Mtindo wa Misiba ya Siku Hizi: Watoto waliozaliwa mijini (1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kupasua ukoo

Mtindo wa Misiba ya Siku Hizi: Watoto waliozaliwa mijini (1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kupasua ukoo

Inategemea

mna kawaida ya kwenda huko?.
Mna hata pa kufikia?.
Kabisa mkuu, tulishamsindikiza jamaa kuzika babake kijijini mkoa fulani, tulipata taabu sana, tulilala wenye coaster, nje baridi mpaka wenye mifupa, guest ya karibu hakuna, maduka ya mahitaji shida, msalani ndiyo ilikuwa kuchimba dawa, literally! Tanzania ni kubwa jamani, kuna maeneo watu wakiondoka hawarudi na sababu ni valid.

Safari ya kurudi, tulipaki njiani somewhere guest, tukawalipa kutuchemshia maji tuoge, turudi mjini tumeondoa harufu ya kijijini.
Hapana kwakweli!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Siyo kosa kusafirisha mwili wa mpendwa wako, lakini siyo suala la kufa na kupona.
Maana hilo si jambo la kiibada kwa hizi dini zetu kubwa.
Kusafirisha mwili ili kumzika alikozaliwa kuna kiasi furani cha upagani.
Maana baadhi ya mira za kiafrika makaburini ni sehemu ya kufanyia IBADA (Maombi).
Kwahiyo baadhi ya makabila yetu hupenda ukaribu na wafu wao ili wasipate usumbufu wakati wa matambiko.
Kuzika mtu mahali au kijijin sio upagani upo ndani ya misaafu mf. Mf Yakob Alifia Misri Ila kuzikwa Kanaani, pia angalia Yusuph nae na kuna wengine wanazikwa kando ya msikiti au kanisa je nao ni upagani?
 
Je, kuna umuhimu wa wazazi kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo? Unawapelekaga watoto wako?

Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania;

Siku za hivi karibuni nimekuwa nikishuhudia matukio mengi sana zaidi ya mara 4 katika misiba niliyopata kuhudhuria ambapo watoto waliozaliwa mijini (1980's - 1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kusababisha mpasuko wa mahusiano ndani ya ukoo.

Kwa hapa Tanzania, makabila yetu yamegawanyika katika makundi makuu mawili. Kuna makabila ambayo kuzika mtu kwao sio jambo la maana sana kiasi kwamba hata ukifia Magomeni wao kukuzika makaburi ya Kinondoni ni kawaida tu.

Kundi la pili ni yale makabila mbayo ni mwiko kabisa kuzika mwili wa ndugu yao nje ya kijiji. Yaaani kama mtu alifia Dar, basi ni lazima asafirishwe mpaka mkoa wa Mara, tena akazikwe katika makaburi ya ukoo.

Hata kama mtu amekufa tuseme huko Ulaya, basi ni lazima aletwe kutoka huko New York mpaka Rorya hukoooo Shirati au Utegi. Juzi hapa nilienda katika msiba mmoja hapa jirani na nilipopanga wa watu wa kabila moja la huko Mkoa wa Kigoma.

Katika msiba huu ndio ninakutana na hiki kisanga cha watoto 3, ambao financially wapo njema sana na mmoja wao ni Country Manager wa kampuni moja ya wazungu huku Dar tena ni mtoto wa kiume.

Sasa wakuu ninaomba kujua chanzo kikuu ni nini? Je, ni wazazi wenyewe kutopenda kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo ya mwaka ili wajuane na mazingira pamoja na ndugu zao wa huko au shida ipo wapi hapa wakuu?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Inategemea wamejengewa misingi gani na wazazi wao, pengine toka kuzaliwa kwao hata huko kijijini hawajawahi kufika, au pengine wazazi wao hawakua na maelewano mazuri na ndugu waliopo kijijini
 
Kwa ufupi sana. Kuna watoto ambao wakishafika mjini na kupatia maisha husahau walipotoka kwa maana ya kupajenga. Sasa wakishakuwa tatizo kubwa hapa mjini wanakuwa na kampani kubwa ya marafiki zao. Linapotekea swala kifo basi huwa ni ngumu sana kuwasafirisha wapendwa wao kwa kuhofia aibu kwakuwa hakuna chochote walichokifanya pale nyumbani cha maendeleo.
 
very complicated

uzuri mkoa A kuliko nyumbani unakujua,ni ww kusuka ama kunyoa
Sasa unaenda kumsalimia/kumuona nani?


Maana wazazi wenyewe hawaishi huko hata kwenda sio kivile...how come we uende tu na haumjui yoyote wala kwa yoyote,zaidi ya kuskia tu kijiji flani kuna flani zaidi sana ulipelekwa mara moja au ndugu wachache uliwaona mara moja mbili tena walivyokuja mjini
 
Mtu amekaa Mkoa A miaka na miaka. Watu "wote" wanaomfahamu wako mkoa A. Kule kwao mkoa B "hakuna" anayemfahamu. Akifa kwa nini apelekwe kijiji cha mkoa "B"? Hata babu yake hakuzaliwa kijiji cha mkoa "B", utakuta na yeye alihamia.
Hapo sasa
 
Kabisa mkuu, tulishamsindikiza jamaa kuzika babake kijijini mkoa fulani, tulipata taabu sana, tulilala wenye coaster, nje baridi mpaka wenye mifupa, guest ya karibu hakuna, maduka ya mahitaji shida, msalani ndiyo ilikuwa kuchimba dawa, literally! Tanzania ni kubwa jamani, kuna maeneo watu wakiondoka hawarudi na sababu ni valid.

Safari ya kurudi, tulipaki njiani somewhere guest, tukawalipa kutuchemshia maji tuoge, turudi mjini tumeondoa harufu ya kijijini.
Hapana kwakweli!

Everyday is Saturday............................... 😎
Sasa shida yote ya nini wakati mjini makaburi yapo mengi tu
 
Sasa 'nimefia' zangu Marekani ( japo sijawahi kufika na huenda hadi nikienda Udongoni sitofika pia ) na inasemekana Nauli ya Kunileta 'Sandukuni' kwa Mbung'o ( Ndege ) kwa sasa ni kama Tsh Milioni 25 mpaka 30 za Kitanzania.

Sasa kwanini tu 'nisizikwe' huko huko Marekani na hiyo Hela itumike kuwasaidia Wazazi wangu na Ndugu zangu huku Tanzania ili na Wao hata wakiwa 'wameshiba' zao Matembele na Maharage yao wanaweza 'wakajifariji' kwa Majirani kuwa wana Ndugu yao Mmoja 'Popoma' amezikwa kwa Donald Trump Marekani na Wakasifiwa vile vile?

Naunga mkono hoja hii.
 
Siku za hivi karibuni nimekuwa nikishuhudia matukio mengi sana zaidi ya mara 4 katika misiba niliyopata kuhudhuria ambapo watoto waliozaliwa mijini (1980's - 1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kusababisha mpasuko wa mahusiano ndani ya ukoo
Kwani ukizikwa kijijini ulikozaliwa ndio tiketi ya kwenda Mbinguni? 'Ujinga huu' ni sawa na ule wa kujengea kaburi wakati wewe mwenyewe unaishi kwenye chumba cha kupanga.

Yaani unamjengea nyumba marehemu wakati watoto wako walio hai bado wamejibanza kwenye nyumba za kupanga! Tamaduni kama hizi inabidi zipitwe na wakati ili kwanza tukabiliane na changamoto za kiuchumi zenye uhitaji wa juu (pressing needs).
 
Huwa nawashangaa watu 'wanaokompliketi ' mambo ya kuzika
Kwenda kuzikwa kijijini kwenu ni kukomplikate? Nyie ndiyo wale ambao mnakata 10 yrs haujatimba kijijini kuonana na mjomba, shangazi, baba mdogo /mkubwa, babu /bibi na wengine kwenye ukoo....
 
Mada hizi zinachanganya sana watu. Mzazi alitokea kijijini, akiomba azikwe kijijini tutajitahidi tumpeleke, lakini uwezo ukipatikana.

Mnaweza kuwa na nia nzuri ya kumpeleka lakini nauli ikawa shida kuipata, sidhani kama mtalazimisha. Mtafanya mtakavyoweza kwa wakati huo.

Binafsi ningependa nizikwe kijijini kwa baba yetu, lakini kama uwezo utakuwepo wakati nafariki na watakao kuwepo wakiweza kunifikisha huko itakuwa vyema, lakini siyo lazima ikiwa uwezo utakuwa mdogo kusafirisha mwili.

Ila kama marehemu uliacha pesa na utaratibu wa kuzikwa kijijini kwenu na isiwe hivyo hapo kweli tuliobaki tutawalaumu vijana.

Kila mtu anapenda apendavyo.
Mleta mada amezungumzia vijana ambao wana uwezo wa kutosha wa kifedha...
 
Kwenda kuzikwa kijijini kwenu ni kukomplikate? Nyie ndiyo wale ambao mnakata 10 yrs haujatimba kijijini kuonana na mjomba, shangazi, baba mdogo /mkubwa, babu /bibi na wengine kwenye ukoo....
Mkuu, mimi nimezaliwa kijijini, nimesoma kijijini na wazazi wangu mpaka leo wako kijijini kwa hiyo there is no way naweza kumaliza miaka hata mitatu bila kwenda. Whether nitazikwa kijijini, makaburi ya kinondoni au maiti yangu ikatoswa baharini mimi naathirika nini? Katika vitu huwa havinipi shida ni hayo masuala ya kuzika
 
Infantry Solder mdogo wangu pamoja na umri wako mdogo lakini unatoaga mada fikirishi za kujadili.
Mtu asikudanganye kupenda kwenu ni maendeleo.Chunguza makabila yasiyopenda kwao hata maendeleo yao yanakuwa hafifu sana.Wazungu ndio maana hata akija Tanzania akifa anapelekwa kwao mwili ukishindikana hata akichomwa moto majivu yanapelekwa kwao.
Mila za kabila flani mtoto akizaliwa hata azaliwe Marekani kitovu kikikatika kitapelekwa hadi kijijini kinachimbiwa ndani ya nyumba hizi ni mila siwezi kujadili.Utakuja kuona makabila yasiyopenda kwao kunakuwa na sababu moja wapo kwa vile kwao hakuna hata nyumba mtu anaona aibu kumpeleka mzazi wake maana atachekwa jinsi kulivyo na hali mbaya.
Maendeleo ya wachaga sio bure ni shauri ya mila hizi za kupenda kwao mkataa kwao ni mtumwa.Ukipata watoto usipowapeleka kwao wanapoteza identity ya kujua asili yao na kujua mila zao ni kweli nakiri tumebadilika lakini nyumbani ni nyumbani tu.Makabila mengine ushirikina unawarudisha nyuma mno kiasi cha kuogopa hata kuzikwa kwao
Moja ya kuzika nyumbani ni alama kwa mfano mkoa wa Kilimanjaro ardhi ni haba sana mtu anapozikwa kwenye shamba lake hata vizazi vya nne vinapopatwa na matatizo ya ardhi kudhulumiana makaburi yanatumika kama beacon ya utambulisho kuwa hapa palikuwa kwa nani.
Hata vitabu vya dini Yakobo alivyofariki mwanaye Yusuph alimpeleka kumzika kwao nchi ya ahadi.
Umeongea vizuri sana mkuu. Tabia ya kupenda kuzika nyumbani kwenu imesaidia sana kujenga umoja kwa watu wa Kilimanjaro wanaoishi mijini kwa kuunda vyama au umoja,ambao hutumika kuchangia ili mmoja wao akifariki wanasaidiana kusafirisha kupitia michango yao. Pia huu umoja umetumika sana kujadili maendeleo huko wanakotoka vijijini na wameweza kusaidia sana kuboresha barabara, mashule etc. Pia hii kitu inaongeza connections za kazi, biashara na fursa mbalimbali maana mara kwa mara unakuta wanakutana kwenye hii misiba huko vijijini au mwezi Desemba. Watu ambao wamekimbilia mijini na hawarudi makwao hata kwenye mazishi mara nyingi wamepotezana jumla maana wako miji tofauti tofauti.
 
Je, kuna umuhimu wa wazazi kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo? Unawapelekaga watoto wako?

Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania;

Siku za hivi karibuni nimekuwa nikishuhudia matukio mengi sana zaidi ya mara 4 katika misiba niliyopata kuhudhuria ambapo watoto waliozaliwa mijini (1980's - 1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kusababisha mpasuko wa mahusiano ndani ya ukoo.

Kwa hapa Tanzania, makabila yetu yamegawanyika katika makundi makuu mawili. Kuna makabila ambayo kuzika mtu kwao sio jambo la maana sana kiasi kwamba hata ukifia Magomeni wao kukuzika makaburi ya Kinondoni ni kawaida tu.

Kundi la pili ni yale makabila mbayo ni mwiko kabisa kuzika mwili wa ndugu yao nje ya kijiji. Yaaani kama mtu alifia Dar, basi ni lazima asafirishwe mpaka mkoa wa Mara, tena akazikwe katika makaburi ya ukoo.

Hata kama mtu amekufa tuseme huko Ulaya, basi ni lazima aletwe kutoka huko New York mpaka Rorya hukoooo Shirati au Utegi. Juzi hapa nilienda katika msiba mmoja hapa jirani na nilipopanga wa watu wa kabila moja la huko Mkoa wa Kigoma.

Katika msiba huu ndio ninakutana na hiki kisanga cha watoto 3, ambao financially wapo njema sana na mmoja wao ni Country Manager wa kampuni moja ya wazungu huku Dar tena ni mtoto wa kiume.

Sasa wakuu ninaomba kujua chanzo kikuu ni nini? Je, ni wazazi wenyewe kutopenda kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo ya mwaka ili wajuane na mazingira pamoja na ndugu zao wa huko au shida ipo wapi hapa wakuu?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Nazani uanze utaratibu wa wazazi kuwaambia watoto wao wapi wazikwe hii itasaidia sana kutatua hio migogoro.

Watu wa vijijini wanalalamika tuu ila ukiwaambia wachangie ata tsh 100 ya kusafirisha mwili hawatoi.
 
Wengine wazazi wamezaliwa mkoa A wakafanyia kazi Mkoa B+C tukazaliwa+kukulia mkoa C ambapo wazazi wanaishi mpaka leo then sisi tunafanya kazi+kuishi mkoa D na tumezalia huku ...hao watoto tutawapeleka wapi hiyo likizo ?wakati kijijini kwa wazee ni mkoa A ambapo dingi mwenyewe haendagi ila Mara chache sana
Hao ni wachache sana, majority wana asili yao walikotoka, hata pale mmojawapo anapoamua kwenda town kutafuta. Hivi ukienda kutafuta maisha town mji wenu kijijini mnauuza au kuutekeleza?
 
Back
Top Bottom