Mtuhumiwa wa Ubakaji amwambia Mwandishi wa Habari β€œAfu we Camera man nikimaliza kesi ntakutafuta”

Mtuhumiwa wa Ubakaji amwambia Mwandishi wa Habari β€œAfu we Camera man nikimaliza kesi ntakutafuta”

Watuhumiwa wanne wa kesi ya Ubakaji na ulawiti ambao ni Askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) MT 140105 Clinton Damas maarufu Nyundo, Amini Lema maarufu Kindamba, Nickson Jackson maarufu Machuche na Askari wa Jeshi la Magereza C 1693 Praygod Mushi wakiondolewa mahakamani jioni hii kurudishwa mahabusu mpaka Agosti 28, 2024 ambapo kesi hiyo itaendelea tena.

Nyundo na wenzake wakati wakitoka Mahakamani mmoja wao alisikika akimwambia Cameraman kuwa akifanikiwa kumaliza kesi yao atamtafuta "Wewe cameraman nikimaliza kesi nitakutafuta" Endelea Kufuatilia kurasa Zetu kufahamu Kuhusu kilichojiri Mahakamani kuhusu Kesi hii leo Agosti 23, 2024.

Kuna tuhuma kuwa baadhi ya watuhumiwa wakiwa wanahojiwa wanaingizwa vitu makalioni ikiwemo dushe.....


Hao wabakaji ni asset mpya kitengoni?
 
Ni utovu wa nidhamu wa Hali ya juu sana,kwanza kwa binadamu aliyelelewa ktk maadili mazuri hapo anajua ni kosa kabisa kuingilia kazi ya mtu pia ni wazi Kuna shida katika makuzi ya sasa maana kwa Hali aliyonayo mtuhumiwa angekuwa anajuta. Na pengine kuwa mtu wa sala na toba na pia mtu mtulivu maana ni kwa Nini awe yeye na siyo mtu mwingine,hili Ndo swala la msingi angekuwa anajiuliza.Naisi wazazi wa Leo Kuna sehemu tunakosea,Ina maana akitoka afanye Tena jinai,duh Dunia inapitia pabaya sana.
Sijajua kama huyu ndugu nae ni askari, lakini kinachoendelea kinatakiwa kiwe ujumbe kwa majeshi yetu.
Imekua ni sifa inayoonekana ya kawaida kwa askari wetu kutokua na maadili, na kwao wanaona kama ni kitu cha kujisifia.

Askari wakiwa mafunzoni na katika kambi zao wanatoka na tabia chafu sana za ulevinuliopindukia, uzinzi, ulawiti na vurugu nyingine nyingi, na imefika hatua jamii inazichukulia kama sifa zao za kawaida.

Jeshi linapaswa kujipambanua kwa kuhakikisha wahitimu wake wanakua mfano mzuri kwa jamii, na sio kujisifu kuwa na nidhamu kwa mamlaka huku wakiendelea kuonesha tabia hizi chafu.

Wakati nataka kuoa, kuna mtu aliwaeleza wakwe zangu kuwa mimi ni askari wa jeshi la wananchi (kitu ambacho si kweli, alinifananisha), nilikataliwa kabisa kwenda kupeleka posa kwenye familia ile hadi sababu ilipokuja kujulikana na mke wangu kueleza kuwa si kweli. Hii inaonesha ni namna gani katika baadhi ya jamii askari wetu wamepakwa matope na hizi sifa za hawa wahuni.
 
Subiri...atajua hajui Lofa huyu..hivi anafikiri kila mtu mfiraji sio....huyu kimbaumbau atashangaa..
 
Nchi ikishafikia hatua kuwa na askari wa aina hii hatari iliyoko ya taifa ni kubwa.

Ingekuwa jambo hili limetokea nchi za watu wenye akili hawa wa geshazikwa kwenye kaburi la pamoja muda huu.

Ile video waliyojirekdi ilitosha kabisa kutenganishwa vichwa na miili yao.

Kwa mtu mwenye akili unashinda kuamini aina ya akili ya watu hawa ambao ni waajiriwa wa serikali.

Mf.Askari JW anapata wapi njaa za kukodiwa na WP ili akafanye unyama kisha kujirekodi?

Hapa nchi imeaibishwa sana pamoja na amiri jeshi mkuu.

Hatuezi kuwa na jeshi linalobaka raia iwe hadharani au mafichoni.

Huu ni mwanzo wa uasi wa wazi. Kwa ajili ya usalama wa nchi hawa hawatakiwi kurudi mtaani wakiwa hai na hapo ndipo italeta heshima ya majeshi.

Jeshi letu linasifika kwa nidhamu sana. Haya mapaka yasiruhusiwe kuwepo kabisa humu duniani.
 
Atamtafuta cameraman baa ya miaka 30 ijayo au sikuhizi Sheria ya ubakaji imebadirika
 
Mkuu naomba tuongee vizri hapa..
Nimestuka mpaka nilitaka kumeza ulimi..

Weka vizr hapo ilikuaje yaani katembeq na msichana na sio mwanafunzi na kafungwa .
Na kafungwa miaka 30
Si unajua mabinti wa uswazi mkuu wazazi hawapo pamoja binti yuko huru tu akaona shule inambana kaacha akiwa sekondari akawa anazurura tu na kubadili wanaume.
Mdogo wangu (binamu)jumba bovu likamuangukia coz yeye akaamua kuweka kambi, Akawa mwanamke wake kabisa wa kudumu. Anaenda kwa dogo analala siku mbili tatu anarudi kwao.
Kesi ilikuwa nyepesi tu Kama mdogo wangu angekubali iishie polisi but dogo alikuwa mbishi akisema amedhalilishwa , binti ni mtu mzima na sio mwanafunzi. (Nadhan mawakili walimdanganya kwa kutumia ile Sheria ya ndoa inayoruhusu binti wa 15yrs kuolewa).
Polisi walitengeneza mazingira ya hela, dogo kashikilia msimamo kesi iende mahakamani yeye hatoi rushwa.
Kilichomkuta ni historia
 
Nyundo na wenzake wakati wakitoka Mahakamani mmoja wao alisikika akimwambia Cameraman kuwa akifanikiwa kumaliza kesi yao atamtafuta "Wewe cameraman nikimaliza kesi nitakutafuta" Endelea Kufuatilia kurasa Zetu kufahamu Kuhusu kilichojiri Mahakamani kuhusu Kesi hii leo Agosti 23, 2024.
Halafu aliyeambiwa cameraman ni mwanamke
Ila naye naona alivutiwa na mapigo akawahi kumwambia "si utanioa "
 
Back
Top Bottom