Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu umetumia akili gani kuandika huu ujumbe? plz jaribu kuu edit Basi ndo uutume Tena maana unatusumbua Sana kuuelewa.[imejaribu kukuelewa lakin kwa taabu sana, hizo sheria zilipitushwa bungeni, Maguful alikuwako, unaweza kutuletea record moja hapa ya maguful kupinga hzo sheria?
Angalau ZK twaweza kupata, leo unamlaumi ZK kuwa ndi waliopitisha sheria mbovu za madin enzi za mkapa wakt ambao huyo ZK wala hakuwepo bungeni?
Huelewi!
Nauliza kabla ya kudandia kujenga hiyo bandari kwa nini tusiboreshe kwanza hizi zilizopo?
Jama ni mzuri lakini hayuko stable sana kimawazo. Unaweza kuta kesho anakuja na bandiko la kupinga huu mradi kwasababu ameona wengi hatujamusapoti.Kwakweli Zitto amewandika mazito ila tu sio mtu wakuaminika... lazima kuna kitu nyuma sio kwa maandalizi ya maandishi hayo, Zitto asingekua mnafiki angekua the best presidential material wa nchi hi, anaupeo mwingi
Labda ulikuwa hufahamu tuu ila ujenzi wa sasa wa bandari ya Dar utajumuisha kuongezwa kwa kina, hivyo hizo generation 4 zitaweza kutia nanga.
Kama swala ni kujenga bandari yenye kina kirefu kwanini tusiijenge ya Mtwara ambayo kiasili kina chake ni kikubwa pia imekaa sehemu nzuri ya kuweza kuhudumia nchi ambazo hazina bandari, kama wapinzani wenyewe ndio hawa waliomtukanaa JK anauza nchi, miswada inaletwa kwa hati ya dharula waendelee kuwa wapinzani milele wala wasipewe nafasi.
Tayari ilishafafanuliwa ni jinsi gani bandari ya Bagamoyo ingeua bandari nyingine na huku nchi ikipoteza mapato ya kodi kama tunataka kushindana na Kenya kuhusu bandri ya Lamu sehemu sahihi ingekuwa ni kujenga bandari ya Tanga na sio kwenda bagamoyo kwa kifupi Zitto anatumika kama alivyotumika kwenye maswala ya madini
tatizo lako ni shule uliyosomaKatika bandari Mtwara ni bandari au dimbwi, bandari unaijua wewe?
Huyu Mwami kuna kipindi Mzee Dr. Harrison Mwakyembe alisema sikutegemea mtu makini Kama Zitto Kabwe anasema serikali inunue mitambo ya IPTL wakati alijua sheria ya Manunuzi PPRA inahitaka kununua vifaa, mali mpya ba si second hand.Kwa hiyo ni kweli? Bagamoyo tukabithi kwa miaka 99 bila ya sisi kupata chochote au siyo. Unapenda
Very learned way of sending across good ideas. Tunatanua bandari zote tulizonazo kwa wakati mmoja, ili uchumi unaotegemea bahari uweze kukua.ZZK anatueleza mkakati wa Bandari ya Bagamoyo kuwa ni gateway ya imports.
Kwa mchumi yeyote ningetegemea angekuwa na in-depth analysis ya how do we strengthen production ya mazao ghafi na processing ili kuwa na certain ya exports.
JK toka 2013 mpaka 2015 anatoka madarakani alisita kusaini a go ahead. Unadhani kwanini year 1 imepita hakusaini,
Year 2 imepita hakusaini.
Year 3 anatoka madarakani early November bila kusaini. Nini alikiona kama sio favourable clauses ya mkataba mpaka 3 years zikakatika hakutia mkono.
Dr. Mpango waziri wa Fedha alikuwa mkuu wa Tume ya Mipango wakati wa JK; bila shaka alikuwa sehemu ya walimshauro JK asiwe "fasta" kusaini.
ZZK uliponda sana initiative za JPM na Prof. Kabudi kukaa na Barick na kushikilia makanikia in the name of tutashitakiwa. Leo hii uongo wako umeonekana wazi mchana peupe.
By the way; show by numerical projections namna gani Bagamoyo port could make a difference kwenye kuongeza revenues ambapo Mtwara, Tanga na Dar zime-fail ili ku-justify hoja yako