Mtu mwenye degree anapoenda kujifunza kazi ya waliokosa Elimu ni ujumbe gani tunapata kuhusu Elimu yetu?

Mtu mwenye degree anapoenda kujifunza kazi ya waliokosa Elimu ni ujumbe gani tunapata kuhusu Elimu yetu?

Nimetoka kuzungumza na mpwa wangu sasa hivi anaomba msaada wa cherehani akajifunze kushona nguo, ndio mradi aliobuni baada ya kusota miaka 2 bila ajira. Amesoma ana degree Bachelor of Arts in Community and Development Studies.

Kaniambia ameshapata mtu wa kumfundisha na mahali pa kujifunzia (baraza fulani hivi). Ninavyofahamu huyo fundi cherehani atakayekuwa anamfundisha mpwa wangu kushona ana elimu ya darasa la saba tu, jamani! Huyu fundi atapata ujumbe gani kuhusu kusomesha mtoto?

Hivi kweli ni sawa kijana asome hadi elimu ya university aishie kuja kufundishwa ushonaji na mtu wa la saba? Kulikuwa na sababu gani ya kupoteza gharama na muda wote huo, si bora tu angeenda ushonaji alipomaliza la saba, labda sasa hivi angekuwa mbali sana. Au kuna mahali tunakosea katika elimu hizi, tuna universities nyingi na courses nyingi lakini kumbe wanachohitaji watu ni ufundi cherehani tu! Tunahangaika na mambo makubwa ya gharama kubwa bure tu!

Interestingly mpwa wangu ana shauku kubwa ya kutekeleza mpango wake huu, anauchukulia serious kabisa, anaanza kesho rasmi! Namtakia kila la heri lakini kwa kweli nashangaa tu, mimi katika makuzi yangu niliona degree ni level kubwa sana, si ya kutumia kwenye cherehani. Lakini basi ndiyo imeshakuwa hivyo.

Tunakwama wapi?
Kwa hiyo degree ulitaka aende wapi?
 
The sad part hata ushauri mzuri anaopata kutoka humu JF unaishia kwenye makabati,hata huu uzi utapita na kubaki kwenye archives za Jamii Forums..sio bure kuna tatizo la kusikia ama kuona kwa viongozi wetu lol
 
Nafikiri tatizo si elimu ila tatizo ni mpwa kuitumia Hiyo elimu

Elimu haikuanzishwa ili Watu waajililiwe ila ilanzishwa ili Watu waweze kutawala mazingira yao vizuri kwa uarahisi

Tunapokwama tunachukulia elimu ni kama njia ya kuajiliwa badala kuchulia kama njia ya kutufungua ufahamu wa kutawala mazingira
Nafikiri tatizo si elimu ila tatizo ni mpwa kuitumia Hiyo elimu

Elimu haikuanzishwa ili Watu waajililiwe ila ilanzishwa ili Watu waweze kutawala mazingira yao vizuri kwa uarahisi

Tunapokwama tunachukulia elimu ni kama njia ya kuajiliwa badala kuchulia kama njia ya kutufungua ufahamu wa kutawala mazingira
Nafikiri tatizo si elimu ila tatizo ni mpwa kuitumia Hiyo elimu

Elimu haikuanzishwa ili Watu waajililiwe ila ilanzishwa ili Watu waweze kutawala mazingira yao vizuri kwa uarahisi

Tunapokwama tunachukulia elimu ni kama njia ya kuajiliwa badala kuchulia kama njia ya kutufungua ufahamu wa kutawala mazingira

Elimu inaweza kumsaidia mtu alieyeipata aweze kutumia mazingira yake kama fursa ya kujipatia rizki yake ya kila siku ikiwa tu elimu hiyo imempa uwezo mhitimu wa kuyamudu mazingira yake, jambo ambalo halipo katika nchi zetu za ulimwengu wa tatu.
Mi nafikiri na ninaamini kwamba ni wakati muafaka sasa elimu yetu kuanzia msingi, sekondari, vyuo vya kati na vya juu imuandae mhitimu ambae atatumia maarifa aliyoyapata kuwa mzalishaji na sio mtoa huduma kama ilivyosasa ambapo taifa linazalisha walimu, wanasheria, wahasibu, madaktari, maafisa utumishi n.k ambao wote hawa ili waweze kuishi kwa kutegemea elimu waliyoipata ni lazima waajiriwe ili waweze kuhudumia, vinginevyo itawabidi kufanya kazi nje ya taaluma zao, kazi ambazo kimsingi angeweza kufanya hata asingeenda shule.
Hivi sasa sio ajabu kuona mhitimu wa chuo kikuu akiuza juice ya miwa, mitumba, mihogo, kupiga debe, dereva wa bodaboda, mama ntilie n.k.
Kimsingi kama taifa kuna haja ya kupitia upya aina ya elimu tunayotoa kwa vijana wetu kwa maslahi yao binafsi, familia zao na taifa kwa ujumla. "HAKUNA TAIFA DUNIANI LILILOPIGA HATUA KIMAENDELEO KWAKUA NA ELIMU INAYOZALISHA WAHUDUMU WENGI KULIKO WAZALISHAJI"
 
Mkuu umegusia kitu cha msingi sana,shukrani sana.
Ufikiri wa jamii, na wewe ukiwemo ndio shida, hakuna kazi za walioelimika na wasioelimika, shuleni huwa tunaenda kusoma ili kupanua mawazo yatakayo tusaidia katika kuendesha maisha yetu.

Sasa hizi degree tunasomea, mengi ni mambo ya utawala, ndipo unajikuta umesomea, utawala wa biashara, au maendeleo ya jamii, lakin, ni biashara gani unayoitawala? skills za hiyo biashara hauna, Au maendeleo ya jamii, je jamii inajihusisha na kazi zipi? hauna hiyo elimu.

Ni kweli kuna kashida kadogo kwenye mfumo wa elimu wetu, nao ni hako ka kuto incoroprate vocational training kwenye mafunzo yetu. Dogo kasoma, kaona anahitaji kujifunza cherehani, ili labda sasa aje atumie elimu yake ya chuo kikuu, kuendesha biashara ya cherehani, kwanza apatie mtaji,kisha ajikite huko. Wazo ambalo ni jema sana, na namuunga mkono 100%. Amini amini nakuambia, kwa moyo ambayo huyo dogo anaonesha, kuna kitu amekiona kwenye huo mchoro wake, na ndio manufaa ya elimu hayo. mwache aende, 5 years anaweza kuwa na story ya tofauti kuliko huyo fundi anaemfundisha? Je Haukusoma habari za mafundi vyerehani waliobahatika kutoka nchini mwetu hapa? Akina Speshoz, na Wengine, Kama Speshoz ni ana had masters kabisa, kaanza na kushona pia ila leo ana biashara kubwa ya fashion na sports. Sasa kwa nini kijana wa miaka 30, ndio anamikataba ya jezi kwa timu mbalimbali nchini, na ndo anaivalisha stars na Wasanii kama Diamondplatunuzm, anashina suti za harusi kwa bei karibu na mshahara wa miezi mitatu wa mwalimu mwenye degree? ni kwa sababu hakuwa fundi cherehani wa kawaida, nini kilimfanya asiwe fundi cherehani wa kawaida, ni Elimu yake ya masters. Na unajua ni kwa nini kwanini sio wote wenye elimu ya masters na hata wengine maprof hawaingizi mkwanja mrefu kama anaongiza yeye saivi? ni kwa sababu yeye nje ya Elimu yake ya mastars ana ujuzi, huo ujuzi ambao wewe unadhani dogo kapotea kuutafuta saivi. Ujuzi wa kushona.

So muache dogo afanye anachoona, na hayo ndiyo matumizi ya elimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo kwenye ufundi anakuwa anawashonea watu pia, koneksheni ni popote.
it depend anashonea wapi ila vigumu sana fundi mshona nguo kuwa na connection kubwa zaidi atakuwa mtuma salam radioni na mtoa maoni kwenye vipindi vya leo tena clouds fm
 
elimu sio njia ya mafanikio ila elimu ni mwongozo wa kila binaadamu kwenye uso wa dunia unaposoma kuna vitu vingi sana atapata kuvielewa ambavyo ni msaada tosha kwenye maisha ya binaadamu wenye elimu wengi ni masikini duniani na wenye elimu ya kati ambayo haina msaada wowote duniani lakini ndo matajiri mkuu hivyo basi tuache tabia ya kuchukulia kwamba ukiwa na elimu basi lazima upate pesa au kazi nzuri tabia hii mbaya sana pia unaweza kuwa darasa la saba ila ukapata kazi nzuri sana na yenye mafanikio makubwa sana wengi tunao kwenye jamii zetu tukae tukitambua elimu ni chanzo cha maarifa tu na si chanzo cha mafanikio.

Sent using Jamii Forums mobile app

elimu sio njia ya mafanikio ila elimu ni mwongozo wa kila binaadamu kwenye uso wa dunia unaposoma kuna vitu vingi sana atapata kuvielewa ambavyo ni msaada tosha kwenye maisha ya binaadamu wenye elimu wengi ni masikini duniani na wenye elimu ya kati ambayo haina msaada wowote duniani lakini ndo matajiri mkuu hivyo basi tuache tabia ya kuchukulia kwamba ukiwa na elimu basi lazima upate pesa au kazi nzuri tabia hii mbaya sana pia unaweza kuwa darasa la saba ila ukapata kazi nzuri sana na yenye mafanikio makubwa sana wengi tunao kwenye jamii zetu tukae tukitambua elimu ni chanzo cha maarifa tu na si chanzo cha mafanikio.

Sent using Jamii Forums mobile app
asante kwa ushauri ila tz wanasiasa ndio wanatuangusha na ndio hao unaosema hawana elimu ila wanamafanikio ndio wanaoshindwa kuweka mazingira bora kwa vijana kuweza kwenda na ushindani wa soko la ajira elimu yetu ipo ipo tu uyu kijana kana kushona angejifunzia kipindi yupo shule

Kuna ugumu gani kijana alikiwa shule ya msingi darasa la sita akafanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi na akifika sekondari baada ya kidato cha nne basi elimu ya ufundi iwe lazima kwa wahitimu wote baada ya hapo ndio vijana wajiunge na vyuo
 
Pamoja na bandiko lako lenye mrengo wa ki 'enzi za nyerere', embu tutolee mfano sasa ambao unaona ni njia sahihi ya msomi wa aina ya mwipwao kufanya hasa hizi za kujiajiri, maana 'white colour job' hazikamatiki.

Ulitegemea kazi za ujasiriamali mtaani zinafundishwa na ma profesa?

Ungelikuwa umepitia angalau Jkt, ungelielewa maana ya mkufunzi na mwanafunzi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimetoka kuzungumza na mpwa wangu sasa hivi anaomba msaada wa cherehani akajifunze kushona nguo, ndio mradi aliobuni baada ya kusota miaka 2 bila ajira. Amesoma ana degree Bachelor of Arts in Community and Development Studies.

Kaniambia ameshapata mtu wa kumfundisha na mahali pa kujifunzia (baraza fulani hivi). Ninavyofahamu huyo fundi cherehani atakayekuwa anamfundisha mpwa wangu kushona ana elimu ya darasa la saba tu, jamani! Huyu fundi atapata ujumbe gani kuhusu kusomesha mtoto?

Hivi kweli ni sawa kijana asome hadi elimu ya university aishie kuja kufundishwa ushonaji na mtu wa la saba? Kulikuwa na sababu gani ya kupoteza gharama na muda wote huo, si bora tu angeenda ushonaji alipomaliza la saba, labda sasa hivi angekuwa mbali sana. Au kuna mahali tunakosea katika elimu hizi, tuna universities nyingi na courses nyingi lakini kumbe wanachohitaji watu ni ufundi cherehani tu! Tunahangaika na mambo makubwa ya gharama kubwa bure tu!

Interestingly mpwa wangu ana shauku kubwa ya kutekeleza mpango wake huu, anauchukulia serious kabisa, anaanza kesho rasmi! Namtakia kila la heri lakini kwa kweli nashangaa tu, mimi katika makuzi yangu niliona degree ni level kubwa sana, si ya kutumia kwenye cherehani. Lakini basi ndiyo imeshakuwa hivyo.

Tunakwama wapi?
We umesema nn na he hichi ili chia dola ndo ukichosomea?
 
Nimetoka kuzungumza na mpwa wangu sasa hivi anaomba msaada wa cherehani akajifunze kushona nguo, ndio mradi aliobuni baada ya kusota miaka 2 bila ajira. Amesoma ana degree Bachelor of Arts in Community and Development Studies.

Kaniambia ameshapata mtu wa kumfundisha na mahali pa kujifunzia (baraza fulani hivi). Ninavyofahamu huyo fundi cherehani atakayekuwa anamfundisha mpwa wangu kushona ana elimu ya darasa la saba tu, jamani! Huyu fundi atapata ujumbe gani kuhusu kusomesha mtoto?

Hivi kweli ni sawa kijana asome hadi elimu ya university aishie kuja kufundishwa ushonaji na mtu wa la saba? Kulikuwa na sababu gani ya kupoteza gharama na muda wote huo, si bora tu angeenda ushonaji alipomaliza la saba, labda sasa hivi angekuwa mbali sana. Au kuna mahali tunakosea katika elimu hizi, tuna universities nyingi na courses nyingi lakini kumbe wanachohitaji watu ni ufundi cherehani tu! Tunahangaika na mambo makubwa ya gharama kubwa bure tu!

Interestingly mpwa wangu ana shauku kubwa ya kutekeleza mpango wake huu, anauchukulia serious kabisa, anaanza kesho rasmi! Namtakia kila la heri lakini kwa kweli nashangaa tu, mimi katika makuzi yangu niliona degree ni level kubwa sana, si ya kutumia kwenye cherehani. Lakini basi ndiyo imeshakuwa hivyo.

Tunakwama wapi?
Hili linaonesha pengo kubwa katika elimu yetu.

Nchi zilizoendelea kwenye elimu hata ushonaji una degree yake. Inaheshimika.

Tuseme mtu anayependa kushona anataka kusomea kushona mpaka level ya degree.

Kwa Tanzania atasoma chuo gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Humu kuna watu twawaita ma GT ila ni wapumbavu kiasili na hawataki kuelewa ku ni wapumbavu.

kuna ubaya gani kufunzwa kazi na drs la 7, mimi nimefunzwa kazi na drs la 7 taasisi flani.Badae nikapewa kuwa msimamizi wao (wakati naenda pale wanajamii hasa marafiki walikuwa wananibeza badae tukikutana wananisifia bora kazi ndogo kuliko kukaa bure)

nimetoka pale nikachukuliwa na taasisi nyingine (inayo fanya kazi sawa na ile ya mwanzo wakanipa kitengo)

la saba ama asiyesoma kukufunza kazi ni kawaida sana,kazi inabaki kwako kujiongeza, kufanya kwa malengo na kujitoa pale.
 
Mimi nimeapa mwanangu nitamsomesha mpaka form 4 tu baada ya hapo namtafutia akasome ujuzi wowote hizi takataka za degree ni upuuzi mtupu hazina impact yoyote mtaani ili utengeneze pesa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Well said
Humu kuna watu twawaita ma GT ila ni wapumbavu kiasili na hawataki kuelewa ku ni wapumbavu.

kuna ubaya gani kufunzwa kazi na drs la 7, mimi nimefunzwa kazi na drs la 7 taasisi flani.Badae nikapewa kuwa msimamizi wao (wakati naenda pale wanajamii hasa marafiki walikuwa wananibeza badae tukikutana wananisifia bora kazi ndogo kuliko kukaa bure)

nimetoka pale nikachukuliwa na taasisi nyingine (inayo fanya kazi sawa na ile ya mwanzo wakanipa kitengo)

la saba ama asiyesoma kukufunza kazi ni kawaida sana,kazi inabaki kwako kujiongeza, kufanya kwa malengo na kujitoa pale.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom