Mtu mwenye degree anapoenda kujifunza kazi ya waliokosa Elimu ni ujumbe gani tunapata kuhusu Elimu yetu?

Kuna coz inaaitwa bee keeping[emoji28][emoji28] ipo UDSM
Wanachofundishwa ni sawa na elimu ya wazee wetu wazamani wasiyokuwa na elimu kabisa wa kimang'ati. Namtu anachukua elimu nadhalia miaka 3 mtoto aliyekulia masaki anayeogopa hata mende tatizo ni pale atakapo maliza kusoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wala siyo la kushangaza wapo hadi wachoma chapati ,
Muhimu mkono kinywani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siyo rahisi kama unavyosema. Graduates wa course hizo ni wengi mno. Wengi wanahangaika mitaani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ni rahisi kama nilivyosema maana nimemaliza kozi tofauti na nimekua nazipata kazi hizo tu kwenye mashirika ya kimataifa...amini nakwambia..kutafuta na kupata kazi ni mbinu tofauti na ku graduate katika kozi husika
 
Matajiri wote ni waliopata ujasiri wa kujiajiri usishangae kesho na keshokutwa ana kampuni ya mitindo halafu wanao ndo maafisa masoko wake
 
Kushona cherehani wala sio tatizo,ila tatizo litaanza pale huyo mpwa wako atakapo amua kuweka mizizi kwenye cherehani pekee Hapo ndipo penye tatizo.

ila kama atashona cherehani kisha akajitanua na kuwaza vingine na vingine cherahani iwe kama mlango tu wa kuingilia basi nadhani mpwa wako chuo hakufika bahati mbaya.

nitashangaa sana kama december mwakani muda kama huu mpwa wako atakua pale pale kwenye kibaraza na cherehani yake,hapo nitasema mpwa wako kweli angetakiwa tu kuishia la saba.

ila kama mwakani Muda kama huu mpwa wako utamuona kaimarika,mtaji wa cherehani umesimama,yupo kwenye ofisi yake basi tambua mpwa wako elimu yake inamsaidia.

Siku zote naumia sana kuona mtu anafanya kazi ile ile miaka na miaka mpk wanambatza jina"fundi nguo" "mshonaji",nk kwakweli naumiaga sana,Mpwa wako kaamua kuja ktk ujasiriamali kamshauri akili isijifungie hapo kwenye chumba cha ushonaji nguo,mwambie asione kafika.

Mwakani akuonyeshe vibiashara vingine alivyovifungua kupitia cherehani hapo ndipo tutampa BIG thumb kweli kweli ila mwakan imefika yupo kibarazani katundka nguo kama yule wa darasa la 7 aaaaah we jua umekula hasara kwa huyo mpwa.
 
Afanye tu kazi kwa bidiiii fungu alilochagua ni jema sana kuliko kazi ya mshahara 800k per month,nakuhakikishia mpwa wako kama yupo seriouz atapoanza tu kufanya hiyo kazi kwa uaminifu miezi 6 tu,Htakua na mawazo tena ya kuajiriwa na kama akitaka kuajiriwa atakua na vigezo vyake vya mwajiri anaetaka kumuajiri ataevifikia ndio atamuajiri.

Nakuhakikishia hutokaa umuone anazunguka na Bahasha tena na Tena,ukimuona ana bahasha ujue n katoka kununua chipsi basi wamemuekea humo kwa kua sku hz hamna mifuko.

Ujasirimali tena fundi kushona ina pesa hiyo kazi jamani sema basi tu watu tunadharau dharau kazi,acha uone mabalaa ya huyo mpwa wako "Nakutahadharisha tu" usije ukamuita mchawi akitoboa maana nakuhakikishia anaenda kutoboa na anapenya kweli.
 
Hapa Mwanza kuna kondakta wa daladala, ana degree ya mambo ya usafirishaji kutoka NIT - Dar (Chuo cha Usafirishaji - DAR), tena sio kwamba ni gari la nyumbani kwao laa hasha!
 
Bado anafaida kubwa sana ya kusoma ,atatumia elimu yake kuongesa ufanisi wa katika kushona kwa kutafuta wateja wengi ,kupanua soko la huduma yake ,kutumia technologia kwenye kushona na mengine mengi .Huwezi kufanya haya kama huna elimu ,ni sawa yawezekana haya anaweza kufanya haya ila ni kwa kuchelewa sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umemuelimisha vizuri. Hili ni tatizo la mindset za watanzania karibu wote, kuwa watu wanasoma ili wapate kazi nzuri zenye marupurupu na mishahara mikubwa. Ukimwongozea hapo tena na u-bosi basi anajiona yeye ni kila kitu. Jamani lengo la elimu siyo kuajiriwa. Lengo la elimu ni kupanua wigo wa kupambana na mazingira. Hapa JF mijadala ya kulaumu kuwa mtu amepoteza muda bure kwenye elimu ipo sana. Hii inaonyesha elimu yetu inavyowaandaa wahitimu wake. Kuna kipindi nilisoma member mmoja alikuwa analaumu kuwa Diamond mwanamuziki hajasoma lakini ana ''mkwanja'' kuliko maprofesa wa vyuo vikuu hivyo elimu haina maana yoyote! Just imagine mawazo fyongo kama haya tena yanatolewa na mtu mwenye elimu ya chuo! Bila kufumua mitaala ya elimu yetu na watu waende shule na vyuoni ili kuelimika na siyo kukariri kwa ajili ya kupasi mitihani kwa matarijio ya ajira nzuri hatutafanikiwa!
 
Kazi ya waliokosa elimu ndio kazi gani hizo ? kila kazi unayofanya ni lazima uwe na elimu nayo sasa umeipataje hiyo elimu utajua mwenyewe
 

Nina dogo anauza Mitumba kigamboni huko kwenye minada.
 
Atafanya hiyo lkn baadaye atapata kiwanda usicheze na mtu shule
 
Mm naona hakuna alichokosea....kuwa fundi Nguo wakati una degree sio tatizo...uzuri degree yake inauhusiano wa karibu na kazi hiyo....kwa kuwa yeye amesoma basi kazi zake zinatakiwa ziwe zenye ubora zaidi ili kuakisi elimu yake ya degree....na akijipanga vizuri mbeleni anaweza kuja kuwa na viwanda vya nguo na akaajiri watu wengine...tuwe kama wahindi...wahindi wengi utawaona vyuoni lakini wakiisha maliza tu...hawaendi kuajiriwa bali kujiajir i. Kumbuka pia kuna group kubwa la wasomi walioajiriwa -na huko kwenye ajira mambo hayaendi sawa hivyo wanatafuta namna ya kutoka wajiajiri lakini mazingira yanawabana...muache mtoto ajiajiri- kuajiriwa ni utumwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…