...ni ka swali tu, viongozi wote hasa wateuliwa na wabunge hawavai kabisa barakoa. Iwe kwenye mazishi, mikusanyiko mbalimbali nk hutawaona wamevaa barakoa.
Au watakuwa washapigwa chanjo kisirisiri wanatupoteza maboya wenzao?
...Leaders lead by examples. Wananchi wengi wenye low reasoning capacity wanasubiri leaders wavae magwanda ndo nao watimbe! Please leaders tunaangamizana!
NB: Mie navaa barakoa, wewe je?
Ndo ivo JK alisema za kuambiwa changanya na zako
Mbona nasikia tetesi kuwa hii second waive eti yenyewe haisikii limao wala tangawizi.Wanajifukiza na kunywa juice ya tangawizi na malimao
Haya malimao sijui tangawizi tununue tu kuchangia uchumi wa wachuuzi, but in real kale kajamaa kakiingia kanakula mpka tangawizi na kanaomba hata ndimu!Mbona nasikia tetesi kuwa hii second waive eti yenyewe haisikii limao wala tangawizi.
Watu Wa Kule kwetu Tarime wanamsemo wao,BHUNU MBHUNDI.
Ni wakati mashirika ya ujasusi duniani kuwapeleleza walio plant huu ugonjwa maana sio wa mungu, thus why 2nd wave wameutengeneza ili utushambulie hasa waafrika ndio maana ukapandikizwa south afrika na brazilHaya malimao sijui tangawizi tununue tu kuchangia uchumi wa wachuuzi, but in real kale kajamaa kakiingia kanakula mpka tangawizi na kanaomba hata ndimu!
Ndio hivyo,Haya malimao sijui tangawizi tununue tu kuchangia uchumi wa wachuuzi, but in real kale kajamaa kakiingia kanakula mpka tangawizi na kanaomba hata ndimu!
Labda utume wasiojulikana wa huku kwetu.Ni wakati mashirika ya ujasusi duniani kuwapeleleza walio plant huu ugonjwa maana sio wa mungu, thus why 2nd wave wameutengeneza ili utushambulie hasa waafrika ndio maana ukapandikizwa south afrika na brazil
Yamezingatiwa?Wakuu ,habarini poleni na majukumu poleni pia na hili janga la corona ,kiufupi mimi niseme corona sio tishio kubwa ila limekuwa overrated,
Ebu kumbuka lile janga la dengue ebu assume dengue ingewapata wazungu au wachina wangekuwa katika hali gani?
Katika kufikiri tu mi nadhani hao mabwana wana weak immune system na pia nadhani dengue is more serious than corona.
Kumbuka hata kipindi cha kujenga railway uko marekani walitumia watu weusi maana ngozi nyeupe they are very weak hata malaralia ambayo asilimia kubwa huku kwetu ni kama homa ya kawaida wenzetu wakipata inakuwa tragedy
Yani corona ni ugonjwa ambao unapata nafuu kwa kujitenga mwenyewe ndani ya siku kadhaa !!! Na pia ni ugonjwa ambao unawakumba wazee sana sana 50+
Wanasema watoto na vijana asilimia kubwa wanaweza hata wasioneshe dalili japokuwa ugonjwa huo wanao mimi nadhani ni kwakua tu maambukizi yake niyakasi na haraka ndo maana umepewa promo ila sio janga kubwa kiivyo cha msingi ni kuzingatia kunawa na sabuni mara kwa mara ,kuvaa mask na gloves ,kuepuka misongamano hutaisha fastaa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Acha tulipie uzembe uliosabishwa na serikali toka mwanzo ilishindwa kuonyesha reaction yoyote unashindwa funga mipaka kisa watalii nani bora kati ya mwananchi na mtalii pesa ina thamani kuliko uhai wetu
Nb: Serikali imehusika kwa uzembe ktk hili.
Hii Tanzania hii, sisi ni sayari nyingine kabisa, wiki iliyopita nilienda msibani huko Chanika tena watoto wa marehemu walisema kabisa mama yao kafa na CORONA, cha kushangaza mvaaji BARAKOA mie watu walikuwa wanishangaa utadhani mimi ndio COVID yenyewe, wengine wanakuja kukupa pole wanataka na kukumbatia kabisa, shee!
Siku covid inakuua wewe brazaj ndio nitaamini kweli covid ni hatari la sivyo nitaishi kadiri ya Imani ya hayati John Pombe Magufuli.Mods, mabibi na mabwana.
Fursa na riziki si lazima kupatikana leo. Bali mazingira ya fursa hayapaswi kungoja kesho.
Huu ni ushauri wa bure kwenu JF, na hasa MODs.
Corona inauwa. Ugonjwa huu upo hapa nchini kama ilivyo kuwa kwingine. Ugonjwa huu unasambaa zaidi kwenye mikusanyiko ya watu isiyozingatia tahadhari zinazo uhusu.
Kuhamasisha watu kujikinga ili waweze kuendelea kuwa hai na bila ya kujali malipo ya hapa duniani ni jambo la thawabu kubwa mno.
Kwa hakika jitihada za kupigania uhai wa watu hazijawahi kupotea bure.
Ikumbukwe kuwa sote tungalifurahi mno kutokumpoteza mpendwa wetu yeyote kutokana na janga hili ambalo kwa hakika linaweza kuepukika.
Kwamba nyie mko na udhibiti wa forum hii, kuridhia uhimizwaji wa watu kuchukua hatua za kujilinda hakuwezi kuchukuliwa na mtu yeyote kuwa ni kosa au usaliti.
Kwani nani asiyefarijika kuona mja mwingine wa mola akiwa hai na salama?
Kwa kuchukua hatua za kujilinda tu tungeepuka misiba hii inayoendelea kutusononesha sana leo.
Ama kwa hakika kuukimbia ukweli hakusaidii. Kama jamii tunayo nafasi ya kuelezana ukweli na kwa pamoja tukasalia salama.
Tunavyoendelea kumwomboleza mpendwa wetu rais Magufuli (rip) kwa namna ambayo kila mmoja wetu anaiona, tujue kuwa ni suala la muda tu.
Kwamba kwa kupiga kelele tu humu JF, kwa pamoja tunaweza kuokoa maisha ya watu wengi, mbona hili ni wazi mno?
Ni kwa mukthadha huu JF kuwa japo nominee wa tuzo ya Nobeli hakuwezi kubakia kuwa kama ndoto isiyowezekana.
Zitendeeni haki nyuzi zinazoasa na kuhimiza watu kuwa salama ikiwamo katika kipindi hiki cha maombolezo.
Ninawasilisha.