Msemaji wa JWTZ kuteuliwa kwenye NEC ya CCM, hii imekaaje?

Msemaji wa JWTZ kuteuliwa kwenye NEC ya CCM, hii imekaaje?

- Lakini Lowassa alipoteuliwa kugombea Urais Chadema haikukushangaza imekushangaza huku? Duh!

le Mutuz Nation

Kila mara nakuambia huwa unakuwa umri kwa maana ya miaka kusonga na sio akili wala uelewa. Mada hapa ni mwanajeshi kuingizwa kwenye vyeo vya kisiasa kulingana na takwa la katiba yetu. Je nikuulize, Lowassa ni mwanajeshi?
 
CCM ndio wenye nchi so wanafanya wanavyotaka! Si unaona hata vikao vya Chama vinafanyika jumba jeupe
 
Kila mara nakuambia huwa unakuwa umri kwa maana ya miaka kusonga na sio akili wala uelewa. Mada hapa ni mwanajeshi kuingizwa kwenye vyeo vya kisiasa kulingana na takwa la katiba yetu. Je nikuulize, Lowassa ni mwanajeshi?

- Nilidhani utai quote Katiba ya Chadema kuhusu Mwanachama mwenye sifa za kugombea urais kwani inasemaje kuhusu Mgombea mgeni ambaye hajamaliza hata miezi mitatu? hahahahaha kila mara nakuambia watoto wachanga kama wewe wapo wodi ya Mwaisela husikii why?

le Mutuz
 
Ni hivi hakuna anayepuuzia masuala ya katiba. Hao walioona kuwa katiba imevunjwa mimi nimewauliza then what? Miaka yote kilio ni kile kile. Uzi ukishafika page ya 8 au 10 basi inaishia hapo. Kama mmeona ni kosa then nini kinafuatia. Au mkishapost humu watu wakawatukana hao CCM basi kifungu cha sheria kilichovunjwa kitanyooka.

Ndugu nimekuwa nikifuatilia majibu yako mengi hapa jukwaani kwenye uzi huu na nyingine pia. Unaoneka kujibu kwa kejeli, dharau na kiburi cha madaraka. Sishangai kwani hata awamu hii inaonyesha kuenda na haiba yako. Hiki kinachofanyika kwako na wengineo wa aina yako hakuna shida kwani mnaamini mna ruhusa ya kufanya chochote kwa utashi wenu na katiba mnaitumia mnapodhani haiwabani. Ila mtambue kuna kitu mnapandikiza bila kujua madhara ya muda mrefu kwa mapenzi yenu ya muda mfupi mtakaokuwa madarakani. Hao wanajeshi kuanza kuwapa vyeo vya kisiasa iko siku mtataka watoke mtashindwa, hao walioona hiyo hatari huko nyuma sio wajinga kulingana na aina yao ya mafunzo. Kumbuka siasa ni ushawishi na sio amri, je kuna mwanajeshi anayefundishwa ushawishi?

Kiburi kilichowajaa kwa sasa ni kweli kitawafanya mfurahi na kujipongeza kwamba mmenyoosha nchi. Lakini kumbuka nchi hii ina vyama vingi vya siasa, hao jamaa watastaafu na wakati huohuo wataona fursa kwenye siasa, huenda wakaamua kujiunga huko. Sipati picha watakapotumia ushawishi wao wa wengine waliowaacha huko vikosini wapate support kupata madaraka ili wawape vyeo pindi wakiingia madarakani. Ni nani akitarajia mawaziri wakuu wastaafu na hata mawaziri wangejiunga kwenye vyama vya upinzani tena kwa kiu ya madaraka? Sumu haionjwi kwa kuilamba. Leo ongozweni na kiburi cha madaraka ila mtakuja kugundua mmechemsha mkiwa wazee na huku madhara yakiwa ndani ya nchi, leo wote tunaona malezi na tamaa ya mali ya vijana wetu, sasa nini kitatokea huko mbeleni muda utaamua.
 
- Nilidhani utai quote Katiba ya Chadema kuhusu Mwanachama mwenye sifa za kugombea urais kwani inasemaje kuhusu Mgombea mgeni ambaye hajamaliza hata miezi mitatu? hahahahaha kila mara nakuambia watoto wachanga kama wewe wapo wodi ya Mwaisela husikii why?

le Mutuz

Mimi sio mwanacdm hivyo kwa bahati mbaya sijui katiba yao inasemaje kuhusu hilo. Ila nikiri ni shabiki wa chama hicho. Pitia post zangu hapa jukwaani, mimi ni mmoja kati ya watu niliopinga na bado naendelea kupinga uwepo wa Lowassa ndani ya cdm tena kama mgombea wa urais. Ila kwa kuwa sio mwanachama hivyo sina nguvu ya kumpinga kwani nadhani wanachama ndio wenye nguvu hiyo kikatiba. Je una lingine mzee?
 
Wwe ndo hujui taratibu sasa nikueleze pamoja na ujinga wako!!ukiacha sheria na katiba na nini sijui;rais ana mamlaka ambayo amepewa kikatiba kufanya unayoyaona!tatizo watz wengi hatujui sheria na elimu imetupita kushoto!isome katiba,mamlaka ya rais halafu ndo uje unitolee povu lako;Ndo maana alimtoa chagonja akambadilisha jeshi na kumpeleka fire,alimtoa mlowola polisi akampeleka takukuru,na hao wote walikuwa wako kazn halaf bado unahoji anakiuka tartibu zipi??
Akili ndogo ni tatizo. Rais akiamua kutumia Katiba kifalme atafanya yote pamoja na hayo unayoyasema. Lakini Rais mwenye upeo mkubwa wa uongozi ni lazima atambue kuwa "si utamaduni wa kitanzania" nikiazima maneno ya Mwalimu Nyerere, kupuuzia misingi ya utawala bora katika nchi ya kidemokrasia
 
Mimi sio mwanacdm hivyo kwa bahati mbaya sijui katiba yao inasemaje kuhusu hilo. Ila nikiri ni shabiki wa chama hicho. Pitia post zangu hapa jukwaani, mimi ni mmoja kati ya watu niliopinga na bado naendelea kupinga uwepo wa Lowassa ndani ya cdm tena kama mgombea wa urais. Ila kwa kuwa sio mwanachama hivyo sina nguvu ya kumpinga kwani nadhani wanachama ndio wenye nguvu hiyo kikatiba. Je una lingine mzee?

- Ok sasa unashangaa CCM kuchagua kiongozi wake ambaye ni mfanyakazi wa Serikali yake! Are serious or just kidding?

le Mutuz
 
Yani kweli kuna watu wanabahati zao,mtu yupo katika ajira ya serikalini anaachishwa na kuletwa kwenye chama, dah vyeti vyangu ngoja viliwe na panya tu
fanya kazi kwa bidii na kujituma mkuu. kwa style hii ya kulalamika nyuma key bodi mbona utasaga meno kwa kipindi kirefu sana
 
Umeshaona fursa kijana ... ?! [emoji23] [emoji23] [emoji23]

Hata Mahakama sasa ziko Lumumba .., usijisumbue ...

Ni wale vilaza kuamka tuu ndio itasaidia, and it might take a decade such a thing to happen ...
Tulia kaka tupige hela we hutaki nivute Ractis
 
Ndugu nimekuwa nikifuatilia majibu yako mengi hapa jukwaani kwenye uzi huu na nyingine pia. Unaoneka kujibu kwa kejeli, dharau na kiburi cha madaraka. Sishangai kwani hata awamu hii inaonyesha kuenda na haiba yako. Hiki kinachofanyika kwako na wengineo wa aina yako hakuna shida kwani mnaamini mna ruhusa ya kufanya chochote kwa utashi wenu na katiba mnaitumia mnapodhani haiwabani. Ila mtambue kuna kitu mnapandikiza bila kujua madhara ya muda mrefu kwa mapenzi yenu ya muda mfupi mtakaokuwa madarakani. Hao wanajeshi kuanza kuwapa vyeo vya kisiasa iko siku mtataka watoke mtashindwa, hao walioona hiyo hatari huko nyuma sio wajinga kulingana na aina yao ya mafunzo. Kumbuka siasa ni ushawishi na sio amri, je kuna mwanajeshi anayefundishwa ushawishi?

Kiburi kilichowajaa kwa sasa ni kweli kitawafanya mfurahi na kujipongeza kwamba mmenyoosha nchi. Lakini kumbuka nchi hii ina vyama vingi vya siasa, hao jamaa watastaafu na wakati huohuo wataona fursa kwenye siasa, huenda wakaamua kujiunga huko. Sipati picha watakapotumia ushawishi wao wa wengine waliowaacha huko vikosini wapate support kupata madaraka ili wawape vyeo pindi wakiingia madarakani. Ni nani akitarajia mawaziri wakuu wastaafu na hata mawaziri wangejiunga kwenye vyama vya upinzani tena kwa kiu ya madaraka? Sumu haionjwi kwa kuilamba. Leo ongozweni na kiburi cha madaraka ila mtakuja kugundua mmechemsha mkiwa wazee na huku madhara yakiwa ndani ya nchi, leo wote tunaona malezi na tamaa ya mali ya vijana wetu, sasa nini kitatokea huko mbeleni muda utaamua.

Tunga kitabu au ungeweza hata ku summarize hizo pumba zote hadi ziwe mchele. Maana nimeshindwa hata kusoma. Tofautisha maana ya comment na insha
 
- Ok sasa unashangaa CCM kuchagua kiongozi wake ambaye ni mfanyakazi wa Serikali yake! Are serious or just kidding?

le Mutuz

Anyway kwa bahati mbaya naongea na kobe aliye juu ya mti. Nadhani ukimuona kobe juu ya mti jua atakuwa kapandishwa. Wewe wakati mwingine nashindwa kujadiliana na wewe japo umri wako ni mkubwa ila kiwango chako cha kufikiri nakifahamu. Wewe hapo ulipo unaweza usione madhara yake kulingana na aina ya maisha uliyolelewa kwani hao wanausalama walikuwa karibu kabisa na familia yenu kutokana na nafasi aliyokuwa nayo mzazi wako. Sikulamu kwa hilo kwani hiyo ni bahati ya kuzaliwa na wala sina inda nayo. Kwa wenye uelewa mpana walijua madhara ya kuwachanganya hao jamaa na siasa hasa kwenye mfumo wa vyama vingi. Leo mnawaweka kwenye madaraka, ila mtakapokaa nao na mijadala yenu watajua ili muwepo madarakani ni lazima wao wawe upande wenu. Itakuja siku hawataona umuhimu wa kusubiri nyie muwape madaraka kwani uwepo wenu unawategemea wao, hivyo wataona bora wakae wao na kisha wawagaie nyie nafasi. Hapo ndio patachimbika. Tunaona vijana wengi wa leo wanachofanya kwenye nafasi za umma ili kukidhi tamaa yao ya kupata utajiri wa harakaharaka. Na huko jeshini kuna vijana pia, watajua ili utoke mapema ni kufanya uwezavyo ili kupata nafasi kwenye siasa. Watakapoanza kukosa nafasi huko ccm wataona nafasi wanaweza kuipata toka vyama vingine vya siasa. Nadhani umeona kilichotokea kwa mawaziri wakuu wawili wastaafu baada ya kukosa walichotaka ndani ya ccm ni nini wamefanya kwa kwenda upinzani kusaka hicho wanachokitaka. Vuta picha ya mbali kwa hawa wanajeshi mnaoanza kuwavuta ndani ya box mkidhani wataishia hapo mnapowagawia.
 
Tunga kitabu au ungeweza hata ku summarize hizo pumba zote hadi ziwe mchele. Maana nimeshindwa hata kusoma. Tofautisha maana ya comment na insha

Jazba. Hiyo ndio raha ya demokrasia unaweza kusema upendacho na kila mtu anaweza kuchangia anavyoona. Huna ulazima kusoma kitu kinachopunguza ufahari wako.
 
Jazba. Hiyo ndio raha ya demokrasia unaweza kusema upendacho na kila mtu anaweza kuchangia anavyoona. Huna ulazima kusoma kitu kinachopunguza ufahari wako.

Jazba unaniletea mimi ambae sikulishi wala sikuvishi. Hunijui sikujui. Kweli bavicha mna matatizo ya akili iko siku mnaweza hata kuweka BIFU na UKUTA AU KIVULI CHAKO
 
Zamani kabla ya mfumo wa vyama vingi, jeshi letu lilikua sehemu ya mfumo wa siasa. Hilo lilifanywa makusudi kwa vile chama ndio kilidhika hatamu hivyo jeshi wakawa na mkoa wa jeshi wa chama..ulikua uamuzi wa busara.
Mara baada ya kuingia mfumo wa vyama vingi Mwalimu alishauri kulitoa jeshi katika mfumo wa vyaka. Katiba ikabadilishwa na kukataza jeshi kujiunga au kuwa mwana chama wa chama chochote cha siasa. Waliruhusiwa kupiga kura tu.
Huu nao ni uamuzi wa husara na hekima kubwa kuchukuliwa. Lengo kulifanya jeshi letu liwe la Tanzania wote bila ya kujali chama cha mtu yoyote. Hii pia ni kuendana na mfumo wa vyma vingi tukiruhusu jeshi kuingilia siasa , wapo watakao na mapenzi na chadema , nccr au cuf....hivyo tutaligawa jeshi letu.
Waasisi wa taifa na mfumo huu waliliona hili. Hivyo ni utaratibu mzuri ....
Sasahaya yasasa hatujui sababu zake ni zipi kuwaingiza katika siasa...
 
akiteuliwa anastaafu uanajeshi, itachukuliwa kuwa amestaafu
That is a hoax!! Let us be serious. Kwa nini tuwaingize wanajeshi wetu kwenye siasa kabla hawajastaafu? Tumeona Trump akiwateuwa wanajeshi kuwa mawaziri wake, lakini ni wale waliostaafu jeshi walio katika mrengo wa Republican, na wala si walio kazini. Vinginevyo ni kuwapandisha vyeo basi.
 
Jazba unaniletea mimi ambae sikulishi wala sikuvishi. Hunijui sikujui. Kweli bavicha mna matatizo ya akili iko siku mnaweza hata kuweka BIFU na UKUTA AU KIVULI CHAKO

Umepandisha jazba mpaka umetoka kwenye hoja ya msingi na kuweka wazi udhaifu wako. Kwa bahati mbaya mimi sio mwanacdm wala sijawahi kuwa mwanacdm. Sasa nimegundua kwanini unaongea kwa kejeli, jazba na dharau. Samahani kwa nilichokuambia nilitaraji ujengaji wa hoja kumbe nimeishia hapa.
 
Back
Top Bottom