Mtakufa malofa na moto mtauingia kwa kuendekeza mpira

Mtakufa malofa na moto mtauingia kwa kuendekeza mpira

Kwanini usiku huwezi kufanya kazi za ziada ukaongeza kipato?
usingizi wa kawaida ni usiku lakini kama una shughuli ya usiku ulilala mchana haikatazwi.Muhimu uwe na muda wa mapumziko angalau mara moja kwa siku.
Iwapo unaangalia mechi kila wakati utapata wapi huo muda wa kuongeza kipato.
 
Unakutana na kikundi cha watu wameshughulika kuzungumza.Unadhani wanapanga mipango ya maana ya kiuchumi kumbe ni mpira wa jana au utakaochezwa leo.

Zamani ilikuwa ni ligi kuu mwaka mara moja na timu maarufu Tanzania ni Simba na Yanga.Sasa hivi ni ligi tu kila siku. Mara ligi ya benki, mara ligi ya nani. Ushabiki haupo wa timu kubwa peke yake bali hata timu za vichochoroni zinawashughulisha watu nchi nzima.

Wenzenu wanatia pesa mfukoni kwa kuuza ving'amuzi,nyinyi mnaliwa tu na kupiga makele.

Mwisho wa yote ni kuharibikiwa afya na kubaki maskini omba omba au kujiingiza kwenye utapeli.Ukiondoka duniani hutakuwa na majibu mazuri kwa Mola wako na moto utauingia.
Aisee wananchi wanashughulika na vitu vya kipumbavu kabisa.
Badala ya kufanya kazi kwa bidii waongeze uchumi,utawakuta wameenda kumpokea mjinga mmoja Airport sijui nauli wanatoa wapi.
Kuna kundi wanajiita machawa hata sijui wanalipwa na nani
Mpira eti mpk mjinga mmoja anajiua kisa Manchester wamefungwa wtf.
Kuna watu wa kuchapa viboko warudi makwao vijijini.
Ndio mana mafisadi yamejaa yanajipigia hela tu.
Kwa akili matope hizo tutaendelea kuwa maskini tu.
Jibu linashabikia mpira halina hela ya kula.
Its insane
 
usingizi wa kawaida ni usiku lakini kama una shughuli ya usiku ulilala mchana haikatazwi.Muhimu uwe na muda wa mapumziko angalau mara moja kwa siku.
Iwapo unaangalia mechi kila wakati utapata wapi huo muda wa kuongeza kipato.
Zijazungumzia usingizi nmezungumzia ngono
 
Hata ufanye kazi vipi,mwisho wa siku mwili unahitaji burudani. Sasa hapo kwenye burudani kila mtu anayo ya kwake, kama ifuatavyo; kuna wapenda mpira, sinema, vinywaji mbalimbali, ngono, safari, utalii sehemu tofauti zikiwemo mbuga za wanyama, muziki, disco, kuogelea, kula, kulala etc...!! Na burudani hizo zina gharama tofauti tofauti. SASA WEWE UNADHANI STAREHE NI WOTE TUPENDE UNAVYOVIPENDA WEWE..!!

Hata starehe yako ikiwa ni savvanah, bado wenzio watatia pesa uliyonunulia savana mfuko, hata upende kwenda mbugani, bado utalipia kuwaona wanyama, utalipa nauli chakula, kulala etc na hivyobado wenzio watatia pesa mfuko. etc kifupi hakuna cha bure. Hivyo kutuambia kuwa .. nanukukuu.. "Wenzenu wanatia pesa mfukoni kwa kuuza ving'amuzi,nyinyi mnaliwa tu na kupiga makele" .. Mwisho wa kunukuu, ni yale yale tu..!!

BTW, hata kama huangalii au huzungumzii kuhusu mpira, kipo kitakachokupa matokea sawasawa na anayezungumzia mpira. Mtatofautiana namna matokeo hayo yanavyowajia..!!

Hii ni sawa na wale wanaowasema wanaokunywa pombe kwamba wakiacha pombe, kwa mwaka mmoja wanaweza kununua gari, WALIPOULIZWA KAMA WAO WANAKUNYWA, WAKASEMA HAPANA, HAWANYWI, WALIPOAMBIWA WAONYESHE MAGARI WALIYOYANUNUA, WAKABAKI KUTOA MACHO TU..!!
Mwanafalsafa mzuri. Vyote ulivyovitaja kama mfanano na mpira bado havilanganiki na mpira.Ukifanya ngono kwa mke wako ni halali na huenda mkapata mtoto.Ukienda kuangalia wanyama unaburudika na kupata mazingatio na kunoa akili yako.Pesa uliyotoa huko inalipa kabisa
Sasa niambie unapoingia uwanjani kuangalia vijana waliochonga viduku na kusuka nywele unapata nini ?
 
Khe, huyu naye katokea wapi, ipo hivi,...
1:kuna walevi wa pombe(ndo starehe yao)
2:kuna wacheza kamari (ndo starehe yao)
3:kuna wapenda ngono (ndo starehe yao)
4:kuna watu wa upinde (ndo starehe yao japo ya kipuuzi poumbaaf zao)
5:kuna sisi machizi soka (ndo starehe yetu), infact kufuatilia mpira ndo starehe ya gharama ndogo kuliko zote na haina madhara yoyote.kaa mbali na sisi au jiunge na sisi.
 
Mpira ni moja ya starehe Faza inaonekana sio mpenzi wa mpira ndio maana unashangaa watu wakijadili mpira...
Nakubali kabisa. Hata mimi ni shabiki mkubwa wa kandanda. Lakini kwa Tanzania hali ni mbaya. Tatizo ni kuwa mpira unatumika kama kitu cha kupumbaza raia wasijielewe. Hili ndilo linafanya nimuunge mkono mwanzisha thread. Mpira wa Bongo unatumia na watawala kufanya raia wasijitambue.
 
Nakubali kabisa. Hata mimi ni shabiki mkubwa wa kandanda. Lakini kwa Tanzania hali ni mbaya. Tatizo ni kuwa mpira unatumika kama kitu cha kupumbaza raia wasijielewe. Hili ndilo linafanya nimuunge mkono mwanzisha thread. Mpira wa Bongo unatumia na watawala kufanya raia wasijitambue.
watawala kujikomba kwa raia kwa mtazamo wa uchaguzi.Mabwanyenye wanaona ni fursa kuwakamua wajinga wafe kabisa ili wao waneemeke na wasitoke kwenye guiness book of records
 
We uko hapa kusengenya huna unachopata zaidi , ukitaka wakuelewe wafate kwenye hayo mabanda uwaambie
😁😁😁 akifanya kama unavyomuelekeza,ataua hukohuko bandani.Hii thread tu,imevamiwa hivi,je angeonekana?
 
Nimesema niliwahi kupenda halafu nikaona ujinga nikawacha.Naamini na nyinyi iko siku mtatia akili muwe kama mimi.
Hakuna mtu anaependa mpira alafu akaacha kushabikia huo ni uongo, hupendi mpira tulia usijone wewe ni bora kuliko wanaopenda
 
watawala kujikomba kwa raia kwa mtazamo wa uchaguzi.Mabwanyenye wanaona ni fursa kuwakamua wajinga wafe kabisa ili wao waneemeke na wasitoke kwenye guiness book of records
Mpira Tanzania hata hawaupendi kama mnavyodhania mkitaka kujua pana Nchi mpira kwao ni kama dini nenda Brazil,Argentina au shuka hapo Liverpool na Santiago hata Italy pia unakuta Mbibi kabisa ana Tiket za gemu na haumwambii kitu kuhusu Timu yake...
 
Hakuna mtu anaependa mpira alafu akaacha kushabikia huo ni uongo, hupendi mpira tulia usijone wewe ni bora kuliko wanaopenda
Kwa mpira mimi najifaharisha kuwa ni bora sana kuliko wote wanaoushabikia.Nimekutana nao wengi ndio maana nikaamua kuja hapa leo.Wanatia huruma sana.Unawaona hivi hivi wanaishi maisha ya wasi wasi sana.Pesa na kula wanataka na huku mpira hawataki uwapite.Kila wakati ni kuwehuka wehuka tu.Hata wakiingia chooni hawamalizi haja vizuri.Akisikia ukelele anatoka haraka akaulize nani kapigwa ngapi.Mimi nimejibanza nawaangalia tu.
 
Unakutana na kikundi cha watu wameshughulika kuzungumza.Unadhani wanapanga mipango ya maana ya kiuchumi kumbe ni mpira wa jana au utakaochezwa leo.

Zamani ilikuwa ni ligi kuu mwaka mara moja na timu maarufu Tanzania ni Simba na Yanga.Sasa hivi ni ligi tu kila siku. Mara ligi ya benki, mara ligi ya nani. Ushabiki haupo wa timu kubwa peke yake bali hata timu za vichochoroni zinawashughulisha watu nchi nzima.

Wenzenu wanatia pesa mfukoni kwa kuuza ving'amuzi,nyinyi mnaliwa tu na kupiga makele.

Mwisho wa yote ni kuharibikiwa afya na kubaki maskini omba omba au kujiingiza kwenye utapeli.Ukiondoka duniani hutakuwa na majibu mazuri kwa Mola wako na moto utauingia.
Hakuna moto.
 
Back
Top Bottom