Mpeni Mungu yaliyo ya Kimungu na Kaisari yaliyo ya Kaisari! Hiki kinachofanywa na Baraza la Maaskofu Katoliki, sio kuchanganya dini na siasa?

Kwa hiyo mwarabu zamani wakati analeta dini hakuwa na pesa, sasa amepata ndiyo anataka alete miradi.

Kwa nini asilete tu hizo pesa bila kutaka kutumia vitega uchumi vyetu?
Unaweza kuniambia mwarabu gani alileta dini ??
 
Mkuki kwa nguruwe. Wanapolihitaji Kanisa huliita. Linapowapa ukweli huligeuka. Hoja za Maaskofu zijibiwe
 

Kwani hata huo mkataba wa Muungano nani aliupigia kura ??
 

Hivi lini serikali iliwaita maaskofu wakasome sala ya mvua , si wanaamua wenyewe ??
 
Ushauri wangu wa bure kwa Rais Mama Samia, kama hawa Maaskofu Katoliki wamewasilisha sauti ya Mungu wa kweli, uzoefu umeonyesha sio vizuri kuwakatalia Maaskofu, na mfano mzuri ni ushauri huu niliompa rafiki yangu Benard Membe
 
Ungesoma bandiko lote ,ungeelewa P ,amemanisha
 
Kwamba CCM ndiyo chama tawala na chama pekee Tanzania...
Mungu atusadie sana waja wake ! Case closed.
 
Maoni ya kupinga jambo lolote la kisiasa yanayotolewa na TEC, ni sawa na amri kwa Wakatoliki wote kuikataa DPW!, Wakotoliki wa CCM, Serikali, Bunge na Mahakama, wanao unga mkono DPW, hivyo baada ya tamko hili, wakiendelea kuunga mkono DPW ni kama kwenda kinyume cha msimamo wa Kanisa Katoliki!.
 
Baraza la maaskovu haliruhisiwi kutoa kauli (matako) ya kukemea au kuipinga uonevu,unyonyaji na ukandamizaji? Kanisa pia lina kazi ya kutetea haki za wananchi kwa kupaaza sauti linapoona haki zao zinakanyagwa na serikali.

Mkuu Pascal Mayalla ameandika andiko lililoyumba. Maana analysis yake ameponda tamko la Maaskofu. Hitimisho ameshauri Mh Rais Samia akubaliane na Maaskofu. Huku ni kuyumba kiuandishi!

Kimsingi mchango wa Kanisa kijamii hapa Tanzania haupimiki. Ukitizama shule za msingi za kanisa, o level na a level schools, vyuo na vyuo vikuu ambavyo vipo affiliated na kanisa, hapo hatujagusa idadi ya hospital na vituo vya afya, na mipango kedekede ya kanisa kwa Kaya masikini kupitia shirika lake la Caritas. Hivyo ni ngumu sana kutenganisha kanisa na jamii na siasa za Tanzania.

Zaidi ikumbukwe Watumishi wengi (sio wote) wa ngazi za juu Serikalini wamefaidika na mifumo hii ya kanisa. Ndiposa taasisi hii ya kanisa katoliki ina-exert special threat kwa Serikali yoyote iliyopo madarakani.

Itoshe kusema, matawi ya filosofia - Epistemolojia na Ontolojia - ni silaha hatari sana ambazo ndio msingi wa kanisa.

Mkuu Pascal Mayalla amefanya haraka sana kukosoa tamko la Maaskofu. Sio kawaida kwa Pascal Mayalla kuandika ima kukosoa ima kupongeza pasina tafakari ya kina.

Unfortunately, this time around mwandamizi Mayalla ameloa.
 
Hebu kidogo fafanua. Kwani Rais anaemfuata mama lazima awe mkristo? Kama ni zamu kati ya wakristo na waislamu basi huo nao ni udini unaleta. Kwani katiba inasema hivyo? Mbona zile zamu za kupishana kati ya mtu kutoka znz na Tz bara siku hizi hamzitaji? mnasema katiba haijaweka zamu lakini kwenye udini mnaashiria kuwe na zamu!
 

Mwandishi mwandamizi na mwanasheria Msomi, ndugu yangu Pascal Mayalla andiko lako hili limeyumba mno. Sidhani kama ulipata wasaa kufanya tafakuri ya kina kabla hujashika kalamu kuweka wino kwenye karatasi.

Kifupi sana, headline ya andiko, analysis yako na hitimisho ulilofikia ni sawa na wasemavyo Wazaramo: zilongwa mbali, zitendwa mbali! Hoja uliyokusudia kufikisha kwa hadhira haieleweki. Ima ulikusudia kuwachanganya wasomaji, faima hadhira imesoma andiko la mwandishi aliyechanganyikiwa.

Vyema upitie upya andiko lako hili walau kuwe na coherence (mtiririko sawiji) wa headline, analytical content na conclusion. Itapendeza!

Nikutakie heri.
 
Andaa andiko lingine la kuomba radhi mkuu muungwana akivuliwa nguo huchuntama sasa chuntama omba radhi, 'who the hell is....' unaelewa maana yake omba radhi umewakosea wazee wa baraza
 
Hata Mimi nashangaa Ila Mambumbumbu wanakataa
 
Well said mkuu!

Zaidi, wakatoliki wakiingia mzigoni, wapwa wao wanaosali jumapili easily wana-join the party! Halafu kwa agenda yenyewe hii ya kuuza rasilimali za nchi, siioni namna Muslems watakataa kushiriki hii sherehe pamoja na Catholics!

Signals mbaya kabisa kwa CCM.
 
Nimesoma tamko la TEC

Kwanza tamko limesomwana mtu mmoja bila kuwepo na askofu mwingine yeyote.

Aliesoma na kuandika tamko amekuwa miongoni mwa watu wanaopinga mkataba wa bandari kwa nyakati tofauti hata kabla ya tamko la leo.
TEC imetumika kama Jukwaa lilisaidia slaa na kitima kufikisha hoja zao.

Rejea mjadala mdaharo uliowashirikisha Rostam,Kitila mkumbo,Zitto,Lema,Shekh Ponda,Balile na Dr Kitima mwenyewe.

Kwenye madaharo watu wote walikubaliana kuhusu umuhimu wa uwekezaji,Kitima pekee ndie alikuwa na hoja tofauti, akasema haoni sababu ya kukabidhi uhuru wetu kwa waarabu,akapinga uwekezaji na kutaka mkataba tuachane nao,tuwaachie vijana wa kitanzania waendeshe,akaongeza kuwa hata wakiiba watatumia pesa hizo humuhumu nchini(ingia youtube andika mdaharo wa bandari utaona ninachokisema)

Leo ameibuka kama katibu wa TEC nafasi iliyowahi kushikwa na Dr.Slaa.

Anatoa tamko kwamba TEC inapinga uwekezaji na wanamuamuru Rais Ufute mkataba.
Kwenye andiko lake ametoa hoja kubwa tatu.

1.Kwenye andiko lake anadai Mihimili iheshimiane,isiingiliwe hapa alimaanisha Kesi ya mwabukusi ambayo kwa vyovyote Kitima alihusika kuifungua .

Kushindwa kwa Mwabukusi ni sawa na kushindwa kwa Kitima,lazima Kitima atafute plan B.

Kitima kwenye andiko lake anasema mihimili isiingiliane,kila muhimili uwe huru.

Kwake anaamini walishindwa kesi kwakuwa mahakama haikuwa na uhuru wa kufanya maamuzi,Kitima ni kama anasema mahakama ilishinikizwa kutoa yale maamuzi.

Halafu anafanya makosa kwenye andiko hilohilo kuhusu hoja hiyo kwa mushinikiza Rais Samia kutengua maamuzi ya bunge ambao ni muhimili mwingine wa dola ambao awali amesema mihimili isiingiliwe.

Hapa anahalalisha kuingiliwa kwa munimili wa Bunge ili kufanikisha malengo yake.

Rais akiingilia bunge atakuwa naendelea kuvunja katiba, kukosea kwa kufanya kile ambacho Kitima anapinga kwenye Tamko lake.

2.Kuhusu hoja ya kutaka Bandari iendeshwe na wazawa,kwamba haijawahi kuendeshwa na wageni,amesahau kuwa Bandari imeendeshwa na TICS kwa miaka 22 hakulisema hili kwa makusudi,huenda anatamani TICS ndio iendelee badala ya DP-World ili kulinda maslahi binafsi aliyonayo bandarini.

Hapa Kitima ni kama ana msalahi binafsi anayoyapigania kwa kutumia mwamvuli wa TEC,hoja yake inamashaka.kumbukeni sakata la ESCROW kuna hadi viongozi wa dini ambao walinufaika na wizi wa ESCROW sio wasafi kwa kiwango hicho.

3.Kitima na Dr.Slaa ni watu wenye Itikadi kali ya ukristo(Udini)

Kuna Wakristo wasiokuwa na ubaguzi halafu kuna Slaa na Kitima waliopea kwenye Udini.

Sio utamaduni wetu Watanzania kunadiliana habari za udini ma Ukabila,lakini kwa muktadha huu nitalisemea ili muwajue vizuri.

kwa nyakati tofauti Kitima ameonesha ni mtu mwenye chuki ya kidini na mdini sana tangu akiwa Makamu mkuu wa chuo cha St Augustine Mwanza.

Nakumbuka wakati wa utawala wa Rais Kikwete kwenye kipindi cha star TV chini ya Dotto Bulendu kitima aliilaumu serikali ya Rais kikwete kwa kuruhusu waarabu wenye ndevu hadi kifuani kuzagaa Kariakoo,alisema kwamba wale wenye ndevu ndio magaidi.kwamba serikali inawatazama haiwachukulii hatua.

Yaani kwenye ule mjadala, kitima akaona ndevu ni tishio kwake.
Ndio maana Tangu utawala uchukuliwe na Rais Magufuli,Mkatoliki mwenzake Kitima hajawahi kujitokeza hadharani kuipinga serikalinya magufulipamoja na chamgamoto zote za Utawala wa Magufuli.

Kadhalika Dr.Slaa,kwenye utawala wa Magufuli hakuwahi kuishambulia serikali kwa lolote hata pale palipokuwa na makosa ya wazi,baadae Slaa alipewa zawadi ya cheo kuwa balozi wa tanzania kwa kazi nzuri ya Kuhujumu demokrasia yetu.

Baadae alirudishwa nyumbani baada ya kumaliza muda wake wakati wa utawala wa Rais samia,hadi hivi karibuni kwenye sakata la mbowe,Slaa alisema mbowe anaweza kuwa gaidi kwamba mashtaka aliyoshtakiwa nayo yalikuwa halali,hapa alitoa kauli ya kumfurahisha Rais samia kwa lengo la kuwinda zawadi ya cheo kipya.
Rais Samia amejipambanua kuwa hataki wapambe,ni kiongozi anaetembea kwenye 4R,msisitizo ukiwa mwafaka wa kitaifa.

Watu kama slaa ambao wanashangilia mauaji na uonevu Rais samia aliona hawawezi kumsaidia.

Pia Rais Samia anaamini katika uongozi wa vijana.Slaa ana zaidi miaka 78.

Baada ya Slaa kukiridhisha kuwa utawala wa Rais Samia hauna mpango wa kumtumia,ndipo akaamua kuungana na Dr.Charles Kitima kuishambukia serikali

Kama Slaa angepewa cheo,muda huu angekuwa anatetea Mkataba wa DP World.

Huu ni uthibitisho kuwa Kitima na Slaa ni wadini sana ambao Kuingia kwa Rais Samia madarakani kwao waliona ni suprise.

Hawakujiadaa kuongozwa na Rais Samia ndio maana Wamekuwa mbogo sio kwenye mkataba wa bandari tu bali kwenye utawala wa Rais Samia kwa ujumla.

Rejea mahojiano ya Slaa na star tv baada ya Rais samia kuapishwa,Slaa aliishambulia serikali na kuituhumu kuhusu kifo cha Rais Magufuli,Slaa akamalizia kwa kusema kama wanataka wanikamate,siogopi kukamatwa.,alionekana ni mtu mwwnye hasira ya kukosa cheo.

Kwa msingi huo,huu ni uthibitisho kuwa Tamko lililoitwa la TEC lina msukumo wa kidini kuliko msukumo wa kisheria na kisiasa.

Nchi yetu ina dini kubwa Mbili,Wakristo na waislaam,tujaalie hilo ni tamko la wakatoliki.

Je na waislaam nao wakitoa tamko lao linalopingana na tamko la TEC?

Vipi walokole nao wakiunga mkono uwekezaji,serikali itafuata msimamo wa dini gani?

Ndio msingi uliosababisha serikali kutamka kuwa haina dini,lengo nikuepuka misuguano inayoweza kuliingiza taifa kwenye machafuko.

Tumeshatoa maoni,serikali imeyasikia na ndani ya serikali kuna watu wa dini zote na wasiokuwa na dini.,kuna wanasheria kuna vyombo mbalimbali vya dola.

Ni imani yangu kuwa Swala la uwekezaji wa Bandari watalifanyia kazi kwa kulinda maslahi ya taifa.

Viongozi wa dini wasiingile utendaji wa serikali ambayo kila mmoja anatambua haina dini.
Tuwapuuze Slaa na kitima,wanataka kutuingiza kwwnye vita yao ya maslahi binafsi kwa Kisingizio cha kulinda rasilimali ,tuulinde umoja wetu uliodumu kwa zaidi ya miaka 50.
Tujifunze Burundi na Rwanda,mauaji ya kimbali yalihamasishwa na viongozi wa dini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…