Mtendaji Mkuu wa TANROADS: Tanzania inashika nafasi ya 9 kwa miundombinu ya barabara na madaraja kati ya nchi 54 za Afrika

Kwamba Mimi ndio nilifanya Utafiti au? Inawezekana wewe una deal na south Africa mjini tuu hujawahi hata fika interior kwao huko.

Tanznaia inafikika Kwa 85% ya Vijijini Kwa Barabara Bora kabisa za gravel achilia mbali Barabara kuu
South Africa ni nchi pekee iliyopo barani Afrika ambayo yenye mtandao mpana zaidi wa barabara Bora zaidi kushinda nchi nyingine zote katika bara hili, hata baadhi ya nchi za Ulaya zimezidiwa na South Africa kwa miundombinu Bora ya barabara.
 
Ila takwimu hazidanganyi.Tqnzania Ina Barabara nzuri sio tuu Barabara kuu Bali Hadi za Vijijini tuko Bora zaidi.
Sahihi lakini si kwa south Africa wametuacha mbali saaaana wanachofanya hao viongozi wetu ni kuwa wanakua watanzania wengi ni mazuzu chochote watakachoongea watanzania watakubali tu. Lakini ukweli kwa south Africa tusidanganyane kabisa.
 
South Africa ni nchi pekee iliyopo barani Afrika ambayo yenye mtandao mpana zaidi wa barabara Bora zaidi kushinda nchi nyingine zote katika bara hili, hata baadhi ya nchi za Ulaya zimezidiwa na South Africa kwa miundombinu Bora ya barabara.
Awezi kukuelewa huyo mkuu. Shida hii nchi yetu Kuna maviongozi maongo sana na yanajua watanzania wengi si wafutiliaji wa mambo
 
Hakika. Yaani Afrika Kusini hii ninayoifahamu mie, (nimefika by the way) ifanane na Uswazi hapa kwenye ubora wa barabara? Barabara zenyewe ni kama hizi za Moro - Mwanza, Makambako - Tunduma, Dar - Nangurukuru. No way
Hahahah huko nangurukuru mbona mbali. Kwenye hizi Province tu za Kinondoni,Temeke na Ilala kuna vituko vya kukata na shoka.

Chukulia kipande cha Veterinary kwenda Mwembeyanga halafu unioneshe South Africa kwenye jiji kongwe kama Dar lenye njia ya kufanana na ile.
 
South Africa ni nchi pekee iliyopo barani Afrika ambayo yenye mtandao mpana zaidi wa barabara Bora zaidi kushinda nchi nyingine zote katika bara hili, hata baadhi ya nchi za Ulaya zimezidiwa na South Africa kwa miundombinu Bora ya barabara.
Halafu pimbi anakwambia tumeipiku south africa bila aibu. Tanzania hii ambayo barabara yenye multiple lanes ni ya Kimara Mwisho mpaka kibaha πŸ˜‚!

Nchi nzima barabara za mikoa ni 2 lanes mtoa mada atakuwa on some serious Narcotics.
 
Labda kama unazungumzia South Africa ya Nachingwea.
 
Utaahira ni pale unapokubali bandiko lililojaa uozo na uongo, hivi South Africa umewahi kufika? In short Tanzania hakuna barabara, yaani hata mwehu aliyewahi kutembea ataona dhahiri shahiri ukweli ulivyo.
 
Barabara zipo nyingi mkuu,kama hizi tunazopita kila siku tupumzishe
 
NAPENDA KUMPONGEZA DR SAMIA KWA KAZI NZURI AIFANYAYO KUHAKIKISHA TUNASONGA MBELE NA TANZANIA INASOMEKA KWENYE RAMANI YA AFRIKA NA DUNIA, HONGERA NI ZA SAMIA NA SI WENGINE.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…