MTWARA: Basi la Shule ya King David lapata ajali, watu 10 Wamefariki na wengine 19 Wakijeruhiwa baada ya gari 'kufeli breki'

MTWARA: Basi la Shule ya King David lapata ajali, watu 10 Wamefariki na wengine 19 Wakijeruhiwa baada ya gari 'kufeli breki'

Kuna taarifa kuwa basi la Shule ya King David iliyoko Manispaa ya Mtwara Mikindani limepata ajali mbaya iliyopelekea vifo vya wanafunzi na dereva wa basi hilo aliyetambulika kwa jina moja Hassan anayekadiriwa kuwa na umri wa mika (54-60)

Miili imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Ligula na majeruhi wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.

Kama Kuna mzazi au mlezi mwenye mtoto huko afuatilie kinachoendelea. Pole kwa wafiwa na majeruhi, Mungu mwenye Enzi awaponye.

======
TAARIFA YA AWALI YA JESHI LA POLISI

Gari namba T207 CTS la Shule ya Msingi na Sekondari ya King David iliyopo Mtwara limepata ajali maeneo ya Mji Mwema, leo Julai 26, 2022 na kusababisha vifo vya Wanafunzi, dereva na Msaidizi.

Msaidizi wa Kamanda wa Polisi wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo amesema kuwa taarifa za awali waliofariki ni Wanafunzi Nane, Dereva mmoja na Mwangalizi wa Wanafunzi.

Naye RPC mwenyewe ACP Nicodemus Katembo alipopatikana alisema majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Ligula lakini watatoa taarifa zaidi baadaye.

UPDATES: 1130HRS

Watu kumi wamefariki dunia wakiwemo wanafunzi nane wa shule ya King David, huku wengine 19 wakijeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kufeli break na kutumbukia kwenye korongo, Mji Mwema mkoani mtwara. Kamanda wa polisi mkoani humo, Nicodemus Katembo amethibitisha

RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI

Kupitia akaunti yake rasmi Twitter, Rais Samia ameandika hivi

''Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa shule ya msingi ya King David na watu wazima 2 vilivyotokea leo asubuhi huko Mtwara Mikindani baada ya gari la shule kutumbulikia shimoni. Nawapa pole wafiwa, Mkuu wa Mkoa na jamaa. Mwenyezi Mungu awarehemu Marehemu na kuwaponya majeruhi.''

View attachment 2304245View attachment 2304246
View attachment 2304248

View attachment 2304261
Mbona haraka sana imetajwa sababu ni kufeli breki.
 
Kuna mzazi amepoteza Mtoto wake wa 1 na wa 2 na ndo hao pekee aliojaliwa. Najitahidi kuvaa viatu vyake miguu yangu inapwaya.
Nimetoka kusoma huko mtandaoni; nikashindwa hata kupata picha huyo mama ana hali gani muda huu. Mungu pekee ndiye anaweza kumpa faraja ya kweli na, kumfunga mikanda ya sirini na kumganga moyo wake. Viatu vyake havitutoshi kabisa.

Mungu apumzishe roho za marehemu wote, na awape afya njema majeruhi wote. Na kwa wafiwa wote; Mungu akawape nguvu na faraja yake isiyo na kikomo
 
Kwenye ile thread yangu ndefu, nilishawahi kutoa hint kuhusiana na swala hili la ajali; kwamba kuna events fulani mahali fulani ambazo huwa zinaonekana ku-coincide vizuri sana na hizi ajali; kwamba event hizo zinapokuwepo ndani ya wiki husika, ajali nazo huwa zinatokea ndani ya wiki hiyo. Kwa upnade mwingine, events hizo zinapokuwa hazipo na ajali nazo zinakuwa hazipo. Unless iwe kwamba kwa wiki hii, coincidence ya aina hii haikutokea. Siwezi kujua kama events zime-coincide na ajli hii sababu kwa wiki hii ninamiss ratiba ya wiki ya mahali ambapo ajali hizi huwa zinaonekana kuumana na matukio yake. Nimejitahidi kujaribu kusikiliza ratiba online lakini mtandao umegoma!
 
Kuna taarifa kuwa basi la Shule ya King David iliyoko Manispaa ya Mtwara Mikindani limepata ajali mbaya iliyopelekea vifo vya wanafunzi na dereva wa basi hilo aliyetambulika kwa jina moja Hassan anayekadiriwa kuwa na umri wa mika (54-60)

Miili imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Ligula na majeruhi wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.

Kama Kuna mzazi au mlezi mwenye mtoto huko afuatilie kinachoendelea. Pole kwa wafiwa na majeruhi, Mungu mwenye Enzi awaponye.

======
TAARIFA YA AWALI YA JESHI LA POLISI

Gari namba T207 CTS la Shule ya Msingi na Sekondari ya King David iliyopo Mtwara limepata ajali maeneo ya Mji Mwema, leo Julai 26, 2022 na kusababisha vifo vya Wanafunzi, dereva na Msaidizi.

Msaidizi wa Kamanda wa Polisi wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo amesema kuwa taarifa za awali waliofariki ni Wanafunzi Nane, Dereva mmoja na Mwangalizi wa Wanafunzi.

Naye RPC mwenyewe ACP Nicodemus Katembo alipopatikana alisema majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Ligula lakini watatoa taarifa zaidi baadaye.

UPDATES: 1130HRS

Watu kumi wamefariki dunia wakiwemo wanafunzi nane wa shule ya King David, huku wengine 19 wakijeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kufeli break na kutumbukia kwenye korongo, Mji Mwema mkoani mtwara. Kamanda wa polisi mkoani humo, Nicodemus Katembo amethibitisha

RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI

Kupitia akaunti yake rasmi Twitter, Rais Samia ameandika hivi

''Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa shule ya msingi ya King David na watu wazima 2 vilivyotokea leo asubuhi huko Mtwara Mikindani baada ya gari la shule kutumbulikia shimoni. Nawapa pole wafiwa, Mkuu wa Mkoa na jamaa. Mwenyezi Mungu awarehemu Marehemu na kuwaponya majeruhi.''

View attachment 2304245View attachment 2304246
View attachment 2304248

View attachment 2304261
IMG-20220726-WA0258.jpg
 
Uzembe Uzembe Uzembe Uzembe Uzembe.
Utasikia tunaanza kuisingizia bahati mbaya.
Utasikia kesho jeshi la polisi linaanza operation maalum dhidi ya haya magari.

Watoto wamekufa bila hatia bali uzembe wa mababa zao, mama zao na kaka zao.
Ndugu hivi ajali zote ni uzembe tumia basi ubongo wako hata kufikiri. Humu karibia wote watatoa lowama kua ni uzembe kitu ambacho sio kweli. Hamjajua chanzo lkn lowama zimekua nyingi sana. Mimi Kuna siku nimetumbukiza gari mtaron kwa kusababishiwa. Bus imeovatake uso kwa uso na Mimi ndo dereva ilinibidi nitumbukize kwenye mtaro.

Sasa ajali kama hiyo wapita njia wote walikua wanatoa lowama kwa uzembe wa dereva ameingiaje huko. Kila mtu alikua akiongea lake. Bila kujua chanzo ni nini?

Sent from my TECNO KG6 using JamiiForums mobile app
 
Huku nilipo magari ya wanafunzi spidi yao huwa ni ndogo, inakuaje huko mpaka madogo wanakufa kabisa daah.

Na vile watoto huwa wanakaa hovyo hovyo ni rahisi zaidi kupata madhara gari ikipata ajali, na huwa wanajazwa mno aisee.
 
Ndugu hivi ajali zote ni uzembe tumia basi ubongo wako hata kufikiri. Humu karibia wote watatoa lowama kua ni uzembe kitu ambacho sio kweli. Hamjajua chanzo lkn lowama zimekua nyingi sana. Mimi Kuna siku nimetumbukiza gari mtaron kwa kusababishiwa. Bus imeovatake uso kwa uso na Mimi ndo dereva ilinibidi nitumbukize kwenye mtaro.

Sasa ajali kama hiyo wapita njia wote walikua wanatoa lowama kwa uzembe wa dereva ameingiaje huko. Kila mtu alikua akiongea lake. Bila kujua chanzo ni nini?

Sent from my TECNO KG6 using JamiiForums mobile app

Kila ajali inayotokea duniani lazima kuna uzembe mahala, inawezekana mzembe sio wewe ila mzembe mwingine amekusababishia ajali, bado itakuwa ni uzembe tu, jaribu kufikiri vizuri.

Mtu akilewa chakari akaendesha gari vibaya na wewe ukammkwepa na kuingia mtaroni, hapo mzembe sio wewe bali uzembe ni wa yule dereva mlevi matokeo ya uzembe wake ni wewe kwenda mtaroni.

Tunaposema uzembe jaribu kuvuta picha kubwa, hapo kwenye hiyo ajali kuna uzembe na umeshaambiwa gari ilifail brakes, kwanini ifail brakes, inafanyiwa ukaguzi kila siku, inafanyiwa maintenance, brakes pads zinabadilishwa kila muda gani, check list ya gari inasemaje?, idadi ya watoto ni kupakia ilikuwa sawa, dereva ana akili timamu, dereva ana afya njema, dereva sio mlevi, dereva analipwa vizuri na kwa wakati?, Hilo hata ukiliangalia tu kwenye picha linaonekana kuwa ni chakavu na hali mbaya.

UKWELI: Magari mengi ya wanafunzi ni yale yaliyochoka na hayawezi kufanya kazi za abiria, mengi ni mabovu na yasiyofaa.
 
Duh.king david maskin asubuh nawaona wenyewe nikiwa nakuja mikindani boma hotel pahali pangu pa kazi
 
Back
Top Bottom