Mtoto wa kaka yangu wa kwanza (First born) amebamiza 'A' za kutosha za darasa la nne mpaka nimeogopa sana, tutafute pesa Elimu nzuri ni gharama

Wanangu wote wamepasua na Siringi
First born kagonga Div One form2,Sec born kagonga A zote drs la 4

Mungu ni mwema sana,namuomba azidi kuwabariki
 
Atajisikia vizuri baada ya kupata KAZI au kujiajiri na kula matunda ya mtoto baada ya kumaliza elimu yake!!
Ni sawa pia ila kwa dunia ya sasa si ya kumtegemea mtoto ni vzuri mzazi akajiandaa na maisha ya uzeeni na akawa na uwezo wa kujitunza kwa akiba aliyonayo.
 
Unachosema ni sahihi mkuu. Shule ina uwezo wa kushape akili ya mtoto mbali na elimu ya darasani.
 
Ni sawa pia ila kwa dunia ya sasa si ya kumtegemea mtoto ni vzuri mzazi akajiandaa na maisha ya uzeeni na akawa na uwezo wa kujitunza kwa akiba aliyonayo.
Huyo mtoto asipoweza kujisimamia Kwa elim hii no hasara hasta kama ukijipanga namma gani!!
Utalea watoto kwenye utu uzima wao!!
 
Kuna shule zinafundisha jamani. Wanafunzi wote wa St. Francis Girls wamepiga 1 ya 7 matokeo ya form two.

Unaweza kuona kama kuna wizi wa mitihani vile lakini hapana. Walimu wake wako vizuri na wanafunzi wako bright. Mchujo wa kusoma pale ni lazima kwenye shule yako ulipotoka uwe unacheza top 5. Siyo mchezo!!

Tusibishe, hizi shule private zinafundisha vizuri. Ukitaka kuamini hilo, angalia matokeo ya form two ya mwanafunzi ambaye darasa la 7 kafanya vizuri private.
 
Unachosema ni sahihi mkuu. Shule ina uwezo wa kushape akili ya mtoto mbali na elimu ya darasani.
Kuna watoto wamemaliza chuo na wamefaulu vizuri tu kwa sababu ya ugumu wa ajira wameamua kujiajiri ambapo wazazi wao wamewafungulia karakana ya kutengeneza vitu vya ujenzi, mageti, madirisha aluminium, paving blocks, furniture n.k aisee the way madogo wanavyofanya biashara wapo so professional na wanajua wanachokifanya na sasa wanapata tenda kwenye miradi kadhaa ya ujenzi.
 
Mkuu umenena vyema kabisaaa.
 
Hao watoto wa hizo shule wana balaaa hao nakumbuka kipindi nasoma kuna ambao nilikuwa nasoma nao tuition kipindi cha likizo aisee walikuwa wanawapa taaaabu sana waalimu wa tuition maana wana walikuwa na maswali mengi ya udadisi
 
Kuwekeza kwenye shule nzuri kwa ajili ya mtoto ni vizuri lakini wazazi wengi wanafuata mkumbo. Mtu anatumia hela nyingi kusomesha mtoto huku akitegemea ajira hizi hizi za bongo ambazo mshahara ni mdogo na pia hakuna career progress.
Mimi nimesoma shule za kawaida za serikali na chuo nimesoma UD , lakini nafanya kazi na watu ambao wamesoma nje ya nchi kuanzia undergraduate mpaka masters lakini kwenye kazi wako low sana ukilinganisha na tuliosoma UD na Mzumbe etc.
Mtu katumia mamilioni kusomesha halafu mnakuja kubanana kwenye hizi ajira za mshahara wa kawaida ili hali wengine wamesoma kwa gharama ndogo.
Pia ni vizuri kuwekeza kwenye practical experience ili kuwawezesha kupata uzoefu wa kazi. Kwenye hizi international organisations au missions kwanza hawataki mavyeti yako wakati wa kuomba kazi , vyeti wanahitaji kama utaratibu tu ,na ukipata kazi ndio wanakuambia uvilete.
 
Kwahiyo unatusimanga sisi wazee wa Kayumba.
 
Dooh!! Mwisho wa yote ni kuongea kingereza na kuchambua siasa.... uvumbuzi na kuleta mabadiliko katika Jamie yako sifuri.. "wabongo tujitadhmini"
Huwa nachukia sana kuona watu wakiziita shule zetu za serikali St. Kayumba na wakati wengi wetu hizo ndiyo shule zilizotulea kwenye elimu ya msingi.

Halafu Sasa huko kwenye hizo shule zao wanazolipa ada mamilioni watoto wao wakitoka huko hawana Cha ajabu chochote wanachokuja nacho zaidi ya kuongea kingereza Kwa kujiamini pamoja na kudeka.

Yaani ni kama vile wanaendaga kununua kingereza Kwa mamilioni ya pesa.

Yaani hakuna innovation skills zozote wanazokuwa nazo hao watoto wao Wala creativity ya aina yoyote, sana sana tu wanawaimbia Hawa wazazi wao nyimbo za father X-mass na kuwatafsiria Nini kinachosemwa na mtangazaji wa CNN.
 
🤣😂😝😝
 
Hao watoto wa hizo shule wana balaaa hao nakumbuka kipindi nasoma kuna ambao nilikuwa nasoma nao tuition kipindi cha likizo aisee walikuwa wanawapa taaaabu sana waalimu wa tuition maana wana walikuwa na maswali mengi ya udadisi
Wachukue walipata division 3 halafu wawafundishe wapate one wote ndio nitaona walimu wako vizuri. Ila mnachukua wote vipanga halafu mnajisifia m.afundisha.
Halafu haohao wakienda vyuo vya serikali wanakua hawana maajabu sababu wamezoea spoon feeding ambazo vyuoni hamna vitu kama hivyo.
 

Lugha ya kiingereza ni muhimu Kwa sasa kuifahamu kiufasaha.
 
wanasomesha watoto wao shule kubwa mkuu, shule za kizungu
Wahindi na waarabu wachace ndio wanaosomesha watoto wao shule za kizungu, tena ni wale ambao wana makampuni ya familia ya kuwarithisha hao watoto.

Hawawasomeshi shule za kizungu kwa ajili ya kuja kuzinguka na bahasha kutafuta ajira.. huwezi kukuta mwanafunzi waliesoma IST yupo kwenye interview za utumishi dodoma
 
Ukienda mlimani city ndio utakutana na maajabu ya watoto wanaosoma hizo Eng
Hzo shule kama mtaala wao ni huu huu wa Tz ni hasara otherwise mtaala wao uwe ni wa Cambridge…And shule za mtaala wa Cambridge ada yao ni kuanzia 20 mil na kuendelea!!
Shule nyingi zinatumia mtaala.wa NECTA. ZA CAMBRIDGE ziko chache sana na kama ylivyosema , ada ni zaidi ya 20m kwa mwaka na inategemea yuko grade gani.
All in all, hata waliosoma hizo zenye mitaala ya CAMBRIDGE haisaidii sana kama soko lao la ajira ni hili hili la Tanzania.
Unawekeza billions kwenye elimu halafu outputs ni ndogo.
Kuna dada mmoja kasoma Feza International baada ya hapo masters Marekani, kaja kuajiriwa ubalozini . Kazi anajifunza kama wengine tu ambao wamesoma vyuo vya bongo. Kazi ni zaidi ya elimu ya darasani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…