Mstari mwekundu wa Iran umeshavukwa lakini bado wanatii amri

Mstari mwekundu wa Iran umeshavukwa lakini bado wanatii amri

Halafu pia we ni muongo na uchambuzi wako hauna mashiko.NETANYAHU MWENYEWE ALISEMA HAKUNA MPAKA WA RAFAH KUFUNGULIWA MPAKA ISRAEL ITOE TAMKO.Ndio maana Emir wa Qatar Althani alitumika kuzungumza na Netanyahu ili aruhusu magari ya msaada kuingia.Akaanza kuruhusu magari 20 kwa siku kuingia mpaka msaada utosheleze.Halafu hujasema kuwa USA anapiga kelele Iran isijihusishe na vita pia ushasahau kama Mfalme Wa Jordan alitamka katika kikao cha Arab peace summit kuwa kama mgogoro ukiendelea na Gaza ikikandamizwa waarabu hawatosita kuingilia vita.Tizama taarifa ya habari kijana USA kila uchwao anatafuta namna ya kuwaziba masikio waarabu kupitia vikao ili wasije kubali wito wa Iran kuisaidia hamas.Naona kuna mengi huyafuatilii yanakupita.Pia haukufuatilia kuwa Muhammad bin Salman amesitisha mahusiano ya kidiplomasia na Israel na amemtamkia Biden kuwa kama Iran itachukua hatua zaidi kuwatetea Palestina basi wao wataungana nao.Wakati huo Jordan,Iraq na Pakistan imefunga balozi za Israel na kuwafukuza na mpaka ndege za Israel haziruhusiwi kutua katika viwanja vyao.Usisahau Pia kuwa Iraq imetamka wazi kuwa kama italazimika mpaka makundi ya washika silaha yataungwa mkono kama ukandamizaji utaendelea Palestina.Hapo tayari hata kama vita itaisha Israel atakua na anguko la kidiplomasia pale middle east na kupitia mkutano wa arab peace summit ulofanyika Misri mataifa ya kiarabu yashakiri na kusema kuwa hawajihisi salama tena kuwepo na Israel kwa yanayoendelea.Kizazi hiki huwenda kinakaa kimya je unadhani kizazi kijacho kitafanyaje na kama hivi Israel supporter wake mkubwa ni USA ???
Mimi huwa nafuatilia maneno yao halafu napima na vitendo vyao.Nikiangalia naona maneno ni mengi na vitendo ni vichache na kinyume cha maneno.
Unavyoona wewe hapa ilipofika Jordan alipaswa kusema au kuchukua hatua ya kuvunja mkataba na kuacha mpaka wazi.Au unavyoona wewe Misri ni wa kulalamika kuwa watu wanakufa kwa njaa au ni kutoa tamko napeleka misaad na ukiizuia au kunipiga napambana na wewe.
Unajua kuwa upekuzi wa malori unafanyika ndani ya Misri na Rafah imepakana na Gaza na haikupakana na Israel.
 
Ndio maana zimepelekwa meli vita2 huko middle East kutoka USA.
Ndio kaka inajulikana kuna meli vita mbili na manowari moja ikiwa na askari maji zaidi ya elfu ishirini.Ila kaka hiyo Iran ioneni hivyo hivyo yeye ndiye aliyetia ugumu wa Russia kuanguka huko Ukraine kwa kumsaidia Russia silaha za makombora na Drones na ukumbuke USA alitoa msaada mkubwa tu huku Ukraine na haukufua dafu.
 
Hakijulikani kitafanyika nini maana kila mmoja anasema muelekeo wa vita unategemea Hassan Nasrallah ataiamuru nini Hizbollah maana hakutoa kauli mpaka sasa.Ila kiuhalisia kama full scale war itaanza kusini mwa Lebanon IDF haina uwezo wa ku repel mashambulio kote kote .Chochote kinaweza kutokea na ndio maana kuna vikao vingi vinakaliwa kujadili mzozo wa Gaza.
Syria naye anaweza kuwa muamuzi mzuri wa vita kwani kila siku vituo vyake na viwanja vya ndege vinapigwa na Israel na hajawahi kurusha makombora kutoka milima ya Golan kushushia Tel Aviv.Hii ingekuwa ni fursa kujibu mapigo kwa ajili ya Gaza na kwake mwenyewe.
 
Ndio kaka inajulikana kuna meli vita mbili na manowari moja ikiwa na askari maji zaidi ya elfu ishirini.Ila kaka hiyo Iran ioneni hivyo hivyo yeye ndiye aliyetia ugumu wa Russia kuanguka huko Ukraine kwa kumsaidia Russia silaha za makombora na Drones na ukumbuke USA alitoa msaada mkubwa tu huku Ukraine na haukufua dafu.
Russia na Ukraine ni kama vita imefika ukingoni.
 
Tangu jeshi la IDF liweke vifaru vyake pembezoni mwa Gaza ikitishia kuingia ndani ya Gaza kuwasaka Hamas,Iran imekuwa ikitoa maonyo makali kwa Israel isithubutu kufanya hivyo kwani itakuwa ni kuvuka mstari mwekundu katika mzozo huo ikiashiria na wao wataingilia kati kupambana kuwatetea wapalestina.

Tangu Ijumaa iliyopita jeshi hilo La IDf limetangaza kuvusha vifaru vyake kuingia Gaza. Ijapokuwa vifaru hivyo vimekuwa vikipata upinzani mkali na kulazimika kurudi nyuma kutoka kwa Hamas, hata hivyo ni kweli vimevuka mpaka na vimeuvuka huo mstari mwekundu uliochorwa na Iran.

Kinyume na kurudisha mapigo kwa kasi Iran imeendelea kutoa matamko ya kubembeleza na kulalamika na kuonya zaidi kwa kusema wao wameambiwa wasiingilie vita hivyo lakini mbona Marekani inazidi kuiunga mkono Israel.

Uungaji mkono huo wa Marekani na washirika wake hasa UK ni kweli upo na uko kwa maneno na vitendo.Bado tu Iran inaendelea kushuhudisha watu kuwa hao walioamrisha wakae kimya wanavunja makubaliano.

Muda huo huo Israel ikiwa imevuka mpaka na ndege zinadondosha mabomu ikiwemo aina mpya ya Iron sitng, nchi kama Saudia zina ratiba ya kukutana na viongozi wa Marekani wiki ijayo kuzungumzia masuala ya Gaza na uwezekano wa kusitisha vita. Inawezekana wanachokusudia kukizungumza sio kusitishwa vita bali wana ajenda nyengine tofauti .

Hayo yote yakitokea Gaza, kule ukanda wa magharibi na mashariki, kiongozi wa PLO ndio kabisa amepiga kimya kama kwamba ni mgonjwa huku walowezi wa kiyahudi wakiwaua wapalestina na kuwafukuza kwenye maumba na mashamba yoa.
Sambamba na walowezi jeshi la IDF limekuwa likipiga kutoka angani kama linavyofanya kule Gaza.

Kuhusu yanayowakuta wapalestina wa upande huo,raisi Biden ametoa tamko jepesi la kutaka walowezi waache kuwapiga wapalestina na upande wa Shinbet, shirika la ujasusi la Israel wametoa matamko kama hayo bila kutaka jeshi la IDF kuacha mashambulizi yake.

Kila mmoja kati ya wale walioonekana kuwa wangekuwa watetezi wakali na wenye sababu za kufanya hivyo kwa wapalestina katika muda ambapo misaada yao ni ya lazima, watakuwa wana sababu zao ambazo hawajaweza kuzidhihirisha.Kubwa linalofanana kwa wote ni kuhofia madaraka na mipango yao kwa hofu kuwa Marekani na Israel zitawapiga au zitawavunjia mipango yao hiyo.

Kwa mfano Saudia wana mradi wa kuigeuza nchi hiyo kuwa pepo ya dunia ambao wasingependa urudi nyuma na hasa kwa vile wameshatumia gharama kubwa sana mpaka hapo walipofika.Watu watasemaje ikiwa miradi hiyo haitokamilika.

Wakati watu wanakufa kwa njaa na kiu Gaza, Misri imetoa sababu za kilemavu za kutokufikisha misaada Gaza ikiilaumu Israel wakati kumbe mpaka wa Rafah wala haujapakana na Israel, ni baina yake na Gaza tu na pia upekuzi wa malori ya misaada hufanyika kilomita 62 ndani ya Misri kabla ya hata kufika huko Rafah.

Iran kwa upande wake iko karibu kukamilisha kurutubisha silaha zake za nyuklia na sijui zikikamilika wanakusudia kumpiga nani.
Kimya cha Mahmoud Abbas na viongozi wenzake wa PLO ni ahadi ya kumilikishwa Palestina pamoja na Gaza kitu ambacho baada ya Israel kufanikiwa kuikamata Gaza kama watafanikiwa wala hakitotekelezwa.
Maelezo na sababu ni kama hizo kwa Syria na Jordan.Kila mmoja akiwa na hofu ya kitu fulani alichonacho mkononi.
Kilichobaki ni Hamas wapigane kwa nafsi zao kwa silaha hafifu walizonazo wakitegemea msaada wa Allah mwenye nguvu za kweli na ambaye rehema zake huenea kote na huja wakati usiotegemewa.

Hapo mwishoni hapo dah 😭😭😭
 
Niwah kusema humu kwa mtoa mada mmoja ....watu wanachukulia kimihemuko ya kidini na skin color hii vita.. wakat wakubwa wa dunia wala hawako huko

Nikasema suluhisho la hii vita ni mpaka wakubwa waamue.. maana wote hao wanachagua upande kutokana na kuangalia watafaidikaje Arab league wote wataishia kutoa matamko.. ni waislam wenzao na ni waraab wenzao.. ila sababu kwa hao the likes of Saudia na iran.. wanaona they have more to loose wakiingia.. na hawana maslah ya moja kwa moja pale ..

Hao Misri, Syria, Iran (nazungumzia viongoz na wafanyabiashara wao) sio raia wa kawaida wa hizo Inchi.. wote wanajua wakishajitoa muhanga kuingia basi hawana maisha marefu kwenye uongozi..na watakosa kula
Mema Ya nchi Zao wakikumbuka ya Sadam
Na ghadafi.. wanapiga kimya

Huyo bashaar wa Syria aliponea chupuchupu kutolea na hapo ni sababu alikuwa anagombewa na wakubw awa Europe wawili.. la
Sivyo kama Mrusi angekuwa hana Maslah Syria zaman sasa hv Syria ni Iraq au Libya ingine

So Iran anaenda kimachale nia ya kuingia anayo ila desire ya kuendelea kula utamu wa kula mema ya nchi ni kubwa so anauma na kupuliza..

Misri utawala wa sasa hv ni puppet wa westerns.. same as Syria.. Jordan na hatak hata kuuguswa maana anajua Akijifanya kidomo ataletewa raman za karne ya kwanza aambiwe jiko la familia ya Musa ilikuwaga hapo pia yeye anapaswa kuchapa lapa..baadhi ya maeneo..

Raia wa kawaida wataandamana nawatapiganana wao kwa wao ila nothing will change

China na Urusi wote wanalaan ila sababu hawana maslah hawana haja ya kujitia hasara

Dunia ya sasa hv tutakusaidia tukiona fursa kwako kama hakuna ache ufe tu.. angalia somali na sudan wanavyochinjana..
Wakubwa wanauza silaha tu

Wakubwa wote maisha yao kuliana timing nani awe wa kwanza kufulia mwingine akamate usukan awe anatawala dunia.. Urusi hatak ya USSR yajirudie, china akiangalia Japan alikuwaga super power akamvimbia USA na Westerns nao anawatumikia anaona mh ngoja kwanza..

Naked Truth 👆👆👆
 
Hii Dunia duh! Ivi ya urusi na ukraini imeisha? Na Sudani ikoje? Na drc ikoje? Kiukweli Dunia inalewesha
 
Ukweli ni kwamba waarabu wameichoka HAMAS, wengi sasa wanataka maendeleo kwenye nchi zao, hawana muda na pumba za dini za vita vita kila wakati, kwa sasa mlichoanzisha pambaneni kukimaliza wenyewe.
Huwa wanaamini kwenye fujo sana. Nchi zao zimeshakuwa magofu mfano hai Libya.
Kitendo cha kuvamia, kuua raia na kuwateka raia kwenda nao Gaza, ni kitendo ambacho hakivumiliki.
 
Kwanini hao Palestina hawashinikizi HAMAS kuwaachia mateka wa Israel ili Israel iache kushambulia?

Na kwanini hawapambani na HAMAS wanaowaponza? Mbona ni kama wanawakumbatia?
 
Mstari mwekundu umevukwa?Yemen washajiunga, na Hezbollah wanajiunga Ijumaa rasmi
 
Mstari mwekundu umevukwa?Yemen washajiunga, na Hezbollah wanajiunga Ijumaa rasmi
Kama unazijua ratiba vizuri.Vipi Syria na Jordan.Na ni ipi ratiba ya Misri.
 
Iran anapigana ila huwezi kumuona.ukisikia Syria na Iraq American military base zinapigwa ni Iran. Yemen , hizbullah hao wote wanafadhiliwa na Iran.
 
Back
Top Bottom