Mpeni Mungu yaliyo ya Kimungu na Kaisari yaliyo ya Kaisari! Hiki kinachofanywa na Baraza la Maaskofu Katoliki, sio kuchanganya dini na siasa?

Siasa ni maisha!

Kila siku wanasiasa wanawahimiza viongozi wa dini kuombea amani na mshikamano.

Hivyo viongozi wa dini wana wajibu wa kukemea pia matendo ya wanasiasa yenye uelekeo wa kutowesha amani na mshikamano siyo kusubiri kuomba tu.

Mungu atapewa vya kwake na Kaisari atapewa spana zake kama hivi.
 
Pilato akamwambia Yesu " Wewe u Mfalme basi"

Basi Pilato akaandika anwani Hii na ikabandikwa juu ya Msalaba " Yesu wa Nazareth Mfalme wa Wayahudi"

Siasa imo ndani ya Dini
 
Tutadili na dhamiri.
Kama lengo ni udini au kumkwamisha Samia hao viongozi ni waache mambo ya hovyo.

Kama lengo ni maslahi ya Taifa na Uzalendo basi viongozi wa dini wasikilizwe.

Sasa Nani wa kupima dhamiri za Watu?
Pasco arudi ktk historia ajiulizwe asili ya siasa ilikoanzia,

Kamwe huwezi kuwatenga watumishi wa Mungu na maisha ya waumini yanayotegemea siasa!!!

Nani akemee RUSHWA na UOVU!!!
 
Paschal unazeeka kwa matatizo sana mzee wangu.. hebu tafakari tena ulichoandika au ni kam kujipendekeza sio kwa umri wako tena na uleweledi wako mzee
 


Interesting times. Unajua maana yake nini?

Mwenye macho haambiwi ona. Wale wanaoomba wazidi kufanya sala na sadaka ili Taifa letu liwe moja na linalool nia mamoja.

Tusijidanganye, hapa tulipofika mambo hayapo sawa
 
Unaongea Kama nani?
 
Huyu Bwana Mayalla a.k.a Njaa (Jiwe's voice) njaa zitammaliza.Baada ya kuukosa uDC kwa Jiwe sasa anajipendekeza kwenye hii regime nyingine!
 
Tunza heshima yako kwa masirahi ya kesho.
 
Tujibu hoja zao, dini na siasa vimetokea wapi tena!! Tusikimbilie dini na madhehebu tujibu hoja walizozitoa kuhusu mkataba . Kwanini turuke ruke kama maharage, tujibu hoja narudia tujibu hoja zao
 
Unaandika kinyume mkuu Ahsante nimekuelewa ujumbe umefika
 
Pascal huwa unajishushia heshima kwa mambo kama haya.

Mosi, kusema kuwa siasa na dini visichangamane ni uongo na unafiki hasa kwako uliyesoma historia ya dini na siasa kwa sababu siasa ni zao la dini na kwa maana hii dini kama mlezi wa siasa.
Hili unakijua Sana halihitaji mijadala labda tu uchawa unakusumbua.

Lakinip, pia ni uwendawazimu wa haki ya juu kwa taasisi za kidini kuiona hatari ya jambo la kitaifa kisha wakaa kimya, maana watakuwa hawajatekekeza wajibu wao mkubwa wa kukemea ambayo Ndiyo kazi yao ya kitume kama ambavyo Yesu alikuwa akiwakemea maaskari wala rushwa na viongozi wa dola Mafarisayo.
 
Wewe pasco mbona mchokozi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…