Msemaji wa JWTZ kuteuliwa kwenye NEC ya CCM, hii imekaaje?

Msemaji wa JWTZ kuteuliwa kwenye NEC ya CCM, hii imekaaje?

MKUU KAMA KUNA KITU CCM WALIJIPANGA BASI NI JESHI , HUHITAJI DARUBINI KUONA KUWA JESHI LINALOITWA LA WANAWANCHI NI JESHI LA CCM, ANGALIA WAKUU WA MIKOA, WILAYA, MABALOZI, NK
USITARAJIE KIKINUKA KUWA ETI JESHI HILO LITAKUWA UPANDE WA MLALA HOI, LITAFUATA MASLAHI YAO AMBAYO YAKO CCM, HIVI UNAWEZA TOFAUTISHA RANGI YA MAZIWA NA TUWI LA NAZI?
 
Ila kama ndie yeye vizuri sana jamaa ni kichwa sana huyu nimewahi kukutana nae na kumsikiliza nikatamani siku moja aje awe mtu mkubwa sana nchi hii.
 
It was clearly stated kuwa hakuna kufanya kazi mbili. Ameshastaafu huyo...au mnataka kila jambo la jeshini liwe published? Endeleeni kumtafuta Ben kama kashikwa ugoni kamlipieni fine arudi kijana wa watu lakini shughuli za uendeshaji wa serikali waachieni wenye mamlaka. Yakwako ndani ya nyumba yanakushinda iweje ufatilie ya jirani. Boss akirudi toka ulaya nadhani atatusaidia suala la kijana mpotevu
 
Tunajenga ukilaza kila mahali ili kuimarisha nguvu ya dikteta UCHWARA,YY ANAJUA KILA KITU,MAKOFI MEEEENGIII!!!!!
 
Tumia akili, jeshi limefungwa kisheria lkn lowassa hajafungwa kisheria. Huu ndio tunaoita kwa kingereza GRAFT CORRUPTION. Taasisi inahongwa ili itoe upendeleo.
Think out of the box, ni jeshi kama taasisi ndiyo limefungwa kisheria kutojihusisha na siasa, mwanajeshi kama raia hajafungwa kisheria kuacha jeshi ili kujihusisha na siasa. Kwa hiyo kwa huyo mteule anaweza kuamua aidha kukataa uteuzi huo na kuendelea na jeshi au akubali uteuzi na kuamua kuacha jeshi iwapo alikuwa bado anaendelea na kazi jeshini.
 
Kwani Lowassa alikuwa mwanajeshi wkt anahamia Chadema.....?issue apa ni mwanajeshi kuteuliwa kuwa kiongozi wa chama cha siasa.

Kaanza kuwa mwanachama siku hiyo hiyo aliyoteuliwa. Kabla hakuwa mwanachama wa chama chochote.

Jibu hilo hapo
 
Think out of the box, ni jeshi kama taasisi ndiyo limefungwa kisheria kutojihusisha na siasa, mwanajeshi kama raia hajafungwa kisheria kuacha jeshi ili kujihusisha na siasa. Kwa hiyo kwa huyo mteule anaweza kuamua aidha kukataa uteuzi huo na kuendelea na jeshi au akubali uteuzi na kuamua kuacha jeshi iwapo alikuwa bado anaendelea na kazi jeshini.
Kipi kinaanza kuacha na kuingia kwenye siasa au kuingia kwenye siasa na baadae ndio unaacha? Ukweli unabaki pale pale kuwa vyombo vyetu vya usalama si huru a kwani ndani yake kuna wanachama wa vyama vya siasa na hivyo hutumika kutimiza matakwa ya chama ya chama kwa hope kuwa Siku moja watapewa nyadhifa mbali mbali wakiwa kazini au baada ya kustafu.
Jambo hili ambalo malaika mtukufu analianza litkapokuja kuturudia tutajuta.
JIFUNZENI KWA SIMBA, AKISHA KULA NYAMA YA BINADAMU HATA WATOTO WAKE HUULIWA. Unafikiri ni kwann?
 
Sawa lkn hii ni picha kuwa wakati alipokua jeshini alikua ni mwanachama wa ccm. Haiwezekani kuwa wamemchukua MTU wasiomjua. Ndio maana tunasema vyombo vyetu vya usalama sio huruma na haviko tayari kuona ccm ikishindwa ndio maana hutumia mbinu yote hata za wizi kuleta ushindi kwa ccm
Kwa haraka na uhakika nchi inageuzwa kuwa ya kidikteta. Na ukiona hivyo ujue wanatafutwa akina Goring, Himmler na Joseph Goebbels. Ee Mungu tuhurumie Watanzania tumekukosea nin!!!!!!!
 
  • Thanks
Reactions: bne
Yani kweli kuna watu wanabahati zao,mtu yupo katika ajira ya serikalini anaachishwa na kuletwa kwenye chama, dah vyeti vyangu ngoja viliwe na panya tu

Alishastaafu muda akawa anafanya kwa mkataba. Na mkataba unasitishwa muda wowote. Ikiwa Lowasa aliacha CCM leo na kesho yake akapewa kadi na kugombea uraisi hamuoni ni ajabu bali hili la mstaafu kupewa majukumu mengine povu linawatoka
 
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
uanajeshi" hii ni nomination tu ambayo mtu yeyote yule leo rais ama yeyote mwenye mamlaka anaweza kumpatia raia? ama ni lazima upitie mchakato flani ktk hao wenye mamlaka ndiyo uwe mwanajeshi. Hivyo basi naamini huwezi kukoma uanajeshi wako eti tu kwa kuacha kuvaa gwanda za kijeshi ama kutimiza majukumu ya kijeshi kwa wakati huo.
Inabidi iwe wazi ukishapitia mafunzo yeyote ya kijeshi wewe ukae mbali na majukumu yote ya kiraia.
 
Kamshtaki basi kama imekuuma
Suala siyo kumshitaki, suala hapa ni uzumbukuku wako usiotaka kuuona ukweli. Jeshi la Wananchi wa Tanzania haliwezi kuchezewa kwa namna linavyoanza kuchezewa na viongozi muflisi wa Chama cha Mapinduzi. Ni lini askari huyu alistaafu na kuchukua kadi ya ccm?
 
NI UKIUKWAJI WA KATIBA AU MAJINA YAMEFANANA KATI YA MSEMAJI WA JWTZ NA HUYU MTEULE WA NEC YA CCM?
JPM JITOKEZE KUUELEZEA UMMA KUHUSU UTATA HUU.​

Msemaji wa JWTZ ni Kanali Ngemela Lubinga.

Katibu Mteule wa NEC ya CCM Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ni Kanali Ngemela Eslom Lubinga.

Katiba ya Jamhuri 1977 inasema :-

SURA YA TISA
MAJESHI YA ULINZI

Ibara ya 147.

Ibara ndogo ya (3),
Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chohote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na haki ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.

Ibara ndogo ya (4),
Kwa madhumuni ya ibara hii, "mwanajeshi" maana yake ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi la Kujenga Taifa.

----------

jamiiforums.com Earn 10$ for every 30 second Task. Internet Job, ok it must be digested more
 
Back
Top Bottom