Mpenzi wangu kagoma kuhamia imani yangu ili tufunge ndoa

Mpenzi wangu kagoma kuhamia imani yangu ili tufunge ndoa

Mboka man

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2020
Posts
478
Reaction score
1,647
Baada ya safari ndefu ya mahusiano tumefikia hatua ya kufunga ndoa ila binti ni mkatoliki mimi msabato mpaka sasa hatujafikia mwafaka nani amfuate nwenzie japo kisheria tumezoea mwanamke anamfata mwanaume lakini yeye hataki na hayupo tiyali kuhama roma.
 
Baada ya safari ndefu ya mahusiano tumefikia hatua ya kufunga ndoa ila binti ni mkatoliki Mimi msabato to mpaka sasa hatujafikia mwafaka nani amfuate nwenzie japo kisheria tumezoea mean mall anamfata mwanaume lakini yy hataki na hayupo tiyali kuhama romA

Kasome hii mkuu Marko 10:7
 
Ndio maana ndoa nyingi sana za siku hizi zinavunjika ovyo ovyo tena mapema sana.
Kwanza kabisa hayo mambo ya imani mlitakiwa kuyaweka sawa sawa mwanzoni kabisa mwa uhusiano wenu na sio muda huu wa kufunga ndoa.

Pili ni kichekesho kikubwa cha kiimani kwa mtu kuhama imani yake kisa kumpata mwanamke au mwanaume. Imani ya mtu ni zaidi ya ndoa yake. Msilazimishe ndoa kuwa msumari wa kupigiliwa kwenye kila kitu cha kimaisha.

Tatu, ndoa ni jambo la kiimani, huwezi kuitenganisha ndoa na imani, kama imani zenu haziwezi kukubaliana kuhusu ndoa yenu ni vyema msioane wala kulazimisha kuoana maana mtaishia kupoteza kimoja. Sasa ili muweze kupata vyote (ndoa na imani) katika maisha yenu ni vyema mkaachana sasa ili kila mtu akatafute mtu wa imani yake wakuja kuoana naye. Wanawake na wanaume wanaotafuta wachumba wa kuoana wamejaa kwenye jamii, na wengi wako vizuri tu kitabia na kimuonekano, nendeni uko.
 
Back
Top Bottom