#COVID19 Mtazamo, Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Serikali na Wananchi kuhusu Ugonjwa wa Corona - COVID-19
Ni muda sasa Dunia ikiwa ina pambana na Janga la Corona.

Modelling ya Wanasayansi nchini Kenya inaonesha kufikia mwishoni mwa mwezi April 2020 kuna uwezekano wa Kenya kuwa na Wagonjwa 10,000. US inaonesha by August 2020 marehemu wanaweza kuwa zaidi ya 82,000. Italy kwa sasa vifo ni zaidi ya 12,000.

Nchi zetu za Africa hasa Tanzania zimewekeza sana katika Siasa na kubakia madarakani na siyo Tafiti za kuliendeleza Taifa. Nchi yetu imeshindwa hata kufanya tafiti za kuzuia magonjwa ya Mhogo!

Siyo kwamba wataalam hawapo nchini, laa asha! Wataalum wapo wengi sana.
Tatizo kuu la Tanzania ni vipaumbele. Mbunge wa Tanzania sifa kuu ajue kusoma na kuandika tu, mshahara mnono, Gari zuri, Allowances kibao, mikopo, Ruzuku on spot akistaafu. Na huyu ndie apange sera za Taifa karne ya 21 dhidi ya US, Germany, Russia na China. Kweli au ni mzaha?

Bunge letu ni muda sasa haliidhinishi pesa za Tafiti karibu 90% hata ya Pesa ndogo ilioombwa. Hakuna nchi itaendelea duniani bila Research & Development. Hizi ndizo huzaa Innovation (patent rights) kwa wagunduzi.

Utashangaa Mjinga mmoja ana ropoka ni muda sasa wa Maprofessor, madaktari , Watafiti na Wahadhiri kuja na Tiba ya Corona! Yaani Professa umlipe Tshs 3m. Researchers Tshs 1.5m na Wahadhiri Tshs 1.5M (bila gari, nyumba kapanga, no allowances, nk). Afu Kibaji na Mlinga uwalipe Tshs 15m kwa Mwezi! Tena bila pesa za Tafiti!

Ni muda sasa:

1. Serikali itenge at least 1% ya GDP kwa ajili ya R&D.
2. Serikali ijenge Vyuo/Centers za Utafiti. Ziwepo za Virus, Bacteria, nk. Ziwepo za Mazao, wanyama, nk. Ziwepo Centers za Gunduzi za bidhaa, huduma, maarifa, nk. Siyo kila kukicha CBE New Branch, UDSM New Branch, Chato University, nk.
3. Serikali itume vijana wa Sayansi Takribani 2000 nchi zote duniani kuiba maarifa kila nyanja. Na kuwarudisha baada ya miaka 10. Hatujachelewa tuanze sasa!

Hivi ni nchi gani hii hadi Toothpick tunaagiza China? Hand Sanitizers MSD wanaagiza China? Mask hadi msaada?

Ni muda muafaka sasa kuheshimu wasomi na Sayansi. Ni muda wa wasomi kuongea. Siyo kila Mjinga anaongea kuhusu CORONA.

Tuendelee kujikinga na Corona kwa kufuata ushauri wa Wataalam wa Afya. Corona inaua vibaya!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hoja nzuri.

1% ya GDP ni kama USD 62 M...pesa ya madafu kama 136 B...Inawezekana... Ila sidhani kama watakusikiliza.
 
tafiti zinaheshimiwa mbona lakini zinatakiwa zitoke kwa mtu husika na kitu fulani , waziri we ujenzi anakuja toa tafiti za corona [emoji50][emoji50]

Nawe hizi tafiti zako unataka ziheshimiwe umezitoa wapi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaongea uharisia sema Tanzania hii,amn atakae kuelewa cos weng wa viongozi ni wanafiki, wana pritend wanalengo kulisaidia taifa kumbe wanataka tu kujinufaisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba kutoa maoni yangu nami kuhusu Corona. Maana naona kila mtu anatoa nami ni mtu acha niishauri serikali kuhusu hili ambalo nimeona kwangu mimi halina tija katika kupambana na Corona hasa jijini Dar es Salaam.

Wafanyabiashara katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam wanashinikizwa kuwa bando ya maji katika biashara zao ili wateja kunawa kabla na baada ya huduma watakayo ni wazo zuri kidogo ila halina mashiko yoyote. Hali hiyo kwa sasa iko hadi kwenye makazi ya watu nao pia wanatakiwa kuwa na ndoo yenye koki na sabuni kwa ajili ya kunawa.

Sasa kuna watu hawa ambao wanapita nyumba kwa nyumba kukagua utekelezaji wa kuwa na ndoo na kama utakuwa huna ndoo katika eneo lako la biashara au makazi basi unakamatwa!!

Hivi nguvu kubwa hii inatumika ili iweje kwa mfano, suala la maambukizi ya Corona liko wazi na kila mmoja anaweza kuwa anajua namna ambavyo inaambukizwa. Wakati huu ambao bado maeneo mbalimbali ya jiji yanaruhusu mikusanyiko ya watu unategemea upambane na Corona kwa kunawa mikono kila mara?

Corona siyo kinyesi kwamba ukikishika mkononi utang'amua kwa haraka virusi hivi hata kwa kugusana na mgonjwa unaweza kuvipata, kwenye daladala huu utaratibu wa level seat sio kwamba ni suluhu ya kuondoa maambukizi hapana ni utaratibu tu uliwekwa ili msongamano usiwepo lakini siyo kwamba maambukizi hayatakuwepo maana navyojua daladala abiria hugusana na mwenzake kwa namna yoyote ile, hili jiji lina joto hivyo watu kutoka jasho ni kawaida sio lazima mikono igusane hata mabega yetu hugusana tena yakiwa na jasho tepetepe.

Nchi baadhi zimesamehe wafungwa ili kuzuia hatari ya maambukizi huko magerezani sisi tunasomba watu wasio na ndoo kuwapeleka serikali za mitaa sijui hawajanunua ndoo hivi tunataka kupambana na Corona kweli au watu?

Hao watu wanaozunguka mitaani wakipata maambukizi unadhani wangapi wataathirika kutokana na shughuli zao wanazofanya kupita nyumba kwa nyumba?

Basi masoko na huduma nyingine za kijamii zifungwe kama kweli tuna nia ya kupambana na huu ugonjwa ila kunawa sioni kama ni dawa wala tiba ya ugonjwa huu ila kuna tahadhari nyingi zaidi za kunawa, fikiria koki ya kwenye ndoo ikishikwa na mgonjwa wa Corona unadhani wadudu wale watakufa au wataendelea kubaki pale na kila mmoja anawazoa na kuondoka nao kwake, ni wangapi hufungua na kufunga ile koki kwa siku, je wote wanakuwa salama?

Tuamue moja kama tunapambana na Corona tupambane na Corona pekee kama tunapambana na watu basi tupambane na watu.

Nisamehe kama nimekosea maana mimi siyo mwanasiasa.
 
Mkuu umeongea point sana. Wanasiasa wanafanya wasomi wa bongo tudharaulike sana. Muda wa kuheshimiana unakuja soon.
 
Na kunawa tunapunguza maradhi mengine kama ya kuhara, fikiria matumizi ya simu, plastiki na nguo virus wa corona huishi kwa siku 3-7! Tuelimishwe namna kutakasa simu zetu ,mifuko, nguo na mikoba pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nami naomba kutoa Mapendekezo yangu Mafupi hapa dhidi ya janga hili la ugonjwa wa Corona Viruses

Kwanzaa kabisa wote tunafahamu huu ugonjwa upo Dar es salaam kama ilivyo tangazwa juzi na waziri wa afya kwamba kuna wagonjwa watatu ambao walikua wakifuatilia kutokan na wale wagonjwa wa Mwanzo walio kua wamesafiri Nje ya nchi
.
Hivyo basi Serikali iweke utaratibu Mzuri wa Vipimo katika vituo vyote vya wasafiri wote wanaosafiri Mikoani Mfano UBUNGO BUS TERMINAL Lengo kubwa Hapa nikuto ruhusu Au kupunguza Maambukizi kutosambaa yakaenda Vijijini ambako tunafahamu idadi kubwa ya wananchi kule ni Wazee pia hapa tutakua tumeweza kuudhibiti ugonjwa kwa Kiasi frani.
 
Huku Dom kwenye kituo kikuu cha daladala (sabasaba) hupandi kwenye daladala km hujanawa ila ikifika usikuu hakuna ndoo wala Maji wala sabuni
Sasa swali langu nikwamba hivyo virusi vinasambaa mchana peke ake??
Na kama vinasambazwa kwa njia ya hewa au kugusa/kugusana kutoka kwa muathirika kunawa kwa mikono mchana pekee kunatosha kuthibiti ugonjwa huuu??
 
Usiku wa leo nimejaribu kutathimini yanayoendelea juu ya corona ni wazi mwisho wa dunia umefika, na hata kama haujafika ni wazi kama mungu akiamua kuituliza corona dunia haiwezi kuwa kama tunavyoiona kwa sasa jinsi ilivyo, nasema mungu akiamua kuituliza kwakuwa hakuna mwanadamu anaweza kulituliza janga hili, ni wazi kutakuwa na mabadiliko makubwa mno.

Kupitia vyanzo mbalimbali nimeona majeneza maelfu kwa maelfu tena ya kwenye nchi zilizoendelea nchi kama Marekani, Hispania, Italy, Uchina n.k. kwa sisi nchi zinazoitwa zinaendelea ni wazi ni kudra za mwenyezi mungu ndio zitatuokoa na sio vinginevyo, sisi hatuna uwezo wa kukabiliana hata chembe na janga hili. Sisi ni kama watoto ambao adui akiingia ndani akampiga baba ni wazi watoto hatutakuwa na cha kufanya.

Nimeona riport ya UN inasema Africa itaanza kuchakazwa na Corona Almost week mbili mpaka tatu zijazo. Ndugu zangu tujiandae na chochote hali ni mbaya kwa wenzetu kuona watu mia saba, mia nane au elfu moja wanakufa kwa siku imekuwa kitu cha kawaida kwa siku za hivi karibuni, fikiria tumefiwa na mtu mmoja tu kwa corona lakini taifa lote limehuzunika, je ikitokea ya uchina huko si tutapoteana ndugu zangu??

EEEEH MWENYEZI MUNGU SIKIA KILIO CHETU WAJA WAKO.
 
Tusitishane watu waenderee kuchapa kazi....hiri naro ritapita muraa furustop.
 
Back
Top Bottom