MSHANGAO: Hadi Uswizi watu wanapanga foleni ndefu kupokea chakula cha bure Corona imeleta maajabu

MSHANGAO: Hadi Uswizi watu wanapanga foleni ndefu kupokea chakula cha bure Corona imeleta maajabu

Tofautisha utajiri wa pesa na utajiri wa chakula. Kuna muda pesa inakosa thamani kwasababu vitu vinakua havipatikani kwasababu ya lockdown, watu hawazalishi vyakula.

Hakuna uhaba wa chakula Ulaya, wana chakula kingi mpaka wanamwaga, wana kila teknolojia ya kuzalisha chakula hata cha Maabara, ...
 
Familia ya Dr Mahiga na Rwakatale wakikubalina na wewe, nami pia nitakubaliana nawe. Inaonekana wewe hayajakupata ndio maana unaona uchumi ni bora kuliko maisha ya watu.
Ndo mjue lock down sio mchezo.
Watu HAWAFANYI kazi watapata wapi hela.?.
Na afadhari hyo serikali inawajali hao raia.
Hivi unadhani magufuli atakuwa anagawa chakula akitangaza lock down?.
museven kajitahidi kuwapa wananchi wake kilo 6 za unga na kilo tatu za maharage.
Zimepita karibia wiki 3 sasa hivi kimyaaaa hagawi tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kupanga kupata chakula cha bure siyo tatizo. Hapa ni suala la kuchagua - kuokoa maisha ya watu ama uchumi. Hakuna mtu anayesema lockdown haina madhara. Ni issue ya kuchagua kati ya mali na maisha ndio inayoongolewa. Waswisi ama Wamarekani ama Waingereza kupata chakula cha bure haku-justify hata kidogo kile kinachofanyika Tanzania.
US watu wanapanga foleni ya chakula cha bure.
Wazungu kabisa wa US na ninaona live Kila siku.
 
Kupanga kupata chakula cha bure siyo tatizo. Hapa ni suala la kuchagua - kuokoa maisha ya watu ama uchumi. Hakuna mtu anayesema lockdown haina madhara. Ni issue ya kuchagua kati ya mali na maisha ndio inayoongolewa. Wengine wamechagua kuokoa maisha na kuacha uchumi ubomoke. Rais wa Ghana alisema, uchumi hujengwa lakini maisha yakiondoka, ndio basi, hayarudi. Mahiga na Rwakatare ndio wameondoka hivyo. Hatutawaona tena. Waswisi ama Wamarekani ama Waingereza kupata chakula cha bure haku-justify hata kidogo kile kinachofanyika Tanzania.
Wale jamaa wa kulilia lock down hauwezi kuwaona hapa.
Sijui waliwaza nini?.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzuka wanajamvi

Kamwe usingewaza tukio kama hili kutokea Uswizi. Korona (pathetic virus) imeleta shida kwa kipindi kifupi sana. View attachment 1446109

Yani watu Uswizi wanapanga foleni ndefu tena ya zaidi kilometre moja kupewa chakula cha bure tena wanawahi kupanga mstari kwaanzia saa kumi na moja asubuhi.
View attachment 1446109View attachment 1446113
Kwa sasa hivi Uswizi imethibitisha watu 30, 305 wana maambukizi ya korona na vifo ni 1800.View attachment 1446121

Uswizi ni nchi inayoongoza kwa maisha bora na malipo mazuri ulaya na duniani hata kwa wabeba boksi.
View attachment 1446118

Hata kwenye kati ya jiji Tajiri duniani Geneva hali ya uchumi imedorora na imeleta hali ngumu ya kiuchumi kwa watu waliokuwa wanafanya kazi kwenye housekeeping, hoteli, migahawa, kilimo na ujenzi
Izo foreni apa Africa zingereta shida sana, angetokea mzeee mmoja akaaribu ustaarabu na fujo ingechachamaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
California foleni ndefu ya makilometa watu na gari zao wanapiga foleni benki ya chakula kupokea chakula cha bure .

Usa anafikiria kuishitaki China kwa kusababisha kwa makusudi au kwa uzembe corona kuenea duniani
 
Kupanga kupata chakula cha bure siyo tatizo. Hapa ni suala la kuchagua - kuokoa maisha ya watu ama uchumi. Hakuna mtu anayesema lockdown haina madhara. Ni issue ya kuchagua kati ya mali na maisha ndio inayoongolewa. Waswisi ama Wamarekani ama Waingereza kupata chakula cha bure haku-justify hata kidogo kile kinachofanyika Tanzania.
Sijui Tanzania imeingiaje hapa, ila nia yamgu ni kumuonyesha niliyem-quote kuwa wazungu wa US wanapanga foleni kubwa tu kupata chajula cha bure. Tofauti na dhana yake kuwa ni wahamiaji ndio wanafanya hivyo.
 
Ni nchi kama Uswisi. Usipofanya kazi, huli.


Uswisi wana social system inayotoa hela ndefu kwa wananchi wake wasio na ajira, na inatosha kununua chakula na mahitaji mengine ya lazima, hivyo Mswisi hahitaji chakula cha bure, ...
 
Uswizi ni nchi inayoongoza kwa maisha bora na malipo mazuri ulaya na duniani hata kwa wabeba boksi.
Na ndio maana imemudu kuwalisha raia wake. Ingekuwa nchi maskini isingemudu kuwalisha raia wake. Kwa ufupi, thread yako inajijibu yenyewe na wala haukutakiwa kushangaa
 
Hakuna uhaba wa chakula Ulaya, wana chakula kingi mpaka wanamwaga, wana kila teknolojia ya kuzalisha chakula hata cha Maabara, ...
Anaye zalisha ni nani ilihali hata wazalishaji wapo lockdown (stay home). Anaye fungua duka au hotel au kiwanda ni nani ilihali wote wapo home lockdown. Anayekwenda kazini kuzalisha hivyo vyakula ni nani mkuu. Tumia akili kidogo basi uelewe hii point yangu.

Kwa kuongezea tu watu wanao weza kuwa vyakula ni wakulima tu ambao wamelima vyakula vyao wenyewe na wamevihifadhi. Matajiri wenye pesa nao pamoja na pesa zao kama hawajanunua chakula kabla ya lockdown lazima wateseke.
 
Anaye zalisha ni nani ilihali hata wazalishaji wapo lockdown (stay home). Anaye fungua duka au hotel au kiwanda ni nani ilihali wote wapo home lockdown. Anayekwenda kazini kuzalisha hivyo vyakula ni nani mkuu. Tumia akili kidogo basi uelewe hii point yangu.

Kwa kuongezea tu watu wanao weza kuwa vyakula ni wakulima tu ambao wamelima vyakula vyao wenyewe na wamevihifadhi. Matajiri wenye pesa nao pamoja na pesa zao kama hawajanunua chakula kabla ya lockdown lazima wateseke.

Supermarket zote zipo wazi na zimejaa vyakula na mahitaji mengine, hakuna uhaba wa chakula Ulaya hata pamoja na lock down, isitoshe siyo kila kitu kimefungwa, machinjio ya wanyama, viwanda vya vyakula vinapiga kazi kama kawa kama vile hospitali au madereva wa treni na mabasi au polisi na jeshi, wote hao lockdown haiwahusu, ...
 
Hakuna Mswisi asilia hata mmoja kwenye hiyo foleni, Mswisi hawezi kupanga foleni ya chakula cha bure leo hii, itachukuwa miaka 20-50 mfululizo ya ,,lockdown” Mswisi kufikia hali hiyo, na Mswisi akifikia hapo ujue Duniani kwingine watakuwa wameanza kula watu, ...
Wewe kidogo unaelewa umejitahidi but sio mbaya kwanza kabisa nianze kuweka sawa Migros sio government ni private owned so tusiingizane chaka kipuuzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swiss population ni 8.6 million people which is 660k ni non swiss na wakimbizi hii nchi isikie tu usijidanganye kabisa level ya development hapa ni miaka 2500 ijayo kwa huko kwetu kwa mzee jiwe kiburi, unawajua mateja ambao huko kwetu wapo vituo vya daladala wanapigwa debe?? Uswiss wanapewa unga bure hawanunui yani jobless anapewa social support unaongelea kitu ambacho nafikir haukijui.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Poor ni relative term, kwa maana ya kwamba mtu anayeitwa ,,poor” Uswisi pesa anayolipwa kwa mwezi na Serikali kwa TZ yetu ni upper middle class, isitoshe, wana vigezo tofauti kabisa na vyetu vya kupima umaskini, na hao wanaoitwa masikini > 85% siyo Waswisi asilia ni wageni/wahamiaji kutoka third World na Ulaya ya Mashariki, ...
Thanks

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom