Mrejesho mtaji wa laki 3: Nimeamua kuuza biashara ya matunda na genge

Ungeleta uboya ningekucheka

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
Pole sana na yaliyokukuta na inaonekana huko serious na kazi. Tumpe moyo kwa kuonyesha kuna watu wema huku jamii forum kwa kumchangia kidogo kidogo. Weka no yako ya M. Pesa kwenye in box yangu ili niweza kukusaidia kidogo nilichonacho.
 
Kama upo mwanza sema eneo lako la biashara niwe nakutembelea na kununua matunda iwe tu Ijumaa kabla ya sabato
usiende kumtongoza halafu akukubalie mwisho wa siku umuache njia panda aje tena na mrejesho wa kulialia mtaji umeliwa na yeye mwenyewe kaliwa.

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
nimecheka balaa...kudos kwa bro aise
 
mi simwonei aibu maana alikula hela yangu kwa kujifanya muhitaji, alikuwa anaitwa Daynamo na Id yake ikaja kuunganishwa na Mkogoti, huwa wanakuwa na Id nyingi anajifanya anakurefer kwa mtu mwingine kumbe ndiyo yeye huyohuyo.
Mimi alikuwa ni mdada, aliandika Uzi mrefu Sana kwamba kwa tatizo lake lilipofikia anaona tu bora afe.... Nikaguswa nikamfata pm kumuuliza Shida Nini akaniambia amepata ajali amevunjika mguu hawezi hata kutembea na hela hana ya kwendea hospital, nikaona story kama haimake sense flani hivi, nikamuhoji hoji akabadili akasema ni mama yake kijijini na sio yeye.

Nikaanza kuwaza huyu atakua ni tapeli, nikamwambia nitakusaidia hatakama ni wewe na mama yako wote mpo ndani ya uwezo, nendeni hospitali wawape control namba niwalipieni, akakataa akaanza na kunisema eti Kama Sina hela au Kama sitaki kumsaidia nisimchoshe anaadika huku anaumwa... Nikamwambia tu sawa nikaachana nae., Baada ya sikumbili nafungua pm nakutana na matusi hayo page nzima
 
Nachelea kusema usipomtaja huyo bwana utakuwa umeusaliti umma wa Jamiiforum utakuwa umeniumiza sana hata mimi kiasi cha kuianza jumatatu na hangover ya pombe na akili iliyokosa nuru sababu ya mada fiche yako
 
Humu JF nimewahi kutapeliwa laki 2.

Mwaka 2014 nilipost tangazo la kumtafuta Dada yangu.

Wakanipigia watu waliodai dada yupo na ana kesi yupo mahabusu na wanahitaji fedha ili wamtoe.

Wakaniunganisha na dada (feki) analia ananiita kaka.

Anadai ana mtoto amemwita jina la baba yangu.

Nilituma hela ili dada atoke.

Baada ya kutuma hela nilianza kupata mashaka. Kupiga simu haipatikani.

Namba ilisajiliwa kwa jina la Henry Ltd

Nikajiona mjinga sana laki 2 imeenda hivi hivi.

Matapeli wa JF mlaaniwe na mbingu mtaisikia.
 
Pole ndo uwazoee binadamu ndivyo walivyo

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
ni nani huyo? kha😆
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…