MSAADA: Mtoto amefaulu Sekondari ya AHMES, lakini shule aliyomaliza darasa la saba imefutiwa matokeo

MSAADA: Mtoto amefaulu Sekondari ya AHMES, lakini shule aliyomaliza darasa la saba imefutiwa matokeo

Wala hakuna connection anaendelea Tu labda kama unataka apangiwe shule za serikali ndio arudie. Matokeo ya darasa la Saba KWA SASA HAKUNA YANAPOTUMIKA Almradi umemaliza
Usimpotoshe mkuu!!

Hawezi kuendelea na masomo ya sekondari kama hajahitimu drs la 7. Ili apate usajili na kutambulika kama bonafide student atakayehitimu form four wanahitaji vitu vifuatavyo!

1. Awe amefanya mtihani wa upimaji kidato Cha pili yaani FTNA. Na hawezi kufanya mtihani huo kama huna PreMS number na hii inatolewa kwa waliomaliza Drs la saba yaani shule ya msingi, of which yeye hasomeki kama mhitimu.

2. Usajili kwa Sasa ni tofauti na zamani. Hata joining instruction ya shule aliyochaguliwa lazima kuna sehemu imemwambia ajaze PreMS namba ya shule ya msingi ndo automatically jina litatokea na atapata verification number ili waweze kum-enroll.

3.Details nyingi Sana za kidato Cha nne zinatokana na taarifa za mwanafunzi shule ya msingi na mitihani wa upimaji kidato Cha pili(form two wanategemea shule ya msingi). Ndiyo maana ukiingiza hizo number analetewa majina yake Kama alivyojiandikisha shule ya msingi.
 
Hawa wasikukatishe tamaa. Mwanao anaendelea kama kawaida. Wengine walimaliza darasa la sita wakaenda form one nani aliwadai matokeo?

Huko sio kala form four na six kwenye complications
Mkuu kuna kitu kinaitwa PreMS number.. usimpotoshe kabisa hatasajiliwa!
 
Mkuu kwa shule ya private hauhitaji matokeo ya darasa la saba. Mimi mwanangu yuko chuo mwaka wa pili alisoma mpaka darasa la sita na kufanya mtihani wa kujiunga na kidato cha kwanza na akafaulu, akaenda secondary private school, kamaliza kaenda A Level na sasa yuko chuo mwaka wa pili. Mpeleke mtoto asome wala usiwaze.
Mkuu mambo yamebadilika
 
Anaenda vzuri ndugu form one akuna sheria inayomzuia sio lazima mim ninandugu zangu awaijui darasa la 7 kabisa walikua wanarushwa madarasa kulingana na performance yao awajawai fanya mtihani wa darasa la saba now wapo wanapambana na module vyuon ukoo
Ni zamani mkuu, kwa sasa utaratibu umebadilika
 
Means walianza form 1 na baadaye wakafanya Mtihani?
 
Sasa Naomba kuuliza tena hiyo Prem Namba Mbona kwenye majina ya Watoto waliofutiwa inaonekana?
 
Wakuu Msaada.

Kijana wangu amemaliza shule ya msingi iliyofutiwa matokeo. Kwenye interview zote nne nilizompeleka amefaulu. Matokeo ya la Saba yaliyotolewa muda si mrefu shule yake imekubwa na tatizo Hilo.

Je, akiendelea na sekondari kwa matokeo yapi ya la Saba yatatumika? Kwa maana kwamba ana uhalali wa kuendelea na private?

Kwenye taarifa za Baraza la Mitihani atakuja atumie taarifa zipi huko mbeleni (hii watanielewa wale wanaojua utaratibu pekee kama hujui hapa pita tu)?

Dogo alipita interview zote zenye ushindani ikiwemo Ahmes sekondari.


Mh RAIS Mama etu.

Sema neno hapa watoto hawana hatia
Mm ninavyoelewa elimu ya msingi ni utambulisho tu.Atachukua cheti cha kumaliza ambacho kitamtambulisha kuwa alimaliza shule ya msingi.Yeye aanze tu sekondari ya private hakuna shida.Wanaofaulu na kuendelea ni wale wanaokwenda shule za serikali.
 
Ninachojua mimi sheria hipo form 4 tu ndo akuna mtahiniwa atakayefanya mtihani wa form4 pasi ya kuhufanya wa form tu basi hyo ya la saba kuwa pingamizi kwa mtoto kuenda form one hapana atoenda shule za serikali tu hila private anapiga mzigo tena kihalali tu sio illegal
Acha kuandika Hipo
 
Mambo yamebadilika. Siku hizi watoto wote wanaomaliza elimu ya darasa la saba majina yao yanatakiwa kuonekana kwenye mfumo.

Kinyume na hapo, mtoto hawezi kupata usajili. Hata kama unampeleka private! Lazima jina lake lionekane kwenye huo mfumo.
Wewe ndiyo mtu unayejua unachoandika.Siku hizi hata uhamisho kwa shule binafsi lazima ufanywe kuanzia kata hadi halimashauri.
 
majeshini kinatakiwa Cha darasa la 7
Wala hakuna connection anaendelea Tu labda kama unataka apangiwe shule za serikali ndio arudie. Matokeo ya darasa la Saba KWA SASA HAKUNA YANAPOTUMIKA Almradi umemaliza
 
Hata ao wanaopewa nafasi ya kurudia baada ya mwaka ni ukatili sababu unawapotezea muda na kuwasumbua wajiandae tena wa mwaka mzima wakati kosa si lao.
Hawa ni watoto wadogo ambao hawana akili ya kuwakatalia waalimu wao na mzazi wake hakuhusika na udanganyifu.

Kwa vile watoto ni wachache wanaweza kupewa mtihani mwingine mapema ikasahihishwa ndani ya siku 21 wakaendelea na elimu ya sekondari.
Jumla ni watoto 2200+
Labda wanafanya hivyo ili shule ziepuke huo mchezo
 
Ushaur wa uhakika :- Huyo mtoto hawez kufanya mtihan wa kidato cha pili bila no ya darasa la saba(hii imeanza tangu 2019 so wanaokomaa unawezekana kwa sababu walivyusha watoto wao zaman polen na endeleen kujidanganya)
Cha kufanya sasa -: Peleka mtoto wako huko alikofaul tena na suggest mpeleke Ahmes maana naijua ni the best mdogo wangu alitoka hapo kidato cha nne akiwa top ten Tanzania
Then serikali itatoa mwongozo hao watoto kurudia mtihan mwakani ye aendelee form one ila mlipie ada za kufanya mtihan mwakan na aje aende aufanye atapata no them ataitumia Ahmes kwenye mtihan wa kidato cha pili na kwa style hiyo hatakuwa amwrudia mwaka
Kumbuka hawa watoto wamefutiwa namba zao, kutokana na vituo vyao kudanganya, hivyo watapewa namba upya ambazo zitaonesha mwaka tofauti
 
Back
Top Bottom