Mtindo wa Misiba ya Siku Hizi: Watoto waliozaliwa mijini (1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kupasua ukoo

Mtindo wa Misiba ya Siku Hizi: Watoto waliozaliwa mijini (1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kupasua ukoo

Watoto hawana mazoea ya kwenda kijijini, msiba upelekwe kijijini, nani akaratibu hizo shughuli za mazishi??

Anayeacha maelekezo akifa akazikwe kijijini aache na nauli kabisa ya kumpeleka huko.

Besides, wakishamzika, wao na vizazi vyao hawarudi huko tena, yaani ndiyo nitolee. Bora azikwe mjini, manispaa itasafisha mazingira ya nyumba yake ya milele.

Everyday is Saturday................................😎
 
Siyo kosa kusafirisha mwili wa mpendwa wako, lakini siyo suala la kufa na kupona.
Maana hilo si jambo la kiibada kwa hizi dini zetu kubwa.
Kusafirisha mwili ili kumzika alikozaliwa kuna kiasi furani cha upagani.
Maana baadhi ya mira za kiafrika makaburini ni sehemu ya kufanyia IBADA (Maombi).
Kwahiyo baadhi ya makabila yetu hupenda ukaribu na wafu wao ili wasipate usumbufu wakati wa matambiko.
Mkuu usije kujitetea kuwa sikukuambia, narudia tena, nikikata moto nizikwe hapa hapa mjini. Sitapendezwa kabisa kuwa mbali na ile mitaa yetu pendwa.
 
Mkuu usije kujitetea kuwa sikukuambia, narudia tena, nikikata moto nizikwe hapa hapa mjini. Sitapendezwa kabisa kuwa mbali na ile mitaa yetu pendwa.
Hahaha, nitazingatia Wosia wako mkuu.
Nadhani makaburi yale Chang'ombe (Wailes) au ya Unubini yanatufaa.
Ikishindikana basi tupelekwe Kisutu au Kinondoni.[emoji120][emoji120]
 
Kuwapeleka watoto vijijini kuna faida nyingi tusizozielewa. Licha ya kujua maneno ya kilugha, watajua ndugu, mila na desturi.

Pia watakwenda shambani na kuona kilimo cha mazao kinavyofanyika. Hili linapanua upeo wao ki elimu. Watoto wa mijini hawajawahi kuona nanasi likiwa shambani.

Watoto wa mijini wengine hawajawahi kuona milima. Ukipita Uruguru pale unawaonyesha watoto milima ya Uruguru na kuwaambia kuwa hii ni mfano ya milima meza kama ya Usambara.
Nakutunuku shahada ya heshima ya udaktari katika nyanja ya ushauri,honorary causa .sasa wewe ni Dk Sky Eclat
 
Infantry Solder mdogo wangu pamoja na umri wako mdogo lakini unatoaga mada fikirishi za kujadili.
Mtu asikudanganye kupenda kwenu ni maendeleo. Chunguza makabila yasiyopenda kwao hata maendeleo yao yanakuwa hafifu sana. Wazungu ndio maana hata akija Tanzania akifa anapelekwa kwao mwili ukishindikana hata akichomwa moto majivu yanapelekwa kwao.

Mila za kabila flani mtoto akizaliwa hata azaliwe Marekani kitovu kikikatika kitapelekwa hadi kijijini kinachimbiwa ndani ya nyumba hizi ni mila siwezi kujadili.Utakuja kuona makabila yasiyopenda kwao kunakuwa na sababu moja wapo kwa vile kwao hakuna hata nyumba mtu anaona aibu kumpeleka mzazi wake maana atachekwa jinsi kulivyo na hali mbaya.

Maendeleo ya wachaga sio bure ni shauri ya mila hizi za kupenda kwao mkataa kwao ni mtumwa.Ukipata watoto usipowapeleka kwao wanapoteza identity ya kujua asili yao na kujua mila zao ni kweli nakiri tumebadilika lakini nyumbani ni nyumbani tu.Makabila mengine ushirikina unawarudisha nyuma mno kiasi cha kuogopa hata kuzikwa kwao

Moja ya kuzika nyumbani ni alama kwa mfano mkoa wa Kilimanjaro ardhi ni haba sana mtu anapozikwa kwenye shamba lake hata vizazi vya nne vinapopatwa na matatizo ya ardhi kudhulumiana makaburi yanatumika kama beacon ya utambulisho kuwa hapa palikuwa kwa nani.

Hata vitabu vya dini Yakobo alivyofariki mwanaye Yusuph alimpeleka kumzika kwao nchi ya ahadi.
 
Watoto ambao hawajazoea kwenda kijijini wanakomaa wazazi wazikwe Dar.. sabab wanaona usumbufu kwenda mkoani kusafisha kaburi ama kuombea wazazi wao makaburini kila baada ya muda..

Pongezi nyingi kwa wachaga.. kwa kuzoesha watoto kwenda moshi mara kwa mara
Tutafika mahali tutakua tunachoma na kupeana majivu

Hizi abudu za makaburi na mashirikina mengine zinauwawa na muendelezo wa evolution na globalization
 
Je, kuna umuhimu wa wazazi kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo? Unawapelekaga watoto wako?

Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania;

Siku za hivi karibuni nimekuwa nikishuhudia matukio mengi sana zaidi ya mara 4 katika misiba niliyopata kuhudhuria ambapo watoto waliozaliwa mijini (1980's - 1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kusababisha mpasuko wa mahusiano ndani ya ukoo.

Kwa hapa Tanzania, makabila yetu yamegawanyika katika makundi makuu mawili. Kuna makabila ambayo kuzika mtu kwao sio jambo la maana sana kiasi kwamba hata ukifia Magomeni wao kukuzika makaburi ya Kinondoni ni kawaida tu.

Kundi la pili ni yale makabila mbayo ni mwiko kabisa kuzika mwili wa ndugu yao nje ya kijiji. Yaaani kama mtu alifia Dar, basi ni lazima asafirishwe mpaka mkoa wa Mara, tena akazikwe katika makaburi ya ukoo.

Hata kama mtu amekufa tuseme huko Ulaya, basi ni lazima aletwe kutoka huko New York mpaka Rorya hukoooo Shirati au Utegi. Juzi hapa nilienda katika msiba mmoja hapa jirani na nilipopanga wa watu wa kabila moja la huko Mkoa wa Kigoma.

Katika msiba huu ndio ninakutana na hiki kisanga cha watoto 3, ambao financially wapo njema sana na mmoja wao ni Country Manager wa kampuni moja ya wazungu huku Dar tena ni mtoto wa kiume.

Sasa wakuu ninaomba kujua chanzo kikuu ni nini? Je, ni wazazi wenyewe kutopenda kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo ya mwaka ili wajuane na mazingira pamoja na ndugu zao wa huko au shida ipo wapi hapa wakuu?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Hao wazazi wambie wawe wanaacha na nauli ya kusafirishia!
 
Kwtu ni muhimu nasisitiza kuzikwa nje ya makaburi mababu ni sawa na kutupwa porini. Wazungu ndio kielelezo cha kuzikwa makwao hata kwa kuchomwa na kulekwa majivu.naona wajumbe wengi wanashauri watu wajiwekee kabisa pesa za kugaramia usafiri wa kupeleka miili yao pindi watakavyokufa ili waliobakia wasisumbuke. Wazungu hufanya hivyo kabla ya umauti wao
 
Je, kuna umuhimu wa wazazi kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo? Unawapelekaga watoto wako?

Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania;

Siku za hivi karibuni nimekuwa nikishuhudia matukio mengi sana zaidi ya mara 4 katika misiba niliyopata kuhudhuria ambapo watoto waliozaliwa mijini (1980's - 1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kusababisha mpasuko wa mahusiano ndani ya ukoo.

Kwa hapa Tanzania, makabila yetu yamegawanyika katika makundi makuu mawili. Kuna makabila ambayo kuzika mtu kwao sio jambo la maana sana kiasi kwamba hata ukifia Magomeni wao kukuzika makaburi ya Kinondoni ni kawaida tu.

Kundi la pili ni yale makabila mbayo ni mwiko kabisa kuzika mwili wa ndugu yao nje ya kijiji. Yaaani kama mtu alifia Dar, basi ni lazima asafirishwe mpaka mkoa wa Mara, tena akazikwe katika makaburi ya ukoo.

Hata kama mtu amekufa tuseme huko Ulaya, basi ni lazima aletwe kutoka huko New York mpaka Rorya hukoooo Shirati au Utegi. Juzi hapa nilienda katika msiba mmoja hapa jirani na nilipopanga wa watu wa kabila moja la huko Mkoa wa Kigoma.

Katika msiba huu ndio ninakutana na hiki kisanga cha watoto 3, ambao financially wapo njema sana na mmoja wao ni Country Manager wa kampuni moja ya wazungu huku Dar tena ni mtoto wa kiume.

Sasa wakuu ninaomba kujua chanzo kikuu ni nini? Je, ni wazazi wenyewe kutopenda kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo ya mwaka ili wajuane na mazingira pamoja na ndugu zao wa huko au shida ipo wapi hapa wakuu?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Wengine wazazi wamezaliwa mkoa A wakafanyia kazi Mkoa B+C tukazaliwa+kukulia mkoa C ambapo wazazi wanaishi mpaka leo then sisi tunafanya kazi+kuishi mkoa D na tumezalia huku ...hao watoto tutawapeleka wapi hiyo likizo ?wakati kijijini kwa wazee ni mkoa A ambapo dingi mwenyewe haendagi ila Mara chache sana
 
Kwa mujibu Wa Dini ya kiislam mtu atazikwa alikofia.Hao wamefuata Sunna hakuna haja ya kuingia gharama ya kusafirisha maiti.
 
Tatizo watu huko baadhi ya vijiji wamekua walozi sana hasa kwa ndugu,na watu wanafanya zao mishe huko mijini wameligundua na kuanza kuzitenga familia zao na vijiji vyao....

Wengi wa watu huko vijijini wanaamini kuwa watu wa mjini wameyapatia maisha lakini hawawasaidii,hivyo kuamua kuwaloga na kuleta usumbufu na matatizo kwenye hizo familia... na mbaya Zaidi hata ukitokea msiba na watoto wakapeleka vijijini basi hao ndugu walozi kwenye hasira nao hutumia nafasi hiyo kuwaangamiza.

Sababu nyingine in uwepo wa dini umefanya hizi mila zionekane hazina umuhimu pia uwepo wa elimu umeonyesha kuwa kusafirisha in gharama zisizo na msingi...hivyo tunazika tu Kinondoni.

Hizo sababu nilipewa na bàadhi ya watu kwa kujaribu kuuliza swali kama lako.
 
Wengine wazazi wamezaliwa mkoa A wakafanyia kazi Mkoa B+C tukazaliwa+kukulia mkoa C ambapo wazazi wanaishi mpaka leo then sisi tunafanya kazi+kuishi mkoa D na tumezalia huku ...hao watoto tutawapeleka wapi hiyo likizo ?wakati kijijini kwa wazee ni mkoa A ambapo dingi mwenyewe haendagi ila Mara chache sana
Very complicated

Uzuri mkoa A kuliko nyumbani unakujua, ni wewe kusuka ama kunyoa
 
Mtu amekaa Mkoa A miaka na miaka. Watu "wote" wanaomfahamu wako mkoa A. Kule kwao mkoa B "hakuna" anayemfahamu. Akifa kwa nini apelekwe kijiji cha mkoa "B"? Hata babu yake hakuzaliwa kijiji cha mkoa "B", utakuta na yeye alihamia.
 
Wengi wa watu huko vijijini wanaamini kuwa watu wa mjini wameyapatia maisha lakini hawawasaidii,hivyo kuamua kuwaloga na kuleta usumbufu na matatizo kwenye hizo familia
Kuna baadhi ya watu bado wanaamini mambo ya kurogana?...
 
Back
Top Bottom