Msajili wa Jumuiya za Kiraia: Makundi ya WhatsApp kusajiliwa Kisheria kwa TZS 200,000/-
Serikali isiyojua mipaka yake. na bado watakuja hadi majumbani kwetu kutudai kodi ya kupumua hewa ya TZ. Hizi ndio priority za awamu ya sita
 
Kwa ukimya wa waTanzania, viongozi nao wamepata god-complex, sasa wanajitengenezea kitu chochote wanaamini kitapita tu bila kelele
 
Whatsapp wanaruhusu tutumie bure, halafu wao wanataka kutoza pesa utasema whatsapp ni ya kwao.
 
Nilisema kuwa serikali ya CCM kutwa wanawaza wapi kuna pesa.
Hii pesa ya Whatsapp sasa itawatokea puani
 
Hii tabia ya serikali ya Tanzania kukosa ubunifu kwenye kukusanya mapato iishe.

Dunia yote sehemu ambayo gari used linatozwa kodi kubwa ni Tanzania.

Gari ambayo kodi yake inachukua sh. Milioni 15 nchi za Zimbabwe na Zambia ambazo hupitisha hizo gari Bandari yetu wanachaji Kodi isoyozidi milioni 5 za Kitanzania.

Ni mara 3 zaidi ya Kodi ukilinganisha na nchi zingine.

Sasa wanataka fedha za vikundi (magroup ya Whatsapp).

Kuna watu hawalali wanatumia akili zao safi ndio walibuni hiyo Whatsapp, baadaye wakabuni hayo magroup.

Sasa watu wavivu ambao hawajui kubuni chochote wanataka pesa za bure.

Ni aibu.
 
Nimeshangaa, hayo makundi ya Watsap yanazalisha nini mpaka yawe chanzo cha mapato, yaani watu mnagroup lenu la familia eti msajiliwe kah!
 
Ule mtandao wa kusambaza Internet kupitia satellite wa Elon Musk ulipigwa zengwe la kisiasa ili wawe na maamuzi ya kuzima data kipindi cha uchaguzi.

Ukiona serikali inakuja na mambo yasiyo na tija ujue imechokwa na inalazimisha kukaa madarakani.
 
hizo ndio dalili za kufilisika kimawzo na fikra yaani familia ama ukoo wenu uwe na kundi lake la whatasup then aje muhuni aseme anataka mlipie laki mbili wakati hata huyo mwenye hiyo programu hawalipishi ni mradi uwe na mtandao tu hii inafikirisha sana , huwezi kuendelea kwa kukumbatia mambo ya hovyo sidhani kama watafanikiwa , kimsingi ni wapuuzi na hawana jipya.
 
Ule mtandao wa kusambaza Internet kupitia satellite wa Elon Musk ulipigwa zengwe la kisiasa ili wawe na maamuzi ya kuzima data kipindi cha uchaguzi.

Ukiona serikali inakuja na mambo yasiyo na tija ujue imechokwa na inalazimisha kukaa madarakani.
ni mashetani kabisa. cha kushangaza machawa watakuja kuunga mkono mpaka kutoa povu la mdomo
 
Huko juu wako sawa kichwani kweli

Ova
 
Kwa hiyo mimi na kundi langu tukalipe laki mbili?


Kundi lenyewe hatuwezi mchangia mtu hata buku 5 mtu akiumwa.

Kwahiyo tunanyimwa haki ya kujumuika pamoja kisa hatuna pesa?

Hata katiba haitaki huu ujinga.
 
Back
Top Bottom