Next Level
JF-Expert Member
- Nov 17, 2008
- 3,153
- 180
Hii thread ni nzuri sana. Nimependa sana mchango wa Malila. Anaonekana ni mjasiria mali mzuri sana na generous. Watu wengi wana mawazo ya kibiashara lakini ni wachoyo kuwashirikisha wengine -- most of us are selfish. Lakini Malila ametoa na ndio maana anaongezewa.
Changamoto kwetu wana JF, tubadilishane mawazo na kukuza JF community!
JF is second to none!
A Ring with a Tanzanite Gem It does not make economic sense for Tanzania, which is the only producer of tanzanite (a name derived from the mineral's country of origin ) in the world, to continue wallowing in poverty. Oil has made the Middle-East Rich. Gold has made South Africa rich- Why is Tanzania poor?
Tanzanite (discovered in 1967 at Merelani Hills, located near the East African towns of Arusha and Moshi in northern Tanzania) is a popular and well-known gemstone and a staple of the jewelry trade. Thanks to the power of promotion in creating demand for what was once a relatively an unknown gemstone, the wholesale price of tanzanite rose by approximately 2,500% between 1970 and 1980. This track record is unmatched by any other gemstone.
Today the demand for Tanzanite, especially in sizes between 6 and 15 carats, continues to be strong. New mining techniques and the liberalization of the Tanzanian economy has helped to boost production in the past few years to make tanzanite more available than ever before in the history of the gemstone.
But why is the price of this precious commodity tumbling to the detriment of Tanzania's economy? Today the local price of uncut Tanzanite has tumbled by 50 per cent, threatening the industry and the future of native miners. Gemstone dealers say that the blue/purple gemstone now fetches USD180 per uncut gramme, down from USD350 in June this year. This is the lowest price recorded in the history of Tanzanite business.
source; http://www.africanexecutive.com/modules/magazine/articles.php?article=3595
dogo Mbaraka Juma (mshiriki wa faidika na bbc) ameshika nafasi ya pili hivyo kakosa USD 5,000 kama mtaji wa kuanzisha mradi wake wa kufuga panya na vyura kwa ajili ya mafunzo ya upasuaji kwa wanafunzi wa A-level (Biology). Mradi huu una-sound kinoma kwani kupatikana kwa hawa specimen huwa shida sana kupatikana hasa kwa shule za Dar. USD 5,000 ni pesa kidogo sana, ningeshauri Mwana JF mmoja ajitolee kumpatia mtaji huyu dogo ili aendeleze ndoto yake, pia atakuwa ameunga mkono bbc ktk kushindanisha vijana kuibua fikra za kijasiliamali.
...a Belgian organization is using rats to alleviate two of Africa's greatest scourges: land mines and tuberculosis.
source; http://www.miller-mccune.com/mice/mine-heir-927
...cruelity to animals bana, angesema hao panya watasaidia ugunduzi wa TB au landmines kweli...
Next Level, tayari umeshaanza kamili kamili kwenye hii project? Me ningependa sana kupata company nijitutumue misuli mkuu!
Utamu uko ktk boriti. Eka moja ni boriti 1200,bei ya boriti moja kwa leo hii ni Tsh 15,000/shambani.kwa hiyo eka moja iliyogharimu Tsh 70,000/ kununua ardhi mpaka kupanda itakupa 1200 x 15,000/=( ) toa gharama za fire break mara moja kwa mwaka. Hakuna kupalilia wala kumwagilia.
Malila et all
Shukhrani kwa mawazo kede kede ya kujenga...mradi kama hii ya misitu inatufaa sana Watanzania tulioko nje sababu haihitaji uangalizi wa kila siku na pia mitaji yake ni midogo.
Wakuu kwanza mnisamehe,sikujua kuwa thread hii inaendelea, asante YY kwa kuni-pm.
Mtiki unakubali sana kanda ya morogoro,karibu mkoa mzima. Tatizo la mtiki unataka hela nyingi mwanzoni hasa kwenye miche. Kilo moja ya mbegu ya mtiki ni Tsh 6000/ lakini ukiwatika utapata miche kama 1000 hivi,na ukilemaa kidogo utaishia kupata miche 800. Soko la mtiki liko nje ya nchi kwa sasa,ila baada ya miaka 2 tutakuwa na kiwanda kilombelo. Maana yake ni kwamba kwa sasa soko la mitiki la ndani halipo. Kwa mjasiriamali mdogo si vizuri kutegemea soko la nje.
Kwa Moro zone msimu mzuri ni march/april, sasa hivi unatakiwa kuwa na kitalu ili ufanye transplanting mwezi march/april. Msederela nao ni mzuri kwa Moro.
Mlingoti/Pines/Cyprus/Muerezi inafanya vizuri sana Iringa/Mbeya/tanga/ Arusha/Songea/Rukwa. Kwa mikoa ifuatayo ardhi inapatikana bila mizengwe; Iringa,Rukwa,Ruvuma, mikoa hii watu bado waaminifu kiasi,manpower ipo. Watu wengi wanafanya vitu vyao huko. Je unataka nikusaidie ili uwekeze ktk misitu ya mbao? Jamaa toka Kenya wanawekeza kinoma Iringa,hadi moyo unauma.
Hilo zao uliloambiwa, sikushauri sana, lakini nina uhakika kiasi kuwa mbao zitakuwepo kwa miaka mingi katika shughuli za ujenzi
Malila et all
Shukhrani kwa mawazo kede kede ya kujenga...mradi kama hii ya misitu inatufaa sana Watanzania tulioko nje sababu haihitaji uangalizi wa kila siku na pia mitaji yake ni midogo.
Wakuu kwanza mnisamehe,sikujua kuwa thread hii inaendelea, asante YY kwa kuni-pm.
Mtiki unakubali sana kanda ya morogoro,karibu mkoa mzima. Tatizo la mtiki unataka hela nyingi mwanzoni hasa kwenye miche. Kilo moja ya mbegu ya mtiki ni Tsh 6000/ lakini ukiwatika utapata miche kama 1000 hivi,na ukilemaa kidogo utaishia kupata miche 800. Soko la mtiki liko nje ya nchi kwa sasa,ila baada ya miaka 2 tutakuwa na kiwanda kilombelo. Maana yake ni kwamba kwa sasa soko la mitiki la ndani halipo. Kwa mjasiriamali mdogo si vizuri kutegemea soko la nje.
Kwa Moro zone msimu mzuri ni march/april, sasa hivi unatakiwa kuwa na kitalu ili ufanye transplanting mwezi march/april. Msederela nao ni mzuri kwa Moro.
Mlingoti/Pines/Cyprus/Muerezi inafanya vizuri sana Iringa/Mbeya/tanga/ Arusha/Songea/Rukwa. Kwa mikoa ifuatayo ardhi inapatikana bila mizengwe; Iringa,Rukwa,Ruvuma, mikoa hii watu bado waaminifu kiasi,manpower ipo. Watu wengi wanafanya vitu vyao huko. Je unataka nikusaidie ili uwekeze ktk misitu ya mbao? Jamaa toka Kenya wanawekeza kinoma Iringa,hadi moyo unauma.
Hilo zao uliloambiwa, sikushauri sana, lakini nina uhakika kiasi kuwa mbao zitakuwepo kwa miaka mingi katika shughuli za ujenzi
Ahsante Mkuu,
Vipi hili tatizo la wanyama kula miti sababu ulinzi kwenye hilo ni gumu sana. Sijui iwapo ninyi limewakuta hilo?
/msitu. Mitiki soko lake liko nje kwa sasa na baadaye tutakuwa na kiwanda pale kilombero hivyo itakuwa rahisi kuuza pale.
Malila nimependa wazo lako, mie nina shamba Mapinga naona watu wamepanda mitiki ila sijaelewa inachukua muda gani kuvunwa? na je gharama zake kwa say eka 3 za kuanzia? na nini faida yake?
Next Level, tayari umeshaanza kamili kamili kwenye hii project? Me ningependa sana kupata company nijitutumue misuli mkuu!
Yes mkuu....currently nakamilisha kuchukua ekari 16 kwa mwaka huu na kuwatika miti hapo Ir...then kny mwezi wa pili or tatu nikupanda....tamcheki Malila as well! Karibu mkuu
Ahsante Mkuu,
Vipi hili tatizo la wanyama kula miti sababu ulinzi kwenye hilo ni gumu sana. Sijui iwapo ninyi limewakuta hilo?
Miti inayoliwa sana na wanyama ni milingoti myekundu,mbuzi wanakula sana ikiwa michanga. Nilichofanya mimi ni kukimbia maeneo ya wafugaji. Mfugaji mmoja alikata miti 20 pines ya kwangu akajengea boma la ng`ombe wao. Kesi ilikuwa mbaya,niliamua kuacha ile kesi kwa sababu sehemu kubwa ya familia ile ni wazee wa miba.
Kwa hiyo licha uhalibifu wa wanyama,na wenye mifugo pia wataka miti yako kwa ujenzi.Kuna wakati wanachoma moto ili kupata majani mapya, mkuu moyo unaweza kusimama siku unaambiwa eka 50 zimeungua moto,kisa jamaa alikuwa anaandaa majani ya mbuzi/ng`ombe wake.
Mkuu next l,
Kumbe ni wewe,siku moja tulikuwa wote Vingunguti bwana,na siku nyingine tulikuwa wote Mkuranga kule porini na yule jamaa dalali feki. Unakumbuka mimi niliachiwa kuendesha Kia fulani ya mjomba wa rafiki yako,rafiki yako na mjomba wake wakapanda Landcruiser ya jamaa yangu. Mimi nikazunguka nyie mkakatisha na Cruiser. Kule mimi nimeshalamba tayari kipande cha kutosha.
Wakuu,
Swali jingine: mmeweza vipi kujiunga pamoja na kutimiza haya malengo? Mnajiongoza vipi na mnatatua vipi migogoro yenu?
Mradi wa kuvuna baada ya miaka 5+ mkiwa zaidi ya 10 na wote muwe kwenye mstari mmoja sio kazi ndogo.
Watanzania ni watu wazuri ila wamekosa kiongozi mwaminifu. Ktk hili sisi sote tumeanika uwezo wetu na udhaifu wetu wazi. Taarifa za kazi yetu ni za wazi,hesabu za kazi yetu(project) ni za wazi, kwa hiyo utakuta mwenye uwezo mkubwa anaweza kushirikiana na mnyonge bila taabu na bado hahisi kubebeshwa mzigo. Mnyonge anacho kitu cha kuchangia ktk project na kigogo ana kitu cha kuchangia ktk project zetu mkuu.
Kundi hili ni la watu wanaojua nini cha kufanya.ni mchanganyiko mzuri kweli,injiniasi,b/nessmen,politicians,students,pastors.
Mpaka sasa ni miaka 3,kila mmoja ameridhika na progress yetu. Kiongozi wetu mkuu ni mwaminifu sana na anaijua njia ya kupita na wenzake. Tumeokoa gharama sana kwa kufanya pamoja.