Mradi wa Bagamoyo: Hujuma Tanzania na ushindi kwa Kenya na Rwanda

Hawa mashujaa wa keyboard ni mzigo. Hivi kwa akili zako za mtandaoni unadhani watu hawajaenda nyuzi 360 na kuona madhara hayo.

Hivi mnadhani nchi inaendeshwa kwa porojo zetu?
 
Ni kweli unalosema kuhusu udogo wa nafasi ya upanuzi hata mkurugenzi wa TPA (D. Kakoko) alishaliongelea hili. Ni kwamba ilitakiwa lile eneo lote mpaka mtoni Kijichi litengwe kwaajili ya bandari na Kakoko alisema kuwaondoa watu itagharimu fedha nyingi za kulipa fidia. Ila hili la kuhusu machanga kurudi wakati wa jioni hilo linaweza kudhibitiwa kwa kuweka "surge barrier'.
Hili la storage teyari wanalifanyia kazi kwa kujenga bandari kavu huko pwani, mizigo ikishushwa itakuwa inapelekwa huko haraka na reli ili kuacha nafasi.
Kuendelea kuijenga Dar es salaam port ni kupoteza fedha tu, ni eneo ambalo tayari sio rafiki labda tuamua DAR ES SALAAM PORT IWE NI KWA RORO TU, MTWARA PORT IWE NI KONTENA PORT, NA TANGA PORT IWE FOR TANKERS.
Hili pia wahusika teyari wanalifanyia kazi, bandari ya Mtwara inapanuliwa ili iweze ku beba mikoa ya kusini na nchi jirani, Tanga vivyo hivyo inafanyiwa ukarabati. Barabara ya kwenda Mbaba bay nayo inatengenezwa ili mizigo kutoka bandari ya Mtwara iende moja kwa moja kupitia barabara hiyo pia baadae wanampango wa kujenga reli.
 

ZZK kasema haikuwa maktaba bali yalikuw amazungumzo ya hawali, so wangeweza bado kuzungumza na kukubaliana na ndipo mkata usainiwe,
 
Kwakweli Zitto amewandika mazito ila tu sio mtu wakuaminika... lazima kuna kitu nyuma sio kwa maandalizi ya maandishi hayo, Zitto asingekua mnafiki angekua the best presidential material wa nchi hi, anaupeo mwingi
Zitto shida yake ni hiyo. Amepoteza kila adimu kwenye maisha, trust. Nani anayemuamini? Nyuma ya kila anachofanya ana sababu zake nyingi binafsi kuliko yale anayosema.
Very interesting indeed!
 
Watu wanaotumia muda mwingi kuwaza namna ya kuhujumu upinzani mambo kama haya watayaweza wapi?

Eti hii ndio serikali iliyojaa madokta na maprofesa!!!
 
Unazungumzia mkataba gani ambao ulikuwa umeingiwa?
 
Namuelewa Zito Kabwe, ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa kujieleza, lakini mimi namuona kama mwanasiasa asiyeaminika! Hubadilika kulingana na mahitaji ya wakati husika
 

Mkuu huoni hapo tayari kuna limitations tayari na gharama kubwa kuifanya bandari kuweza kupokea hizo meli kubwa, Congestion ya meli bado tutashindwa kuiondoa baadala yake tutakuwa tumeipunguza hasa pale itakapofikia point ya kuwa na flow kubwa ya meli (japo siamini kama hiyo flow kubwa itakuwepo wakati bado production yetu ni very low). "surge barrier" bado ni issue kwa maana ya gharama na sina uhakika kama itawork kulingana na eneo lenyewe.

Kama waziri ameshakubari pale ni pafinyu baadala ya kutupa hela kwanini tusiangalie option nyingine, Hizo gharama za yote hayo na mengine uliyoonyesha kwanini tusikae na mchina mezani tukashare cost?? na masharti yakapungua na ujenzi ukawa na shareholder watatu GOVT, CHINESE NA ARABS with our 30%shares na tukaweka hela kabisa na sio free shares, Dar es salaam port ikawa just as backup port lakini pia ikatumiwa na fishing trawler's
Hili la storage teyari wanalifanyia kazi kwa kujenga bandari kavu huko pwani, mizigo ikishushwa itakuwa inapelekwa huko haraka na reli ili kuacha nafasi.

Point yangu ni ile ile, haya magharama yote yangechanganywa tukawa na hela yakutosha tutakaa na Mchina tukawa na shares zetu hata 30% na ARABS na CHINESE wakagawana hiyo 75% na masharti yakapungua na hiyo package yao ikaja kama ilivyo huku sisi tukineemeka kwenye kodi, ajira kwa watu wetu, miji kujengeka na kutanuka, bado tuna gawio kwenye 30% shares na multiplying effect itaenda mbali zaidi mikoa na mikoa na Tanzania inaweza kuwa Hub ya chinese business East africa na hizi land locked zote.


Hili pia wahusika teyari wanalifanyia kazi, bandari ya Mtwara inapanuliwa ili iweze ku beba mikoa ya kusini na nchi jirani, Tanga vivyo hivyo inafanyiwa ukarabati. Barabara ya kwenda Mbaba bay nayo inatengenezwa ili mizigo kutoka bandari ya Mtwara iende moja kwa moja kupitia barabara hiyo pia baadae wanampango wa kujenga reli.
[/QUOTE]


Tanga na Mtwara bado linazungumzika kupitia pointi zangu za juu na ukiangalia fikra za hawa wawekezeaji, Kwenye makubaliano ya Bagamoyo port tunaweza kuwabana wakaturuhusu tukasafirisha Korosho,Makaa ya mawe na graphite kupitia Mtwara port, lakini tukiweka reli ile old gauge kuconnect Mtwara na Songea na reli ya Tazara Ili zile shunting za meli ndogo kutoka Bagamoyo zitakuwa zinapeleka mizigo pale kwa ajili ya Songea na Nyanda za juu hata Malawi.

Tukitumia hizi fursa vizuri na kuchanga karata zetu vizuri tukizingatia kuboresha maisha ya watu wetu tunaweza kupiga hatua kwa haraka sana.
 
haya ngoja tusikilize na upande mwengine ila ile safari ya Kenyata kule Chato hata mimi naanza kuamini Jiwe anatumika na Kenya
Nalog off
 
Moshi wa Ruangwa umeisha? maana sidhani hao wamiliki wa huo moshi watakubali afike 2035 huku Bashite kipindi hicho ni waziri mkuu
Hahaha mkuu una stress sana na Magu
 
Kwanini Serikali isiifanye Kigamboni kuwa mji wa Bandari na Viwanda kwa kupanua Bandari ya Dar es Salaam tukaachana na hizi kelele za Bagamoyo?
 
MH. ZITO KABWE, hongera sana kwa ufafanuzi wako japo usiwe na wivu kwa sababu Kenya inazidi kutusua kiuchumi kwa kuanzisha miradi mikubwa yenye tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

Kuna siku nilisema kwamba Kenya ni nchi yenye rasilimali chache ila inaoongozwa na watu wenye akili kubwa sana. Natumai kupitia huu uzi wako umewathibitishia watanzania kwamba Kenya iko mbele ya Tanzania kwa kila kitu i.e mentally, economically, politically and socially.
 
Bado don't see any new substance. It's just an obvious stuff.
 

Do you know what is behind the LAPSSET contract? Kenyans have no clear picture of how much the project will cost and how long it will take to fund the project.
 
Hawa mashujaa wa keyboard ni mzigo. Hivi kwa akili zako za mtandaoni unadhani watu hawajaenda nyuzi 360 na kuona madhara hayo.

Hivi mnadhani nchi inaendeshwa kwa porojo zetu?
Wewe na wenzako porojo zenu zimeleta maendeleo yapi? Miaka 50 Nchi haina maendeleo wewe shujaa wa keyboard Mbona humwambii magufuli kuwa nyerere alinunua Ndege 14 na hazikuleta maendeleo? Tanzania ni Nchi yenye rasilimali nyingi kuliko mataifa kibao Duniani lakini chini ya CCM imekuwa Nchi masikini wa kutupwa, hutukupaswa kuhubiri flyover sasa ni vitu vilitakiwa viwepo Nchini siku nyingi lakini kwa kuwa CCM ni chukua chako mapema na CCM ni ile ile endeleeni kuitafuna Nchi mpaka mwisho wa Dunia.
 

Wakenya ni wajanja hata Bandari Mombasa kutoa mzigo ni jengo moja tu kila kitu kimepangiliwa vizuri siyo lazima kuwa na wakala wakati wa kutoa mzigo wako.

Lakini Bandari ya Dsm hawana mpangilio kuna usumbufu mwingi mara hakuna Network ndiyo maana wageni hawaitaki Bandari ya Dsm, mabasi vyombo vya usafiri ni 24 hrs wana viwanda vingi, Serikali inaheshimu mahakama na vyama vya upinzani kuna utendaji mzuri kimfumo kwa ujumla
 
Kwanini Serikali isiifanye Kigamboni kuwa mji wa Bandari na Viwanda kwa kupanua Bandari ya Dar es Salaam tukaachana na hizi kelele za Bagamoyo?

Kile kichochoro cha huko feri ndiyo Tatizo na kukipanua kile ni gharama kubwa sana ni sawa na kujenga Bandari ingine mpya kubwa
 
Dah hapa ndo naamini watanzania tuna minyoo kichwani.

1. Hivi wachina wajenge afu wasilipe kodi hata cent lakini wawe huru kufanya biashara.
2. Wakae kwenye ardhi yetu miaka 99
3. Haturuhusiwi kuendeleza bandari yeyote zilizopo
4. Wasimamie wao for the whole period kweli. Ndugu zangu hawa hawa


Wanapinga miradi kama
1. Stiglers gorge
2. Reli
3. Ndege
I ambayo hii unakwenda kwa mwananchi wa kawaida moja kwa moja.
Sijui watanzania tunataka nini


Sisi hatukuwa tayari kupata uhuru au tunatakiwa kutawaliwa kidikteta for while hadi hadi tupate akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…