho!!?Molemo Media inakushauri kutumia njia mbalimbali kushawishi wajumbe wa mkutano mkuu kumpigia kura mgombea unayempenda.