Mtazamo wangu kuhusu siasa za Tanzania na Rais Magufuli

Mtazamo wangu kuhusu siasa za Tanzania na Rais Magufuli

Kusema kuwa Tanzania inakandamiza ushoga kwa kukataa sio kuichafua Tanzania? Anadai kinachofanyika ndani ya chupa cha mashoga hakihusu serikali sio kuichafuta Tanzania?

Swali langu linabaki pale pale Tundu Lisu anazunguka kwa mabeberu akiwabembeleza na kupeleka hoja ili Tanzania iwekewe vikwazo mbalimbali na inyimwe misaada kitu ambacho kinalenga kuwaathiri waTanzania wote kwa ujumla na si Magufuli yeye kama yeye (ila kwa chuki zake tu binafsi juu ya Magu).

Nadhani kwa hapa tulipofikia tunaweza kufunga huu mjadala naona kama hatuelewani, ila unayemkubali wewe anatetea ushoga na kutaka Tanzania tunyimwe misaada kwa kuwekewa vikwazo huku akiwa hatafakari inatuathiri vipi sisi kam Tanzania. .
Mkuu labda nikuulize kitu, kwanini umebezi kwenye Chuki ya Lisu dhidi ya Jiwe na siyo Chuki ya Jiwe dhidi ya Lisu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..kuna mchangiaji amedai Tz haijawahi kujenga reli tangu tupate uhuru. Kuwa Jpm ndiyo Raisi wa kwanza kujenga reli ktk Tanganyika / Tanzania huru.

..nilichofanya mimi ni kumkumbusha kuhusu ujenzi wa TAZARA ambao ulikuwa ktk miaka ya 70.
Financier wa TAZARA (interest free loan kwa maneno mengine ni reli ya msaada co kwmb tulijenga) [emoji116][emoji116]
"The TAZARA Railway" The TAZARA Railway

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kusema kuwa Tanzania inakandamiza ushoga kwa kukataa sio kuichafua Tanzania? Anadai kinachofanyika ndani ya chupa cha mashoga hakihusu serikali sio kuichafuta Tanzania?

Swali langu linabaki pale pale Tundu Lisu anazunguka kwa mabeberu akiwabembeleza na kupeleka hoja ili Tanzania iwekewe vikwazo mbalimbali na inyimwe misaada kitu ambacho kinalenga kuwaathiri waTanzania wote kwa ujumla na si Magufuli yeye kama yeye (ila kwa chuki zake tu binafsi juu ya Magu).

Nadhani kwa hapa tulipofikia tunaweza kufunga huu mjadala naona kama hatuelewani, ila unayemkubali wewe anatetea ushoga na kutaka Tanzania tunyimwe misaada kwa kuwekewa vikwazo huku akiwa hatafakari inatuathiri vipi sisi kam Tanzania. .

..Je, Jpm aliyewapokea walawiti watoto ikulu unamuelezeaje? How do you defend that?

..Je, hudhani kwamba kitendo hicho kinaichafua Tz?

..hao tunawaomba misaada ingawa baadhi yao wanaunga mkono ushoga lakini wote wanapinga ulawiti watoto. Lakini hapa Tz tumeona walawiti watoto ndiyo watu wa maana wa kupokewa Ikulu na taarifa zake kusambazwa na vyombo vya habari vya serikali.

..Nchi hii itawekewa vikwazo kwasababu ya UKATILI wa serikali ya awamu ya 5, siyo kwasababu TL amependekeza tuwekewe vikwazo. Mabeberu wana wawakilishi wao hapa nchini na wanaona kinachoendelea.
 
Kimsingi tungeona umeongea jipya iwapo ungekuwa neutral, huu upande uliolalia ndio waliolalia wengi ambao wameshindwa kuwashawishi wenye akili timamu. Kwa maneno marahisi umekuja kumsifu Magufuli na kumponda Tundu Lissu au upinzani, bila ku-balance hiki ulichikosema. Tumeshaamka zamani sana.

Sasa ngoja nikupe upande wa pili wa shilingi. Ukweli ni kuwa chuki ndani ya nchi hii imeletwa na Magufuli kwakuwa hawezi siasa za ushindani, na hatakaa aziweze. Kimsingi Magufuli hakupaswa kuwa rais kwani hana uwezo wa urais na hana busara ya kuwa rais.

Nafasi pekee aliyopaswa kuwa nayo ni waziri wa ujenzi, na kama ni ya juu kabisa, basi ni uwaziri mkuu. Nyuzi kama hii ya kwako sio ww tu umeileta, ila siku za karibuni kuna nyuzi kama hizi, huenda zinakuja kwa bahati mbaya, lakini nadhani ni mkakati maalum.

Ushauri, ni vyema Magufuli afanye kazi yake ya urais na aheshimu box la kura. Tulishatoka utumwani misri enzi za chama kimoja, sio yeye tu, hakuna mtu yoyote ndani ya nchi hii ataweza kuturudisha ndani ya mfumo wa chama kimoja.

Kama alidhani akitekeleza baadhi mambo na kuondoa uhuru wa vyombo vya habari, tutamsujudia na kumkubali yeye au chama chake basi amechemsha. Afahamu kila kizazi kina utashi wake, CCM ni chama cha kizazi kilichopita, sio kwamba hakijafanya chochote, lakini sio chama cha kizazi hiki.

Hivyo mshauri asipoteze muda wake kwa kujenga baadhi ya miundombinu, akidhani watu wa kizazi hiki watamkubali yeye au chama chake, sana sana ataishia kuiingiza nchi hii kwenye chuki kubwa na hata machafuko. Aelewe wakati ni ukuta.

Ati wasema Tumeshaamka zamani sana, lakini wakati mtakapovuta blanketi kutakuwa kumekucha.

Hoja yako kuwa asipoteze muda wake kwa kujenga baadhi ya miundombinu, akidhani watu wa kizazi hiki watamkubali yeye au chama chake ni hoja ya kitoto kabisa. Mpiga kura, hasa wa vijijini, anahitaji huduma bora ya afya, elimu, maji na miundo mbinu ya usafirishaji itakayomwezesha aweze kufanya shughuli zake za kijamii, kisiasa na hasa kiuchumi kwa majira na misimu yote ya mwaka.

Unadai ati Kama alidhani akitekeleza baadhi mambo na kuondoa uhuru wa vyombo vya habari, tutamsujudia na kumkubali yeye au chama chake basi amechemsha, ni fikra za mfa maji kisiasa. Siasa za majukwaani zimepitwa na wakati. Na siasa za kwenye vyombo vya habari au/na mitandao ya kijamii ni za udaku tu.

Sijui kwa nini viongozi wa upinzani wanaamini kuwa Tume Huru ya Uchaguzi ndiyo itawaingiza madarakani!! Wakumbuke tu kuwa wahenga walinena Mkono mtupu haulambwi.
 
Kwa mtazamo wangu nadhani si kwamba raisi Magufuli anapinga mhimili wa bunge, hili limedhihirishwa na mkataba alioingia Muheshimiwa Kangi Lugola. Kwa kauli yake kupinga mkataba ule Kwa kuwa haukushirikisha bunge wala serikali yake wala wizara nyingine husika Kama Wizara Ya Fedha. Nafikiri tu kwa raisi magufuli kukubali kupeleka mambo mengi ambayo anafanya sasa bungeni basi hayo mambo yangebaki kwenye ubishani yasingefanyika.
Mistari ya mwanzo tu umeshafeli.
Hopeless!

Sina sababu ya kusoma hadi huko mwisho.
 
“Siasa sio Matusi au Chuki, Hoja Hupingwa Kwa Hoja”
Mtu anaye vaa nguo iliyo andikwa pray for Lissu kwanini aswekwe ndani?. Udikteta wa Magu ulikuwa bayana kabisa kwenye swala la Lissu. Alafu wewe unaita ni tofauti za kisia , be serious bwana!.

Mtu anapigwa risasi nyingi hadharani namna Ile afu no uchunguzi, unamnyima matibabu, unamnyima mshahara, unazuia hata marafiki kumpa pole, unazuia hata wanaotaka kumwombea!

Unakamata hata wenye kuvaa nguo tu iloandikwa tumwombee unawaweka, unamvua ubunge, unaweka mbunge mwengine kisha unarudi kuwatangazia kuwa utawashushia neema kwani "Lissu si mbunge wao!."
Ndugu yangu wewe kama hayo yote unayaita tofauti ndogo za kisiasa basi na wewe ni dikteta tena mwandamizi kabsaaa.
 
Acha upuuzi.

Weka tume huru ya uchaguzi, achana na hizo porojo ndefu.

Bei ya haki yako ni barabara? Unayo akili timamu kweli?
Kwako wewe bei yako ni Mbowe na genge lake la wanasiasa waongo na wenye uchu wa madaraka, ambao wako tayari kwa lolote, ikiwa ni pamoja na kuwaingiza WaTz wasio na hatia mitaani, kwa kile wanachodai "demokrasia" ili waingie Ikulu kutimiza ndoto zao binafsi!

Mbowe na genge lake, tangu wamepata hayo madaraka wamewafanyia nini walio wapa kura ya KULA, zaidi ya kutumia ruzuku kwa maslahi yao binafsi!

Wajumbe wa Tume ya Uchaguzi ni sehemu ndogo sana ya wapiga kura kuathiri matokeo.

Endelea na kuwa NYUMBU lakini kumbuka hata mamba wamo kwenye kundi lenu.
 
Mimi binafsi sipingi UKAWA, na nasikitika kwa kuwa umoja huo umekuwa wa kipindi cha uchaguzi tu. Kuna haja ya kuungana vyama vya upinzani na kuua vyama vingi ambavyo havina tija sana kwa waTanzania

Unajua vita vya panzi ni furaha kwa kunguru, watu tunahangaika na siasa za kubishana ila sio za kujenga kitu ambacho si kizuri kwa taifa letu. Watu wamkosoe serikali hii sikatai, hata serikali ya marekani inakosolewa na hakuna anayekosolewa kama Trump

Ila ukweli utabaki kuna mda wa kupiga kelel na mda wa kushauri serikali kwa namna yeyote ijue mahitaji ya Tanzania. Tukibaki tunabishana tu bila kuweka mbinu mbadala au nini kifanyike kuna maana?
Kama unatambua hata Trump anakosolewa ushawahi kuona anawaua wakosoaji wake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nachokisema kinajidhihirisha hapa
Wengi waliokuwa upinzani ni kama hawana hija
Kilichobaki ni fedheha, kukufanya ujisikie kilaza, na kukutukana

Hawakatai na wala hawapingi so simple minded hawa watu sijui kwa nini
Na wanadhani watatuletea maendeleo kwa matusi na kejeli
Hali kadhalika si dhani kama unaweza kuleta maendeleo yaliyomazuri kwa kudhulumu maisha ya watu. Binafsi sikubaliani na siasa za kuuana. Ila kama mtazihalalisha hata ninyi ni vyema mkaandaa shingo zenu ili mzionje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bila kumung'unya maneno, kiongozi wetu anaonyesha wazi kuwa ana matatizo. Kiuongozi, kiafya ya akili na amekosa kabisa hata hekima kidogo tu ya kiuongozi.

Mnaandika maneno mengi, lkn huyu Rais hafai hata kabisa kuongoza taifa hili.

Kuhusu Lissu, mnataka afanyaje wakati ni wazi pia kuwa waliotaka kumuua kwa kumrushia risasi 38 wanakingiwa kifua na serikali?
Si hilo tu, anafanyiwa Dhihaka na rais eti alikuwa mbunge anaezurura tu huko nje ilhali alipigwa risasi na watu ambao wanakingiwa kifua na serikali ya Magufuli?

Huyu mtu wenu mwambieni ukweli, kwamba ameharibu sana nchi hii! Na hata kama anatutisha tusiseme haya wazi lkn watanzania wengi wanamnafikia, hawampendi na wanamlaani!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na tatizo lako na wengine nikumpa uMungu kwamba hajakosea, hakosei, ana nia nzuri na kumruhusu asifuate taratibu tulizojiwekea kwa kisingizio cha kazi.

Hii nchi haijawahi simama kabla ya uhuru na baada ya uhuru.
Tuliwahi fikia literacy rate zaidi ya 90 na sasa si hivyo. Zimewahi kujengwa shule nyingi sana kabla yake.
Tumewahi kuwa na viwanda vingi na kusafirisha bidhaa nyingi nje.
Kuna watu nchi hii (pengine na yeye) wamesoma bure mpaka chuo kikuu.
Barabara na madaraja mengi makubwa yamejengwa kabla hajawa yeye raisi.
Zilikuwepo ndege nyingi kuliko zilizopo sasa.

Kutwa watu wanatukaririsha humu kuwa uncle ndo kila kitu. Nina uhakika kwa unyoofu wa mwenendo wako watanzania wengi tu wakumzidi. Kwenye milioni 55 hatukosi wachapa kazi hata CCM wapo na
hakuwaweka yeye wala uwepo wao CCM sio sababu yake.

Kwa nini tupoteze nguvu nyingi kumpamba mtu ambaye anafanya wajibu wake na tayari kuna waliomzidi kabla yake yote kwa gharama ya kuumiza na kuwanyanyasa wengine?
Kwa nini tuwazuie wengine wasifanye wanayotakiwa kwa misingi ya nchi kisa mapenzi ya mtu mmoja?
Kwa nini tusherekee wengine kuumizwa kisa madaraja?
Kwa nini tumuache akiharibu mifumo ya haki na utawala ambayo tulikuwa tunaiboresha?
Kwa nini tusiwaze wengine kutuongoza ati kuna mmoja kafanya vizuri wakati yeye angali si maarufu alipata fursa hiyo akafika hapo? Je angezuiliwa afanyavyo maana yake angejengea wapi hizo ndoto zake?

Kwa nini turuhusu watendaji malaki walio nchi hii kuishi kama digidigi wakiwindwa wakose ubunifu watende kama maroboti wakati wanatumia rasilimali za nchi?

Nasisitiza huyu ni mtu na atakufa. Muda hausimami. Kama falme ambao ndugu huhakishiwa maisha bora na bado wapo wanaopinduliwa hakuna namna watu milioni wakataka udumu. Na kuwakandamiza siku zote hutengeneza roho za kupinga. Ni heri tuziruhusu katika amani kuliko kuacha zikue zilete hatari.
Samahani Mfiaukweli mataga ni nini?
Mimi sijasema Magu hana mapungufu yake mbona mnanipiga mawe, Magu sio Mungu
Tubishane kwa Hoja tu ila sio kelele

Nifundishe na mie nielewe ambacho unadhani sikielewi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ati wasema Tumeshaamka zamani sana, lakini wakati mtakapovuta blanketi kutakuwa kumekucha.

Hoja yako kuwa asipoteze muda wake kwa kujenga baadhi ya miundombinu, akidhani watu wa kizazi hiki watamkubali yeye au chama chake ni hoja ya kitoto kabisa. Mpiga kura, hasa wa vijijini, anahitaji huduma bora ya afya, elimu, maji na miundo mbinu ya usafirishaji itakayomwezesha aweze kufanya shughuli zake za kijamii, kisiasa na hasa kiuchumi kwa majira na misimu yote ya mwaka.

Unadai ati Kama alidhani akitekeleza baadhi mambo na kuondoa uhuru wa vyombo vya habari, tutamsujudia na kumkubali yeye au chama chake basi amechemsha, ni fikra za mfa maji kisiasa. Siasa za majukwaani zimepitwa na wakati. Na siasa za kwenye vyombo vya habari au/na mitandao ya kijamii ni za udaku tu.

Sijui kwa nini viongozi wa upinzani wanaamini kuwa Tume Huru ya Uchaguzi ndiyo itawaingiza madarakani!! Wakumbuke tu kuwa wahenga walinena Mkono mtupu haulambwi.

Kwani huduma bora kwa hao watu wa vijijini zinaletwa na ccm au ni kutokana na kodi za wananchi? Siasa za majukwaani hazijawahi kupitwa na wakati maana ndio siasa zenyewe. Labda kama hujui siasa ni nini. Siasa za kwenye vyombo vya habari na mitandaoni ni kutokana na nyakati, hizi ni nyakati digital, taarifa nyingi hupatikana mitandaoni.

Acha upotoshaji, wapinzani hawataki tume huru ya uchaguzi ili kuwapeleka ikulu, wapinzani wanahitaji tume huru ya uchaguzi ili mshindi apatikane kwa uhalali. Huenda unabishana kuhusu uwepo wa tume huru bila kujua hata wanaoidai wanamaanisha nini. Tatizo lililopo sio kuwa hamshindi baadhi ya sehemu kihalali, bali huwa sehemu kubwa ya ushindi wenu ni kupitia udhaifu wa tume mnayolazimisha iendelee kuwepo.
 
Kwahyo unataka kusema kwmb Tanzania inahitaji Rais mwenye siasa nyingi kuliko kutenda, ckia nikwambie mnyonge tumnyonge ila haki yake tumpe, mm cjampigia kura Rais Magufuli lkn pia hata maisha yng co mazuri kivile but haitoshi kuwa mbinafsi kwa kutoona juhudi anazofanya Magu, japo ni kweli ana mapungufu yake lkn kwa hali tuliyokuwa nayo ilitupasa kuwa na rais huyu, umeongelea kuhusu siasa kubanwa, cjui uhuru wa habari, je watu wanakula uhuru wa habari?, watu wanatembea juu ya uhuru wa habari? Watu wanakunywa uhuru wa habari? Nikukumbushe tu kwmb tangu tupate uhuru nchi hii hatujawahi kujenga reli zaidi ya kuhangaika na reli ya mkoloni, je hilo hulioni unaona uhuru wa habari, ni kweli uhuru wa habari kwa ss umebanwa, je unaonaje uhuru wa habari kubanwa kwa miaka 10 lkn kupata reli kwa vizazi na vizazi au kukosa reli, miundombinu bora, maji safi na salama, vituo vya afya lkn kuwa huo uhuru wa habari ambao kila cku tulijiongopea kuwa nao ilihali watu wana EPA nchi, wana ESCROW nchi kila cku.

Watanzania tuache unafki na ubinafsi, tusimame pamoja kujenga nchi, siasa hazijawahi kutupeleka popote zaidi ya kutuumiza tu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Unaweza kuleta ushahidi kuwa siasa na uhuru wa vyombo vya habari unazuia ujenzi wa reli, unanyima utoaji wa huduma za jamii nk? Kenya hapo wana uhuru wa vyombo vya habari, wanafanya siasa, huduma za jamii zipo, wana reli kama yetu na inafanya kazi sio hata iko kwenye ujenzi. Na isitoshe uchumi wao uko juu kuliko wakwetu. Mbona huko Kenya hayo yamewezekana. Acheni Utetezi wa kipuuzi, kama hamna hoja kaeni kimya.
 
Mimi binafsi sina chama, si kwa sababu nataka iwe ivyo, ni kwa sababu sijaona chama Tanzania chenye misimamo nayotaka mimi.

Rais Magufuli na Bunge:
Kwa mtazamo wangu nadhani si kwamba raisi Magufuli anapinga mhimili wa bunge, hili limedhihirishwa na mkataba alioingia Muheshimiwa Kangi Lugola. Kwa kauli yake kupinga mkataba ule Kwa kuwa haukushirikisha bunge wala serikali yake wala wizara nyingine husika Kama Wizara Ya Fedha. Nafikiri tu kwa raisi magufuli kukubali kupeleka mambo mengi ambayo anafanya sasa bungeni basi hayo mambo yangebaki kwenye ubishani yasingefanyika.

Kupeleka majadiliano bungeni inakuwa Kama mbwa ukimshika mkia hata afanye vipi atafanya unavyotaka wewe. Serikali yetu ingekuwa imeshikiliwa mkia ingebweka tu ila bunge lingekuwa linapoteza mda mwingi kwenye mabishano ya kisiasa yasiyo zaa matunda na mambo mengi yangesimama kama tulivyoona serikali zilizopita. Hapa tuna kubwa la kujifunza, kutokuwa Na uwiano mzuri kati ya serikali Na bunge.

Raisi Magufuli na Misimamo Yake Kisiasa:
Nakumbuka raisi Magufuli alivyoingia madarakani katika mambo aliyoyafanya mwanzo Ni kupinga siasa zisifanyike wakati uchaguzi umepita. Kwa wapinzani waliona Kama wananyimwa kuwa huru kisiasa kiasi cha kumwita Magufuli Ni ditekta. Upande wa pili kwa raisi Magufuli alipinga hili ili kupisha maendeleo yafanywe na wale viongozi waliochaguliwa, akisisitizia, siasa za majukwaa zimepita sasa waliochaguliwa wafanye siasa za ktekeleza yale waliyoyaimba kwenye majukwaa. Lakini kitu ambacho nakiwaza tu Ni kuwa raisi Magufuli aliruhusu waliochaguliwa wawe wapinzani au awe CCM anaruhusiwa kufanya siasa kwenye jimbo lake hususani madiwani Na wabunge.

Mimi binafsi niko wilaya ya Ubungo Na nimepita sana Pwani huko na hata mkoani Kilimanjaro ambapo ni nyumbani, lakini sijaona madiwani au wabunge walioita mikutano kujadili lipi lifanyike kuleta maendeleo (nimeuliza maeneo mengi ila hiki ndicho kinachoendelea). Nani kaenda kufanya mikutano ya hadhara kakataliwa kwenye jimbo lake?

Magufuli na Tundu Lisu:
Kwanza kabisa nasikitika Sana kwa mheshimiwa Tundu Lisu kupigwa risasi mchana kweupe na jambo hili kupelekwa kisiasa. Ila nimeona jambo ndani ya Mheshimiwa Tundu Lisu na chuki yake dhidi ya raisi Magufuli. Binafsi wanasiasa wanachukiana ila chuki zao ni za kisiasa wakiwa kwenye mziki wanacheza pamoja, binafsi sijui chuki hizi zililetwa na nini ila wao binafsi wanaelewa kindaki ndaki sio tunashabikia tu. Ila nasikitika sana kitendo cha mheshimiwa Tundu Lisu kwenda kuichafua Tanzania ili tusipewe misaada kwa chuki yake binafsi dhidi ya raisi, bila kujali anachikiomba anawaathiri vipi wa Tanzania.

Mheshimiwa Tundu Lissu anazunguka sehemu nyingi duniani kutaka wajitenge Na Tanzania wakati familia yake, ndugu zake Na ukoo wake wapo Tanzania. Amezunguka akiomba mabeberu watunyime misaada kitu ambacho hajui kingemuathiri kila mTanzania. Amediriki kukubaliana Na mabeberu tena nimesikitika Sana kusikia mheshimiwa Tundu Lisu akisapoti ushoga kabisa kwa mdomo wake mwenyewe na kuikandia serikali ya Tanzania ka kukataa ushiga ilihali anajua tamaduni hizi kwetu hazipo. Mbali na kuichafua Tanzania hao mabeberu bado wamekuwa mstari wa mbele kuleta misaada na kuikopesha Tanzania.

Mheshimiwa Tundu Lisu amekosa uzalendo kuhusu Tanzania juu ya chuki yake dhidi ya Magufuli. Kama alikuwa na mashtaka binafsi juu ya Magufuli sikatai ila hana ulazima wa kuichafua Tanzania na kuchinganisha na nchi rafiki, hata Magufuli akitoka madarakani uhusiano uliopo kati ya Tanzania na nchi nyingine utabaki, anapotaka kuuvuruga hata aje raisi mwingine lile doa litakuwepo tu ..

Raisi Magufuli hata Kama anayoyafanya analazimisha Kwa wananchi wa Tanzania na yatabaki kwa wananchi wa Tanzania. Hizo ndege si zake Ni za waTanzania, Na juhudi hizi zinaonekana ni za kujenga Tanzanua; huku Tundu Lisu anabomoa kile kinachojengwa kwa wa Tanzania. Tanzania inasonga mbele Kwa shida kwa raha ila inasonga mbele.

Siasa na Taaluma:
Kwa mtazamo wangu tu nchi yetu imeshindwa kutofautisha siasa na taaluma, hapo mwanzo tulikuwa tuko kwenye shimo dogo tu ila kwa sasa tuko kwenye shimo kubwa sana. Raisi Magufuli kwa kuchagua viongozi wenye taaluma zao kwa asilimia kubwa ameua nguvu nzito kwenye taaluma yetu. Kila m Tanzania sasa amekuwa mwanasiasa kitu ambacho kimekuwa sana katika utawala huu wa awamu ya tano. Ukienda chuoni, mashuleni, jeshini na maofisini watu wengi wamekuwa wanaacha taaluma zao na kuingia kwenye siasa. Baadhi ya viongozi au taaluma (mfano maprofesa, madokta, wanajeshi) ambao wamechaguliwa na raisi wetu wangeweza kuwa walimu wazuri wazalishe wanasiasa wazuri ila wameacha kuzalisha wanasiasa na wamekuwa ndio wanasiasa wakubwa. Sasa kumekuwa na taaluma mbovu kwa sababu ya siasa za kupita, ila manufaa ya taaluma si ya kupita.

Magufuli na Wananchi Wake:
Kwa mtazamo wangu kuna wananchi wanakubali Sana kazi na mwenendo wa serikali ya raisi Magufuli. Ila pia kuna wananchi wanachukia sana mwenendo wa serikali hii ya awamu ya tano kwa mitazamo yao mingi tu. La kusikitisha kipindi hiki cha miaka mitano wananchi wamepandikizwa chuki mbaya ambazo Ni kinyume Na utamaduni wetu Kama waTanzania. Chuki hizi zinaonekana mpaka baina ya ndugu Na ndugu huku watu wakiwa wamesahau siasa si chuki. Mfano tu humu ndani ya JF nimesoma nyuzi nyingi humu ndani watu wameshindwa kabisa kubishana kwa hoja majibu yao yanakuwa mfano “nenda kachukue buku saba lumbumba”, huku jukwaa hili la siasa likikosa sifa kabisa kwa kuwa na matusi mengi ambayo nashindwa kuyaandika hapa kwa maadili yangu yalivyo. Nahimiza tu watu wawe CCM, CHADEMA, au chama chochote kile siasa sio ‘Matusi’ “Hoja Hupingwa Kwa Hoja”

Siasa za Upinzani:

Kwa mtazamo wangu tu siasa zimebadilika Sana Kwa wapinzania Kwa sasa zile siasa za kusema tutajenga mashule, hospitali, barabara, tutaleta maji nk Kwa sasa hazisikiki. Nimekuwa najiuliza Sana Kwa nini hazisikiki? Nimegundua kuwa Kwa sasa vitu vingi vimejengwa au kuboreshwa Na serikali hii ya awamu ya Tano. Wapinzani wa raisi Magufuli kwa asilimia kubwa kazi zao zimekuwa ni kuponda tu huku huku hawawi mbele kusema kipi kifanyike. Kwa akili ya kawaida tu huwezi kuwa mmekaa kibarazani aje mwenye nyumba awaulize ‘mmekula nataka kuwaletea chakula’ alafu mmoja wenu ajibu “sie tumeshiba” huku mnakuta wengine wana njaa kali amewasemea bila kuwauliza kama wanahitaji kula. Kwa sasa siasa zimekita kwenye udikteta wa raisi Magufuli na kuponda yale anayofanya huku wakiwa hawasemi nini kifanyike tusonge mbele..

Kwa mtazamo wangu tu Wapinzani kuleta maendeleo si lazima wawe wamechaguliwa: Kwa jinsi nilivyoona wapinzani wakiwa msatri wa mbele kuomba michango ya kuwatoa wenzao gerezani au kuomba hela za hospitali za mheshimiwa Tundu Lisu basi wangeweza kutumia njia hizo hizo kukusanya michango kwa waTanzania ili kuleta maendeleo. Hata Kama hili lingepingwa wapinzani hawa wangeweza kuanzisha utaratibu Kwa viongozi waliowachaguliwa ndani ya upinzani kuleta maendeleo Kwa michango ya wananchi wenyewe ILA zingeonekana Ni juhudi zao ndio zimeleta maendeleo. Wapinzani wanaonekana kuwa wamesahau kabisa kuwa ‘Maendeleo Hayana Chama”

La mwisho ningependa sana kuona siku moja upinzani umeshika madaraka Tanzania ila si kwa upinzani huu naouona sasa. Na ningependa sana kuona CCM inavunjwa Na kuanzishwa chama kipya chenye wanasiasa mahiri wanaoweza kuleta mabadiliko ya kweli Tanzania Kwa wananchi wake. Ningependelea sana kuona siasa zenye tija na maendeleo kwa waTanzania wote bila kujali wametokea vyama gani vya siasa. .
Umetuhadaa kuwa hauna chama ila dalili zote zinaonyesha Wewe ni kada mwaminifu.Ukweli utatuweka huru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siasa za wapinzani ni matusi, hakuna mpinzani aliyenijibu hapa bila kutukana
Unashangaa kuwa watu wako influenced na siasa???? serious? unavyotetea hapa upinzani are you not influenced? haijakuathiri? is that not the reason you are arguing?

Am sorry, but am not an idiot you believe everyone must be. Nina uwezo wa kufikiri, nina kumbukumbu na nina exposure kwenye mambo mengi tu. Sina tabia ya kuamini kitu bila kufanya verification.
Sasa tuje upande wako, unadai Tundu Lissu anaichafua Tanzania; kwa kudai hivyo unaashiria kuwa unaamini hao watu wanaomsikiliza Lissu ni wapumbavu sana kiasi kwamba ama hawawezi wenyewe kufanya verification ya kile wanachoambiwa au hakuna chanzo kingine wanakoweza kupata habari husika. By the same token, imani yako ni kuwa Kila anaemkosoa Magufuli ni mpinzani. Sasa huo ndio upumbavu wenyewe niliokuuliza, maana mtu mwenye akili timamu ni lazima atajua kuwa HAIWEZEKANI watu wote wakawa na mawazo yanayofanana hata kama wamezaliwa mapacha achilia mbali kuwa wanachama wa chama kimoja.

Una hiari ya kumuabudu Magufuli, lakini usitake, usilazimishe wala kutarajia Kila mtu afanye hivyo. Not everyone is a nincompoop.
 
Hahah
Unalazimisha vitu amabvyo havipo viwe
Unalazimisha maneno juu ya kinywa changu
Unalenga kuwa Magufuli kazuia uchunguzi juu ya Lisu kitu hapocho hakipo
Nionyeshe ushahidi hata wa makala ya gazeti wapi Magu alipinga uchunguzi wa Lisu?????

Mie unanipush ili nionekane namtetea Magu kwa kitu amabcho hakina ukweli ndani yake
Unaibadilisha mada iwe juu ya tukio la Lisu
Hulku swali langu hata moja hujibu huku ukiwa pamoja na Lisu kwa sababu tu hata akitetea ushoga na kuitaka kubomoa maendeleo yetu

Magu ana mapungufu yake, Lisu nae ana yake ila at least Magu hakubali ushoga aiseee
Turudi kwenye Mada yangu kuwa chuki kati ya Lisu na Magu inatuathiri sie huku mabishano yake hayana faia yeyote kwetu
Nimeshakwambia kama Magufuli ana nia njema kwanini asiruhusu huo uchunguzi huru? nini kinachoshindikana hapo.

Tena nikakwambia, utaviamini vipi vyombo vya usalama Tz wakati Lissu akipigwa risasi ulinzi uliondolewa nyumbani kwake?

Sijaona majibu uliyotoa kuhusu hilo.

Na ujue tena kwamba, Lissu kupinga baadhi ya mambo yakiyokuwa yakiendelea Tz ulikuwa ni mtazamo wake, wajibu wenu ulikuwa ni kumjibu muonekane jambo mlilofanya mlikuwa sahihi, sio kukimbilia kumuita Lissu msaliti, huo ni uoga.

Halafu unasemaje nakuwekea maneno mdomoni, hujui unachokiandika ndio kina akisi mawazo yako, so either uandike au uongee yote ni yaleyale.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Magufuli is a country bumpkin.

Sent from my typewriter using Tapatalk
And has turned Tanzania into a laughing stock. Mtu gani mwenye akili anaeweza kumsema vibaya housegirl wake mbele ya wageni (hata kama mtu huyo ana kosa)? Busara ya kawaida kabisa ni kusubiri wageni waondoke ndipo unamkosoa. Sasa Rais anaewafokea subordinates wake hadharani na kuwauliza watu wasiojua hata taratibu "eti wananchi, hawa niwafanye nini" ni Rais au kituko? Hana ofisi?
 
Back
Top Bottom