Msaada: Biashara unayoweza kufanya kwa mtaji wa Tsh. Milioni 20

Msaada: Biashara unayoweza kufanya kwa mtaji wa Tsh. Milioni 20

Au awe anabeti. Anatengeneza mkeka wa kesho Leo usiku, asubuhi anaingia kazini. Jioni anasubiri maokoto huku akiandaa mkeka mwingine.
Ila nyie madogo janja daah sasa acheze kamari tena daah ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚, na mtu anataka kufanya investment inayoonekana ?
 
Lakini kumbuka hela za haraka, hupotea haraka pia. Mimi niliweka 25m miaka mitatu imepita saivi inasoma 34+ sio haba
Kwa miezi 36 umeingiza mil 9

Hii ni wastani wa sh laki mbili na nusu kwa mwezi.
Ukiwekeza mil hizo 25 kwa kuingiza 250k kila mwezi ni waste. Ila kama umehifadhi tuu huku ukiendelea kutafuta hela kwa namna ulivuoingiza hiyo mil 25, that's something
 
Mkuu kwa 20m unapata eneo la 3m huko chaka unajenga kajumba kenye mapokezi na sero hakatamaliza 10m alafu unaajiri askari 2 unawalipa 300k kila mmoja mdogo mdogo unatafuta na vibaka wawili utarudisha hela yako ndani ya muda mfupi na ww unakua mkuu wa kituo unavimba mjini. Pesa yako itarudi na faida hadi utanikumbuka
Una kitu utafika mbali
 
Nunua viwanja viwanja vya mili 3 vitatu = vifanyie Hati kwa mil 1 vyote jumla mil 10 .Kisha tumia mil 2 kwa kila kimoja kujenga msingi wa Romani ya vyumba 3 na inua course 3 jumla utatumia mil mil6 uwekezaji wote mil 16 .Kisha acha miez 4 afu .andikishana na ndugu yako mnaetofautiana ubini kuwa umemuuzia vyote milion 8 *3 inakuwa mil24 .Kisha akae miezi 2 atangaze anaviuza mil 12 vyote .jumla mil 36 .
Kwakisema ni rahisi sana โ€ฆ.. haya tupe na changamoto zake
 
Kipindi unawaza ufanye nini kata million 2 kwenye hiyo kibunda anza kupaisha kindege aka aviator weka dau la ten ten na usiwe na tamaa kikipaa kwanzia odd 2 chukua mpaka linazama utakuwa hukosi laki kila siku
 
Una experience nayo? Ili uniambie zaidi
Unatafuta laini za uwakala mitandao pendwa pamoja uwakala wa bank pendwa

Unajenga vizuri madirisha yako Ili kusiwe na direct contact kati ya wahudumu na wateja

Kama inawezekana jengea nondo Kwa ndani ya ofisi yako Ili pesa na simu zote ziwe zinalala humo humo

Wewe ukienda kukagua unaangalia cash ipo shilingi ngapi na masalio yapo shilingi ngapi unajumlisha yote unapata jumla ya mtaji wako
 
Mkuu kwa 20m unapata eneo la 3m huko chaka unajenga kajumba kenye mapokezi na sero hakatamaliza 10m alafu unaajiri askari 2 unawalipa 300k kila mmoja mdogo mdogo unatafuta na vibaka wawili utarudisha hela yako ndani ya muda mfupi na ww unakua mkuu wa kituo unavimba mjini. Pesa yako itarudi na faida hadi utanikumbuka
๐Ÿ˜„ ๐Ÿคฃ ๐Ÿ˜‚
Dah,
Kwamba kuna biashara ya SERO za binafsi?!!!
Unakuwa wakala wa Polisi, au?
 
Unadhani Kila mtu ana muda, mazingira sawa na wewe. Mtu kaajiriwa ndichi huko na bado kazini anatoka saa 11 jioni. Ila ndo hivyo anayo hiyo 20m , aiweke chini ya godoro?
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ kuliko kuweka chini ya Godoro bora afungue account UTT
 
HABARI.
Kwa upande wangu na mimi ningependa kutoa Ushauri kwa mtoa uzi. Kutokana na experience yangu niliopitia mtaani.

Kwanza kabisa ningependa kujua mtoa Uzi hiyo 20m ni ya kutoka wapi, yaani ni ya mkopo wa benki, akiba ambayo alikua amejiwekea ama vipi. Hii itasaidia kujua aina ya biashara pia ya kumshauri, maana unaweza ukamshauri biashara ya kuwekeza kisha baada ya miaka 10 ndo uone return kumbe hela ni ya mkopo kila mwezi anatakiwa kurudisha kiasi kadhaa. Kwa maana hiyo ningependa kutoa ushauri wa jumla ili kama kuna mtu mwingine anapenda mawazo na ana muda pia basi ajifunze


So mimi ningependa kushauri kutokana na mawazo mawili
1. Kama hela ni ya mkopo. Basi unahitaji biashara ya kuleta faida baada ya muda mfupi. Na tukifikia hapo sasa inshu ya stress free inakua hamna tena maana biashara za aina hii lazima ukutane na stress na ni LAZIMA WEWE UWE MWANGALIZI MKUU WA HIYO BIASHARA, maana biashara inaingiza hela kila siku kama umeweka mtu mwingine aisimamie lazima akupige.
Biashara zenyewe ni.

a) Kununua makinikia ya mgodini na kwenda kuuza kwenye Plant ama kwenda kuyachenjua mwenyewe na kupata dhahabu ya moja kwa moja. (Hii biashara inahitaji uwe mkoani na uwe mkoa wenye hiyo migodi) lasivyo kutakua hamna usimamizi wako na kumbuka nimesema bila usimamiz unapigwa. Huezi kukosa 3m kwa mzigo

b) Biashara ya Clasher (mashine ya kusagia mawe ya dhahabu)
Hapa kidogo kuna urahisi wa usimamizi japo sio sana, utahitaji kuzitembelea mara moja moja clasher zako, na hii biashara unachofanya ni kununua clasher 2 kwa jumla ya bei ya 8m mpaka 9m kwa Clasher na hapo utakua umetumia 16m au 18m kisha ukiweka kwenye mgodi unampa mtu anaehusika pale mgodi (wakiwa wawili ndio vizuri zaidi) awe ana operate/wana operate kisha wanakuletea hesabu kila mwezi, kiasi kinachozidi ni cha kwao hesabu huwa ni 800k kwa mwezi kwa Clasher 2 itakua 1.6m kwa mwezi ndani ya mwaka utakua umerudisha mtaji unaanza kusoma faida. (Hii hata mimi nafanya)

c)Biashara ya kuchimba madini ya Gemstones
Nenda Morogoro pale chimba madini hayo yapo mengi sana, na soko na return yake ni ya uhakika (Hii nina ndugu anafanya)

d) Biashara ya kununua vitu (nguo, viatu, vifaa vya simu na simu zake, urembo, mashine za kilimo na mashine za kawaida) kutoka China ama nchi za nje.
20m ni hela inayotosha kufunga mzigo wa kutosha kutoka china na ukaja kuuza bongo, kumbuka usimamizi inabidi uwepo wew mwenyew, utapeli unahusika hapa sana kama hautakua makini. Anza kwa kutengeneza masoko yako kkoo, buguruni, manzese, mbezi (hapa nime assume unakaa dar.) Kisha kafunge mzigo China uje uwasambazie (Hii kaka yangu anafanya)

e) Nunua mazao kwa wakulima kisha nenda kauze nchi za nje (mahindi/matunda/korosho/parachichi)
Hii biashara pia inahitaji muda wako sana na usimamizi wa hali ya juu. Kuanzia shambani unapoenda kununua mafekeche ya kiserikali mpaka masoko ya uko nje kwenyewe, ko muongozo mzuri unahitajika hapa.

ASANTENI SANA
 
Mkuu Mbogo_beichee , stay blessed kwa mchango wako mzuri sana.

Hizo ideas 1 (d) & (e) nina mpango nazo hivi karibuni early next year, moja wapo:

(d) Kufuata mzigo China na kuja kuuza kwa Jumla/wholesale hapa Tz.

Hapa bado naendelea kufanya utafiti ni bidhaa gani inayotoka chap chap pasipo usumbufu wa kuiuza. Hata kama Faida ni kidogo lakini iwe yenye mzunguko mkubwa.

(e) Kununua mazao ya nafaka (specifically nalenga mchele) na kupeleka kuuza nje ya nchi.

Hapa pia bado naendelea kujifunza by desk research ili kufahamu yote ya msingi ikiwemo changamoto zake na mengineyo.
 
Back
Top Bottom