Mtu Mweusi [Mwafrika] sio uzao wa Adam na Hawa

Mtu Mweusi [Mwafrika] sio uzao wa Adam na Hawa

Awali ya yote ningependa kuwasalimu wanajamii wenzangu habari zenu, natumai ni wazima wa afya.

Nina maswali kadhaa ambayo ningependa kupata majawabu kutoka kwenu wana Jamiiforums yatakayo kuwa msaada na faida kwa jamii nzima na kubadili
taswira na mtazamo wa jamii nzima juu ya asili ya mtu mweusi [ mwafrika ] na uwepo wake hapa duniani.
Maswali:
1. Je mtu mweusi[ Mwaafrika ] ni uzao wa Adamu na Hawa ?

2. Je Adamu na Hawa walikuwapo pekee duniani ? na Afrika kulikuwa hakuna watu?

3. Je uzao wa mtu mweusi ni kutoka ndani ya Afrika au nje ya Afrika ? Na Kama ni kutoka nje ni kutoka kwa nani watu wa bara la Ulaya [wazungu], watu wa Mashariki ya Kati, watu wa Asia ya mbali au watu wa bara la Amerika?

4. Je inawezekana mtu mweupe kwa mweupe [ mfano mzungu kwa mzungu ] kuzaa mtu mweusi?

N.b: Matusi na lugha za kuudhi hazitakiwi , pia unaweza kuongeza maswali yako kama kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.
Mkuu, jaribu kujielimisha kuhusu matokeo ya utafiti wa sayansi. Siku hizi wataalamu hukubaliana kwamba Homo Sapiens (sisi sote) alianza Afrika na kusambaa kote duniani. Rangi si kitu sana kibiolojia; watu walibadilika katika mwendo wa miaka elfu nyingi.

Maana rangi nyeusi-nyeusi ni kinga dhidi miale ya uruajimno (ultraviolet) inayosababisha kansa kwa watu wanaokosa rangi hiyo. Kinyume rangi nyeusi ya ngozi inapunguza uwezo wa kujenga "Vitamini D" mwilini hivyo watu weusi-weusi wana weza kuwa na magonjwa kutokana na uhaba huo wa vitamini D (hasa kudhoofika kwa mifupa tangu utotoni).
Hivyo watoto wenye rangi nyeupenyeupe kidogo walistawi vizuri zaidi katika maeneo penye Jua kidogo huko kaskazini.

Mengine ni kanuni zilizotambuliwa na Bwana Darwin na wanabiolojia / matibabu: waliofaa aidi kwa mazingira walistawi zaidi na hivyo kiasi ha "weupe" na "weusi" kiliongezeka polepole katika maeneo tofauti ya Dunia.

Hii utaona pia Uhindini Kusini penye watu weusi sana (wasiofanana na Waafrika) na kule Amerika karibu na Ikweta.
 
Usihangaike sena,Mkuu

Kwa mujibu wa kitabu cha Quran sura 15 aya ya 28(al hijr 15:28)..

MwenyeziMungu(allah),Alimwambia Muhammad:-

"ewe Muhammad unakumbuka nilipowambia Malaika kuwa nitamuumba Binaadamu kutoka katika udongo MWEUSI wa ufinyazi,ambao huleta sauti pale unapokauka"...

Aya inaonyesha wazi kuwa binadamu wa mwanzo alikuwa mtu mweusi,Adam alikuwa mtu mweusi..

Sura inaendelea kuwa, baada ya Mungu kumuumba kiumbe hicho chenye rangi nyeusi,aliwambia Malaika wamsujudie

Kwa mujibu wa Quran,HAWA ametoka kwenye ubavu wa kushoto wa Adam,kwa maana hiyo Hawa nae alikuwa binaadam mweusi..

Hiyo ndio sayansi ya Quran,huo ndio ukweli wa mambo

Kitaalamu kutoa rangi nyeusi unaweza kutoa rangi yoyote ile..
Kama ndio hivyo mtu wa kwanza alikuwa mtu mweusi [ Adamu na Hawa ] .je watu wa rangi nyingine hapa duniani walitoka wapi ?

N.b: jibu swali hilo , pia ukilejea swali namba 4.
 
Kwa nini ?
Swali lako la creation theory umelitoa kwenye vitabu vya kiimani alafu unajifanya hujui kuhusu vitabu vya kiimani (huna dini), swali kwako Adam na Hawa uliwajulia wapi km sio kupitia vitabu vya kiimani?

Na hio inaonyesha ima umesimuliwa au umesoma kuhusu hao viumbe wa kwanza kuumbwa na Mwenyezi-Mungu na swali la pili km huna dini na uhamini kuhusu Mungu unadhani hao viumbe ambao ni watangulizi wa binadamu wote katika uumbaji kwa imani uliyopo unaamini walitokea kutoka wapi?
 
Mkuu, jaribu kujielimisha kuhusu matokeo ya utafiti wa sayansi. Siku hizi wataalamu hukubaliana kwamba Homo Sapiens (sisi sote) alianza Afrika na kusambaa kote duniani. Rangi si kitu sana kibiolojia; watu walibadilika katika mwendo wa miaka elfu nyingi. Maana rangi nyeusi-nyeusi ni kinga dhidi miale ya uruajimno (ultraviolet) inayosababisha kansa kwa watu wanaokosa rangi hiyo. Kinyume rangi nyeusi ya ngozi inapunguza uwezo wa kujenga "Vitamini D" mwilini hivyo watu weusi-weusi wana weza kuwa na magonjwa kutokana na uhaba huo wa vitamini D (hasa kudhoofika kwa mifupa tangu utotoni).
Hivyo watoto wenye rangi nyeupenyeupe kidogo walistawi vizuri zaidi katika maeneo penye Jua kidogo huko kaskazini.
Mengine ni kanuni zilizotambuliwa na Bwana Darwin na wanabiolojia / matibabu: waliofaa aidi kwa mazingira walistawi zaidi na hivyo kiasi ha "weupe" na "weusi" kiliongezeka polepole katika maeneo tofauti ya Dunia.
Hii utaona pia Uhindini Kusini penye watu weusi sana (wasiofanana na Waafrika) na kule Amerika karibu na Ikweta.
Je wazungu wakikaa Afrika na wakajamiana baina ya Wazungu kwa wazungu mtoto atakaye toka hapo atakuwa mweusi mfano Kama Mangala ? Na je Weusi wakienda kuishi ulaya na waka jamiana weusi kwa weusi mtoto atatoka mweupe mfano Kama Billget ?

N.b Rejea swali namba 4.
 
Anhaa sawa . Je alikuwa ni mtu wa rangi gani ? Na kipi kilipelekea uzao wake kuleta watu wa rangi tofauti ?
Quran inasema mtu wa mwanzo duniani alikuwa mweusi,Science inasema mtu wa mwanzo katokea Afrika,..Afrika ni ya watu weusi

Hapo Dini na Science zimekubaliana, mazingira na chakula ndiyo yanayomfanya mtu abadilike
 
Swali lako la creation theory umelitoa kwenye vitabu vya kiimani alafu unajifanya hujui kuhusu vitabu vya kiimani (huna dini), swali kwako Adam na Hawa uliwajulia wapi km sio kupitia vitabu vya kiimani? Na hio inaonyesha ima umesimuliwa au umesoma kuhusu hao viumbe wa kwanza kuumbwa na Mwenyezi-Mungu na swali la pili km huna dini na uhamini kuhusu Mungu unadhani hao viumbe ambao ni watangulizi wa binadamu wote katika uumbaji kwa imani uliyopo unaamini walitokea kutoka wapi?
Mkuu Nadhari ya “ Creation Theory” hii unaipata katika masomo mbalimbali ikiwemo Geography, History, Biology na sio katika vitabu tu vya kiimani vya kikristo na kiislamu .

Na swala la mimi kutokuwa na dini hayo ni maamuzi yangu binafsi amabayo hata wewe na mtu yoyote yule hapa duniani hawezi kuyabadali yapo hivyo na yata endelea kuwa hivyo. turudi kwenye maswali yangu Kama utakuwa na majawabu karibu kutoa majawabu yako na kuyatetea.
 
Bila shaka huo ni mtazamo wako ila hakuna ukweli wowote.
Nadhani unafaham ama ushawahi kumskia malikia wa Sheba kutoka Ethiopia,
Malkia wa Sheba alizaa na Mfalme Suleman, mtoto aliitwa Meneliki wa Kwanza naye akamza Menelik II, Menelik II akamzaa Haile Sellasie
Swali je hao wote walikuwa watu weupe na ikumbukwe Suleman ni uzao wa Daudi generation ya Baba wa Iman Ibrahim.

Ungesema habar za Evolution kibiologia angalau ungekuwa unaelekea kweny fact japo hakuna empirical evidence.
Habari hizi unazithibitishaje ?
 
Quran inasema mtu wa mwanzo duniani alikuwa mweusi,Science inasema mtu wa mwanzo katokea Afrika,..Afrika ni ya watu weusi

Hapo Dini na Science zimekubaliana, mazingira na chakula ndiyo yanayomfanya mtu abadilike
Je watu weusi walioenda kuishi Ulaya wamekuwa wazungu? Na je wazungu waliokuja kuishi Afrika wame kuwa weusi ?
 
Mtu mweusi na mtu mweupe Ni watu wawili tofauti kabisa.

Mtu mweusi hakutokana kwenye uzao wa mtu mweupe na vilevile, mtu mweupe hakutokana kwenye uzao wa mtu mweusi.

Hata Biblia yenyewe imeshindwa kueleza kwamba watu weusi wametokea wapi. Biblia inaongelea kuhusu Wana wa Israel ambao Ni weupe (hakuna sehemu imeelezea mu Israel alibadilika na kuwa mtu mweusi).
 
Kama ndio hivyo mtu wa kwanza alikuwa mtu mweusi [ Adamu na Hawa ] .je watu wa rangi nyingine hapa duniani walitoka wapi ?

N.b: jibu swali hilo , pia ukilejea swali namba 4.
Mazingira na chakula ndiyo yanayombadilisha mtu..

Mwili wa binadamu ni mkusanyiko wa chemikali,mwilli wa binaadamu unabadilika kutokana na unaulisha hizo chemical,..

Hali ya hewa inachangia sana muonekano wa binaadamu,ngozi huweza kubadilika kutokana na kupata jua sana au kukosa jua....

Zaidi Miaka milioni 4 binaadamu wote walikuwa rangi moja,walibadilika kutokana na wapi wanaishi
 
Mkuu Nadhari ya “ Creation Theory” hii unaipata katika masomo mbalimbali ikiwemo Geography, History, Biology na sio katika vitabu tu vya kiimani vya kikristo na kiislamu .
Na swala la mimi kutokuwa na dini hayo ni maamuzi yangu binafsi amabayo hata wewe na mtu yoyote yule hapa duniani hawezi kuyabadali yapo hivyo na yata endelea kuwa hivyo. turudi kwenye maswali yangu Kama utakuwa na majawabu karibu kutoa majawabu yako na kuyatetea.
Emu nitajie kitabu kimoja tu cha biology ambacho kimeelezea vizuri kuhusu 'Adam na Hawa' na kimewataja na kuwaelezea vizuri ili na mimi niingie kwenye maktaba yangu nijaribu kukagua hizo rejea yaweza ikawa nilipitwa na wakati nikasahau kukisoma
 
Mtu mweusi na mtu mweupe Ni watu wawili tofauti kabisa.

Mtu mweusi hakutokana kwenye uzao wa mtu mweupe na vilevile, mtu mweupe hakutokana kwenye uzao wa mtu mweusi.

Hata Biblia yenyewe imeshindwa kueleza kwamba watu weusi wametokea wapi. Biblia inaongelea kuhusu Wana wa Israel ambao Ni weupe (hakuna sehemu imeelezea mu Israel alibadilika na kuwa mtu mweusi).
Sawa wewe kwa upande wako mtu mweusi katokana na jamii yake yenyewe ya watu weusi au katokana na jamii ya rangi nyingine?
 
Asili ya Mzungu ni mchanganyiko wa binadamu na alliens wakiwemo majini. Ukisoma biblia waliitwa majitu uzao wa malaika waliofanya ngono na wanawake wa kibinadamu waliokutwa uchi wakioga mtoni wakazaliwa majitu.
 
Mazingira na chakula ndiyo yanayombadilisha mtu..

Mwili wa binadamu ni mkusanyiko wa chemikali,mwilli wa binaadamu unabadilika kutokana na unaulisha hizo chemical,..

Hali ya hewa inachangia sana muonekano wa binaadamu,ngozi huweza kubadilika kutokana na kupata jua sana au kukosa jua....

Zaidi Miaka milioni 4 binaadamu wote walikuwa rangi moja,walibadilika kutokana na wapi wanaishi
Je unawezaje kulithibitisha Hilo?
 
Je watu weusi walioenda kuishi Ulaya wamekuwa wazungu? Na je wazungu waliokuja kuishi Afrika wame kuwa weusi ?
Miaka milioni nyingi inasemekana Watu walitoka bonde la ufa na kufanya safari ya vikundi,wengine walielekea bara Ulaya,Asia,wengine walielekea kusini mwa Afrika..

Baada ya millioni mingi ya miaka kupita wengine walifanya safari ya kurudi walikotoka..

Binaadamu walizagaa duniani wakizunguka zunguka..

Mtu wa mwanzo kuchimbuliwa na wanaakiologia katika nchi ya Ireland na Denmark,walikuwa na nasaba za mtu mweusi,wakati hizo ni nchi za Wazungu,nchi za bara la Ulaya
 
Emu nitajie kitabu kimoja tu cha biology ambacho kimeelezea vizuri kuhusu 'Adam na Hawa' na kimewataja na kuwaelezea vizuri ili na mimi niingie kwenye maktaba yangu nijaribu kukagua hizo rejea yaweza ikawa nilipitwa na wakati nikasahau kukisoma
Kasome topic kwenye biology inayozungumzia creation theory na evoulution theoory.
 
Asili ya Mzungu ni mchanganyiko wa binadamu na alliens wakiwemo majini. Ukisoma biblia waliitwa majitu uzao wa malaika waliofanya ngono na wanawake wa kibinadamu waliokutwa uchi wakioga mtoni wakazaliwa majitu.
Je asili ya mtu mweusi ni nini?
 
Mkuu Nadhari ya “ Creation Theory” hii unaipata katika masomo mbalimbali ikiwemo Geography, History, Biology na sio katika vitabu tu vya kiimani vya kikristo na kiislamu .
Na swala la mimi kutokuwa na dini hayo ni maamuzi yangu binafsi amabayo hata wewe na mtu yoyote yule hapa duniani hawezi kuyabadali yapo hivyo na yata endelea kuwa hivyo. turudi kwenye maswali yangu Kama utakuwa na majawabu karibu kutoa majawabu yako na kuyatetea.
Ikiwezekana pia nitajie na hivyo vitabu vya History na Geography ambavyo vimewaelezea kwa uzuri kuhusu 'Adam na Hawa' pasina kuhusisha rejea zozote za vitabu vya kiimani
 
Je unawezaje kulithibitisha Hilo?
Hahaha...
You are what you eat..
Nenda kaishi greenland,usipate jua,halafu uwe unakula samaki tu utaona kama ngozi yako na muonekano wako na utakachokizaa hakitobadilika..

Mkuu,hizi nazaria(theory),ni matokeo ya milioni ya miaka ..
 
Ikiwezekana pia nitajie na hivyo vitabu vya History na Geography ambavyo vimewaelezea kwa uzuri kuhusu 'Adam na Hawa' pasina kuhusisha rejea zozote za vitabu vya kiimani
Mkuu unataka nadharia ya Creation Theory au unataka maisha yote ya Adam na Hawa yaelezewe kwenye kitabu cha Historia na Jiografia ?
 
Back
Top Bottom