Mpangaji agoma kuhama baada ya mkataba kuisha. Nitumie mbinu gani kumtoa kwenye nyumba yangu?

Mpangaji agoma kuhama baada ya mkataba kuisha. Nitumie mbinu gani kumtoa kwenye nyumba yangu?

Wenye nyumba basi mjue hata hao wapangaji wanatafuta.

Yaani amelipa kodi, amelipa dalali, eti na hela ya mwezi mmoja ya security.

Mpe hela yake hiyo uliyokaa nayo ya security, huo mwezi mmoja aliokaa bure hesabia ni notice.

Hivi mkifa mtaondoka na hizo nyumba ? Muwe na imani pia.

Usifikirie sina nyumba za kupangisha, sawa eeh.
Shangazi Pumbavu huyu
Yaani hana HATA haya ati security
Nyooooooiooo kawapata wajiingaa
 
Nimekwisha fanya mahesabu na yeye kumjulisha ; in fact gharama za matengenezo ni kubwa kuliko deposit yake! Hivyo anadaiwa pamoja na kodi ya nyumba kwa muda wote anaondelea kukaa na funguo!
Kuna vitu vilivyovunjika yaani kama vitasa,komeo?madirisha?ambavyo vinaonekana waziwazi sio kwa hisia.
Mimi nikwambie tu ukweli hasara utakayokuja kuipata mbeleni ni kubwa kuliko hiyo pesa unayoing'ang'ania kuishikilia vitu vingine ni busara tu inahitajika sio kutumia nguvu na ubabe halafu ukizingatia mtu mwenyewe unayeshindana naye ni mwanamke anaweza kukusingizia jambo lolote na watu wakaamini ili apate huruma ya watu na vyombo vya sheria.
Sasa angalia unavyotaabika kaondoka na funguo maana yake hutoweza kupangisha hadi mwezi atakaoamua kurudi sasa hapo hasara ya nani?
Ungemuita tu muyajenge kiungwana aende kwa amani kwani mpangaji ataondoka na nyumba yako?ataondoka yeye nyumba yako atakuachia,biashara ya nyumba hainaga hasara.
 
Mtendaji ataruka vipi wakati kutakuwepo na Mjumbe na Polisi?
Polisi na mjumbe huwa wanakuja tu kishabiki wanajua hawawezi kukosa hela ya maji ila mwisho wa siku kesi ikienda mbele zaidi wanajitoa unabaki peke yako hiyo wala sio dawa.
Hapo mtego wake uko hivi mkienda kuvunja huyo mwanamke ataenda mahakamani kushitaki kwamba amevunjiwa nyumba na imesababisha upotevu wa milioni 20 kwa hivyo atataka alipwe milioni 20 kisha aondoke na vitu vyake.
Baada ya hapo polisi na mjumbe wakiitwa mahakamani watasema sisi tulikuwa mashahidi tu lakini hatuhusiki na chochote kwa hiyo mwenye nyumba ndio anajua kiundani ugomvi wake na mpangaji basi hapo wanakuwa washajitoa unabaki peke yako.
 
Ikiwa ulichotueleza ndo kipo km kilivyo bila ya kuweka udanganyifu basi jambo la kukusaidia kupata stahiki zako ni kufuata taratibu za kumfikisha mahakamani ......hakuna zaidi ya hilo.Maana huyo ni mbabaishaji na anapewa kichwa na wababaishaji wenzake
 
Adhabu yotehiyo ya nini.

Kuna mzee kopindi cha magu. Aliwaambia wapangaji wanangu hali ni ngumu...kila mmoja wenu azingatie mkataba. Ila kama unatatizo niambie usikae kimya.

Kuna binti alimwambia kama huna ukipata utanipa alikaa bure kwa muda na baasae akampa yule mzee kama milioni kama asante.

Wenye nyumba tuishi kwa upendo.wapangaji wanashukran sana wakitendewa ubinadamu
Kuna wapangaji ni jeuri kipindukia badala ya kuwa Walpole wakiwa na shida wanataka kufanya Janja Janja ya kutaka kukwepa kodi! Huwezi kuwasaidia wahuni !
 
Wana BODI naomba ushauri. Wapangaji wangu wote naingia nao mkataba wa miezi sita. Ambao ni renewable .

Katika mkataba kuna kipengele cha security deposit Sawa na kodi ya mwezi ambayo hutumika kutengeneza nyumba mkataba ukiisha.

Mpangaji wangu mmoja single mother mkataba wake ulikwisha mwezi January mwaka huu lakini amegoma kuhama akidai arudishiwe deposit yake ndio ahame kabla nyumba haijakaguliwa ; lakini amekwisha kaa hiyo nyumba mwaka mmoja na nusu na nyumba inahitajika matengenezo.

Amegoma kuondoka na sasa amefunga nyumba na kuacha vitu vyake ndani na kutoweka na funguo!

Ameisha kaa zaidi ya mwezi bila kulipa kodi na hata bill ya maji hajalipa! Nimekwenda serikali ya mtaa kutoa taarifa nao hawana msaada.

Nitumie mbinu gani kumtoa kwenye nyumba yangu?
Acha kutegemea nyumba za kupanga mkuu fanya kazi, ungekuwa na kazi usingelikua na malumbano na wapangaji wako
 
Wenye nyumba basi mjue hata hao wapangaji wanatafuta.

Yaani amelipa kodi, amelipa dalali, eti na hela ya mwezi mmoja ya security.

Mpe hela yake hiyo uliyokaa nayo ya security, huo mwezi mmoja aliokaa bure hesabia ni notice.

Hivi mkifa mtaondoka na hizo nyumba ? Muwe na imani pia.

Usifikirie sina nyumba za kupangisha, sawa eeh.
Mbona povu? Mpangaji?
 
Wenye nyumba basi mjue hata hao wapangaji wanatafuta.

Yaani amelipa kodi, amelipa dalali, eti na hela ya mwezi mmoja ya security.

Mpe hela yake hiyo uliyokaa nayo ya security, huo mwezi mmoja aliokaa bure hesabia ni notice.

Hivi mkifa mtaondoka na hizo nyumba ? Muwe na imani pia.

Usifikirie sina nyumba za kupangisha, sawa eeh.
inaonekana huna nyumba wala hujawai kupangisha mtu wapangaji tunawakabidhi nyumba kwenye mazingira mazuri ila matusi wanayofanya wakati wanaondoka hata io secutity deposit hua haitoshi
 
Polisi na mjumbe huwa wanakuja tu kishabiki wanajua hawawezi kukosa hela ya maji ila mwisho wa siku kesi ikienda mbele zaidi wanajitoa unabaki peke yako hiyo wala sio dawa.
Hapo mtego wake uko hivi mkienda kuvunja huyo mwanamke ataenda mahakamani kushitaki kwamba amevunjiwa nyumba na imesababisha upotevu wa milioni 20 kwa hivyo atataka alipwe milioni 20 kisha aondoke na vitu vyake.
Baada ya hapo polisi na mjumbe wakiitwa mahakamani watasema sisi tulikuwa mashahidi tu lakini hatuhusiki na chochote kwa hiyo mwenye nyumba ndio anajua kiundani ugomvi wake na mpangaji basi hapo wanakuwa washajitoa unabaki peke yako.
Atathibisha vipi kuwa kaibiwa? hizo hela wakati mashahidi walikuwepo wakati vyombo vinatolewa?
 
Wana BODI naomba ushauri. Wapangaji wangu wote naingia nao mkataba wa miezi sita. Ambao ni renewable .

Katika mkataba kuna kipengele cha security deposit Sawa na kodi ya mwezi ambayo hutumika kutengeneza nyumba mkataba ukiisha.

Mpangaji wangu mmoja single mother mkataba wake ulikwisha mwezi January mwaka huu lakini amegoma kuhama akidai arudishiwe deposit yake ndio ahame kabla nyumba haijakaguliwa ; lakini amekwisha kaa hiyo nyumba mwaka mmoja na nusu na nyumba inahitajika matengenezo.

Amegoma kuondoka na sasa amefunga nyumba na kuacha vitu vyake ndani na kutoweka na funguo!

Ameisha kaa zaidi ya mwezi bila kulipa kodi na hata bill ya maji hajalipa! Nimekwenda serikali ya mtaa kutoa taarifa nao hawana msaada.

Nitumie mbinu gani kumtoa kwenye nyumba yangu?
Ninachokiona hapo ni Kuna kutunushiana misuli......na kirahisi rahisi humuwezi na atakusumbua sana ukizingatia status yake ni watu wasiojali ,ikiwa anaweza kufunga nyumba na akaenda kuishi popote na haoni ttzo huyo atakusumbua sana



Suluhisho ni mambo mawili.....mosi,jishushe na ukubali hiyo hasara Ili akurudishie nyumba yako Ili uendelee kufanya biashara na wateja wengine
Pili..fuata taratibu za kumfikisha mahakamani Ili ukapambanie kupata Haki yako ukiwa unatambua kuwa Kuna kupoteza rasilimali muda na fedha zaidi Ili kupata hiyo haki unayoidai



I
 
Polisi na mjumbe huwa wanakuja tu kishabiki wanajua hawawezi kukosa hela ya maji ila mwisho wa siku kesi ikienda mbele zaidi wanajitoa unabaki peke yako hiyo wala sio dawa.
Hapo mtego wake uko hivi mkienda kuvunja huyo mwanamke ataenda mahakamani kushitaki kwamba amevunjiwa nyumba na imesababisha upotevu wa milioni 20 kwa hivyo atataka alipwe milioni 20 kisha aondoke na vitu vyake.
Baada ya hapo polisi na mjumbe wakiitwa mahakamani watasema sisi tulikuwa mashahidi tu lakini hatuhusiki na chochote kwa hiyo mwenye nyumba ndio anajua kiundani ugomvi wake na mpangaji basi hapo wanakuwa washajitoa unabaki peke yako.
Sio kweli. Kodi ikiisha wewe ni mvamizi kwenye eneo la mtu: kwa kifupi huna haki katika eneo hilo.
 
Ninachokiona hapo ni Kuna kutunushiana misuli......na kirahisi rahisi humuwezi na atakusumbua sana ukizingatia status yake ni watu wasiojali ,ikiwa anaweza kufunga nyumba na akaenda kuishi popote na haoni ttzo huyo atakusumbua sana



Suluhisho ni mambo mawili.....mosi,jishushe na ukubali hiyo hasara Ili akurudishie nyumba yako Ili uendelee kufanya biashara na wateja wengine
Pili..fuata taratibu za kumfikisha mahakamani Ili ukapambanie kupata Haki yako ukiwa unatambua kuwa Kuna kupoteza rasilimali muda na fedha zaidi Ili kupata hiyo haki unayoidai



I
Ahsante kwa ushauri. Nadhani Nita Pambana nae mpaka mwisho! Hii ni aina ya utapeli. Ukimuachia Huyu atazoea na kumfanyia mtu mwingine.
 
Deposit ya nyokweeee 😀 😀 😀 yani utapeli kila kona alafu huyu unakuta ni mbaba mtu mzima ila tamaa za hela na kukosa utu kumemjaaa sasa hizo kodi unazolipwa haitoshi kufanya ukarabati mpangaji akitoka au mpya akiingia??ukarabati gani huo au unakuwa unajenga upya??
 
Deposit ya nyokweeee 😀 😀 😀 yani utapeli kila kona alafu huyu unakuta ni mbaba mtu mzima ila tamaa za hela na kukosa utu kumemjaaa sasa hizo kodi unazolipwa haitoshi kufanya ukarabati mpangaji akitoka au mpya akiingia??ukarabati gani huo au unakuwa unajenga upya??
Mambo ya nyumba utayajua wapi wakati bado unakaa nyumbani kwa shemeji yako!
Nyumba hujengwa kwa mkopo wa benki hivyo hiyo kodi ndio inalipia mkopo wewe bwege!
 
Ikiwa mkataba wako ulipitia kwenye mikono ya kisheria na kutiwa balaka Zote, harafu mteja wako wa nyumba/mpangaji wako aliupitia mkataba akaridhia akiwa na akili timamu akamwaga saini yake kwamba amekubaliana na masharit yaliyowekwa, basi Fata mkondo ule ule wa kisheria hupaswi kutumia nguvu anaweza aka kutengeneza hata kesi, ukivunja kufuri atakuja kudai ametibiwa hata fedha, mshirikishe mwanasheria wako nadhani kwa taaluma zao zipo mbinu huwa wanatumia hata polisi huwa wanashirikishwa kuhamisha,, ingawa unapotaka kumtoa mpangaji wako inabidi umuandalie notes ya miez 3 kabla ya kuhama kwake hapo Kuna kumpatia muda wa yeye kujipanga na kutafuta nyumba nyingine,, sas ukimtoa na ukichukulia hajapata hifadhi unategemea atakwenda wapi? Unaweza kuta kwa muda huu Hana fedha maisha yetu ni siri kubwa,, unaonaje ukibeba utu Bila kujari Sana changamoto zake au changamoto unazopitia? Kitendo cha kutafuta ushauri ni ishara tosha busara unazo,, kama ikikupendeza mbebe kwa utu sisi binadamu hujui kwa sas anapitia changamoto gani, miongoni Mwa matendo ya huruma ni kama maamuzi yako kwa sasa! Inawezekana uliwahi pitia nyumba za kupanga ktk maombi yako kwenye mafanikio uliapa hautokuja kuwafanyia wengine kama ulivyo fanyika kipindi upo nyumba za kupanga,, au na wew ulinyanyasika na wewe unataka kulipa visasi? Naziona busara zako,, ombi langu usitoe au kufanya maamuzi ukiwa na hasira au kushinikizwa ingawa ni haki yako na tupo kwenye mwezi mtukufu na kwaresma beba utu njia ya mafanikio ni ngumu!
 
Wenye nyumba basi mjue hata hao wapangaji wanatafuta.

Yaani amelipa kodi, amelipa dalali, eti na hela ya mwezi mmoja ya security.

Mpe hela yake hiyo uliyokaa nayo ya security, huo mwezi mmoja aliokaa bure hesabia ni notice.

Hivi mkifa mtaondoka na hizo nyumba ? Muwe na imani pia.

Usifikirie sina nyumba za kupangisha, sawa eeh.
Unaondokaje na funguo za nyumba yangu ukijua unadaiwa. Kama sio ukorofi na kulilia kupigwa ni nini.
 
Back
Top Bottom