mng'ato
JF-Expert Member
- Oct 27, 2014
- 29,200
- 49,076
ACT WAZALENDO umeitelekeza siku hizi.Bwawa hili litajengwa tu
waseme wafanyeje Tumeamua Litajengwa
na wanao tukwamisha Wajiandae kukwama wao
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
ACT WAZALENDO umeitelekeza siku hizi.Bwawa hili litajengwa tu
waseme wafanyeje Tumeamua Litajengwa
na wanao tukwamisha Wajiandae kukwama wao
Ukiona hivyo, ujue KICHAA hamshirikishi VP kwenye maamz mengi ya uendeshaji wa masuala ya Taifa
Wewe jamaa yangu fikirisha akili yako,maendeleo yoyote yale duniani yana gharama zake,before hamjafanikiwa angalieni kwanza impact za hilo swala
kumbuka SIYO wewe unayehitaji kuishi hata samaki na viumbe wa ardhin nao wanastahiki ya kuishi.
pia naomba niongeze SIKU zote msipende kuchanganya siasa na taaluma.
sipingi ujenz wa mradi hapana lakini.je ujenz huo utaweza kwenda sawia na ecology+,mfumo wa bonde la pale?????
SITAKI yajitokeze ya kihansi
sawa Mimi Sina akili mtakapokuja fanya ukanda wa pwani uwe JANGWA NDO MTAELEWAWewe jamaa yangu fikirisha akili yako,maendeleo yoyote yale duniani yana gharama zake,
Tembelea maeneo yanachimbwa madini,migodi mikubwa kama North Mara,Geita Gold Mine,nakadhalika ,uone jinsi mazingira yalivyokua na yanavyofanana kwa sasa, bepari kalenga mzigo tu,na si vinginevyo
Tukiwa na Umeme na Maji ya kijitosheleza tutakuwa tumejikwamua kimaendeleo na kiuchumi. Na hili suala "Wakoloni" hawataki kulisikia, ili waendelee kututawala kwa kutumia miradi ya Maji na Nishati ya Umeme.Kwani kwao wazungu siwanao umeme wakutosha mbona sisi hawataki tuwe nao?
Haihitaji elimu ya ekolojia au haidrolojia kujua kuwa ripoti za WWF ni biased;SIYO madesa kiongozi
unayo elimu yoyote kuhusiana na hydrology? achilia mbali mambo ya uhifadhi???????
Tutaamini vipi kwamba mradi huu hatutaambiwa "wamepewa watu wa Ulaya" baada ya yeye kuondoka madarakani?Gesi tayari ina mikataba tata isiyo na manufaa ya kutosha kwetu. Kumbuka tushaambiwa gesi mabepari washaichukua. Magufuli anafanya kitu sahihi mkii
Nathani kunamahali watanzania hatuna maarifa na ufahamu wa kutosha. Moja ya maeneo hayo ni umuhimu wa Mazingira!Mradi ujengwe tu maana manufaa ya kiuchumi ni makubwa kuliko hizo athari za kimazingira. Tunahitaji umeme wa uhakika kwa nchi nzima. Hao viumbe laki 2 watakaoathirika wamehesabu mpaka nyoka na kenge wasio na faida kwetu.
Kwa hiyo viumbe 200,000 n muhimu kuliko WaTz MIL 50? Mungu amemtupatia dunia tuitawale, siyo itutawale... Yaani vipepeo, mbu, kenge nk vituzuie kupata umeme. Tutachekwa kila mahali, mpaka na shetani!Heshima kwenu wakuu,
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano Mheshimiwa January Makamba, huenda akatumbuliwa kutokana na kuwa kikwazo katika Ujenzi wa Stiegler's Gorge Hydroelectric Power Station.
Inasemekana January Makamba kaunda tume ya Wataalam wa kuchunguza athari zinazoweza kutokea iwapo Mradi huo Utajengwa.
Inadaiwa Sababu alizozitoa Kwa jicho la kitaalam ni kwamba wanatumiwa na Watu wasiopenda Mradi huu Ujengwe.
Leo katika uzinduzi wa Daraja la Mfugale, rais Magufuli amesikika akilalamikia wataalam ambao walifanya utafiti huo wa mradi wa umeme na akasema atashangaa hao wataalam wakiendelea kukaa ofisini. Amewatuhumu kwamba wanatumiwa ili Watanzania wanyonge wasitumie umeme wa bei rahisi waendelee kutumia umeme wa mafuata ambayo ni ghari.
Amedai wataalam wa mazingira walikuja na sababu za hovyo kabisa kwamba kila mtu atazishangaa. Kwamba mtu anatakiwa akajisaidie KM 20 kutoka kwenye mradi, Udongo utakaotumika unatakiwa uwe unapimwa, Gari ikiharibika haitakiwi itengenezewe kwenye mradi, mchicha kutoka maneo yale hautakiwi kwamba vitaharibu uoto wa asili.
Kadai maji yale yanatoka huko Mbeya na vinyesi na wanyama wamefia humo. Akashangaa hao wataalam ambao sio wazalendo wanatoka wapi?.
Rais kasema Mradi wa Stiegler's Gorge Hydroelectric Power Station lazima ujengwe.
View attachment 879376
STIEGLER’S gorge inapatikana katika hifadhi ya Selous (SGR) yenye ukubwa wa kilometa za mraba 50,000 ambayo ilipitishwa kuwa moja ya Sehemu yenye URITHI WA DUNIA mwaka 1982. Katika moja ya tafiti zilizofanyika huko nyuma miaka ya 1960s na baadae miaka ya 1980s ulitanabaisha uwezekano wa kujengwa bwawa kubwa kwa ajili ya kuzalisha umeme 2100MW kwa kutumia Maji kutoka katika bonde la mto Rufiji.
Baadae umoja wa mataifa kupitia mashirika mbalimbali yahusuyo uhifadhi na utunzaji wa mazingira, zilifanya utafiti wa kubaini kama kuna athari zozote za kiokolojia na za kimazingira zingeweza kutokea iwapo mradi huo wa ujenzi wa bwawa kubwa lenye takribani kilometa za mraba 12,000 utatekelezwa.
Umoja wa mataifa kupitia mashirika yake ya IUCN(Shirika la uhifadhi wa uasilia) na UNESCO zilipendekeza kusitishwa kwa mradi huo baada ya kubaini madhara makubwa kwa wanyama na binadamu waishio katika bonde hilo la mto Rufiji.
JE, MADHARA HAYO NI YAPI YATAKAYOTOKANA NA UJENZI WA MRADI HUO?
Madhara nitayaeleza kwa kifupi kama yalivyoelezwa katika Ripoti ya WWF kama ifuatavyo;
1) Ikolojia katika hifadhi ya Selous na bonde la mto Rufiji utaathiriwa. Zaidi ya viumbe hai 200,000 watakuwa kwenye hatari.
2) Shughuli za kijamii na kiuchumi zitaathiriwa sana hasa maeneo ya Mkondo wa chini(downstream) wa bonde hilo la mto Rufiji. Mmomonyoko wa ardhi, ukosefu wa rutuba na hatari ya kuzorota kwa bandari kwa sababu zile sediments(masalia) yote ambayo yalitakiwa kufika kwenye downstream yatabakia kwenye hilo Bwawa kubwa litakalojengwa.
3) Ujangili kuongezeka maradufu zaidi ilivyo sasa katika hifadhi ya Selous, ambayo itaiweka hifadhi hiyo katika hali mbaya mnoo. Mpaka sasa hifadhi hiyo iliyo na hadhi ya URITHI WA DUNIA imetajwa kuwa katika moja ya maeneo yaliyo kwenye hatari kutokana na ujangili. Hivyo serikali iliweka mikakati ya kupunguza tatizo hilo, lakini ujuo wa hili bwawa utakizana na jitiahada hizo za kuirudisha Hifadhi ya Selous kurudi katika ubora wake.
Pia katika Ripoti ya 2017 iliyotolewa na taasisi ya kimataifa inayojihusisha na masuala ya Uasilia la WWF(World Wide Fund for Nature), baada ya kufanya utafiti wao walipendekeza mradi huo usitishwe kutoka na madhara yatakayo tokea baadae.
Bwana la umeme linatarajiwa kujengwa lina ukubwa wa taifa la Switzerland ambalo ni maarufu kwa wanyama tofauti.
Shirika la kimataifa la uhifadhi wa wanyama pori WWF, limesema kuwa linaitaka serikali kufanya utafiti wa kina wa mazingira katika eneo hilo ili kuhakikisha madhara yote yanabainika kabla ya mipango yoyote ya mradi huo kuanza.
Mradi huo unatarajiwa kugharimu dola bilioni mbili za Marekani
JE, HAKUNA MBADALA WA KUZALISHA 2100MW ILI KUIOKOA HIFADHI HIYO?
Nchi yetu imejaaliwa nishati nyingi ambazo tunaweza tukazitumia kupata Megawati 2100 na zaidi.
1)Tunaweza kuzalisha umeme wa maji kutoka bonde la Mto Rufiji mbali na bwawa la stiegler’s gorge
2) Tuna gesi ya kutosha, na uzuri pia kuna miradi ambayo ipo kwenye PSMP(mpango wa kuongeza umeme katika gridi ya taifa) shida ni kuwa tunataka vya haraka haraka haraka ambavyo vitatugharimu hapo baadae. Tatizo gesi sio tegemeo tena kwa upande mwingine.Rais Magufuli: Mabepari wametunyang'anya gesi yetu hatuwezi kuitumia kwa uhuru - JamiiForums
3) Kuna uwezekano mkubwa wa uwepo wa Geothermal katika bonde la Rift valley, kwa kuwa wenzetu Kenya ambao wamepitiwa bonde hilo wanafurahia uwepo wa geothermal kwao.
4) Tuna Makaa ya mawe tunaweza kutumia kuzalisha umeme.
5) Pia kuna utafiti uliofanyika unaeleza kuwa tuna uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia Upepo katika mikoa ya katikati ya TZ (singida, Dodoma)
MAAMUZI YA KISIASA
Mwaka Jana, Juni 2017 Rais Magufuli alitoa kauli ya kutekeleza mradi huo wa ujenzi wa bwawa hilo la STIEGLER’S GORGE na kupuuza tafiti zilizofanywa zinazoonesha athari za kimazingira za mradi huo. Badala ya kutumia nishati mbadala zilizopo.
Lakini kupitia taasisi zetu za ndani yaani RUBADA(Mamlaka ya uendelezaji wa bonde la mto Rufiji) na NEMC wote wametoa baraka zao za mradi wa ujenzi wa bwawa kubwa la STIEGLER’S gorge kwa ajili ya uzalishaji umeme uendelee.
Tanzania yakataa agizo la UNESCO la kuitaka kusitisha ujenzi wa mradi wa Stiegler's Gorge Selous - JamiiForums
Zaidi ya miti milioni 2 kukatwa kupisha mradi wa umeme wa Stiegler's gorge - JamiiForums
Gesi wameichukuaje chukuaje hawa Mabeberu wakati inapatikana Mtwara pale? Fafanua plse!!!Gesi tayari ina mikataba tata isiyo na manufaa ya kutosha kwetu. Kumbuka tushaambiwa gesi mabepari washaichukua. Magufuli anafanya kitu sahihi mkii
Kwa CCM hii hilo sahau, tunaambiwa hata gesi si yetu tena ni ya mabeberu!!SWALA LINALOHUSU NISHAT YA TAIFA NALIUNGA MKONO. HATA LEO SERIKALI IKISEMA INATAKA IRUTUBISHE URANIUM KWA AJILI HIYO NITAUNGA MKONO.
ila tu mikataba na zoezi zima lisihusishe aina yoyote ya ufisadi/upigaji 10%
ahsante!
Nashangaa, na ni hapo hapo selous game reserveKWANINI WAZUNGU WAKATI WANTAKA URANIUMU MATAIFA YALIKUBALI ENEO KUMEGWA LAKINI KWENYE SISI KUZALISHA UMEME IMEKUWA SHIDA
siyo bure , kwa taarifa yako huyu ndiye aliyewezesha kubadilisha kura mil 3 unusu kuwa mil 8 , sasa mguse uone moto !January kavumiliwa sana